< Yoshua 8 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Usiogope, wala usivunjike moyo. Chukua jeshi lote la vita uende pamoja nalo kuishambulia Ai. Kwa kuwa nimeshamweka mikononi mwako mfalme wa Ai, pamoja na watu wake, mji wake na nchi yake.
Then the Lord said to Joshua, Have no fear and do not be troubled: take with you all the fighting-men and go up against Ai: for I have given into your hands the king of Ai and his people and his town and his land:
2 Utafanya Ai na mfalme wake kama ulivyofanya kwa mji wa Yeriko na mfalme wake, isipokuwa mnaweza kuchukua mateka wake na mifugo wake, kwa ajili yenu. Weka waviziaji upande wa nyuma ya mji.”
And you are to do to Ai and its king as you did to Jericho and its king: but their goods and their cattle you may take for yourselves: let a secret force be stationed to make a surprise attack on the town from the back.
3 Basi Yoshua na jeshi lote wakainuka kushambulia Ai. Akachagua watu mashujaa elfu thelathini walio bora miongoni mwa wapiganaji wake, akawapeleka wakati wa usiku
So Joshua and the fighting-men got ready to go up against Ai; and Joshua took thirty thousand men of war, and sent them out by night.
4 akiwaagiza: “Sikilizeni kwa makini. Mtavizia nyuma ya mji. Msiende mbali sana na mji. Wote kuweni macho.
And he gave them their orders, saying, Go and take up your position secretly at the back of the town: do not go very far away, and let all of you be ready:
5 Mimi na watu walio pamoja nami, tutaukabili mji, kisha itakuwa hapo watu watakapotoka nje kupigana nasi, kama walivyofanya hapo kwanza, sisi tutawakimbia.
And I and all the people with me will come near the town, and when they come out against us as they did before, we will go in flight from them;
6 Watatufuatilia mpaka tutakapokuwa tumewavuta mbali na mji kwa kuwa watasema, ‘Wanatukimbia, kama walivyofanya hapo awali.’ Hivyo tutakapowakimbia,
And they will come out after us, till we have got them away from the town; for they will say, They have gone in flight from us as before; so we will go in flight before them;
7 ninyi inawapasa mwinuke mtoke huko mafichoni na kuuteka mji. Bwana Mungu wenu atautia mkononi mwenu.
Then you will get up from your secret position and take the town, for the Lord your God will give it up into your hands.
8 Mtakapokuwa mmeuteka mji, uteketezeni kwa moto. Fanyeni kama vile Bwana alivyoamuru. Angalieni, nimewaagiza.”
And when you have taken the town, put fire to it, as the Lord has said: see, I have given you your orders.
9 Ndipo Yoshua akawatuma watu, nao wakaenda mahali pa kujificha, wakawa wanavizia kati ya Betheli na Ai, kuelekea upande wa magharibi wa Ai, lakini Yoshua akalala miongoni mwa watu usiku huo.
So Joshua sent them out: and they took up a secret position between Beth-el and Ai, on the west side of Ai: but Joshua kept with the people that night.
10 Asubuhi na mapema siku iliyofuatia, Yoshua akawakutanisha watu wake, na yeye na viongozi wa Israeli wakawa mbele ya watu kwenda Ai.
And early in the morning Joshua got up, and put the people in order, and he and the chiefs of Israel went up before the people to Ai.
11 Watu wote wa vita waliokuwa pamoja naye walipanda, wakakaribia na kufika mbele ya mji. Wakapiga kambi kaskazini mwa Ai, pakiwa na bonde kati yao na huo mji.
And all the fighting-men who were with him went up and came near the town, and took up a position on the north side of Ai facing the town, with a valley between him and the town.
12 Yoshua alikuwa amewachukua watu wapatao elfu tano, akawaweka katika uavizi kati ya Betheli na Ai, upande wa magharibi wa mji.
And taking about five thousand men, he put them in position for a surprise attack on the west side of Ai, between Beth-el and Ai.
13 Wakawaweka askari katika maeneo yao: wale wote waliokuwa kambini wakawa kaskazini ya mji na wale waliokuwa wakivizia wakawa upande wa magharibi. Usiku huo Yoshua akaenda katika lile bonde.
So all the people were in their places, the army on the north side of the town and the secret force on the west; and that night Joshua went down into the valley.
14 Mfalme wa Ai alipoona jambo hili, yeye pamoja na watu wote wa mji wakatoka kwa haraka asubuhi na mapema, ili kukutana na Israeli katika vita mahali fulani panapotazamana na Araba. Lakini hakujua kwamba kulikuwa kumewekwa waviziaji dhidi yake nyuma ya mji.
Now when the king of Ai saw it, he got up quickly and went out to war against Israel, he and all his people, to the slope going down to the valley; but he had no idea that a secret force was waiting at the back of the town.
15 Yoshua na Israeli wote wakaruhusu kurudishwa nyuma mbele yao, na kuelekea jangwani.
Then Joshua and all Israel, acting as if they were overcome before them, went in flight by way of the waste land.
16 Watu wote wa Ai wakaitwa ili kuwafuatia, nao wakavutwa kumfuatia Yoshua mbali na mji.
And all the people in Ai came together to go after them; and they went after Joshua, moving away from the town.
17 Hakuna hata mwanaume mmoja aliyebakia Ai wala Betheli ambaye hakufuatia Israeli. Wakauacha mji wazi na kuwafuatia Israeli.
There was not a man in Ai and Beth-el who did not go out after Israel; and the town was open and unwatched while they went after Israel.
18 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Inua huo mkuki ulio mkononi mwako kuuelekeza Ai, kwa kuwa nitautia huo mji mkononi mwako.” Hivyo Yoshua akauelekeza mkuki wake Ai.
And the Lord said to Joshua, Let your spear be stretched out against Ai; for I will give it into your hands. So Joshua took up his spear, stretching it out in the direction of the town.
19 Mara tu alipofanya hivi, wale watu waliokuwa mavizioni wakaondoka upesi kutoka mahali pao na kukimbilia mbele. Wakaingia ndani ya mji, wakauteka na kuutia moto kwa haraka.
Then the secret force came quickly from their place, and running forward when they saw his hand stretched out, went into the town and took it, and put fire to it straight away.
20 Watu wa Ai wakaangalia nyuma, wakauona moshi wa huo mji ukielekea angani lakini hawakuwa na nafasi ya kutoroka kwa upande wowote, kwa kuwa wale Waisraeli waliokuwa wanawakimbia kuelekea jangwani walikuwa wamegeuka nyuma kuwakabili wakimbizaji wao.
Then the men of Ai, looking back, saw the smoke of the town going up to heaven, and were unable to go this way or that: and the people who had gone in flight to the waste land were turned back on those who were coming after them.
21 Basi Yoshua na Israeli wote walipoona kwamba waviziaji wameshauteka mji na moshi ulikuwa unapaa juu kutoka kwenye mji, wakawageukia watu wa Ai na kuwashambulia.
And when Joshua and all Israel saw that the town had been taken by the surprise attack, and that the smoke of the town had gone up, turning round they overcame the men of Ai.
22 Wale waviziaji nao pia wakatoka nje ya mji dhidi yao, hivi kwamba wakashikiwa katikati, Waisraeli wakiwa pande zote mbili. Israeli wakawaua, bila kuwaachia yeyote aliyenusurika wala aliyetoroka.
Then the other force came out of the town against them, so that they were being attacked on this side and on that: and Israel overcame them and let not one of them get away with his life.
23 Lakini wakamchukua mfalme wa Ai akiwa hai na kumleta kwa Yoshua.
But the king of Ai they made prisoner, and took him to Joshua.
24 Israeli ilipomaliza kuwaua wanaume wote wa Ai katika mashamba na jangwani walipokuwa wamewafukuzia, na baada ya kila mmoja wao kuuawa kwa upanga, Waisraeli wote wakarudi Ai na kuwaua wale waliokuwa wamebakia mjini.
Then, after the destruction of all the people of Ai in the field and in the waste land where they went after them, and when all the people had been put to death without mercy, all Israel went back to Ai, and put to death all who were in it without mercy.
25 Watu kumi na mbili elfu, waume kwa wake, waliangamia siku ile, yaani watu wote wa Ai.
On that day twelve thousand were put to death, men and women, all the people of Ai.
26 Kwa maana Yoshua hakuurudisha ule mkono wake uliokuwa umeuinua mkuki hadi alipomaliza kuwaangamiza wote walioishi Ai.
For Joshua did not take back his hand with the outstretched spear till the destruction of the people of Ai was complete.
27 Lakini Israeli wakajichukulia mifugo na nyara za mji huu, kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Yoshua.
But the cattle and the goods from that town, Israel took for themselves, as the Lord had given orders to Joshua.
28 Kwa hiyo Yoshua akauchoma moto mji wa Ai na kuufanya kuwa lundo la magofu la kudumu, mahali pa ukiwa hadi leo.
So Joshua gave Ai to the flames, and made it a waste mass of stones for ever, as it is to this day.
29 Akamwangika mfalme wa Ai kwenye mti na kumwacha hapo mpaka jioni. Wakati wa jua kutua, Yoshua akawaamuru wautoe mwili wake kwenye mti na kuutupa kwenye ingilio la lango la mji. Kisha wakalundika mawe makubwa mengi juu yake, ambayo yamesalia mpaka leo.
And he put the king of Ai to death, hanging him on a tree till evening: and when the sun went down, Joshua gave them orders to take his body down from the tree, and put it in the public place of the town, covering it with a great mass of stones, which is there to this day.
30 Kisha Yoshua akajenga madhabahu ya Bwana, Mungu wa Israeli, katika Mlima wa Ebali,
Then Joshua put up an altar to the Lord, the God of Israel, in Mount Ebal,
31 kama Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa amewaamuru Waisraeli. Akaijenga sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose: madhabahu ya mawe yasiyochongwa, ambayo juu yake hakuna chombo cha chuma kilichotumika. Hapo juu yake wakamtolea Bwana sadaka za kuteketezwa na kutoa sadaka za amani.
In the way ordered by Moses, the servant of the Lord, as it is recorded in the book of the law of Moses, an altar of uncut stones, untouched by any iron instrument: and on it they made burned offerings and peace-offerings to the Lord.
32 Pale, mbele ya Waisraeli Yoshua akanakili juu ya hayo mawe sheria ya Mose, aliyokuwa ameiandika.
And he made there on the stones a copy of the law of Moses, writing it before the eyes of the children of Israel.
33 Israeli yote, wageni na wazawa sawasawa, wakiwa na wazee wao, maafisa na waamuzi, walikuwa wamesimama pande zote mbili za Sanduku la Agano la Bwana, wakiwaelekea wale waliokuwa wamelichukua, yaani makuhani, ambao ni Walawi. Nusu ya watu ilisimama mbele ya Mlima Gerizimu na nusu hiyo ingine ikasimama mbele ya Mlima Ebali, kama vile Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa ameamuru hapo mwanzo alipotoa maagizo ya kuwabariki watu wa Israeli.
And all Israel, those who were Israelites by birth, as well as the men from other lands living with them, and their responsible men and their overseers and judges, took their places round the ark, in front of the priests, the Levites, whose work it was to take up the ark of the Lord's agreement; half of them were stationed in front of Mount Gerizim and half in front of Mount Ebal, in agreement with the orders for the blessing of the children of Israel which Moses, the servant of the Lord, had given.
34 Hatimaye, Yoshua akasoma maneno yote ya sheria, yaani baraka na laana, kama vile ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria.
And after, he gave them all the words of the law, the blessing and the curse, as it is all recorded in the book of the law;
35 Hakuna neno lolote katika yale yote ambayo Mose alikuwa ameamuru ambalo Yoshua hakulisomea kusanyiko lote la Israeli, ikiwa ni pamoja na wanawake na watoto, na wageni walioishi miongoni mwao.
Reading to all the meeting of Israel, with the women and the children and the men from other lands who were living among them, every word of the orders which Moses had given.

< Yoshua 8 >