< Yoshua 6 >

1 Basi malango ya Yeriko yalifungwa kwa uthabiti kwa ajili ya Waisraeli. Hakuna mtu yeyote aliyetoka au kuingia.
Jericho's gates were shut and barred because of the Israelites. Nobody was allowed in or out.
2 Kisha Bwana akamwambia Yoshua, “Tazama, nimeitia Yeriko mikononi mwako, pamoja na mfalme wake na watu wake wa vita.
But the Lord told Joshua, “I'm handing over the city of Jericho to you, along with its king and its army of warriors.
3 Zunguka mji mara moja pamoja na watu wote wenye silaha. Fanya hivi kwa siku sita.
March around the city with your armed men once a day for six days.
4 Uwe na makuhani saba wakibeba mabaragumu ya pembe za kondoo dume mbele ya Sanduku. Siku ya saba, mzunguke mji mara saba, nao makuhani wakipiga baragumu hizo.
Seven priests are to go ahead of the Ark, each carrying a ram's horn. On the seventh day, march seven times around the city, with the priests blowing their rams' horns.
5 Utakapowasikia wamepaliza sauti kubwa ya baragumu, watu wote wapige kelele kwa sauti kuu, kisha ukuta wa mji utaanguka na watu watapanda, kila mtu akiendelea mbele.”
When you hear a long blast on the rams' horns, everyone shall give a really loud shout. The city walls will collapse, and every man can go right in.”
6 Ndipo Yoshua mwana wa Nuni akaita makuhani na kuwaambia, “Chukueni Sanduku la Agano la Bwana na makuhani saba wachukue baragumu za pembe za kondoo dume mbele yake.”
So Joshua, son of Nun, sent for the priests, and told them, “Pick up the Ark of Agreement, and have seven priests carry seven rams' horns and go ahead of the Ark of the Lord.”
7 Naye akawaagiza watu, “Songeni mbele! Mkauzunguke mji, na walinzi wenye silaha watangulie mbele ya Sanduku la Bwana.”
Then he told the people, “Move out! March around the city with the armed men up front ahead of the Ark of the Lord!”
8 Baada ya Yoshua kuzungumza na watu, wale makuhani saba wenye kuzibeba zile baragumu saba mbele za Bwana, wakatangulia mbele, wakipiga baragumu zao na Sanduku la Agano la Bwana likawafuata.
When Joshua finished speaking to the people, the seven priests carrying the seven rams' horns in the presence of the Lord started out, blowing the horns, with the Ark following behind.
9 Walinzi waliokuwa na silaha wakaenda mbele ya hao makuhani waliopiga hizo baragumu na hao walinzi wa nyuma wakafuata Sanduku. Wakati wote huu baragumu zilikuwa zikipigwa.
Some of the armed men marched ahead of the priests blowing the horns, while some followed the Ark, the horns being blown continually.
10 Bali Yoshua alikuwa amewaagiza watu, “Msipige kelele ya vita, msipaze sauti zenu, wala kusema neno lolote mpaka siku ile nitakayowaambia mpige kelele. Ndipo mtapiga kelele!”
However, Joshua ordered them, “Don't shout, don't even talk. Don't say anything until I tell you all to shout—then shout!”
11 Basi akalipeleka Sanduku la Bwana kuzungushwa huo mji, likizungushwa mara moja. Kisha watu wakarudi kambini kulala.
So the Ark of the Lord was carried around the city, circling it once. Then they returned to the camp and spent the night there.
12 Yoshua akaamka mapema asubuhi iliyofuata nao makuhani wakalichukua Sanduku la Bwana.
Joshua got up early in the morning, and the priests picked up the Ark of the Lord.
13 Wale Makuhani saba wakizibeba zile baragumu saba wakatangulia mbele ya Sanduku la Bwana wakizipiga. Watu wenye silaha wakatangulia mbele yao na walinzi wa nyuma wakalifuata Sanduku la Bwana, huku baragumu hizo zikiendelea kulia.
The seven priests with the seven rams' horns went ahead of the Ark of the Lord, blowing the horns. The armed men went before them and behind the Ark of the Lord, the horns being blown continually.
14 Siku ya pili wakauzunguka mji mara moja na kurudi kambini. Wakafanya hivi kwa siku sita.
So on the second day they marched around the city, circling it once, and returned to the camp. They did this for a total of six days.
15 Siku ya saba, wakaamka asubuhi na mapema wakauzunguka mji kama walivyokuwa wakifanya, isipokuwa siku ile waliuzunguka mji mara saba.
On the seventh day they got up at dawn and marched around the city in the usual way, except that this day they circled the city seven times.
16 Walipouzunguka mara ya saba, makuhani walipopiga baragumu kwa sauti kubwa, Yoshua akawaamuru watu akisema, “Pigeni kelele! Kwa maana Bwana amewapa mji huu!
The seventh time around when the priests blew the horns, Joshua told the people, “Shout! For today the Lord has given the city to you!
17 Mji huu pamoja na vyote vilivyomo ndani yake utawekwa wakfu kwa Bwana. Ila Rahabu tu, yule kahaba na wote ambao wako pamoja naye nyumbani mwake ndio watakaosalimishwa, kwa sababu aliwaficha wale wapelelezi tuliowatuma.
The city and everything in it is to be set apart for the Lord and destroyed. Only Rahab the prostitute and all those with her in her house shall be spared, because she hid the spies we sent.
18 Lakini mjiepushe na vitu vilivyowekwa wakfu, msije mkachukua chochote katika hivyo, msije mkajiletea maangamizi katika maskani ya Israeli na kuiletea taabu.
But stay away from everything set apart for the Lord, for if you were to take anything you too would be liable to be destroyed, and you would also bring disaster on the camp of Israel.
19 Fedha yote na dhahabu, vyombo vya shaba na chuma ni vitakatifu kwa Bwana, lazima viletwe katika hazina yake.”
All the silver and the gold, and everything made of bronze and iron, are holy to the Lord and they must be placed in the Lord's treasury.”
20 Wakati baragumu zilipopigwa, watu walipiga kelele, na katika sauti ya baragumu, na watu kupaza sauti, ukuta ukaanguka; hivyo kila mtu akapanda akiendelea mbele na kuuteka mji.
So as soon as they heard the sound of the horns, the people gave a loud shout, and the city walls collapsed. The men went in right away and captured the city.
21 Wakauweka mji wakfu kwa Bwana, na kila chenye uhai ndani yake walikiangamiza kwa upanga, wanaume kwa wanawake, vijana kwa wazee, ngʼombe, kondoo na punda.
They destroyed everything in the city: men and women, young and old, cattle, sheep, and donkeys, all were killed by the sword.
22 Yoshua akawaambia wale watu wawili waliokuwa wameipeleleza nchi, “Nendeni nyumbani kwa yule kahaba, mleteni pamoja na wote waliomo nyumbani mwake, kulingana na kiapo chenu kwake.”
Joshua had told the two men who had gone to explore the land, “Go to the house of Rahab the prostitute and bring her out together with all her family, as you promised.”
23 Basi wale vijana waliofanya upelelezi wakaenda kumleta Rahabu, baba yake na mama yake, na ndugu zake na watu wote waliokuwa pamoja naye. Wakaleta jamaa yake yote na kuwaweka mahali nje ya kambi ya Israeli.
So the spies went and brought out Rahab, her father and mother, and all who were with her. They brought out the whole family and took them to a place near the Israelite camp.
24 Kisha wakauchoma mji wote na kila kitu kilichokuwamo ndani yake. Lakini fedha, dhahabu, vyombo vya shaba na vya chuma wakaviweka katika hazina ya nyumba ya Bwana.
Then the Israelites burned down the city and everything in it, except for the silver and the gold, and everything made of bronze and iron, which they placed in the treasury of the Lord's house.
25 Lakini Yoshua akamhifadhi Rahabu yule kahaba, jamaa yake yote na wote waliokuwa wa kwake, kwa sababu aliwaficha watu waliotumwa na Yoshua kuipeleleza Yeriko, naye anaishi miongoni mwa Waisraeli hata leo.
Joshua spared Rahab the prostitute and her family because she hid the men Joshua had sent to spy out Jericho. And she lives among the Israelites to this day.
26 Wakati ule Yoshua akatamka kiapo hiki akasema, “Aliyelaaniwa mbele za Bwana ni mtu atakayeinuka kuujenga tena mji huu wa Yeriko: “Kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza wa kiume ataiweka misingi yake; kwa gharama ya mtoto wake wa mwisho atayaweka malango yake.”
At that time Joshua declared a curse, saying: “Cursed before the Lord is anyone who attempts to rebuild this city of Jericho. He lays its foundation at the cost of his firstborn son; he sets up its gates at the cost of his youngest son.”
27 Hivyo Bwana alikuwa pamoja na Yoshua, na sifa zake zikaenea katika nchi yote.
So the Lord was with Joshua, and his fame spread throughout the land.

< Yoshua 6 >