< Yoshua 8 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Usiogope, wala usivunjike moyo. Chukua jeshi lote la vita uende pamoja nalo kuishambulia Ai. Kwa kuwa nimeshamweka mikononi mwako mfalme wa Ai, pamoja na watu wake, mji wake na nchi yake.
Forsothe the Lord seide to Josue, Nether drede thou `withoutforth, `nether drede thou withynne; take with thee al the multitude of fiyteris, and rise thou, and stie in to the citee of Hay; lo, Y haue bitake in thin hond the king therof, and the puple, and the citee, and the lond.
2 Utafanya Ai na mfalme wake kama ulivyofanya kwa mji wa Yeriko na mfalme wake, isipokuwa mnaweza kuchukua mateka wake na mifugo wake, kwa ajili yenu. Weka waviziaji upande wa nyuma ya mji.”
And thou schalt do to the citee of Hay, and to the king therof, as thou didist to Gerico, and to the king therof; sotheli ye schulen take to you the prey, and alle lyuynge beestis; sette thou `aspies, ethir buyschementis, to the citee bihynde it.
3 Basi Yoshua na jeshi lote wakainuka kushambulia Ai. Akachagua watu mashujaa elfu thelathini walio bora miongoni mwa wapiganaji wake, akawapeleka wakati wa usiku
And Josue roos, and al the oost of fiyteris with hym, to stie in to Hay; and bi nyyte he sente thretti chosen thousynde of stronge men;
4 akiwaagiza: “Sikilizeni kwa makini. Mtavizia nyuma ya mji. Msiende mbali sana na mji. Wote kuweni macho.
and comaundide to hem, and seide, Sette ye buyschementis bihynde the citee, and go ye not ferthere; and alle ye schulen be redi;
5 Mimi na watu walio pamoja nami, tutaukabili mji, kisha itakuwa hapo watu watakapotoka nje kupigana nasi, kama walivyofanya hapo kwanza, sisi tutawakimbia.
forsothe Y, and the tothir multitude which is with me, schulen come on the contrarie side ayens the citee; and whanne thei schulen go out ayens vs, as we diden bifore, we schulen fle, and turne the backis,
6 Watatufuatilia mpaka tutakapokuwa tumewavuta mbali na mji kwa kuwa watasema, ‘Wanatukimbia, kama walivyofanya hapo awali.’ Hivyo tutakapowakimbia,
til thei pursuen, and ben drawun away ferthir fro the citee; for thei schulen gesse, that we schulen fle as bifore.
7 ninyi inawapasa mwinuke mtoke huko mafichoni na kuuteka mji. Bwana Mungu wenu atautia mkononi mwenu.
Therfor while we schulen fle, and thei pursue, ye schulen ryse fro the buyschementis, and schulen waste the citee; and youre Lord God schal bitake it in to youre hondis.
8 Mtakapokuwa mmeuteka mji, uteketezeni kwa moto. Fanyeni kama vile Bwana alivyoamuru. Angalieni, nimewaagiza.”
And whanne ye han take it, `brenne ye it; `so ye schulen do alle thingis, as Y comaundide.
9 Ndipo Yoshua akawatuma watu, nao wakaenda mahali pa kujificha, wakawa wanavizia kati ya Betheli na Ai, kuelekea upande wa magharibi wa Ai, lakini Yoshua akalala miongoni mwa watu usiku huo.
And Josue lefte hem, and thei yeden to the place of buyschementis, and saten bitwixe Bethel and Hay, at the west coost of the citee of Hay. Forsothe Josue dwellide `in that nyyt in the myddis of the puple.
10 Asubuhi na mapema siku iliyofuatia, Yoshua akawakutanisha watu wake, na yeye na viongozi wa Israeli wakawa mbele ya watu kwenda Ai.
And he roos eerli, and noumbride felowis, and stiede with the eldere in the frount of the oost, and was cumpassid with the helpe of fiyteris.
11 Watu wote wa vita waliokuwa pamoja naye walipanda, wakakaribia na kufika mbele ya mji. Wakapiga kambi kaskazini mwa Ai, pakiwa na bonde kati yao na huo mji.
And whanne thei hadden come, and hadden stied ayens the citee, thei stoden at the north coost of the citee, bitwixe which citee and hem the valei was in the myddis.
12 Yoshua alikuwa amewachukua watu wapatao elfu tano, akawaweka katika uavizi kati ya Betheli na Ai, upande wa magharibi wa mji.
`Sotheli he hadde chose fyue thousynde men, and hadde sette in buyschementis bitwixe Bethauen and Hay, in the west part of the same citee.
13 Wakawaweka askari katika maeneo yao: wale wote waliokuwa kambini wakawa kaskazini ya mji na wale waliokuwa wakivizia wakawa upande wa magharibi. Usiku huo Yoshua akaenda katika lile bonde.
Sotheli al the tothir oost dresside scheltroun to the north, so that the laste men of the multitude touchiden the west coost of the citee. Therfor Josue yede in that nyyt, and stood in the myddis of the valei;
14 Mfalme wa Ai alipoona jambo hili, yeye pamoja na watu wote wa mji wakatoka kwa haraka asubuhi na mapema, ili kukutana na Israeli katika vita mahali fulani panapotazamana na Araba. Lakini hakujua kwamba kulikuwa kumewekwa waviziaji dhidi yake nyuma ya mji.
and whanne the kyng of Hai had seyn that, he hastide eerli, and yede out with al the oost of the citee, and he dresside scheltrun ayens the deseert; and wiste not that buyschementis weren hid bihinde the bak.
15 Yoshua na Israeli wote wakaruhusu kurudishwa nyuma mbele yao, na kuelekea jangwani.
Forsothe Josue and al the multitude `of Israel yauen place, feynynge drede, and fleynge bi the weie of wildirnesse; and thei crieden togidere,
16 Watu wote wa Ai wakaitwa ili kuwafuatia, nao wakavutwa kumfuatia Yoshua mbali na mji.
and excitiden hem silf togidere, and pursueden hem. And whanne thei hadden go awey fro the citee,
17 Hakuna hata mwanaume mmoja aliyebakia Ai wala Betheli ambaye hakufuatia Israeli. Wakauacha mji wazi na kuwafuatia Israeli.
and sothely not oon hadde left in the citee of Hai and Bethauen, that `pursuede not Israel, and thei leften the citees opyn, as thei hadden broke out,
18 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Inua huo mkuki ulio mkononi mwako kuuelekeza Ai, kwa kuwa nitautia huo mji mkononi mwako.” Hivyo Yoshua akauelekeza mkuki wake Ai.
the Lord seide to Josue, `Reise thou the scheeld which is in thin hond, ayens the citee of Hay; for Y schal yyue it to thee.
19 Mara tu alipofanya hivi, wale watu waliokuwa mavizioni wakaondoka upesi kutoka mahali pao na kukimbilia mbele. Wakaingia ndani ya mji, wakauteka na kuutia moto kwa haraka.
And whanne he hadde reisid the scheld ayens the citee, buyschementis, that weren hid, riseden anoon; and thei yeden to the citee, and token, and brenten it.
20 Watu wa Ai wakaangalia nyuma, wakauona moshi wa huo mji ukielekea angani lakini hawakuwa na nafasi ya kutoroka kwa upande wowote, kwa kuwa wale Waisraeli waliokuwa wanawakimbia kuelekea jangwani walikuwa wamegeuka nyuma kuwakabili wakimbizaji wao.
Forsothe the men of the citee, that pursueden Josue, bihelden, and siyen the smoke of the citee stie `til to heuene; and thei myyten no more fle hidur and thidur; most sithen thei that hadden feyned fliyt, and yeden to wildirnesse, withstoden stronglieste `ayens the pursueris.
21 Basi Yoshua na Israeli wote walipoona kwamba waviziaji wameshauteka mji na moshi ulikuwa unapaa juu kutoka kwenye mji, wakawageukia watu wa Ai na kuwashambulia.
And Josue siy, and al Israel, that the citee was takun, and the smoke of the citee stiede; and he turnede ayen, and smoot the men of Hay.
22 Wale waviziaji nao pia wakatoka nje ya mji dhidi yao, hivi kwamba wakashikiwa katikati, Waisraeli wakiwa pande zote mbili. Israeli wakawaua, bila kuwaachia yeyote aliyenusurika wala aliyetoroka.
Sotheli also thei that hadden take and brent the citee, yeden out of the cytee ayens her men, and bigunnen to smyte the myddil men of enemyes; and whanne aduersaries weren slayn `on euer ethir part, so that no man of so greet multitude was sauyd,
23 Lakini wakamchukua mfalme wa Ai akiwa hai na kumleta kwa Yoshua.
thei tokun also the kyng of Hay lyuynge, and brouyten to Josue.
24 Israeli ilipomaliza kuwaua wanaume wote wa Ai katika mashamba na jangwani walipokuwa wamewafukuzia, na baada ya kila mmoja wao kuuawa kwa upanga, Waisraeli wote wakarudi Ai na kuwaua wale waliokuwa wamebakia mjini.
Therfor, whanne alle men weren slayn, that pursueden Israel goynge to deseert, and felden bi swerd in the same place, the sones of Israel turneden ayen, and smytiden the citee.
25 Watu kumi na mbili elfu, waume kwa wake, waliangamia siku ile, yaani watu wote wa Ai.
Forsothe thei that `felden doun in the same dai, fro man `til to womman, weren twelue thousynde of men, alle men of the citee of Hay.
26 Kwa maana Yoshua hakuurudisha ule mkono wake uliokuwa umeuinua mkuki hadi alipomaliza kuwaangamiza wote walioishi Ai.
Sotheli Josue withdrow not the hond, which he hadde dressid an hiy holdynge `the scheld, til alle the dwelleris of Hay weren slayn.
27 Lakini Israeli wakajichukulia mifugo na nyara za mji huu, kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Yoshua.
Forsothe the sones of Israel departiden to hem silf the werk beestis, and the preye of the citee, as the Lord comaundide to Josue;
28 Kwa hiyo Yoshua akauchoma moto mji wa Ai na kuufanya kuwa lundo la magofu la kudumu, mahali pa ukiwa hadi leo.
which brente the citee, and made it an euerlastynge biriel.
29 Akamwangika mfalme wa Ai kwenye mti na kumwacha hapo mpaka jioni. Wakati wa jua kutua, Yoshua akawaamuru wautoe mwili wake kwenye mti na kuutupa kwenye ingilio la lango la mji. Kisha wakalundika mawe makubwa mengi juu yake, ambayo yamesalia mpaka leo.
And he hangide the king therof in a iebat, `til to the euentid and the goynge doun of the sunne. And Josue comaundide, and thei puttiden doun his deed bodi fro the cros; and thei `castiden forth him in thilke entryng of the citee, and gaderiden on hym a greet heep of stoonus, which heep dwellith `til in to present dai.
30 Kisha Yoshua akajenga madhabahu ya Bwana, Mungu wa Israeli, katika Mlima wa Ebali,
Thanne Josue bildide an auter to the Lord God of Israel in the hil of Hebal,
31 kama Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa amewaamuru Waisraeli. Akaijenga sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose: madhabahu ya mawe yasiyochongwa, ambayo juu yake hakuna chombo cha chuma kilichotumika. Hapo juu yake wakamtolea Bwana sadaka za kuteketezwa na kutoa sadaka za amani.
as Moises, the `seruaunt of the Lord, comaundide to the sones of Israel, and it is writun in the book of Moises lawe, an auter of stoonys vnpolischid, whiche yrun touchide not. And he offride theron brent sacrifice to the Lord, and he offride pesible sacrifices;
32 Pale, mbele ya Waisraeli Yoshua akanakili juu ya hayo mawe sheria ya Mose, aliyokuwa ameiandika.
and he wroot on the stoonys the Deutronomye of Moises lawe, `which he hadde declarid bifor the sones of Israel.
33 Israeli yote, wageni na wazawa sawasawa, wakiwa na wazee wao, maafisa na waamuzi, walikuwa wamesimama pande zote mbili za Sanduku la Agano la Bwana, wakiwaelekea wale waliokuwa wamelichukua, yaani makuhani, ambao ni Walawi. Nusu ya watu ilisimama mbele ya Mlima Gerizimu na nusu hiyo ingine ikasimama mbele ya Mlima Ebali, kama vile Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa ameamuru hapo mwanzo alipotoa maagizo ya kuwabariki watu wa Israeli.
Sotheli al the puple, and the grettere men in birthe, and the duykis, and iugis stoden on `euer either side of the arke, in the siyt of preestis and dekenes, that baren the arke of boond of pees of the Lord; as a comeling, so and a man borun in the lond; the mydil part of hem stood bisidis the hil Garasym, and the myddil part stood bisidis the hil Hebal, as Moises, the `seruaunt of the Lord, comaundide. And first `sotheli he blesside the puple of Israel.
34 Hatimaye, Yoshua akasoma maneno yote ya sheria, yaani baraka na laana, kama vile ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria.
Aftir these thingis he redde alle the wordis of blessyng and of cursyng, and alle thingis that weren writun in the book of lawe.
35 Hakuna neno lolote katika yale yote ambayo Mose alikuwa ameamuru ambalo Yoshua hakulisomea kusanyiko lote la Israeli, ikiwa ni pamoja na wanawake na watoto, na wageni walioishi miongoni mwao.
He lefte no thing vntouchid of these thingis that Moises comaundide; but he declaride alle thingis bifor al the multitude of Israel, to wymmen, and litle children, and to comelyngis that dwelliden among hem.

< Yoshua 8 >