< Yoshua 6 >
1 Basi malango ya Yeriko yalifungwa kwa uthabiti kwa ajili ya Waisraeli. Hakuna mtu yeyote aliyetoka au kuingia.
Now, Jericho, was shut up and barred because of the sons of Israel, —none came out and none went in.
2 Kisha Bwana akamwambia Yoshua, “Tazama, nimeitia Yeriko mikononi mwako, pamoja na mfalme wake na watu wake wa vita.
Then said Yahweh unto Joshua, See, I have delivered, into thy hand, Jericho and her king, —the mighty men of valour.
3 Zunguka mji mara moja pamoja na watu wote wenye silaha. Fanya hivi kwa siku sita.
So then ye shall compass the city all ye men of war, going round the city, once, —thus, shall thou do six days.
4 Uwe na makuhani saba wakibeba mabaragumu ya pembe za kondoo dume mbele ya Sanduku. Siku ya saba, mzunguke mji mara saba, nao makuhani wakipiga baragumu hizo.
And, seven priests, shall bear the seven rams’ horns before the ark, and, on the seventh day, shall ye compass the city seven times, —and, the priests, shall blow with the horns.
5 Utakapowasikia wamepaliza sauti kubwa ya baragumu, watu wote wapige kelele kwa sauti kuu, kisha ukuta wa mji utaanguka na watu watapanda, kila mtu akiendelea mbele.”
And it shall come to pass, when the ram’s horn soundeth, when ye hear the sound of the horn, that all the people shall shout with a great shout, —and then shall the wall of the city fall down under it, and the people shall go up, every man straight before him.
6 Ndipo Yoshua mwana wa Nuni akaita makuhani na kuwaambia, “Chukueni Sanduku la Agano la Bwana na makuhani saba wachukue baragumu za pembe za kondoo dume mbele yake.”
Then called Joshua son of Nun unto the priests, and said unto them, Bear ye the ark of the covenant, —and let, seven priest, bear seven rams horns, before the ark of Yahweh.
7 Naye akawaagiza watu, “Songeni mbele! Mkauzunguke mji, na walinzi wenye silaha watangulie mbele ya Sanduku la Bwana.”
Then said he unto the people, Pass on and compass the city, —and let, the armed host, pass on before the ark of Yahweh.
8 Baada ya Yoshua kuzungumza na watu, wale makuhani saba wenye kuzibeba zile baragumu saba mbele za Bwana, wakatangulia mbele, wakipiga baragumu zao na Sanduku la Agano la Bwana likawafuata.
And it was so, when Joshua had spoken unto the people, that, the seven priests who were bearing the seven rams’ horns before Yahweh, passed on and blew with the horns, —the ark of the covenant of Yahweh also coming after them.
9 Walinzi waliokuwa na silaha wakaenda mbele ya hao makuhani waliopiga hizo baragumu na hao walinzi wa nyuma wakafuata Sanduku. Wakati wote huu baragumu zilikuwa zikipigwa.
And, the armed host, went on before the priests who blew with the horns, —and, the rear-guard, came after the ark, going on and blowing with the horns.
10 Bali Yoshua alikuwa amewaagiza watu, “Msipige kelele ya vita, msipaze sauti zenu, wala kusema neno lolote mpaka siku ile nitakayowaambia mpige kelele. Ndipo mtapiga kelele!”
Now, unto the people, had Joshua given command, saying—Ye shall not shout nor let your voice be heard, neither shall there go out of your mouth, a word, —until the day when I say unto you Shout! then shall ye shout.
11 Basi akalipeleka Sanduku la Bwana kuzungushwa huo mji, likizungushwa mara moja. Kisha watu wakarudi kambini kulala.
So he caused the ark of Yahweh to compass the city, going round once, —and they came into the camp, and lodged in the camp.
12 Yoshua akaamka mapema asubuhi iliyofuata nao makuhani wakalichukua Sanduku la Bwana.
And Joshua rose early in the morning, —and the priests bare the ark of Yahweh;
13 Wale Makuhani saba wakizibeba zile baragumu saba wakatangulia mbele ya Sanduku la Bwana wakizipiga. Watu wenye silaha wakatangulia mbele yao na walinzi wa nyuma wakalifuata Sanduku la Bwana, huku baragumu hizo zikiendelea kulia.
and, the seven priests who bare the seven rams’ horns before the ark of Yahweh, went on and on, and blew with the horns, —with, the armed host going on before them, and, the rear-guard, coming after the ark of Yahweh, going on and blowing with the horns.
14 Siku ya pili wakauzunguka mji mara moja na kurudi kambini. Wakafanya hivi kwa siku sita.
So they compassed the city on the second day once, and returned into the camp, —thus, did they, six days.
15 Siku ya saba, wakaamka asubuhi na mapema wakauzunguka mji kama walivyokuwa wakifanya, isipokuwa siku ile waliuzunguka mji mara saba.
And it came to pass, on the seventh day, that they rose early at the uprisings of the dawn, and compassed the city after this manner, seven times, —only on that day they compassed the city seven times.
16 Walipouzunguka mara ya saba, makuhani walipopiga baragumu kwa sauti kubwa, Yoshua akawaamuru watu akisema, “Pigeni kelele! Kwa maana Bwana amewapa mji huu!
And it came to pass, at the seventh time—when the priests blew with the horns, then did Joshua say unto the people—Shout, for Yahweh hath delivered unto you the city.
17 Mji huu pamoja na vyote vilivyomo ndani yake utawekwa wakfu kwa Bwana. Ila Rahabu tu, yule kahaba na wote ambao wako pamoja naye nyumbani mwake ndio watakaosalimishwa, kwa sababu aliwaficha wale wapelelezi tuliowatuma.
And it shall be, that, as for the city, devoted, shall it be and all that is therein unto Yahweh, —nevertheless, Rahab the harlot, shall live, she and all who are with her in the house, because she hid the messengers whom we sent.
18 Lakini mjiepushe na vitu vilivyowekwa wakfu, msije mkachukua chochote katika hivyo, msije mkajiletea maangamizi katika maskani ya Israeli na kuiletea taabu.
But, in any wise, do, ye, beware of what is devoted, lest ye should covet, and then take of what is devoted, —and so cause the camp of Israel to be devoted, and bring trouble upon it.
19 Fedha yote na dhahabu, vyombo vya shaba na chuma ni vitakatifu kwa Bwana, lazima viletwe katika hazina yake.”
But, as for all silver and gold and vessels of bronze and iron, hallowed, it is to Yahweh, —unto the treasury of Yahweh, shall it come.
20 Wakati baragumu zilipopigwa, watu walipiga kelele, na katika sauti ya baragumu, na watu kupaza sauti, ukuta ukaanguka; hivyo kila mtu akapanda akiendelea mbele na kuuteka mji.
So the people shouted, when the horns were blown, —yea it came to pass, when the people heard the sound of the horn, that the people shouted with a great shout, and the wall fell down under it, and the people went up into the city every man straight before him, and so they captured the city.
21 Wakauweka mji wakfu kwa Bwana, na kila chenye uhai ndani yake walikiangamiza kwa upanga, wanaume kwa wanawake, vijana kwa wazee, ngʼombe, kondoo na punda.
And they devoted all that were in the city, both man and woman, both young and old, —and ox and sheep and ass, with the edge of the sword.
22 Yoshua akawaambia wale watu wawili waliokuwa wameipeleleza nchi, “Nendeni nyumbani kwa yule kahaba, mleteni pamoja na wote waliomo nyumbani mwake, kulingana na kiapo chenu kwake.”
But, unto the two men who spied out the land, Joshua said, Go into the house of the woman, the harlot, —and bring out thence the woman and all that she hath, as ye aware unto her.
23 Basi wale vijana waliofanya upelelezi wakaenda kumleta Rahabu, baba yake na mama yake, na ndugu zake na watu wote waliokuwa pamoja naye. Wakaleta jamaa yake yote na kuwaweka mahali nje ya kambi ya Israeli.
So the young men the spies went in and brought out Rahab and her father and her mother and her brethren and all that she had, yea, all her kindred, brought they out, —and set them outside the camp of Israel.
24 Kisha wakauchoma mji wote na kila kitu kilichokuwamo ndani yake. Lakini fedha, dhahabu, vyombo vya shaba na vya chuma wakaviweka katika hazina ya nyumba ya Bwana.
But, the city, burned they with fire, and all that was therein, —save only, the silver and the gold and the vessels of bronze and of iron, put they into the treasury of the house of Yahweh.
25 Lakini Yoshua akamhifadhi Rahabu yule kahaba, jamaa yake yote na wote waliokuwa wa kwake, kwa sababu aliwaficha watu waliotumwa na Yoshua kuipeleleza Yeriko, naye anaishi miongoni mwa Waisraeli hata leo.
And, Rahab the harlot and the household of her father and all that she had, did Joshua save alive, so she hath dwelt in the midst of Israel until this day, —because she hid the messengers whom Joshua sent to spy out Jericho.
26 Wakati ule Yoshua akatamka kiapo hiki akasema, “Aliyelaaniwa mbele za Bwana ni mtu atakayeinuka kuujenga tena mji huu wa Yeriko: “Kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza wa kiume ataiweka misingi yake; kwa gharama ya mtoto wake wa mwisho atayaweka malango yake.”
And Joshua imposed an oath at that time, saying, —Cursed be the man before Yahweh who shall raise up and build this city—Jericho, At the price of his firstborn, shall he lay its foundation, and, at the price of his youngest, shall he set up its doors.
27 Hivyo Bwana alikuwa pamoja na Yoshua, na sifa zake zikaenea katika nchi yote.
And so it was that Yahweh was with Joshua, —and his fame was in all the land.