< Yoshua 4 >

1 Wakati taifa lote lilipokwisha kuvuka Mto Yordani, Bwana akamwambia Yoshua,
Pripetilo se je, ko je vse ljudstvo dokončalo prehod čez Jordan, da je Gospod spregovoril Józuetu, rekoč:
2 “Chagua watu kumi na wawili miongoni mwa watu, kila kabila mtu mmoja,
»Vzemi dvanajst mož izmed ljudstva, iz vsakega rodu moža
3 nawe uwaambie wachukue mawe kumi na mawili katikati ya Mto Yordani, palepale makuhani waliposimama, wayachukue na kuyaweka mahali mtakapokaa usiku huu wa leo.”
in jim zapovej, rekoč: ›Iz srede Jordana, iz kraja, kjer so trdno stala stopala duhovnikov, vzemite dvanajst kamnov in odnesli jih boste s seboj prek [Jordana] in jih pustili na kraju za nastanitev, kjer boste to noč prenočili.‹«
4 Basi Yoshua akawaita watu kumi na wawili ambao alikuwa amewachagua kutoka miongoni mwa Waisraeli, mtu mmoja kutoka kila kabila,
Potem je Józue poklical dvanajst mož, ki jih je postavil izmed Izraelovih otrok, iz vsakega rodu moža
5 naye akawaambia, “Mtangulie mbele ya Sanduku la Bwana Mungu wenu, mwende katikati ya Mto Yordani. Kila mmoja wenu atainua jiwe begani mwake, kufuatana na hesabu ya makabila ya Waisraeli,
in Józue jim je rekel: »Pojdite čez pred skrinjo Gospoda, svojega Boga, v sredo Jordana in vsak izmed vas naj na svojo ramo vzame kamen, glede na število rodov Izraelovih otrok,
6 kuwa kama ishara katikati yenu. Siku zijazo, wakati watoto wenu watakapowauliza, ‘Ni nini maana ya mawe haya?’
da bo to lahko znamenje med vami, da ko vaši otroci vprašajo svoje starše, v času, ki pride, rekoč: ›Kaj mislite s temi kamni?‹
7 waambieni kwamba maji ya Mto Yordani yaliyokuwa yakitiririka yalitindika mbele ya Sanduku la Agano la Bwana. Wakati lilipovuka Yordani, maji ya Yordani yalitindika. Mawe haya yatakuwa kumbukumbu kwa watu wa Israeli milele.”
Potem jim boste odgovorili: ›Da so bile vode Jordana odrezane pred skrinjo Gospodove zaveze. Ko je ta šla čez Jordan, so bile jordanske vode odsekane in ti kamni bodo Izraelovim otrokom v spomin na veke.‹«
8 Hivyo Waisraeli wakafanya kama Yoshua alivyowaagiza. Wakachukua mawe kumi na mawili kutoka katikati ya Mto Yordani, kulingana na hesabu ya kabila za Waisraeli kama Bwana alivyomwambia Yoshua, nao wakayabeba hadi kambini mwao, mahali walipoyatua chini.
Izraelovi otroci so storili, kakor je Józue zapovedal in iz srede Jordana vzeli dvanajst kamnov, kakor je Gospod govoril Józuetu, glede na število rodov Izraelovih otrok in jih s seboj odnesli preko [Jordana] na kraj, kjer so prenočili in tam so jih odložili.
9 Yoshua akayasimamisha yale mawe kumi na mawili ambayo yalikuwa katikati ya Mto Yordani, mahali pale ambapo miguu ya makuhani waliobeba Sanduku la Agano iliposimama. Nayo yako huko mpaka leo.
Józue je dvanajst kamnov postavil v sredo Jordana, na kraj, kjer so stala stopala duhovnikov, ki so nosili skrinjo zaveze in tam so do današnjega dne.
10 Makuhani waliobeba lile Sanduku walibakia wakiwa wamesimama katikati ya Mto Yordani mpaka kila kitu Bwana alichomwamuru Yoshua kilipokuwa kimefanywa na watu, sawasawa na vile Mose alivyokuwa amemwamuru Yoshua. Watu wakafanya haraka kuvuka,
Kajti duhovniki, ki so nosili skrinjo, so stali v sredi Jordana, dokler ni bila končana vsaka stvar, ki jo je Gospod zapovedal Józuetu, da spregovori ljudstvu, glede na vse, kar je Mojzes zapovedal Józuetu in ljudstvo je pohitelo in šlo čez.
11 na mara tu watu wote walipokwisha kuvuka, Sanduku la Bwana na makuhani wakavuka watu wakiwa wanatazama.
Pripetilo se je, ko je vse ljudstvo dokončalo prehod čez [Jordan], da je šla čez skrinja in duhovniki v prisotnosti ljudstva.
12 Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase wakavuka mbele ya Waisraeli, wakiwa wamevaa silaha, kama Mose alivyowaamuru.
Rubenovi otroci, Gadovi otroci in polovica Manásejevega rodu so oboroženi šli čez pred Izraelovimi otroki, kakor jim je govoril Mojzes.
13 Kiasi cha watu 40,000 waliojiandaa kwa vita walivuka mbele za Bwana hadi nchi tambarare za Yeriko kwa ajili ya vita.
Okoli štirideset tisoč pripravljenih za vojno je šlo čez pred Gospodom v bitko k ravninam Jerihe.
14 Siku ile Bwana akamtukuza Yoshua mbele ya Israeli yote, nao wakamheshimu siku zote za maisha yake, kama vile walivyomheshimu Mose.
Na ta dan je Gospod poveličal Józueta v očeh vsega Izraela in oni so se ga bali, kakor so se bali Mojzesa, vse dni njegovega življenja.
15 Basi Bwana akamwambia Yoshua,
Gospod je spregovoril Józuetu, rekoč:
16 “Waamuru hao makuhani wanaolibeba Sanduku la Ushuhuda, wapande kutoka ndani ya Mto Yordani.”
»Zapovej duhovnikom, ki nosijo skrinjo pričevanja, da pridejo gor, ven iz Jordana.«
17 Kwa hiyo Yoshua akawaamuru hao makuhani akisema, “Pandeni kutoka ndani ya Mto Yordani.”
Józue je torej zapovedal duhovnikom, rekoč: »Pridite gor iz Jordana.«
18 Nao makuhani wakapanda kutoka ndani ya Mto Yordani wakilibeba hilo Sanduku la Agano la Bwana. Mara tu walipoiweka miguu yao penye kingo, nje ya mto, maji ya Yordani yakarudi kufurika kama ilivyokuwa kabla.
Pripetilo se je, ko so duhovniki, ki so nosili skrinjo Gospodove zaveze, prišli gor iz srede Jordana in so bili podplati duhovniških stopal dvignjeni na suho zemljo, da so se vode Jordana vrnile na svoj kraj in stekle čez vse svoje bregove, kakor so počele poprej.
19 Siku ya kumi ya mwezi wa kwanza watu walipanda kutoka Yordani na kupiga kambi huko Gilgali, kwenye mpaka wa mashariki ya Yeriko.
In ljudstvo je prišlo gor iz Jordana na deseti dan prvega meseca ter se utaborilo v Gilgálu, na vzhodni meji Jerihe.
20 Naye Yoshua akayasimamisha huko Gilgali yale mawe kumi na mawili ambayo walikuwa wameyachukua katikati ya Mto Yordani.
Tistih dvanajst kamnov, ki so jih vzeli iz Jordana, je Józue postavil v Gilgálu.
21 Akawaambia Waisraeli, “Wazao wenu watakapowauliza baba zao siku zijazo wakisema, ‘Mawe haya maana yake ni nini?’
Izraelovim otrokom je spregovoril, rekoč: »Ko bodo vaši otroci vprašali svoje očete, v času, ki pride, rekoč: ›Kaj pomenijo ti kamni?‹
22 Basi waambieni, ‘Israeli ilivukia mahali pakavu katika Mto Yordani.’
Potem boste svojim otrokom dali vedeti, rekoč: ›Izrael je po suhih tleh prešel preko tega Jordana.
23 Kwa maana Bwana Mungu wenu alikausha maji ya Yordani mbele yenu, hadi mlipomaliza kuvuka. Bwana Mungu wenu alifanya haya kwa Mto Yordani sawasawa na kile alichoifanyia Bahari ya Shamu wakati alipoikausha mbele yetu hadi tulipomaliza kuvuka.
Kajti Gospod, vaš Bog, je izpred vas posušil vode Jordana, dokler niste prešli čez, kakor je Gospod, vaš Bog, storil Rdečemu morju, ki ga je posušil pred nami, dokler nismo prešli čez,
24 Alifanya hivi ili kwamba mataifa yote ya dunia yapate kujua kuwa mkono wa Bwana ni wenye nguvu, na ili kwamba kila wakati mpate kumcha Bwana Mungu wenu.”
da bi vsa ljudstva zemlje lahko poznala Gospodovo roko, da je ta mogočna, da se boste lahko na veke bali Gospoda, svojega Boga.‹«

< Yoshua 4 >