< Yoshua 9 >
1 Basi ikawa wafalme wote waliokuwa magharibi mwa Yordani waliposikia juu ya haya yote, wale waliokuwa katika nchi ya vilima, upande wa magharibi mwa vilima na katika pwani yote ya hiyo Bahari Kuu, hadi kufikia Lebanoni (wafalme wa Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi),
And when these things were heard, all the kings across the Jordan, who lived among the mountains and plains, along the coastline and shores of the great sea, also those who were living near Lebanon, the Hittite, and the Amorite, the Canaanite, the Perizzite, and the Hivite, and the Jebusite,
2 wakajiunga pamoja ili kupigana vita dhidi ya Yoshua na Israeli.
gathered themselves together, so that they might fight against Joshua and Israel, with one mind and with the same resolve.
3 Hata hivyo, watu wa Gibeoni waliposikia juu ya hayo yote Yoshua aliyowatendea watu wa Yeriko na Ai,
But those who were living in Gibeon, hearing all that Joshua had done to Jericho and Ai,
4 nao wakaamua kufanya hila: Wakajifanya kama wajumbe wakiwa na punda waliobebeshwa mizigo wakiwa na magunia yaliyochakaa na viriba vya mvinyo vikuukuu vyenye nyufa zilizozibwa.
planning cleverly, took for themselves provisions, placing old sacks upon their donkeys, and wineskins that had torn and been sewed up,
5 Walivaa miguuni mwao viatu vilivyoraruka na kushonwa kisha wakavaa nguo kuukuu. Chakula chao kilikuwa mkate uliokauka na kuingia koga.
and having very old shoes, which had been sewn with patches indicating their age, and being clothed in old garments, having also loaves, which they carried as food for the journey, which were hard and broken into pieces.
6 Ndipo wakamwendea Yoshua kambini huko Gilgali wakamwambia yeye pamoja na watu wa Israeli, “Tumetoka katika nchi ya mbali, fanyeni mkataba nasi.”
And they traveled to Joshua, who at that time was staying in the camp at Gilgal. And they said to him, and to all of Israel with him, “We have come from a far away land, desiring to make peace with you.” And the sons of Israel responded to them, and said,
7 Basi watu wa Israeli wakawaambia hao Wahivi, “Lakini huenda mnakaa karibu nasi, twawezaje basi kufanya mapatano nanyi?”
“Perhaps instead, you live in the land which ought to be ours by lot, and we would be unable to form a pact with you.”
8 Wakamwambia Yoshua, “Sisi ni watumishi wako.” Yoshua akawauliza, “Ninyi ni nani, nanyi mnatoka wapi?”
But they said to Joshua, “We are your servants.” And Joshua said to them: “But who are you? And where are you from?”
9 Nao wakamjibu: “Watumishi wako wametoka nchi ya mbali sana kwa ajili ya umaarufu wa Bwana Mungu wenu. Kwa kuwa tumesikia taarifa zake: hayo yote aliyofanya huko Misri,
They responded: “Your servants have arrived, from a very far away land, in the name of the Lord, your God. For we have heard about the fame of his power, all the things that he has done in Egypt,
10 pia yale yote aliyowatendea wafalme wawili wa Waamori mashariki ya Yordani; huyo Sihoni mfalme wa Heshboni na Ogu mfalme wa Bashani, aliyetawala huko Ashtarothi.
and to the two kings of the Amorites, who were beyond the Jordan: Sihon, the king of Heshbon, and Og, the king of Bashan, who was at Ashtaroth.
11 Basi wazee wetu na wale wote wanaoishi katika nchi yetu walituambia, ‘Chukueni chakula cha safari; nendeni mkakutane na watu hao na kuwaambia, “Sisi tu watumishi wenu, fanyeni mapatano nasi.”’
And our elders, and all the inhabitants of our land, have said to us: ‘Take in hand provisions for the very long journey, and meet with them, and say: We are your servants; form a pact with us.’
12 Mkate huu wetu ulikuwa wa moto tulipoufunga siku tulipoanza safari kuja kwenu, lakini sasa angalia jinsi ulivyokauka na kuota ukungu.
Lo, the loaves were taken up warm when we departed from our houses, so that we might come to you. Now they have become dry and broken, due to age.
13 Viriba hivi vya mvinyo vilikuwa vipya tulipovijaza, lakini ona jinsi vilivyo na nyufa. Nguo zetu na viatu vimechakaa kwa ajili ya safari ndefu.”
These wineskins were new when we filled them, now they are torn and broken. The garments we are wearing, and the shoes we have on our feet, due to the great length of the distance, have become worn and are nearly consumed.”
14 Basi watu wa Israeli wakavikagua vyakula vyao bila kupata shauri kutoka kwa Bwana.
And so they accepted this, because of their provisions, and they did not consult the mouth of the Lord.
15 Ndipo Yoshua akafanya mapatano ya amani pamoja nao kuwaacha waishi, nao viongozi wa kusanyiko wakathibitisha kwa kiapo.
And Joshua made peace with them, and entering into a pact, he promised that they would not be put to death. The leaders of the multitude also swore to them.
16 Siku ya tatu baada ya hao kufanya mapatano na Wagibeoni, Waisraeli wakapata habari kuwa hao watu ni jirani zao waliokuwa wanaishi karibu nao.
Then, three days after the pact was formed, they heard that they lived in the vicinity, and that they would soon be among them.
17 Ndipo wana wa Israeli wakasafiri na siku ya tatu wakafika kwenye miji yao ya Gibeoni, Kefira, Beerothi na Kiriath-Yearimu.
And so the sons of Israel moved the camp, and they arrived at their cities on the third day, those which are called: Gibeon, and Chephirah, and Beeroth, and Kiriath-jearim.
18 Lakini Waisraeli hawakuwashambulia kwa kuwa viongozi wa kusanyiko walikuwa wamewaapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli. Kusanyiko lote likanungʼunika dhidi ya hao viongozi,
And they did not strike them, because the leaders of the multitude had sworn to them in the name of the Lord, the God of Israel. And so all of the common people murmured against the leaders.
19 lakini viongozi wote wakawajibu, “Tumeshawaapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli, kwa hiyo hatuwezi kuwagusa sasa.
And they responded to them: “We have sworn to them in the name of the Lord, the God of Israel, and for that reason, we are not able to touch them.
20 Hivi ndivyo tutakavyowafanyia: Tutawaacha waishi, ili ghadhabu isije juu yetu kwa kuvunja kiapo tulichowaapia.”
But we shall do this to them: Certainly, let them be preserved so that they may live, lest the wrath of the Lord be stirred up against us, since we would have sworn falsely.
21 Wakaendelea kusema, “Waacheni waishi, lakini wawe wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya jamii yote.” Hivyo ahadi waliyoweka viongozi kwao ikawa hivyo.
But though they live, let them serve the entire multitude by cutting wood and carrying water.” And while they were discussing these things,
22 Kisha Yoshua akawaita Wagibeoni na kuwaambia, “Kwa nini mmetudanganya kwa kutuambia, ‘Tunaishi mbali nanyi,’ wakati ambapo ninyi mnaishi karibu nasi?
Joshua called the Gibeonites, and he said to them: “Why would you be willing to deceive us by fraud, saying, ‘We live very far away from you,’ when you are in our midst?
23 Sasa mko chini ya laana: Daima mtakuwa wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu.”
Therefore, you shall be under a curse, and your stock shall not cease to be cutters of wood and carriers of water, into the house of my God.”
24 Wakamjibu Yoshua, “Watumwa wako waliambiwa waziwazi jinsi Bwana Mungu wenu alivyomwamuru mtumishi wake Mose kuwapa ninyi nchi hii yote na kuwaangamiza wakazi wake wote toka mbele zenu. Kwa hiyo tuliogopa mno kwa ajili ya uhai wetu kwa sababu yenu, ndiyo maana tukafanya neno hili.
And they responded: “It was reported to us, your servants, that the Lord your God had promised his servant Moses that he would give you the entire land, and that he would destroy all its inhabitants. Therefore, we were very afraid, and we made a provision for our lives, compelled by the dread of you, and we undertook this counsel.
25 Sasa tupo mikononi mwako. Tufanyieni lolote mnaloona kuwa jema na haki kwako.”
And now we are in your hand. Act toward us as it seems good and right to you.”
26 Kwa hiyo Yoshua akawaokoa mikononi mwa Waisraeli, nao hawakuuawa.
Therefore, Joshua did just as he had said, and he freed them from the hand of the sons of Israel, so that they would not be killed.
27 Siku hiyo Yoshua akawafanya Wagibeoni wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya jamii na kwa ajili ya madhabahu ya Bwana mahali pale ambapo Bwana angepachagua. Hivyo ndivyo walivyo hadi hivi leo.
And he decreed on that day, that they would be in the ministry of all the people and of the altar of the Lord, cutting wood and carrying water, even until this present time, in the place which the Lord had chosen.