< Yoshua 5 >

1 Basi wafalme wote wa Waamori magharibi ya Yordani na wafalme wote wa Kanaani waliokuwa kwenye pwani waliposikia jinsi Bwana alivyoukausha Mto Yordani mbele ya Waisraeli hata tulipokwisha kuvuka, mioyo yao ikayeyuka kwa hofu, wala hawakuwa na ujasiri kuwakabili Waisraeli.
Quand donc tous les rois des Amorrhéens qui habitaient au-delà du Jourdain, vers le côté occidental, et tous les rois de Chanaan qui possédaient les lieux voisins de la grande mer, apprirent que le Seigneur avait séché le cours du Jourdain devant les enfants d’Israël, jusqu’à ce qu’ils eussent passé, leur cœur défaillit, et le courage les abandonna, parce qu’ils craignaient l’entrée des enfants d’Israël.
2 Wakati huo Bwana akamwambia Yoshua, “Tengeneza visu vya mawe magumu sana na uwatahiri Waisraeli tena.”
Alors le Seigneur dit à Josué: Fais-toi des couteaux de pierre, et circoncis pour la seconde fois les enfants d’Israël.
3 Kwa hiyo Yoshua akatengeneza visu vya mawe magumu sana na kutahiri Waisraeli huko Gibeath-Haaralothi.
Il fit ce qu’avait commandé le Seigneur, et il circoncit les enfants d’Israël sur la colline de la circoncision.
4 Hii ndiyo sababu ya Yoshua kufanya hivyo: Wanaume wote waliotoka Misri, wote wenye umri wa kwenda vitani, walikufa jangwani wakiwa njiani baada ya kuondoka Misri.
Or voici la cause de la seconde circoncision: Tous les mâles d’entre le peuple, qui sortirent de l’Egypte, tous hommes de guerre, moururent dans le désert pendant les très longs détours du chemin;
5 Watu wote waliotoka Misri walikuwa wametahiriwa, lakini watu wote waliozaliwa jangwani wakiwa safarini toka Misri walikuwa hawajatahiriwa.
Et ils avaient été tous circoncis; mais le peuple qui naquit dans le désert
6 Waisraeli walitembea jangwani miaka arobaini mpaka wanaume wote wale waliokuwa na umri wa kwenda vitani wakati waliondoka Misri walipokwisha kufa, kwa kuwa hawakumtii Bwana. Kwa maana Bwana alikuwa amewaapia kuwa wasingeweza kuona nchi ambayo alikuwa amewaahidi baba zao katika kuapa kutupatia, nchi inayotiririka maziwa na asali.
Pendant quarante années de marche dans cette très vaste solitude, fut incirconcis, jusqu’à ce que fussent consumés ceux qui n’avaient pas écouté la voix du Seigneur, et à qui auparavant il avait juré qu’il ne leur montrerait pas la terre où coulent du lait et du miel.
7 Kwa hiyo akawainua wana wao baada yao na hawa ndio hao ambao Yoshua aliwatahiri. Walikuwa hawajatahiriwa bado kwa sababu walikuwa safarini.
Les fils de ceux-ci succédèrent à leurs pères, et furent circoncis par Josué, parce qu’ils étaient incirconcis, comme ils étaient nés, et que pendant le chemin personne ne les avait circoncis.
8 Baada ya taifa lote kutahiriwa, waliendelea kukaa kambini mpaka walipokuwa wamepona.
Mais après qu’ils furent tous circoncis, ils demeurèrent campés dans le même lieu, jusqu’à ce qu’ils fussent guéris.
9 Bwana akamwambia Yoshua, “Leo nimeiondoa aibu ya Wamisri kutoka kwenu.” Basi mahali pale pakaitwa Gilgali hadi leo.
Alors le Seigneur dit à Josué: Aujourd’hui, j’ai ôté l’opprobre de l’Egypte de dessus vous. Et ce lieu a été appelé du nom de Galgala jusqu’au présent jour.
10 Jioni ya siku ya kumi na nne ya mwezi, wakiwa kambini huko Gilgali katika tambarare za Yeriko, Waisraeli wakaadhimisha Pasaka.
Et les enfants d’Israël demeurèrent à Galgala, et firent la Pâque, au quatorzième jour du mois, vers le soir, dans les plaines de Jéricho.
11 Siku iliyofuata Pasaka, katika siku ile ile, wakala mazao ya nchi, mikate isiyotiwa chachu na nafaka za kukaanga.
Et ils mangèrent des fruits de la terre le jour suivant, des pains azymes et de la farine séchée au feu de la même année.
12 Mana ilikoma siku iliyofuata baada ya Waisraeli kula chakula kilichotoka katika nchi; hapakuwa na mana tena kwa ajili ya Waisraeli, ila mwaka huo walikula mazao ya nchi ya Kanaani.
Et la manne cessa après qu’ils eurent mangé des fruits de la terre, et les enfants d’Israël n’usèrent plus de cette nourriture, mais ils mangèrent des fruits de la terre de Chanaan de la présente année.
13 Basi wakati Yoshua alipokuwa karibu na Yeriko, akainua macho, akaona mtu aliyesimama mbele yake, akiwa na upanga mkononi uliofutwa kwenye ala. Yoshua akamwendea na kumuuliza, “Je, wewe uko upande wetu au upande wa adui zetu?”
Or, comme Josué était dans la campagne de la ville de Jéricho, il leva les yeux et vit un homme debout en face de lui, tenant un glaive nu; et il alla vers lui, et dit: Es-tu des nôtres ou de nos ennemis?
14 Akajibu, “La, siko upande wowote, lakini mimi nimekuja nikiwa jemadari wa jeshi la Bwana.” Yoshua akaanguka kifudifudi hadi chini, akasujudu, akamuuliza, “Je, Bwana, una ujumbe gani kwa mtumishi wako?”
Il répondit: Nullement, mais je suis le prince de l’armée du Seigneur, et maintenant je viens. Josué tomba incliné vers la terre. Et, adorant, il dit: Que dit mon Seigneur à son serviteur?
15 Jemadari wa jeshi la Bwana akajibu, “Vua viatu vyako, kwa maana mahali hapa unaposimama ni patakatifu.” Naye Yoshua akafanya hivyo.
Ôte, dit-il, ta chaussure de tes pieds; car le lieu dans lequel tu es est saint. Et Josué fit comme il lui avait été commandé.

< Yoshua 5 >