< Yoshua 8 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Usiogope, wala usivunjike moyo. Chukua jeshi lote la vita uende pamoja nalo kuishambulia Ai. Kwa kuwa nimeshamweka mikononi mwako mfalme wa Ai, pamoja na watu wake, mji wake na nchi yake.
Na LEUM GOD El fahk nu sel Joshua, “Nimet kom sangeng ku sensen. Fahla ac us mwet mweun lom nukewa utyak nu Ai. Nga fah oru tuh kom fah kutangla tokosra lun Ai ac nga fah usot facl sac ac ma nukewa we tuh in ma lowos.
2 Utafanya Ai na mfalme wake kama ulivyofanya kwa mji wa Yeriko na mfalme wake, isipokuwa mnaweza kuchukua mateka wake na mifugo wake, kwa ajili yenu. Weka waviziaji upande wa nyuma ya mji.”
Ma nukewa kom tuh oru in acn Jericho ac nu sin tokosra we kom in oru oapana in acn Ai ac nu sin tokosra we. Tusruktu, ma lalos nukewa wi kosro natulos kowos ku in eis lowos. Akola kowos in mweunelos in lukma, tukun siti ah yak.”
3 Basi Yoshua na jeshi lote wakainuka kushambulia Ai. Akachagua watu mashujaa elfu thelathini walio bora miongoni mwa wapiganaji wake, akawapeleka wakati wa usiku
Ouinge Joshua ac mwet mweun lal elos akola in mweuni mwet Ai. El sulela tausin tolngoul mwet pisrla ke mweun ac supwalosla ke fong,
4 akiwaagiza: “Sikilizeni kwa makini. Mtavizia nyuma ya mji. Msiende mbali sana na mji. Wote kuweni macho.
ac fahk nu selos, “Kowos som ac wikwik akngusrikya tukun siti ah, ac tupan pacl in mweun. Nimet som loesla liki siti ah.
5 Mimi na watu walio pamoja nami, tutaukabili mji, kisha itakuwa hapo watu watakapotoka nje kupigana nasi, kama walivyofanya hapo kwanza, sisi tutawakimbia.
Nga ac mwet mweun lula uh ac fah kalukyang nu ke mutunpot in siti uh. Ke pacl se ma mwet Ai elos ac ilme in lain kut oana elos oru meet ah, na kut fah forla ac kaingkunulos.
6 Watatufuatilia mpaka tutakapokuwa tumewavuta mbali na mji kwa kuwa watasema, ‘Wanatukimbia, kama walivyofanya hapo awali.’ Hivyo tutakapowakimbia,
Elos fah ukwe kut nwe ke na kut pwanulosla loes liki siti sac. Elos ac nunku mu kut kaingkunulos oana kut tuh kaingkunulos meet ah.
7 ninyi inawapasa mwinuke mtoke huko mafichoni na kuuteka mji. Bwana Mungu wenu atautia mkononi mwenu.
Na kowos fah tuyak liki acn kowos wikwik we, ac utyak ac sruokya siti sac. LEUM GOD lowos el ac fah sot nu inpouwos.
8 Mtakapokuwa mmeuteka mji, uteketezeni kwa moto. Fanyeni kama vile Bwana alivyoamuru. Angalieni, nimewaagiza.”
Tukun kowos sruokya siti sac, kowos esukak, oana ke LEUM GOD El sapkin. Pa ingan sap ku kowos in fahsr kac.”
9 Ndipo Yoshua akawatuma watu, nao wakaenda mahali pa kujificha, wakawa wanavizia kati ya Betheli na Ai, kuelekea upande wa magharibi wa Ai, lakini Yoshua akalala miongoni mwa watu usiku huo.
Ouinge Joshua el supwalosla, ac elos som nu yen elos ac wikwik we inmasrlon acn Bethel ac Ai, layen roto in Ai. Ac Joshua el mutana in lohm sin mwet mweun in fong sac.
10 Asubuhi na mapema siku iliyofuatia, Yoshua akawakutanisha watu wake, na yeye na viongozi wa Israeli wakawa mbele ya watu kwenda Ai.
Toang na ke lotu tok ah, Joshua el tukakek ac pangon mwet mweun ah nu sie. Na el ac mwet kol lun mwet Israel kololosla nu Ai.
11 Watu wote wa vita waliokuwa pamoja naye walipanda, wakakaribia na kufika mbele ya mji. Wakapiga kambi kaskazini mwa Ai, pakiwa na bonde kati yao na huo mji.
Na mwet mweun ma welul ah elos kalukyang apkuran nu ke mutunpot lun siti sac ac tulokunak lohm nuknuk selos layen nu eir in Ai, ac oasr sie infahlfal inmasrlolos ac Ai.
12 Yoshua alikuwa amewachukua watu wapatao elfu tano, akawaweka katika uavizi kati ya Betheli na Ai, upande wa magharibi wa mji.
El eis apkuran in mwet tausin limekosr ac sap elos in wikla inmasrlon Bethel ac Ai, layen roto in Ai.
13 Wakawaweka askari katika maeneo yao: wale wote waliokuwa kambini wakawa kaskazini ya mji na wale waliokuwa wakivizia wakawa upande wa magharibi. Usiku huo Yoshua akaenda katika lile bonde.
Na mwet mweun elos akola nu ke mweun. Pusiyen mwet uh elos muta eir, ac mwet lula ah elos muta roto. Ac Joshua el mongla in fong sac infahlfal sac.
14 Mfalme wa Ai alipoona jambo hili, yeye pamoja na watu wote wa mji wakatoka kwa haraka asubuhi na mapema, ili kukutana na Israeli katika vita mahali fulani panapotazamana na Araba. Lakini hakujua kwamba kulikuwa kumewekwa waviziaji dhidi yake nyuma ya mji.
Ke tokosra Ai el liye mwet mweun lal Joshua, el sa in mukuila. El ac mwet lal nukewa fahla suiya Infahlfal Jordan in mweuni mwet Israel, acn se na ma elos tuh mweun we meet ah. Ac el tia etu lah oasr pac mwet mweun akola in tuku tokolos ac lainulos.
15 Yoshua na Israeli wote wakaruhusu kurudishwa nyuma mbele yao, na kuelekea jangwani.
Joshua ac mwet mweun lal elos oru acnu mu elos kaingkunulos ac elos kaing nu yen mwesis.
16 Watu wote wa Ai wakaitwa ili kuwafuatia, nao wakavutwa kumfuatia Yoshua mbali na mji.
Suliyuk mwet nukewa in siti sac in tuku ac ukwe mwet lal Joshua, ac ke elos ukwal Joshua, elos loeselik liki siti sac.
17 Hakuna hata mwanaume mmoja aliyebakia Ai wala Betheli ambaye hakufuatia Israeli. Wakauacha mji wazi na kuwafuatia Israeli.
Mwet Ai nukewa elos som ukwe mwet Israel, ac mutunpot in siti sac ikakelik na ac wangin mwet lula in karingin.
18 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Inua huo mkuki ulio mkononi mwako kuuelekeza Ai, kwa kuwa nitautia huo mji mkononi mwako.” Hivyo Yoshua akauelekeza mkuki wake Ai.
Na LEUM GOD El fahk nu sel Joshua, “Kolla osra soko inpoum an nu Ai, tuh nga ac sot siti sac nu sum.” Na Joshua el oru oana ke fwack nu sel.
19 Mara tu alipofanya hivi, wale watu waliokuwa mavizioni wakaondoka upesi kutoka mahali pao na kukimbilia mbele. Wakaingia ndani ya mji, wakauteka na kuutia moto kwa haraka.
Ke pacl se na ma el kolla osra soko ah, na mwet ma wikwik likin siti ah elos sulaklak na tuyak ac kasrusr nu ke siti sac. Elos utyak sruokya siti sac ac esukak.
20 Watu wa Ai wakaangalia nyuma, wakauona moshi wa huo mji ukielekea angani lakini hawakuwa na nafasi ya kutoroka kwa upande wowote, kwa kuwa wale Waisraeli waliokuwa wanawakimbia kuelekea jangwani walikuwa wamegeuka nyuma kuwakabili wakimbizaji wao.
Ke mwet Ai elos tapulla elos liye lah fosryak siti ah. Tusruktu, wangin acn elos ku in kaingla nu we mweyen mwet Israel su kaing nu yen mwesis ah elos forla ac lainulos.
21 Basi Yoshua na Israeli wote walipoona kwamba waviziaji wameshauteka mji na moshi ulikuwa unapaa juu kutoka kwenye mji, wakawageukia watu wa Ai na kuwashambulia.
Ke Joshua ac mwet lal ah liye lah mwet wialos ah eisla ac esukak siti sac, elos forla ac mutawauk in uni mwet Ai ah.
22 Wale waviziaji nao pia wakatoka nje ya mji dhidi yao, hivi kwamba wakashikiwa katikati, Waisraeli wakiwa pande zote mbili. Israeli wakawaua, bila kuwaachia yeyote aliyenusurika wala aliyetoroka.
Na mwet Israel ma esukak siti sac elos tufoki ac wi mweuni mwet Ai. Elos raunelosla ac onelosla ac wangin sie selos moulla ku kaingla,
23 Lakini wakamchukua mfalme wa Ai akiwa hai na kumleta kwa Yoshua.
sayen tokosra Ai. Sruhu el ac utukla nu yorol Joshua.
24 Israeli ilipomaliza kuwaua wanaume wote wa Ai katika mashamba na jangwani walipokuwa wamewafukuzia, na baada ya kila mmoja wao kuuawa kwa upanga, Waisraeli wote wakarudi Ai na kuwaua wale waliokuwa wamebakia mjini.
Ke mwet Israel elos onela kewa mwet Ai ah yen mwesis ma elos ukwalosla nu we ah, na elos folokla nu in siti lun mwet Ai ac onela mwet nukewa ma lula we.
25 Watu kumi na mbili elfu, waume kwa wake, waliangamia siku ile, yaani watu wote wa Ai.
Pisen mwet Ai, mukul ac mutan, pa singoul luo tausin, ac elos nukewa anwuki in len sac.
26 Kwa maana Yoshua hakuurudisha ule mkono wake uliokuwa umeuinua mkuki hadi alipomaliza kuwaangamiza wote walioishi Ai.
Joshua el kolla na osra soko inpaol ah nwe ke na mwet nukewa in Ai anwukla.
27 Lakini Israeli wakajichukulia mifugo na nyara za mji huu, kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Yoshua.
Mwet Israel elos eis kosro ac ma nukewa lun mwet Ai tuh in ma lalos, in oana ke LEUM GOD El tuh fahk nu sel Joshua.
28 Kwa hiyo Yoshua akauchoma moto mji wa Ai na kuufanya kuwa lundo la magofu la kudumu, mahali pa ukiwa hadi leo.
Ouinge Joshua el esukak acn Ai ac wanginla ma fac nwe misenge.
29 Akamwangika mfalme wa Ai kwenye mti na kumwacha hapo mpaka jioni. Wakati wa jua kutua, Yoshua akawaamuru wautoe mwili wake kwenye mti na kuutupa kwenye ingilio la lango la mji. Kisha wakalundika mawe makubwa mengi juu yake, ambayo yamesalia mpaka leo.
Joshua el unilya tokosra lun acn Ai ac srupsrulak ke sak soko, na el sripsrip we nwe ke na ekela. Ke faht ah tili, Joshua el sap elos eisya manol ac sisya mutunpot in siti uh. Ac elos elosak yol in eot se nu facl, su oanna nwe misenge.
30 Kisha Yoshua akajenga madhabahu ya Bwana, Mungu wa Israeli, katika Mlima wa Ebali,
Na Joshua el etoak sie loang Fineol Ebal nu sin LEUM GOD lun Israel.
31 kama Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa amewaamuru Waisraeli. Akaijenga sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose: madhabahu ya mawe yasiyochongwa, ambayo juu yake hakuna chombo cha chuma kilichotumika. Hapo juu yake wakamtolea Bwana sadaka za kuteketezwa na kutoa sadaka za amani.
El orala oana Moses, mwet kulansap lun LEUM GOD, el tuh sapkin nu sin mwet Israel. El oru fal nu ke lumah ma aketeyuki in book in Ma Sap lal Moses — “sie loang orekla ke eot ma tia akfwelyeyuk ke kutena osra.” Elos orekmakin loang se inge nu ke mwe kisa firir ac mwe kisa in akinsewowo lalos nu sin LEUM GOD.
32 Pale, mbele ya Waisraeli Yoshua akanakili juu ya hayo mawe sheria ya Mose, aliyokuwa ameiandika.
Joshua el simusla ma sap fin eot ah ye mutun mwet nukewa, in oana ke Moses el tuh simusla meet ah.
33 Israeli yote, wageni na wazawa sawasawa, wakiwa na wazee wao, maafisa na waamuzi, walikuwa wamesimama pande zote mbili za Sanduku la Agano la Bwana, wakiwaelekea wale waliokuwa wamelichukua, yaani makuhani, ambao ni Walawi. Nusu ya watu ilisimama mbele ya Mlima Gerizimu na nusu hiyo ingine ikasimama mbele ya Mlima Ebali, kama vile Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa ameamuru hapo mwanzo alipotoa maagizo ya kuwabariki watu wa Israeli.
Mwet kol, mwet matu, mwet nununku, ac mwet Israel nukewa, wi mwetsac su muta inmasrlolos, elos takla tu sisken Tuptup in Wuleang lun LEUM GOD. Tafu selos tu pe Fineol Gerizim ac tafu selos tu pe Fineol Ebal, ac ngetani nu yurin mwet tol Levi su us Tuptup sac inmasrlolos, oana ke Moses, mwet kulansap lun LEUM GOD, el tuh sap elos in oru ke pacl in eis mwe insewowo.
34 Hatimaye, Yoshua akasoma maneno yote ya sheria, yaani baraka na laana, kama vile ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria.
Tukun ma inge Joshua el riteak nukewa kas in Ma Sap ah, kas in akinsewowo ac kas in selnga, oana ke simla in book in Ma Sap.
35 Hakuna neno lolote katika yale yote ambayo Mose alikuwa ameamuru ambalo Yoshua hakulisomea kusanyiko lote la Israeli, ikiwa ni pamoja na wanawake na watoto, na wageni walioishi miongoni mwao.
Ma sap nukewa lal Moses Joshua el riteak nu sin mwet nukewa su tukeni ah, weang pacna mutan ac tulik ac mwetsac su muta inmasrlolos.

< Yoshua 8 >