< Yoshua 5 >
1 Basi wafalme wote wa Waamori magharibi ya Yordani na wafalme wote wa Kanaani waliokuwa kwenye pwani waliposikia jinsi Bwana alivyoukausha Mto Yordani mbele ya Waisraeli hata tulipokwisha kuvuka, mioyo yao ikayeyuka kwa hofu, wala hawakuwa na ujasiri kuwakabili Waisraeli.
And it came to pass, when all the kings of the Amorites who were over the Jordan westward, and all the kings of the Canaanites who were by the sea, heard how that Yahweh had dried up the waters of the Jordan, from before the sons of Israel, until they had passed over, that their heart melted, and there was no spirit in them any more, because of the sons of Israel.
2 Wakati huo Bwana akamwambia Yoshua, “Tengeneza visu vya mawe magumu sana na uwatahiri Waisraeli tena.”
At that time, said Yahweh unto Joshua, Make thee knives of flint, —and again circumcise the sons of Israel, a second time.
3 Kwa hiyo Yoshua akatengeneza visu vya mawe magumu sana na kutahiri Waisraeli huko Gibeath-Haaralothi.
So Joshua made him knives of flint, —and circumcised the sons of Israel, at the Hill of Foreskins.
4 Hii ndiyo sababu ya Yoshua kufanya hivyo: Wanaume wote waliotoka Misri, wote wenye umri wa kwenda vitani, walikufa jangwani wakiwa njiani baada ya kuondoka Misri.
Now, this, is the cause why Joshua did circumcise, —all the people who came forth out of Egypt, who were males, all the men of war, died in the desert, by the way, after they came forth out of Egypt.
5 Watu wote waliotoka Misri walikuwa wametahiriwa, lakini watu wote waliozaliwa jangwani wakiwa safarini toka Misri walikuwa hawajatahiriwa.
For, though all the people who came forth had been circumcised, yet, all the people who were born in the desert by the way, after they came forth out of Egypt, had they not circumcised.
6 Waisraeli walitembea jangwani miaka arobaini mpaka wanaume wote wale waliokuwa na umri wa kwenda vitani wakati waliondoka Misri walipokwisha kufa, kwa kuwa hawakumtii Bwana. Kwa maana Bwana alikuwa amewaapia kuwa wasingeweza kuona nchi ambayo alikuwa amewaahidi baba zao katika kuapa kutupatia, nchi inayotiririka maziwa na asali.
Because, for forty years, did the sons of Israel journey in the desert, until all the nation who were men of war, who came forth out of Egypt, were consumed, because they hearkened not unto the voice of Yahweh, —unto whom Yahweh sware that he would not let them see the land, which Yahweh sware unto their fathers, that he would give unto us, a land flowing with milk and honey.
7 Kwa hiyo akawainua wana wao baada yao na hawa ndio hao ambao Yoshua aliwatahiri. Walikuwa hawajatahiriwa bado kwa sababu walikuwa safarini.
Their sons, therefore, whom he had raised up in their stead, them, did Joshua circumcise, —for, uncircumcised, they were, in that they had not circumcised them by the way.
8 Baada ya taifa lote kutahiriwa, waliendelea kukaa kambini mpaka walipokuwa wamepona.
And so it came to pass, when they had made an end of circumcising all the nation, they remained in their place, in the camp, until they were healed.
9 Bwana akamwambia Yoshua, “Leo nimeiondoa aibu ya Wamisri kutoka kwenu.” Basi mahali pale pakaitwa Gilgali hadi leo.
Then said Yahweh unto Joshua, To-day, have I rolled away the reproach of Egypt from off you. Wherefore the name of that place is called Gilgal ["a rolling away"]unto this day.
10 Jioni ya siku ya kumi na nne ya mwezi, wakiwa kambini huko Gilgali katika tambarare za Yeriko, Waisraeli wakaadhimisha Pasaka.
Thus then the sons of Israel encamped in Gilgal, —and kept the passover on the fourteenth day of the month, in the evening, in the waste plains of Jericho.
11 Siku iliyofuata Pasaka, katika siku ile ile, wakala mazao ya nchi, mikate isiyotiwa chachu na nafaka za kukaanga.
And they did eat of the corn of the land, on the morrow of the passover, unleavened cakes and parched ears of corn, —on this selfsame day.
12 Mana ilikoma siku iliyofuata baada ya Waisraeli kula chakula kilichotoka katika nchi; hapakuwa na mana tena kwa ajili ya Waisraeli, ila mwaka huo walikula mazao ya nchi ya Kanaani.
And the manna ceased on the morrow, when they had eaten of the corn of the land, neither had the sons of Israel manna any more, —so they did eat of the yield of the land of Canaan throughout that year.
13 Basi wakati Yoshua alipokuwa karibu na Yeriko, akainua macho, akaona mtu aliyesimama mbele yake, akiwa na upanga mkononi uliofutwa kwenye ala. Yoshua akamwendea na kumuuliza, “Je, wewe uko upande wetu au upande wa adui zetu?”
And it came to pass, while Joshua was at Jericho, that he lifted up his eyes, and looked, and lo! a man standing over against him, with his sword drawn, in his hand, —so Joshua went unto him, and said to him, For us, art thou, or for our adversaries?
14 Akajibu, “La, siko upande wowote, lakini mimi nimekuja nikiwa jemadari wa jeshi la Bwana.” Yoshua akaanguka kifudifudi hadi chini, akasujudu, akamuuliza, “Je, Bwana, una ujumbe gani kwa mtumishi wako?”
And he said—Nay, but, I, as prince of the host of Yahweh, have, now, come. So Joshua fell on his face to the earth, and worshipped, and said unto him, What is my lord speaking unto his servant?
15 Jemadari wa jeshi la Bwana akajibu, “Vua viatu vyako, kwa maana mahali hapa unaposimama ni patakatifu.” Naye Yoshua akafanya hivyo.
Then said the prince of the host of Yahweh unto Joshua—Slip off thy sandals from thy feet, for, as for the place whereon thou art standing, holy, it is. And Joshua did so.