< Yoshua 6 >

1 Basi malango ya Yeriko yalifungwa kwa uthabiti kwa ajili ya Waisraeli. Hakuna mtu yeyote aliyetoka au kuingia.
And Jericho [was] shutting and shut up because of [the] people of Israel there not [was one] going out and there not [was one] coming.
2 Kisha Bwana akamwambia Yoshua, “Tazama, nimeitia Yeriko mikononi mwako, pamoja na mfalme wake na watu wake wa vita.
And he said Yahweh to Joshua see I have given in hand your Jericho and king its [the] mighty [men] of strength.
3 Zunguka mji mara moja pamoja na watu wote wenye silaha. Fanya hivi kwa siku sita.
And you will go around the city all [the] men of war you will encircle the city a time one thus you will do six days.
4 Uwe na makuhani saba wakibeba mabaragumu ya pembe za kondoo dume mbele ya Sanduku. Siku ya saba, mzunguke mji mara saba, nao makuhani wakipiga baragumu hizo.
And seven priests they will carry seven trumpets of rams' horns before the ark and on the day seventh you will go round the city seven times and the priests they will give a blast on the trumpets.
5 Utakapowasikia wamepaliza sauti kubwa ya baragumu, watu wote wapige kelele kwa sauti kuu, kisha ukuta wa mji utaanguka na watu watapanda, kila mtu akiendelea mbele.”
And it will be when blow - on [the] horn of ram's horn (just as hear you *Q(K)*) [the] sound of the trumpet they will shout all the people a shout loud and it will fall [the] wall of the city in place its and they will go up the people everyone before himself.
6 Ndipo Yoshua mwana wa Nuni akaita makuhani na kuwaambia, “Chukueni Sanduku la Agano la Bwana na makuhani saba wachukue baragumu za pembe za kondoo dume mbele yake.”
And he called Joshua [the] son of Nun to the priests and he said to them lift up [the] ark of the covenant and seven priests they will carry seven trumpets of rams' horns before [the] ark of Yahweh.
7 Naye akawaagiza watu, “Songeni mbele! Mkauzunguke mji, na walinzi wenye silaha watangulie mbele ya Sanduku la Bwana.”
(And he said *Q(K)*) to the people pass on and go round the city and the armed [man] he will pass on before [the] ark of Yahweh.
8 Baada ya Yoshua kuzungumza na watu, wale makuhani saba wenye kuzibeba zile baragumu saba mbele za Bwana, wakatangulia mbele, wakipiga baragumu zao na Sanduku la Agano la Bwana likawafuata.
And it was when had said Joshua to the people and seven the priests [who] were carrying seven [the] trumpets of rams' horns before Yahweh they passed on and they gave a blast on the trumpets and [the] ark of [the] covenant of Yahweh [was] going after them.
9 Walinzi waliokuwa na silaha wakaenda mbele ya hao makuhani waliopiga hizo baragumu na hao walinzi wa nyuma wakafuata Sanduku. Wakati wote huu baragumu zilikuwa zikipigwa.
And the armed [man] [was] walking before the priests ([who] give a blast on *Q(K)*) the trumpets and the rearguard [was] walking behind the ark walking and giving blasts on the trumpets.
10 Bali Yoshua alikuwa amewaagiza watu, “Msipige kelele ya vita, msipaze sauti zenu, wala kusema neno lolote mpaka siku ile nitakayowaambia mpige kelele. Ndipo mtapiga kelele!”
And the people he commanded Joshua saying not you must shout and not you must make heard voice your and not it will go out from mouth your a word until [the] day say I to you shout and you will shout.
11 Basi akalipeleka Sanduku la Bwana kuzungushwa huo mji, likizungushwa mara moja. Kisha watu wakarudi kambini kulala.
And he caused to go around [the] ark of Yahweh the city it encircled [it] a time one and they went the camp and they stayed in the camp.
12 Yoshua akaamka mapema asubuhi iliyofuata nao makuhani wakalichukua Sanduku la Bwana.
And he rose early Joshua in the morning and they lifted the priests [the] ark of Yahweh.
13 Wale Makuhani saba wakizibeba zile baragumu saba wakatangulia mbele ya Sanduku la Bwana wakizipiga. Watu wenye silaha wakatangulia mbele yao na walinzi wa nyuma wakalifuata Sanduku la Bwana, huku baragumu hizo zikiendelea kulia.
And seven the priests [who] were carrying seven [the] trumpets of rams' horns before [the] ark of Yahweh [were] walking continuously and they gave blasts on the trumpets and the armed [man] [was] walking before them and the rearguard [was] walking behind [the] ark of Yahweh (walking *Q(K)*) and giving blasts on the trumpets.
14 Siku ya pili wakauzunguka mji mara moja na kurudi kambini. Wakafanya hivi kwa siku sita.
And they went around the city on the day second a time one and they returned the camp thus they did six days.
15 Siku ya saba, wakaamka asubuhi na mapema wakauzunguka mji kama walivyokuwa wakifanya, isipokuwa siku ile waliuzunguka mji mara saba.
And it was - on the day seventh and they rose early when came up the dawn and they went around the city according to the custom this seven times only on the day that they went round the city seven times.
16 Walipouzunguka mara ya saba, makuhani walipopiga baragumu kwa sauti kubwa, Yoshua akawaamuru watu akisema, “Pigeni kelele! Kwa maana Bwana amewapa mji huu!
And it was at the time seventh they gave a blast the priests on the trumpets and he said Joshua to the people shout for he has given Yahweh to you the city.
17 Mji huu pamoja na vyote vilivyomo ndani yake utawekwa wakfu kwa Bwana. Ila Rahabu tu, yule kahaba na wote ambao wako pamoja naye nyumbani mwake ndio watakaosalimishwa, kwa sababu aliwaficha wale wapelelezi tuliowatuma.
And it will be the city a devoted thing it and all that [is] in it to Yahweh only Rahab the prostitute she will live she and every [one] who [is] with her in the house for she hid the messengers whom we sent.
18 Lakini mjiepushe na vitu vilivyowekwa wakfu, msije mkachukua chochote katika hivyo, msije mkajiletea maangamizi katika maskani ya Israeli na kuiletea taabu.
And only you keep from the devoted thing[s] lest you should totally destroy and you will take any of the devoted thing[s] and you will make [the] camp of Israel into a devoted thing and you will trouble it.
19 Fedha yote na dhahabu, vyombo vya shaba na chuma ni vitakatifu kwa Bwana, lazima viletwe katika hazina yake.”
And all - silver and gold and articles of bronze and iron [is] a holy thing it to Yahweh [the] treasury of Yahweh it will go.
20 Wakati baragumu zilipopigwa, watu walipiga kelele, na katika sauti ya baragumu, na watu kupaza sauti, ukuta ukaanguka; hivyo kila mtu akapanda akiendelea mbele na kuuteka mji.
And it shouted the people and they gave a blast on the trumpets and it was when heard the people [the] sound of the trumpet and they shouted the people a shout loud and it fell the city wall in place its and it went up the people the city towards everyone before himself and they captured the city.
21 Wakauweka mji wakfu kwa Bwana, na kila chenye uhai ndani yake walikiangamiza kwa upanga, wanaume kwa wanawake, vijana kwa wazee, ngʼombe, kondoo na punda.
And they totally destroyed all that [was] in the city from man and unto woman from young man and unto old [man] and unto ox[en] and sheep and donkey[s] to [the] mouth of [the] sword.
22 Yoshua akawaambia wale watu wawili waliokuwa wameipeleleza nchi, “Nendeni nyumbani kwa yule kahaba, mleteni pamoja na wote waliomo nyumbani mwake, kulingana na kiapo chenu kwake.”
And to two the men who had spied out the land he said Joshua go [the] house of the woman the prostitute and bring out from there the woman and every [one] who [belongs] to her just as you swore to her.
23 Basi wale vijana waliofanya upelelezi wakaenda kumleta Rahabu, baba yake na mama yake, na ndugu zake na watu wote waliokuwa pamoja naye. Wakaleta jamaa yake yote na kuwaweka mahali nje ya kambi ya Israeli.
And they went the young men who had spied out and they brought out Rahab and father her and mother her and brothers her and every [one] who [belonged] to her and all famili her they brought out and they put them from [the] outside of [the] camp of Israel.
24 Kisha wakauchoma mji wote na kila kitu kilichokuwamo ndani yake. Lakini fedha, dhahabu, vyombo vya shaba na vya chuma wakaviweka katika hazina ya nyumba ya Bwana.
And the city they burned with fire and all that [was] in it only - the silver and the gold and [the] articles of bronze and iron they put [the] treasury of [the] house of Yahweh.
25 Lakini Yoshua akamhifadhi Rahabu yule kahaba, jamaa yake yote na wote waliokuwa wa kwake, kwa sababu aliwaficha watu waliotumwa na Yoshua kuipeleleza Yeriko, naye anaishi miongoni mwa Waisraeli hata leo.
And Rahab the prostitute and [the] household of father her and every [one] who [belonged] to her he let live Joshua and she has dwelt in [the] midst of Israel until the day this for she hid the messengers whom he had sent Joshua to spy out Jericho.
26 Wakati ule Yoshua akatamka kiapo hiki akasema, “Aliyelaaniwa mbele za Bwana ni mtu atakayeinuka kuujenga tena mji huu wa Yeriko: “Kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza wa kiume ataiweka misingi yake; kwa gharama ya mtoto wake wa mwisho atayaweka malango yake.”
And he administered an oath Joshua at the time that saying [is] cursed the person before Yahweh who he will arise and he will rebuild the city this Jericho with firstborn his he will found it and with young [son] his he will set up gates its.
27 Hivyo Bwana alikuwa pamoja na Yoshua, na sifa zake zikaenea katika nchi yote.
And he was Yahweh with Joshua and it was [the] report of him in all the land.

< Yoshua 6 >