< Yoshua 4 >

1 Wakati taifa lote lilipokwisha kuvuka Mto Yordani, Bwana akamwambia Yoshua,
Lorsque toute la nation eut achevé de passer le Jourdain, Yahweh dit à Josué:
2 “Chagua watu kumi na wawili miongoni mwa watu, kila kabila mtu mmoja,
« Prenez douze hommes parmi le peuple, un homme par tribu,
3 nawe uwaambie wachukue mawe kumi na mawili katikati ya Mto Yordani, palepale makuhani waliposimama, wayachukue na kuyaweka mahali mtakapokaa usiku huu wa leo.”
et donnez-leur cet ordre: De ce lieu-ci, du milieu du Jourdain, de l'endroit où les prêtres se sont tenus de pied ferme, prenez douze pierres, transportez-les avec vous et déposez-les dans le lieu où vous camperez cette nuit. »
4 Basi Yoshua akawaita watu kumi na wawili ambao alikuwa amewachagua kutoka miongoni mwa Waisraeli, mtu mmoja kutoka kila kabila,
Josué appela les douze hommes qu'il avait choisis parmi les enfants d'Israël, un homme par tribu,
5 naye akawaambia, “Mtangulie mbele ya Sanduku la Bwana Mungu wenu, mwende katikati ya Mto Yordani. Kila mmoja wenu atainua jiwe begani mwake, kufuatana na hesabu ya makabila ya Waisraeli,
et il leur dit: « Passez devant l'arche de Yahweh, votre Dieu, au milieu du Jourdain, et que chacun de vous prenne une pierre sur son épaule, selon le nombre des tribus des enfants d'Israël,
6 kuwa kama ishara katikati yenu. Siku zijazo, wakati watoto wenu watakapowauliza, ‘Ni nini maana ya mawe haya?’
afin que ce soit un signe au milieu de vous. Lorsque vos enfants vous demanderont un jour: Que signifient pour vous ces pierres?
7 waambieni kwamba maji ya Mto Yordani yaliyokuwa yakitiririka yalitindika mbele ya Sanduku la Agano la Bwana. Wakati lilipovuka Yordani, maji ya Yordani yalitindika. Mawe haya yatakuwa kumbukumbu kwa watu wa Israeli milele.”
Vous leur direz: Les eaux du Jourdain ont été coupées devant l'arche de l'alliance de Yahweh; lorsqu'elle passa le Jourdain, les eaux du Jourdain furent coupées. Et ces pierres seront à jamais un mémorial pour les enfants d'Israël. »
8 Hivyo Waisraeli wakafanya kama Yoshua alivyowaagiza. Wakachukua mawe kumi na mawili kutoka katikati ya Mto Yordani, kulingana na hesabu ya kabila za Waisraeli kama Bwana alivyomwambia Yoshua, nao wakayabeba hadi kambini mwao, mahali walipoyatua chini.
Les enfants d'Israël firent comme Josué avait ordonné. Ils prirent douze pierres du milieu du Jourdain, comme Yahweh l'avait dit à Josué, selon le nombre des tribus des enfants d'Israël, et, les ayant emportées avec eux au lieu où ils devaient passer la nuit, ils les y déposèrent.
9 Yoshua akayasimamisha yale mawe kumi na mawili ambayo yalikuwa katikati ya Mto Yordani, mahali pale ambapo miguu ya makuhani waliobeba Sanduku la Agano iliposimama. Nayo yako huko mpaka leo.
Josué dressa douze pierres au milieu du Jourdain, à la place où s'étaient arrêtés les pieds des prêtres qui portaient l'arche de l'alliance; et elles y sont restées jusqu'à ce jour.
10 Makuhani waliobeba lile Sanduku walibakia wakiwa wamesimama katikati ya Mto Yordani mpaka kila kitu Bwana alichomwamuru Yoshua kilipokuwa kimefanywa na watu, sawasawa na vile Mose alivyokuwa amemwamuru Yoshua. Watu wakafanya haraka kuvuka,
Les prêtres qui portaient l'arche se tinrent au milieu du Jourdain jusqu'à l'entier accomplissement de ce que Yahweh avait ordonné à Josué de dire au peuple, selon tout ce que Moïse avait prescrit à Josué; et le peuple se hâta de passer.
11 na mara tu watu wote walipokwisha kuvuka, Sanduku la Bwana na makuhani wakavuka watu wakiwa wanatazama.
Lorsque tout le peuple eut achevé de passer, l'arche de Yahweh et les prêtres passèrent devant le peuple.
12 Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase wakavuka mbele ya Waisraeli, wakiwa wamevaa silaha, kama Mose alivyowaamuru.
Les fils de Ruben, les fils de Gad et la demi-tribu de Manassé passèrent en armes devant les enfants d'Israël, comme Moïse le leur avait dit.
13 Kiasi cha watu 40,000 waliojiandaa kwa vita walivuka mbele za Bwana hadi nchi tambarare za Yeriko kwa ajili ya vita.
Environ quarante mille hommes, armés pour le combat, passèrent devant Yahweh dans les plaines de Jéricho.
14 Siku ile Bwana akamtukuza Yoshua mbele ya Israeli yote, nao wakamheshimu siku zote za maisha yake, kama vile walivyomheshimu Mose.
En ce jour-là, Yahweh éleva Josué aux yeux de tout Israël, et ils le craignirent, comme ils avaient craint Moïse, tous les jours de sa vie.
15 Basi Bwana akamwambia Yoshua,
Yahweh parla à Josué en disant:
16 “Waamuru hao makuhani wanaolibeba Sanduku la Ushuhuda, wapande kutoka ndani ya Mto Yordani.”
« Ordonne aux prêtres qui portent l'arche du témoignage de sortir du Jourdain. »
17 Kwa hiyo Yoshua akawaamuru hao makuhani akisema, “Pandeni kutoka ndani ya Mto Yordani.”
Et Josué donna cet ordre aux prêtres: « Sortez du Jourdain. »
18 Nao makuhani wakapanda kutoka ndani ya Mto Yordani wakilibeba hilo Sanduku la Agano la Bwana. Mara tu walipoiweka miguu yao penye kingo, nje ya mto, maji ya Yordani yakarudi kufurika kama ilivyokuwa kabla.
Lorsque les prêtres qui portaient l'arche de l'alliance de Yahweh furent sortis du milieu du Jourdain, et que la plante de leur pied se posa sur la terre sèche, les eaux du fleuve retournèrent à leur place et se répandirent comme auparavant par-dessus toutes ses rives.
19 Siku ya kumi ya mwezi wa kwanza watu walipanda kutoka Yordani na kupiga kambi huko Gilgali, kwenye mpaka wa mashariki ya Yeriko.
Le peuple sortit du Jourdain le dixième jour du premier mois, et il campa à Galgala à l'extrémité orientale du territoire de Jéricho.
20 Naye Yoshua akayasimamisha huko Gilgali yale mawe kumi na mawili ambayo walikuwa wameyachukua katikati ya Mto Yordani.
Josué dressa à Galgala les douze pierres qu'ils avaient prises du Jourdain,
21 Akawaambia Waisraeli, “Wazao wenu watakapowauliza baba zao siku zijazo wakisema, ‘Mawe haya maana yake ni nini?’
et il dit aux enfants d'Israël: « Lorsque vos enfants demanderont un jour à leurs pères: Que signifient ces pierres?
22 Basi waambieni, ‘Israeli ilivukia mahali pakavu katika Mto Yordani.’
Vous en instruirez vos enfants, en disant: Israël a passé ce Jourdain à sec.
23 Kwa maana Bwana Mungu wenu alikausha maji ya Yordani mbele yenu, hadi mlipomaliza kuvuka. Bwana Mungu wenu alifanya haya kwa Mto Yordani sawasawa na kile alichoifanyia Bahari ya Shamu wakati alipoikausha mbele yetu hadi tulipomaliza kuvuka.
Car Yahweh, votre Dieu, a mis à sec devant vous les eaux du Jourdain jusqu'à ce que vous eussiez passé, comme Yahweh, votre Dieu, l'avait fait à la mer Rouge, qu'il mit à sec devant nous jusqu'à ce que nous eussions passé:
24 Alifanya hivi ili kwamba mataifa yote ya dunia yapate kujua kuwa mkono wa Bwana ni wenye nguvu, na ili kwamba kila wakati mpate kumcha Bwana Mungu wenu.”
afin que tous les peuples de la terre apprennent que la main de Yahweh est puissante, et afin que vous ayez toujours la crainte de Yahweh, votre Dieu. »

< Yoshua 4 >