< Yoshua 8 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Usiogope, wala usivunjike moyo. Chukua jeshi lote la vita uende pamoja nalo kuishambulia Ai. Kwa kuwa nimeshamweka mikononi mwako mfalme wa Ai, pamoja na watu wake, mji wake na nchi yake.
and to say LORD to(wards) Joshua not to fear and not to to be dismayed to take: take with you [obj] all people: soldiers [the] battle and to arise: rise to ascend: rise [the] Ai to see: behold! to give: give in/on/with hand: power your [obj] king [the] Ai and [obj] people his and [obj] city his and [obj] land: country/planet his
2 Utafanya Ai na mfalme wake kama ulivyofanya kwa mji wa Yeriko na mfalme wake, isipokuwa mnaweza kuchukua mateka wake na mifugo wake, kwa ajili yenu. Weka waviziaji upande wa nyuma ya mji.”
and to make: do to/for Ai and to/for king her like/as as which to make: do to/for Jericho and to/for king her except spoil her and animal her to plunder to/for you to set: put to/for you to ambush to/for city from after her
3 Basi Yoshua na jeshi lote wakainuka kushambulia Ai. Akachagua watu mashujaa elfu thelathini walio bora miongoni mwa wapiganaji wake, akawapeleka wakati wa usiku
and to arise: rise Joshua and all people: soldiers [the] battle to/for to ascend: rise [the] Ai and to choose Joshua thirty thousand man mighty man [the] strength and to send: depart them night
4 akiwaagiza: “Sikilizeni kwa makini. Mtavizia nyuma ya mji. Msiende mbali sana na mji. Wote kuweni macho.
and to command [obj] them to/for to say to see: behold! you(m. p.) to ambush to/for city from after [the] city not to remove from [the] city much and to be all your to establish: prepare
5 Mimi na watu walio pamoja nami, tutaukabili mji, kisha itakuwa hapo watu watakapotoka nje kupigana nasi, kama walivyofanya hapo kwanza, sisi tutawakimbia.
and I and all [the] people which with me to present: come to(wards) [the] city and to be for to come out: come to/for to encounter: toward us like/as as which in/on/with first: previous and to flee to/for face: before their
6 Watatufuatilia mpaka tutakapokuwa tumewavuta mbali na mji kwa kuwa watasema, ‘Wanatukimbia, kama walivyofanya hapo awali.’ Hivyo tutakapowakimbia,
and to come out: come after us till to tear we [obj] them from [the] city for to say to flee to/for face: before our like/as as which in/on/with first: previous and to flee to/for face: before their
7 ninyi inawapasa mwinuke mtoke huko mafichoni na kuuteka mji. Bwana Mungu wenu atautia mkononi mwenu.
and you(m. p.) to arise: rise from [the] to ambush and to possess: take [obj] [the] city and to give: give her LORD God your in/on/with hand: power your
8 Mtakapokuwa mmeuteka mji, uteketezeni kwa moto. Fanyeni kama vile Bwana alivyoamuru. Angalieni, nimewaagiza.”
and to be like/as to capture you [obj] [the] city to kindle [obj] [the] city in/on/with fire like/as word LORD to make: do to see: behold! to command [obj] you
9 Ndipo Yoshua akawatuma watu, nao wakaenda mahali pa kujificha, wakawa wanavizia kati ya Betheli na Ai, kuelekea upande wa magharibi wa Ai, lakini Yoshua akalala miongoni mwa watu usiku huo.
and to send: depart them Joshua and to go: went to(wards) [the] ambush and to dwell between Bethel Bethel and between [the] Ai from sea: west to/for Ai and to lodge Joshua in/on/with night [the] he/she/it in/on/with midst [the] people
10 Asubuhi na mapema siku iliyofuatia, Yoshua akawakutanisha watu wake, na yeye na viongozi wa Israeli wakawa mbele ya watu kwenda Ai.
and to rise Joshua in/on/with morning and to reckon: list [obj] [the] people and to ascend: rise he/she/it and old: elder Israel to/for face: before [the] people [the] Ai
11 Watu wote wa vita waliokuwa pamoja naye walipanda, wakakaribia na kufika mbele ya mji. Wakapiga kambi kaskazini mwa Ai, pakiwa na bonde kati yao na huo mji.
and all [the] people: soldiers [the] battle which with him to ascend: rise and to approach: approach and to come (in): towards before [the] city and to camp from north to/for Ai and [the] valley (between him *Q(k)*) and between [the] Ai
12 Yoshua alikuwa amewachukua watu wapatao elfu tano, akawaweka katika uavizi kati ya Betheli na Ai, upande wa magharibi wa mji.
and to take: take like/as five thousand man and to set: make [obj] them to ambush between Bethel Bethel and between [the] Ai from sea: west to/for city
13 Wakawaweka askari katika maeneo yao: wale wote waliokuwa kambini wakawa kaskazini ya mji na wale waliokuwa wakivizia wakawa upande wa magharibi. Usiku huo Yoshua akaenda katika lile bonde.
and to set: put [the] people: soldiers [obj] all [the] camp which from north to/for city and [obj] heel his from sea: west to/for city and to go: continue Joshua in/on/with night [the] he/she/it in/on/with midst [the] valley
14 Mfalme wa Ai alipoona jambo hili, yeye pamoja na watu wote wa mji wakatoka kwa haraka asubuhi na mapema, ili kukutana na Israeli katika vita mahali fulani panapotazamana na Araba. Lakini hakujua kwamba kulikuwa kumewekwa waviziaji dhidi yake nyuma ya mji.
and to be like/as to see: see king [the] Ai and to hasten and to rise and to come out: come human [the] city to/for to encounter: toward Israel to/for battle he/she/it and all people his to/for meeting: time appointed to/for face: before [the] Arabah and he/she/it not to know for to ambush to/for him from after [the] city
15 Yoshua na Israeli wote wakaruhusu kurudishwa nyuma mbele yao, na kuelekea jangwani.
and to touch Joshua and all Israel to/for face: before their and to flee way: direction [the] wilderness
16 Watu wote wa Ai wakaitwa ili kuwafuatia, nao wakavutwa kumfuatia Yoshua mbali na mji.
and to cry out all [the] people which (in/on/with Ai *Q(K)*) to/for to pursue after them and to pursue after Joshua and to tear from [the] city
17 Hakuna hata mwanaume mmoja aliyebakia Ai wala Betheli ambaye hakufuatia Israeli. Wakauacha mji wazi na kuwafuatia Israeli.
and not to remain man: anyone in/on/with Ai and Bethel Bethel which not to come out: come after Israel and to leave: forsake [obj] [the] city to open and to pursue after Israel
18 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Inua huo mkuki ulio mkononi mwako kuuelekeza Ai, kwa kuwa nitautia huo mji mkononi mwako.” Hivyo Yoshua akauelekeza mkuki wake Ai.
and to say LORD to(wards) Joshua to stretch in/on/with javelin which in/on/with hand your to(wards) [the] Ai for in/on/with hand your to give: give her and to stretch Joshua in/on/with javelin which in/on/with hand his to(wards) [the] city
19 Mara tu alipofanya hivi, wale watu waliokuwa mavizioni wakaondoka upesi kutoka mahali pao na kukimbilia mbele. Wakaingia ndani ya mji, wakauteka na kuutia moto kwa haraka.
and [the] to ambush to arise: rise haste from place his and to run: run like/as to stretch hand his and to come (in): come [the] city and to capture her and to hasten and to kindle [obj] [the] city in/on/with fire
20 Watu wa Ai wakaangalia nyuma, wakauona moshi wa huo mji ukielekea angani lakini hawakuwa na nafasi ya kutoroka kwa upande wowote, kwa kuwa wale Waisraeli waliokuwa wanawakimbia kuelekea jangwani walikuwa wamegeuka nyuma kuwakabili wakimbizaji wao.
and to turn human [the] Ai after them and to see: behold! and behold to ascend: rise smoke [the] city [the] heaven [to] and not to be in/on/with them hand: power to/for to flee here/thus and here/thus and [the] people [the] to flee [the] wilderness to overturn to(wards) [the] to pursue
21 Basi Yoshua na Israeli wote walipoona kwamba waviziaji wameshauteka mji na moshi ulikuwa unapaa juu kutoka kwenye mji, wakawageukia watu wa Ai na kuwashambulia.
and Joshua and all Israel to see: see for to capture [the] to ambush [obj] [the] city and for to ascend: rise smoke [the] city and to return: return and to smite [obj] human [the] Ai
22 Wale waviziaji nao pia wakatoka nje ya mji dhidi yao, hivi kwamba wakashikiwa katikati, Waisraeli wakiwa pande zote mbili. Israeli wakawaua, bila kuwaachia yeyote aliyenusurika wala aliyetoroka.
and these to come out: come from [the] city to/for to encounter: toward them and to be to/for Israel in/on/with midst these from this and these from this and to smite [obj] them till lest to remain to/for him survivor and survivor
23 Lakini wakamchukua mfalme wa Ai akiwa hai na kumleta kwa Yoshua.
and [obj] king [the] Ai to capture alive and to present: bring [obj] him to(wards) Joshua
24 Israeli ilipomaliza kuwaua wanaume wote wa Ai katika mashamba na jangwani walipokuwa wamewafukuzia, na baada ya kila mmoja wao kuuawa kwa upanga, Waisraeli wote wakarudi Ai na kuwaua wale waliokuwa wamebakia mjini.
and to be like/as to end: finish Israel to/for to kill [obj] all to dwell [the] Ai in/on/with land: country in/on/with wilderness which to pursue them in/on/with him and to fall: kill all their to/for lip: edge sword till to finish they and to return: return all Israel [the] Ai and to smite [obj] her to/for lip: edge sword
25 Watu kumi na mbili elfu, waume kwa wake, waliangamia siku ile, yaani watu wote wa Ai.
and to be all [the] to fall: kill in/on/with day [the] he/she/it from man and till woman two ten thousand all human [the] Ai
26 Kwa maana Yoshua hakuurudisha ule mkono wake uliokuwa umeuinua mkuki hadi alipomaliza kuwaangamiza wote walioishi Ai.
and Joshua not to return: return hand his which to stretch in/on/with javelin till which to devote/destroy [obj] all to dwell [the] Ai
27 Lakini Israeli wakajichukulia mifugo na nyara za mji huu, kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Yoshua.
except [the] animal and spoil [the] city [the] he/she/it to plunder to/for them Israel like/as word LORD which to command [obj] Joshua
28 Kwa hiyo Yoshua akauchoma moto mji wa Ai na kuufanya kuwa lundo la magofu la kudumu, mahali pa ukiwa hadi leo.
and to burn Joshua [obj] [the] Ai and to set: make her mound forever: enduring devastation till [the] day: today [the] this
29 Akamwangika mfalme wa Ai kwenye mti na kumwacha hapo mpaka jioni. Wakati wa jua kutua, Yoshua akawaamuru wautoe mwili wake kwenye mti na kuutupa kwenye ingilio la lango la mji. Kisha wakalundika mawe makubwa mengi juu yake, ambayo yamesalia mpaka leo.
and [obj] king [the] Ai to hang upon [the] tree till time [the] evening and like/as to come (in): besiege [the] sun to command Joshua and to go down [obj] carcass his from [the] tree and to throw [obj] her to(wards) entrance gate [the] city and to arise: raise upon him heap stone great: large till [the] day: today [the] this
30 Kisha Yoshua akajenga madhabahu ya Bwana, Mungu wa Israeli, katika Mlima wa Ebali,
then to build Joshua altar to/for LORD God Israel in/on/with mountain: mount (Mount) Ebal
31 kama Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa amewaamuru Waisraeli. Akaijenga sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose: madhabahu ya mawe yasiyochongwa, ambayo juu yake hakuna chombo cha chuma kilichotumika. Hapo juu yake wakamtolea Bwana sadaka za kuteketezwa na kutoa sadaka za amani.
like/as as which to command Moses servant/slave LORD [obj] son: descendant/people Israel like/as to write in/on/with scroll: book instruction Moses altar stone complete which not to wave upon them iron and to ascend: offer up upon him burnt offering to/for LORD and to sacrifice peace offering
32 Pale, mbele ya Waisraeli Yoshua akanakili juu ya hayo mawe sheria ya Mose, aliyokuwa ameiandika.
and to write there upon [the] stone [obj] second instruction Moses which to write to/for face son: descendant/people Israel
33 Israeli yote, wageni na wazawa sawasawa, wakiwa na wazee wao, maafisa na waamuzi, walikuwa wamesimama pande zote mbili za Sanduku la Agano la Bwana, wakiwaelekea wale waliokuwa wamelichukua, yaani makuhani, ambao ni Walawi. Nusu ya watu ilisimama mbele ya Mlima Gerizimu na nusu hiyo ingine ikasimama mbele ya Mlima Ebali, kama vile Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa ameamuru hapo mwanzo alipotoa maagizo ya kuwabariki watu wa Israeli.
and all Israel and old: elder his and official and to judge him to stand: stand from this and from this to/for ark before [the] priest [the] Levi to lift: bear ark covenant LORD like/as sojourner like/as born half his to(wards) opposite mountain: mount (Mount) Gerizim and [the] half his to(wards) opposite mountain: mount (Mount) Ebal like/as as which to command Moses servant/slave LORD to/for to bless [obj] [the] people Israel in/on/with first: previous
34 Hatimaye, Yoshua akasoma maneno yote ya sheria, yaani baraka na laana, kama vile ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria.
and after so to call: read out [obj] all word [the] instruction [the] blessing and [the] curse like/as all [the] to write in/on/with scroll: book [the] instruction
35 Hakuna neno lolote katika yale yote ambayo Mose alikuwa ameamuru ambalo Yoshua hakulisomea kusanyiko lote la Israeli, ikiwa ni pamoja na wanawake na watoto, na wageni walioishi miongoni mwao.
not to be word from all which to command Moses which not to call: read out Joshua before all assembly Israel and [the] woman and [the] child and [the] sojourner [the] to go: walk in/on/with entrails: among their

< Yoshua 8 >