< Yoshua 8 >
1 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Usiogope, wala usivunjike moyo. Chukua jeshi lote la vita uende pamoja nalo kuishambulia Ai. Kwa kuwa nimeshamweka mikononi mwako mfalme wa Ai, pamoja na watu wake, mji wake na nchi yake.
Kemudian TUHAN berkata kepada Yosua, “Jangan takut dan jangan berkecil hati. Bawalah semua laki-laki yang bisa berperang dan seranglah kota Ai. Ketahuilah, Aku sudah menyerahkan raja Ai, seluruh rakyatnya, kotanya, dan negerinya kepadamu.
2 Utafanya Ai na mfalme wake kama ulivyofanya kwa mji wa Yeriko na mfalme wake, isipokuwa mnaweza kuchukua mateka wake na mifugo wake, kwa ajili yenu. Weka waviziaji upande wa nyuma ya mji.”
Musnahkanlah kota Ai dan rajanya sama seperti kalian memusnahkan kota Yeriko dan rajanya. Tetapi kali ini kalian boleh mengambil barang-barang jarahan dan ternak menjadi milikmu. Suruhlah sebagian pasukan untuk bersembunyi di belakang kota itu untuk bersiap-siap menyergap.”
3 Basi Yoshua na jeshi lote wakainuka kushambulia Ai. Akachagua watu mashujaa elfu thelathini walio bora miongoni mwa wapiganaji wake, akawapeleka wakati wa usiku
Maka Yosua dan seluruh pasukannya bersiap-siap mendaki ke kota Ai. Yosua memilih tiga puluh ribu orang pejuang terbaik dan mengutus mereka pergi pada malam hari.
4 akiwaagiza: “Sikilizeni kwa makini. Mtavizia nyuma ya mji. Msiende mbali sana na mji. Wote kuweni macho.
Dia memerintahkan mereka, “Perhatikan! Bersembunyilah dan bersiaplah untuk menyerbu kota itu dari belakang. Jangan terlalu jauh dari kota itu. Kalian semua harus tetap siaga.
5 Mimi na watu walio pamoja nami, tutaukabili mji, kisha itakuwa hapo watu watakapotoka nje kupigana nasi, kama walivyofanya hapo kwanza, sisi tutawakimbia.
Saya dan seluruh pasukan yang bersama saya akan maju menyerang kota itu. Waktu mereka keluar melawan kami seperti sebelumnya, kami akan berbalik dan lari dari mereka.
6 Watatufuatilia mpaka tutakapokuwa tumewavuta mbali na mji kwa kuwa watasema, ‘Wanatukimbia, kama walivyofanya hapo awali.’ Hivyo tutakapowakimbia,
Kami akan memancing mereka untuk mengejar kami sampai jauh dari kota, supaya mereka mengira bahwa kami melarikan diri seperti sebelumnya. Sementara kami lari,
7 ninyi inawapasa mwinuke mtoke huko mafichoni na kuuteka mji. Bwana Mungu wenu atautia mkononi mwenu.
kalian harus keluar dari persembunyian dan menyerbu kota itu, karena TUHAN Allahmu akan menyerahkannya kepada kalian.
8 Mtakapokuwa mmeuteka mji, uteketezeni kwa moto. Fanyeni kama vile Bwana alivyoamuru. Angalieni, nimewaagiza.”
Sesudah menguasai kota itu, kalian harus membakarnya sesuai dengan perkataan TUHAN. Ingatlah perintahku ini.”
9 Ndipo Yoshua akawatuma watu, nao wakaenda mahali pa kujificha, wakawa wanavizia kati ya Betheli na Ai, kuelekea upande wa magharibi wa Ai, lakini Yoshua akalala miongoni mwa watu usiku huo.
Maka mereka pergi ke tempat persembunyian di antara kota Betel dan kota Ai, di sebelah barat kota Ai. Mereka menunggu di sana, sementara Yosua bermalam di perkemahan Israel malam itu.
10 Asubuhi na mapema siku iliyofuatia, Yoshua akawakutanisha watu wake, na yeye na viongozi wa Israeli wakawa mbele ya watu kwenda Ai.
Besoknya, Yosua bangun pagi-pagi sekali dan menyiapkan pasukannya. Dia bersama para tua-tua Israel memimpin pasukan itu mendaki ke kota Ai.
11 Watu wote wa vita waliokuwa pamoja naye walipanda, wakakaribia na kufika mbele ya mji. Wakapiga kambi kaskazini mwa Ai, pakiwa na bonde kati yao na huo mji.
Semua pasukan bersamanya mendaki menuju kota itu dan berkemah di sebelah utara kota Ai. Ada sebuah lembah yang memisahkan mereka dengan kota itu.
12 Yoshua alikuwa amewachukua watu wapatao elfu tano, akawaweka katika uavizi kati ya Betheli na Ai, upande wa magharibi wa mji.
Lalu Yosua memilih sekitar lima ribu orang dan menyuruh mereka bersembunyi di antara kota Betel dan Ai, di sebelah barat kota itu.
13 Wakawaweka askari katika maeneo yao: wale wote waliokuwa kambini wakawa kaskazini ya mji na wale waliokuwa wakivizia wakawa upande wa magharibi. Usiku huo Yoshua akaenda katika lile bonde.
Jadi, sebagian pasukan ditempatkan di markas utama di sebelah utara kota, sedangkan sebagian lain bersembunyi di sebelah barat kota itu. Yosua turun ke lembah dan bermalam di sana.
14 Mfalme wa Ai alipoona jambo hili, yeye pamoja na watu wote wa mji wakatoka kwa haraka asubuhi na mapema, ili kukutana na Israeli katika vita mahali fulani panapotazamana na Araba. Lakini hakujua kwamba kulikuwa kumewekwa waviziaji dhidi yake nyuma ya mji.
Begitu raja Ai melihat pasukan Israel di seberang lembah, dia mengumpulkan orang-orang kota itu dan mereka segera keluar pagi-pagi benar ke arah lembah Yordan untuk berperang melawan Israel. Dia tidak tahu bahwa sebagian pasukan Israel sedang bersembunyi di belakang kota untuk menyerbu.
15 Yoshua na Israeli wote wakaruhusu kurudishwa nyuma mbele yao, na kuelekea jangwani.
Yosua dan pasukan yang bersamanya berpura-pura kalah. Mereka melarikan diri ke arah daerah belantara.
16 Watu wote wa Ai wakaitwa ili kuwafuatia, nao wakavutwa kumfuatia Yoshua mbali na mji.
Semua laki-laki di kota itu dikerahkan untuk mengejar Yosua dan pasukannya. Karena mengejar Yosua, mereka pun terpancing keluar dari kota.
17 Hakuna hata mwanaume mmoja aliyebakia Ai wala Betheli ambaye hakufuatia Israeli. Wakauacha mji wazi na kuwafuatia Israeli.
Tidak ada seorang lelaki pun yang tertinggal di kota Ai maupun Betel. Mereka semua mengejar orang Israel sehingga kota mereka dibiarkan terbuka begitu saja.
18 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Inua huo mkuki ulio mkononi mwako kuuelekeza Ai, kwa kuwa nitautia huo mji mkononi mwako.” Hivyo Yoshua akauelekeza mkuki wake Ai.
Lalu TUHAN berkata kepada Yosua, “Acungkanlah tombakmu ke arah kota Ai, karena Aku akan menyerahkan kota itu kepadamu.” Dan Yosua mengacungkan tombak di tangannya ke arah kota itu.
19 Mara tu alipofanya hivi, wale watu waliokuwa mavizioni wakaondoka upesi kutoka mahali pao na kukimbilia mbele. Wakaingia ndani ya mji, wakauteka na kuutia moto kwa haraka.
Begitu Yosua mengacungkan tombaknya, pasukan yang bersembunyi langsung keluar dan lari menyerang kota Ai. Mereka merebut kota itu dan segera membakarnya.
20 Watu wa Ai wakaangalia nyuma, wakauona moshi wa huo mji ukielekea angani lakini hawakuwa na nafasi ya kutoroka kwa upande wowote, kwa kuwa wale Waisraeli waliokuwa wanawakimbia kuelekea jangwani walikuwa wamegeuka nyuma kuwakabili wakimbizaji wao.
Setelah Yosua dan seluruh Israel yang berada di daerah belantara melihat bahwa pasukan mereka yang lain sudah berhasil merebut kota dan asap mengepul dari kota itu ke langit, mereka pun berbalik menyerang pasukan Ai. Ketika orang Ai menoleh ke belakang dan melihat asap dari kota, mereka tidak bisa lari ke mana-mana.
21 Basi Yoshua na Israeli wote walipoona kwamba waviziaji wameshauteka mji na moshi ulikuwa unapaa juu kutoka kwenye mji, wakawageukia watu wa Ai na kuwashambulia.
22 Wale waviziaji nao pia wakatoka nje ya mji dhidi yao, hivi kwamba wakashikiwa katikati, Waisraeli wakiwa pande zote mbili. Israeli wakawaua, bila kuwaachia yeyote aliyenusurika wala aliyetoroka.
Sementara itu, pasukan Israel di kota Ai keluar menyerang mereka dari belakang sehingga orang Ai terperangkap di antara pasukan-pasukan Israel. Pasukan Israel menghabisi mereka. Tidak ada satu pun yang selamat atau berhasil melarikan diri
23 Lakini wakamchukua mfalme wa Ai akiwa hai na kumleta kwa Yoshua.
kecuali raja Ai. Mereka menangkap dia hidup-hidup lalu membawanya kepada Yosua.
24 Israeli ilipomaliza kuwaua wanaume wote wa Ai katika mashamba na jangwani walipokuwa wamewafukuzia, na baada ya kila mmoja wao kuuawa kwa upanga, Waisraeli wote wakarudi Ai na kuwaua wale waliokuwa wamebakia mjini.
Setelah pasukan Israel menghabisi semua orang Ai di ladang-ladang dan daerah belantara, mereka semua kembali ke Ai dan membunuh sisa penduduknya.
25 Watu kumi na mbili elfu, waume kwa wake, waliangamia siku ile, yaani watu wote wa Ai.
Pada hari itu seluruh penduduk kota Ai mati, baik laki-laki maupun perempuan. Semuanya dua belas ribu orang.
26 Kwa maana Yoshua hakuurudisha ule mkono wake uliokuwa umeuinua mkuki hadi alipomaliza kuwaangamiza wote walioishi Ai.
Yosua terus mengacungkan tombaknya dan tidak menurunkan tangan sampai seluruh penduduk Ai dibunuh.
27 Lakini Israeli wakajichukulia mifugo na nyara za mji huu, kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Yoshua.
Hanya hewan ternak dan barang-barang jarahan yang diambil orang Israel, sesuai dengan perintah TUHAN kepada Yosua.
28 Kwa hiyo Yoshua akauchoma moto mji wa Ai na kuufanya kuwa lundo la magofu la kudumu, mahali pa ukiwa hadi leo.
Yosua membakar habis kota Ai sehingga tempat itu menjadi timbunan reruntuhan selamanya, telantar sampai saat kitab ini ditulis.
29 Akamwangika mfalme wa Ai kwenye mti na kumwacha hapo mpaka jioni. Wakati wa jua kutua, Yoshua akawaamuru wautoe mwili wake kwenye mti na kuutupa kwenye ingilio la lango la mji. Kisha wakalundika mawe makubwa mengi juu yake, ambayo yamesalia mpaka leo.
Lalu Yosua menggantung raja Ai di atas tiang dan membiarkannya sampai sore. Ketika matahari terbenam, mayatnya diturunkan dan dibuang di gerbang pintu masuk kota, atas perintah Yosua. Lalu mayat itu ditimbun dengan banyak batu, dan tumpukan batu itu masih ada sampai saat kitab ini ditulis.
30 Kisha Yoshua akajenga madhabahu ya Bwana, Mungu wa Israeli, katika Mlima wa Ebali,
Pada waktu itu, Yosua mendirikan mezbah kurban bagi TUHAN, Allah Israel, di gunung Ebal.
31 kama Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa amewaamuru Waisraeli. Akaijenga sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose: madhabahu ya mawe yasiyochongwa, ambayo juu yake hakuna chombo cha chuma kilichotumika. Hapo juu yake wakamtolea Bwana sadaka za kuteketezwa na kutoa sadaka za amani.
Hal ini sesuai dengan perintah Musa kepada umat Israel, yang tertulis di dalam kitab Taurat, “Sebuah mezbah kurban yang dibuat dari batu-batu yang belum pernah dipahat dan belum tersentuh alat-alat besi.” Di mezbah itu mereka mempersembahkan kurban yang dibakar habis dan kurban tanda damai kepada TUHAN.
32 Pale, mbele ya Waisraeli Yoshua akanakili juu ya hayo mawe sheria ya Mose, aliyokuwa ameiandika.
Di sana, di hadapan orang-orang Israel, Yosua menyalin hukum yang disampaikan oleh Musa ke atas lempengan batu.
33 Israeli yote, wageni na wazawa sawasawa, wakiwa na wazee wao, maafisa na waamuzi, walikuwa wamesimama pande zote mbili za Sanduku la Agano la Bwana, wakiwaelekea wale waliokuwa wamelichukua, yaani makuhani, ambao ni Walawi. Nusu ya watu ilisimama mbele ya Mlima Gerizimu na nusu hiyo ingine ikasimama mbele ya Mlima Ebali, kama vile Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa ameamuru hapo mwanzo alipotoa maagizo ya kuwabariki watu wa Israeli.
Seluruh bangsa Israel, baik pendatang maupun orang Israel asli, bersama para tua-tua, para pemimpin, dan hakim-hakim mereka, dibagi menjadi dua kelompok. Setengah dari bangsa Israel berdiri di lereng gunung Gerizim, dan setengah yang lain berdiri di lereng gunung Ebal. Kedua kelompok ini saling berhadapan. Di antara mereka berdiri imam-imam Lewi yang memikul peti perjanjian TUHAN. Semua itu dilakukan sesuai dengan perintah yang Musa berikan tentang memberkati bangsa Israel.
34 Hatimaye, Yoshua akasoma maneno yote ya sheria, yaani baraka na laana, kama vile ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria.
Sesudah itu, Yosua membacakan semua hukum yang ditulis Musa di dalam kitab Taurat, termasuk janji TUHAN untuk memberkati umat-Nya apabila mereka taat, dan kutukan apabila mereka tidak taat.
35 Hakuna neno lolote katika yale yote ambayo Mose alikuwa ameamuru ambalo Yoshua hakulisomea kusanyiko lote la Israeli, ikiwa ni pamoja na wanawake na watoto, na wageni walioishi miongoni mwao.
Yosua membacakan seluruh isi kitab itu kepada seluruh umat Israel, termasuk semua perempuan, anak-anak, serta para pendatang yang tinggal di antara mereka.