< Yoshua 4 >

1 Wakati taifa lote lilipokwisha kuvuka Mto Yordani, Bwana akamwambia Yoshua,
Or il arriva que quand tout le peuple eut achevé de passer le Jourdain, parce que l'Eternel avait parlé à Josué; [et lui avait] dit:
2 “Chagua watu kumi na wawili miongoni mwa watu, kila kabila mtu mmoja,
Prenez du peuple douze hommes, [savoir] un homme de chaque Tribu;
3 nawe uwaambie wachukue mawe kumi na mawili katikati ya Mto Yordani, palepale makuhani waliposimama, wayachukue na kuyaweka mahali mtakapokaa usiku huu wa leo.”
Et leur commandez, en disant: Prenez d'ici du milieu du Jourdain, du lieu où les Sacrificateurs s'arrêtent [de pied] ferme, douze pierres, que vous emporterez avec vous, et vous les poserez au lieu où vous logerez cette nuit.
4 Basi Yoshua akawaita watu kumi na wawili ambao alikuwa amewachagua kutoka miongoni mwa Waisraeli, mtu mmoja kutoka kila kabila,
Josué appela les douze hommes qu'il avait ordonnés d'entre les enfants d'Israël, un homme de chaque Tribu;
5 naye akawaambia, “Mtangulie mbele ya Sanduku la Bwana Mungu wenu, mwende katikati ya Mto Yordani. Kila mmoja wenu atainua jiwe begani mwake, kufuatana na hesabu ya makabila ya Waisraeli,
Et il leur dit: Passez devant l'Arche de l'Eternel votre Dieu, au milieu du Jourdain, et que chacun de vous lève une pierre sur son épaule, selon le nombre des Tribus des enfants d'Israël;
6 kuwa kama ishara katikati yenu. Siku zijazo, wakati watoto wenu watakapowauliza, ‘Ni nini maana ya mawe haya?’
Afin que cela soit un signe parmi vous; [et] quand vos enfants interrogeront à l'avenir leurs pères, en disant: Que signifient ces pierres-ci?
7 waambieni kwamba maji ya Mto Yordani yaliyokuwa yakitiririka yalitindika mbele ya Sanduku la Agano la Bwana. Wakati lilipovuka Yordani, maji ya Yordani yalitindika. Mawe haya yatakuwa kumbukumbu kwa watu wa Israeli milele.”
Alors vous leur répondrez que les eaux du Jourdain ont été suspendues devant l'Arche de l'alliance de l'Eternel, que les eaux, [dis-je], du Jourdain ont été arrêtées quand elle passa le Jourdain; c'est pourquoi ces pierres-là serviront de mémorial aux enfants d'Israël à jamais.
8 Hivyo Waisraeli wakafanya kama Yoshua alivyowaagiza. Wakachukua mawe kumi na mawili kutoka katikati ya Mto Yordani, kulingana na hesabu ya kabila za Waisraeli kama Bwana alivyomwambia Yoshua, nao wakayabeba hadi kambini mwao, mahali walipoyatua chini.
Les enfants d'Israël donc firent comme Josué avait commandé. Ils prirent douze pierres du milieu du Jourdain, ainsi que l'Eternel l'avait commandé à Josué, selon le nombre des Tribus des enfants d'Israël, ils les emportèrent avec eux au lieu où ils devaient loger, et les posèrent là.
9 Yoshua akayasimamisha yale mawe kumi na mawili ambayo yalikuwa katikati ya Mto Yordani, mahali pale ambapo miguu ya makuhani waliobeba Sanduku la Agano iliposimama. Nayo yako huko mpaka leo.
Josué aussi dressa douze pierres au milieu du Jourdain, au lieu où les pieds des Sacrificateurs qui portaient l'Arche de l'alliance s'étaient arrêtés; [et] elles y sont demeurées jusqu'à ce jour.
10 Makuhani waliobeba lile Sanduku walibakia wakiwa wamesimama katikati ya Mto Yordani mpaka kila kitu Bwana alichomwamuru Yoshua kilipokuwa kimefanywa na watu, sawasawa na vile Mose alivyokuwa amemwamuru Yoshua. Watu wakafanya haraka kuvuka,
Les Sacrificateurs donc qui portaient l'Arche, se tinrent debout au milieu du Jourdain, jusqu'à ce que tout ce que l'Eternel avait commandé à Josué de dire au peuple fût accompli, suivant toutes les choses que Moïse avait commandées à Josué; et le peuple se hâta de passer.
11 na mara tu watu wote walipokwisha kuvuka, Sanduku la Bwana na makuhani wakavuka watu wakiwa wanatazama.
Et quand tout le peuple eut achevé de passer, alors l'Arche de l'Eternel passa, et les Sacrificateurs devant le peuple.
12 Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase wakavuka mbele ya Waisraeli, wakiwa wamevaa silaha, kama Mose alivyowaamuru.
Et les enfants de Ruben, et les enfants de Gad, et la moitié de la Tribu de Manassé passèrent en armes devant les enfants d'Israël, comme Moïse leur avait dit.
13 Kiasi cha watu 40,000 waliojiandaa kwa vita walivuka mbele za Bwana hadi nchi tambarare za Yeriko kwa ajili ya vita.
Ils passèrent, [dis-je], vers les campagnes de Jérico environ quarante mille hommes en équipage de guerre, devant l'Eternel, pour combattre.
14 Siku ile Bwana akamtukuza Yoshua mbele ya Israeli yote, nao wakamheshimu siku zote za maisha yake, kama vile walivyomheshimu Mose.
En ce jour-là l'Eternel éleva Josué, à la vue de tout Israël, et ils le craignirent comme ils avaient craint Moïse, tous les jours de sa vie.
15 Basi Bwana akamwambia Yoshua,
Or l'Eternel avait parlé à Josué, en disant:
16 “Waamuru hao makuhani wanaolibeba Sanduku la Ushuhuda, wapande kutoka ndani ya Mto Yordani.”
Commande aux Sacrificateurs, qui portent l'Arche du Témoignage, qu'ils montent hors du Jourdain.
17 Kwa hiyo Yoshua akawaamuru hao makuhani akisema, “Pandeni kutoka ndani ya Mto Yordani.”
Et Josué avait commandé aux Sacrificateurs, en disant: Montez hors du Jourdain.
18 Nao makuhani wakapanda kutoka ndani ya Mto Yordani wakilibeba hilo Sanduku la Agano la Bwana. Mara tu walipoiweka miguu yao penye kingo, nje ya mto, maji ya Yordani yakarudi kufurika kama ilivyokuwa kabla.
Or sitôt que les Sacrificateurs, qui portaient l'Arche de l'alliance de l'Eternel, furent montés hors du milieu du Jourdain, et que les Sacrificateurs eurent mis sur le sec les plantes de leurs pieds, les eaux du Jourdain retournèrent en leur lieu, et coulèrent comme auparavant, par dessus tous les rivages.
19 Siku ya kumi ya mwezi wa kwanza watu walipanda kutoka Yordani na kupiga kambi huko Gilgali, kwenye mpaka wa mashariki ya Yeriko.
Le peuple donc monta hors du Jourdain le dixième jour du premier mois, et ils se campèrent en Guilgal, à l'Orient de Jérico.
20 Naye Yoshua akayasimamisha huko Gilgali yale mawe kumi na mawili ambayo walikuwa wameyachukua katikati ya Mto Yordani.
Josué aussi dressa en Guilgal ces douze pierres qu'ils avaient prises du Jourdain.
21 Akawaambia Waisraeli, “Wazao wenu watakapowauliza baba zao siku zijazo wakisema, ‘Mawe haya maana yake ni nini?’
Et il parla aux enfants d'Israël, et leur dit: Quand vos enfants interrogeront à l'avenir leurs pères, et leur diront: Que [signifient] ces pierres-ci?
22 Basi waambieni, ‘Israeli ilivukia mahali pakavu katika Mto Yordani.’
Vous l'apprendrez à vos enfants, en [leur] disant, Israël a passé ce Jourdain à sec.
23 Kwa maana Bwana Mungu wenu alikausha maji ya Yordani mbele yenu, hadi mlipomaliza kuvuka. Bwana Mungu wenu alifanya haya kwa Mto Yordani sawasawa na kile alichoifanyia Bahari ya Shamu wakati alipoikausha mbele yetu hadi tulipomaliza kuvuka.
Car l'Eternel votre Dieu fit tarir les eaux du Jourdain devant vous, jusqu'à ce que vous fussiez passés; comme l'Eternel votre Dieu avait fait à la mer Rouge, laquelle il mit à sec devant nous, jusqu'à ce que nous fussions passés.
24 Alifanya hivi ili kwamba mataifa yote ya dunia yapate kujua kuwa mkono wa Bwana ni wenye nguvu, na ili kwamba kila wakati mpate kumcha Bwana Mungu wenu.”
Afin que tous les peuples de la terre connaissent que la main de l'Eternel est forte; [et] afin que vous craigniez toujours l'Eternel votre Dieu.

< Yoshua 4 >