< Yoshua 4 >

1 Wakati taifa lote lilipokwisha kuvuka Mto Yordani, Bwana akamwambia Yoshua,
بالکلیه گذشتند، خداوند یوشع را خطاب کرده، گفت:۱
2 “Chagua watu kumi na wawili miongoni mwa watu, kila kabila mtu mmoja,
«دوازده نفر از قوم، یعنی از هر سبطیک نفر را بگیرید.۲
3 nawe uwaambie wachukue mawe kumi na mawili katikati ya Mto Yordani, palepale makuhani waliposimama, wayachukue na kuyaweka mahali mtakapokaa usiku huu wa leo.”
و ایشان را امر فرموده، بگویید: از اینجا از میان اردن از جایی که پایهای کاهنان قایم ایستاده بود، دوازده سنگ بردارید، وآنها را با خود برده، در منزلی که امشب در آن فرود می‌آیید بنهید.»۳
4 Basi Yoshua akawaita watu kumi na wawili ambao alikuwa amewachagua kutoka miongoni mwa Waisraeli, mtu mmoja kutoka kila kabila,
پس یوشع آن دوازده مردرا که از بنی‌اسرائیل انتخاب کرده بود، یعنی از هرسبط یک نفر طلبید.۴
5 naye akawaambia, “Mtangulie mbele ya Sanduku la Bwana Mungu wenu, mwende katikati ya Mto Yordani. Kila mmoja wenu atainua jiwe begani mwake, kufuatana na hesabu ya makabila ya Waisraeli,
و یوشع به ایشان گفت: «پیش تابوت یهوه، خدای خود به میان اردن بروید، و هر کسی از شما یک سنگ موافق شماره اسباط بنی‌اسرائیل بر دوش خود بردارد.۵
6 kuwa kama ishara katikati yenu. Siku zijazo, wakati watoto wenu watakapowauliza, ‘Ni nini maana ya mawe haya?’
تا این در میان شما علامتی باشد هنگامی که پسران شمادر زمان آینده پرسیده، گویند که مقصود شما ازاین سنگها چیست؟۶
7 waambieni kwamba maji ya Mto Yordani yaliyokuwa yakitiririka yalitindika mbele ya Sanduku la Agano la Bwana. Wakati lilipovuka Yordani, maji ya Yordani yalitindika. Mawe haya yatakuwa kumbukumbu kwa watu wa Israeli milele.”
آنگاه به ایشان بگویید: که آبهای اردن از حضور تابوت عهد خداوندشکافته شد، یعنی هنگامی که آن از اردن می گذشت، آبهای اردن شکافته شد، پس این سنگها به جهت بنی‌اسرائیل برای یادگاری ابدی خواهد بود.»۷
8 Hivyo Waisraeli wakafanya kama Yoshua alivyowaagiza. Wakachukua mawe kumi na mawili kutoka katikati ya Mto Yordani, kulingana na hesabu ya kabila za Waisraeli kama Bwana alivyomwambia Yoshua, nao wakayabeba hadi kambini mwao, mahali walipoyatua chini.
و بنی‌اسرائیل موافق آنچه یوشع امر فرموده بود کردند، و دوازده سنگ از میان اردن به طوری که خداوند به یوشع گفته بود، موافق شماره اسباط بنی‌اسرائیل برداشتند، و آنها را با خود به‌جایی که در آن منزل گرفتند برده، آنها را در آنجانهادند.۸
9 Yoshua akayasimamisha yale mawe kumi na mawili ambayo yalikuwa katikati ya Mto Yordani, mahali pale ambapo miguu ya makuhani waliobeba Sanduku la Agano iliposimama. Nayo yako huko mpaka leo.
و یوشع در وسط اردن، در جایی که پایهای کاهنانی که تابوت عهد را برداشته بودند، ایستاده بود، دوازده سنگ نصب کرد و در آنجا تاامروز هست.۹
10 Makuhani waliobeba lile Sanduku walibakia wakiwa wamesimama katikati ya Mto Yordani mpaka kila kitu Bwana alichomwamuru Yoshua kilipokuwa kimefanywa na watu, sawasawa na vile Mose alivyokuwa amemwamuru Yoshua. Watu wakafanya haraka kuvuka,
و کاهنانی که تابوت را برمی داشتند دروسط اردن ایستادند، تا هر‌آنچه خداوند یوشع راامر فرموده بود که به قوم بگوید تمام شد، به حسب آنچه موسی به یوشع امر کرده بود و قوم به تعجیل عبور کردند.۱۰
11 na mara tu watu wote walipokwisha kuvuka, Sanduku la Bwana na makuhani wakavuka watu wakiwa wanatazama.
و بعد از آنکه تمامی قوم بالکل گذشتند، واقع شد که تابوت خداوند وکاهنان به حضور قوم عبور کردند.۱۱
12 Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase wakavuka mbele ya Waisraeli, wakiwa wamevaa silaha, kama Mose alivyowaamuru.
و بنی روبین و بنی جاد و نصف سبط منسی مسلح شده، پیش روی بنی‌اسرائیل عبور کردند چنانکه موسی به ایشان گفته بود.۱۲
13 Kiasi cha watu 40,000 waliojiandaa kwa vita walivuka mbele za Bwana hadi nchi tambarare za Yeriko kwa ajili ya vita.
قریب به چهل هزار نفر مهیاشده کارزار به حضور خداوند به صحرای اریحابرای جنگ عبور کردند.۱۳
14 Siku ile Bwana akamtukuza Yoshua mbele ya Israeli yote, nao wakamheshimu siku zote za maisha yake, kama vile walivyomheshimu Mose.
و در آن روز خداوند، یوشع را در نظرتمامی اسرائیل بزرگ ساخت، و از او در تمام ایام عمرش می‌ترسیدند، چنانکه از موسی ترسیده بودند.۱۴
15 Basi Bwana akamwambia Yoshua,
و خداوند یوشع را خطاب کرده، گفت:۱۵
16 “Waamuru hao makuhani wanaolibeba Sanduku la Ushuhuda, wapande kutoka ndani ya Mto Yordani.”
«کاهنانی را که تابوت شهادت را برمی دارند، بفرما که از اردن برآیند.»۱۶
17 Kwa hiyo Yoshua akawaamuru hao makuhani akisema, “Pandeni kutoka ndani ya Mto Yordani.”
پس یوشع کاهنان راامر فرموده، گفت: «از اردن برآیید.»۱۷
18 Nao makuhani wakapanda kutoka ndani ya Mto Yordani wakilibeba hilo Sanduku la Agano la Bwana. Mara tu walipoiweka miguu yao penye kingo, nje ya mto, maji ya Yordani yakarudi kufurika kama ilivyokuwa kabla.
و چون کاهنانی که تابوت عهد خداوند را برمی داشتند ازمیان اردن برآمدند و کف پایهای کاهنان برخشکی گذارده شد، آنگاه آب اردن بجای خودبرگشت و مثل پیش بر تمامی کناره هایش جاری شد.۱۸
19 Siku ya kumi ya mwezi wa kwanza watu walipanda kutoka Yordani na kupiga kambi huko Gilgali, kwenye mpaka wa mashariki ya Yeriko.
و در روز دهم از ماه اول، قوم از اردن برآمدند و در جلجال به‌جانب شرقی اریحا اردوزدند.۱۹
20 Naye Yoshua akayasimamisha huko Gilgali yale mawe kumi na mawili ambayo walikuwa wameyachukua katikati ya Mto Yordani.
و یوشع آن دوازده سنگ را که از اردن گرفته بودند، در جلجال نصب کرد.۲۰
21 Akawaambia Waisraeli, “Wazao wenu watakapowauliza baba zao siku zijazo wakisema, ‘Mawe haya maana yake ni nini?’
وبنی‌اسرائیل را خطاب کرده، گفت: «چون پسران شما در زمان آینده از پدران خود پرسیده، گویند: که این سنگها چیست؟۲۱
22 Basi waambieni, ‘Israeli ilivukia mahali pakavu katika Mto Yordani.’
آنگاه پسران خود راتعلیم داده، گویید که اسرائیل از این اردن به خشکی عبور کردند.۲۲
23 Kwa maana Bwana Mungu wenu alikausha maji ya Yordani mbele yenu, hadi mlipomaliza kuvuka. Bwana Mungu wenu alifanya haya kwa Mto Yordani sawasawa na kile alichoifanyia Bahari ya Shamu wakati alipoikausha mbele yetu hadi tulipomaliza kuvuka.
زیرا یهوه، خدای شما، آب اردن را از پیش روی شما خشکانید تا شماعبور کردید، چنانکه یهوه خدای شما به بحرقلزم کرد که آن را پیش روی ما خشکانید تا ماعبور کردیم.۲۳
24 Alifanya hivi ili kwamba mataifa yote ya dunia yapate kujua kuwa mkono wa Bwana ni wenye nguvu, na ili kwamba kila wakati mpate kumcha Bwana Mungu wenu.”
تا تمامی قومهای زمین دست خداوند را بدانند که آن زورآور است، و از یهوه، خدای شما، همه اوقات بترسند.»۲۴

< Yoshua 4 >