< Yoshua 6 >
1 Basi malango ya Yeriko yalifungwa kwa uthabiti kwa ajili ya Waisraeli. Hakuna mtu yeyote aliyetoka au kuingia.
Now Jericho was closed as well as fortified, out of fear of the sons of Israel, and no one dared to depart or to enter.
2 Kisha Bwana akamwambia Yoshua, “Tazama, nimeitia Yeriko mikononi mwako, pamoja na mfalme wake na watu wake wa vita.
And the Lord said to Joshua: “Behold, I have given Jericho into your hand, with its king and all the strong men.
3 Zunguka mji mara moja pamoja na watu wote wenye silaha. Fanya hivi kwa siku sita.
Have all the warriors circle the city once each day; you shall do so for six days.
4 Uwe na makuhani saba wakibeba mabaragumu ya pembe za kondoo dume mbele ya Sanduku. Siku ya saba, mzunguke mji mara saba, nao makuhani wakipiga baragumu hizo.
Then, on the seventh day, the priests shall take the seven trumpets, which are used on the jubilee, and they shall precede the ark of the covenant. And you shall circle the city seven times, and the priests shall sound the trumpets.
5 Utakapowasikia wamepaliza sauti kubwa ya baragumu, watu wote wapige kelele kwa sauti kuu, kisha ukuta wa mji utaanguka na watu watapanda, kila mtu akiendelea mbele.”
And when the voice of the trumpet sounds longer and with interruptions, and it increases in your ears, then all the people shall cry out together with a very great shout, and the walls of the city shall fall to the foundation, and they shall enter it, each from a place opposite where they are standing.”
6 Ndipo Yoshua mwana wa Nuni akaita makuhani na kuwaambia, “Chukueni Sanduku la Agano la Bwana na makuhani saba wachukue baragumu za pembe za kondoo dume mbele yake.”
Then Joshua, the son of Nun, called the priests, and he said to them, “Take the ark of the covenant, and let seven other priests take the seven trumpets of the jubilee, and advance before the ark of the Lord.”
7 Naye akawaagiza watu, “Songeni mbele! Mkauzunguke mji, na walinzi wenye silaha watangulie mbele ya Sanduku la Bwana.”
He also said to the people, “Go, and circle the city, armed, preceding the ark of the Lord.”
8 Baada ya Yoshua kuzungumza na watu, wale makuhani saba wenye kuzibeba zile baragumu saba mbele za Bwana, wakatangulia mbele, wakipiga baragumu zao na Sanduku la Agano la Bwana likawafuata.
And when Joshua had finished his words, and the seven priests sounded the seven trumpets before the ark of the covenant of the Lord,
9 Walinzi waliokuwa na silaha wakaenda mbele ya hao makuhani waliopiga hizo baragumu na hao walinzi wa nyuma wakafuata Sanduku. Wakati wote huu baragumu zilikuwa zikipigwa.
and all the armed soldiers went ahead, the remainder of the common people followed the ark, and the sound of the trumpets grew louder everywhere.
10 Bali Yoshua alikuwa amewaagiza watu, “Msipige kelele ya vita, msipaze sauti zenu, wala kusema neno lolote mpaka siku ile nitakayowaambia mpige kelele. Ndipo mtapiga kelele!”
But Joshua had instructed the people, saying, “You shall not cry out, nor shall your voice be heard, and no word at all shall proceed from your mouth, until the day arrives on which I will say to you, ‘Cry out, and shout.’”
11 Basi akalipeleka Sanduku la Bwana kuzungushwa huo mji, likizungushwa mara moja. Kisha watu wakarudi kambini kulala.
Thus, the ark of the Lord circled the city once each day, and returning to the camp, it remained there.
12 Yoshua akaamka mapema asubuhi iliyofuata nao makuhani wakalichukua Sanduku la Bwana.
And so, with Joshua, arising in the night, the priests took the ark of the Lord,
13 Wale Makuhani saba wakizibeba zile baragumu saba wakatangulia mbele ya Sanduku la Bwana wakizipiga. Watu wenye silaha wakatangulia mbele yao na walinzi wa nyuma wakalifuata Sanduku la Bwana, huku baragumu hizo zikiendelea kulia.
and seven of them took the seven trumpets, which are used in the jubilee, and they preceded the ark of the Lord, walking and sounding the trumpets. And the armed men went before them, and the remainder of the common people followed the ark, and they were blaring the trumpets.
14 Siku ya pili wakauzunguka mji mara moja na kurudi kambini. Wakafanya hivi kwa siku sita.
And they circled the city on the second day, once, and they returned to the camp. They did so for six days.
15 Siku ya saba, wakaamka asubuhi na mapema wakauzunguka mji kama walivyokuwa wakifanya, isipokuwa siku ile waliuzunguka mji mara saba.
Then, on the seventh day, rising at first light, they circled the city, just as had been ordered, seven times.
16 Walipouzunguka mara ya saba, makuhani walipopiga baragumu kwa sauti kubwa, Yoshua akawaamuru watu akisema, “Pigeni kelele! Kwa maana Bwana amewapa mji huu!
And at the seventh circling, when the priests sounded the trumpets, Joshua said to all of Israel: “Shout! For the Lord has delivered the city to you.
17 Mji huu pamoja na vyote vilivyomo ndani yake utawekwa wakfu kwa Bwana. Ila Rahabu tu, yule kahaba na wote ambao wako pamoja naye nyumbani mwake ndio watakaosalimishwa, kwa sababu aliwaficha wale wapelelezi tuliowatuma.
And let this city be anathema, with all the things that are within it, before the Lord. May only Rahab the harlot live, with all who are with her in the house. For she hid the messengers whom we sent.
18 Lakini mjiepushe na vitu vilivyowekwa wakfu, msije mkachukua chochote katika hivyo, msije mkajiletea maangamizi katika maskani ya Israeli na kuiletea taabu.
But you must be careful that you do not touch any of those things, as you have been instructed, for then you would be guilty of transgression, and all the camp of Israel would be under sin and would be troubled.
19 Fedha yote na dhahabu, vyombo vya shaba na chuma ni vitakatifu kwa Bwana, lazima viletwe katika hazina yake.”
But whatever gold and silver there will be, and vessels of brass or of iron, let these be consecrated to the Lord and be stored in his treasuries.”
20 Wakati baragumu zilipopigwa, watu walipiga kelele, na katika sauti ya baragumu, na watu kupaza sauti, ukuta ukaanguka; hivyo kila mtu akapanda akiendelea mbele na kuuteka mji.
Therefore, with all the people shouting, and the trumpets blaring, after the voice and the sound increased in the ears of the multitude, the walls promptly fell to ruin. And each one climbed up at the place which was opposite where he was. And they seized the city.
21 Wakauweka mji wakfu kwa Bwana, na kila chenye uhai ndani yake walikiangamiza kwa upanga, wanaume kwa wanawake, vijana kwa wazee, ngʼombe, kondoo na punda.
And they put to death all who were in it, from man even to woman, from infant even to elder. Likewise, the oxen and sheep and donkeys, they struck down with the edge of the sword.
22 Yoshua akawaambia wale watu wawili waliokuwa wameipeleleza nchi, “Nendeni nyumbani kwa yule kahaba, mleteni pamoja na wote waliomo nyumbani mwake, kulingana na kiapo chenu kwake.”
But Joshua said to the two men who had been sent to explore, “Enter the house of the harlot woman, and bring her out, and all the things that are hers, just as you assured her by oath.”
23 Basi wale vijana waliofanya upelelezi wakaenda kumleta Rahabu, baba yake na mama yake, na ndugu zake na watu wote waliokuwa pamoja naye. Wakaleta jamaa yake yote na kuwaweka mahali nje ya kambi ya Israeli.
And the youths entered, and they led out Rahab, and her parents, also her brothers, and all her goods and kindred, and they caused them to dwell outside the camp.
24 Kisha wakauchoma mji wote na kila kitu kilichokuwamo ndani yake. Lakini fedha, dhahabu, vyombo vya shaba na vya chuma wakaviweka katika hazina ya nyumba ya Bwana.
Then they set fire to the city and all the things that were within it, except the gold and silver, and the vessels of brass or of iron, which they consecrated into the treasury of the Lord.
25 Lakini Yoshua akamhifadhi Rahabu yule kahaba, jamaa yake yote na wote waliokuwa wa kwake, kwa sababu aliwaficha watu waliotumwa na Yoshua kuipeleleza Yeriko, naye anaishi miongoni mwa Waisraeli hata leo.
Yet truly, Joshua caused Rahab the harlot, and her father’s household, and all she had, to survive. And they lived in the midst of Israel, even to the present day. For she hid the messengers, whom he had sent to explore Jericho. At that time, Joshua made an invocation, saying:
26 Wakati ule Yoshua akatamka kiapo hiki akasema, “Aliyelaaniwa mbele za Bwana ni mtu atakayeinuka kuujenga tena mji huu wa Yeriko: “Kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza wa kiume ataiweka misingi yake; kwa gharama ya mtoto wake wa mwisho atayaweka malango yake.”
“Cursed before the Lord is the man who will raise up and rebuild the city of Jericho! With his firstborn, may he lay its foundation, and with the last of his children, may he set up its gates.”
27 Hivyo Bwana alikuwa pamoja na Yoshua, na sifa zake zikaenea katika nchi yote.
And so the Lord was with Joshua, and his name was made known throughout all the land.