< Yoshua 4 >

1 Wakati taifa lote lilipokwisha kuvuka Mto Yordani, Bwana akamwambia Yoshua,
I stalo se, když již všecken národ přešel Jordán, (nebo byl řekl Hospodin k Jozue, řka:
2 “Chagua watu kumi na wawili miongoni mwa watu, kila kabila mtu mmoja,
Vezměte sobě z lidu dvanácte mužů, po jednom muži z každého pokolení,
3 nawe uwaambie wachukue mawe kumi na mawili katikati ya Mto Yordani, palepale makuhani waliposimama, wayachukue na kuyaweka mahali mtakapokaa usiku huu wa leo.”
A přikažte jim, řkouce: Vezměte sobě odsud z prostřed Jordánu, s místa, na němž stály nohy kněžské nepohnutě, dvanácte kamenů, a vyneste je s sebou, a sklaďte v ležení, v kterémž přes tuto noc pozůstanete),
4 Basi Yoshua akawaita watu kumi na wawili ambao alikuwa amewachagua kutoka miongoni mwa Waisraeli, mtu mmoja kutoka kila kabila,
Že povolav Jozue dvanácti mužů, kteréž k tomu zřídil z synů Izraelských, po jednom muži z každého pokolení,
5 naye akawaambia, “Mtangulie mbele ya Sanduku la Bwana Mungu wenu, mwende katikati ya Mto Yordani. Kila mmoja wenu atainua jiwe begani mwake, kufuatana na hesabu ya makabila ya Waisraeli,
I řekl jim Jozue: Jděte před truhlou Hospodina Boha svého do prostřed Jordánu a vezměte sobě každý kámen jeden na rameno své, vedlé počtu pokolení synů Izraelských,
6 kuwa kama ishara katikati yenu. Siku zijazo, wakati watoto wenu watakapowauliza, ‘Ni nini maana ya mawe haya?’
Aby to bylo na znamení mezi vámi. Když by potom tázali se synové otců svých, řkouce: K čemu jsou vám ti kamenové?
7 waambieni kwamba maji ya Mto Yordani yaliyokuwa yakitiririka yalitindika mbele ya Sanduku la Agano la Bwana. Wakati lilipovuka Yordani, maji ya Yordani yalitindika. Mawe haya yatakuwa kumbukumbu kwa watu wa Israeli milele.”
Odpovíte jim, že se rozdělily vody Jordánské před truhlou smlouvy Hospodinovy, (když, pravím, šla přes Jordán, rozdělily se vody Jordánské), i zůstávají kamenové tito na památku synům Izraelským až na věky.
8 Hivyo Waisraeli wakafanya kama Yoshua alivyowaagiza. Wakachukua mawe kumi na mawili kutoka katikati ya Mto Yordani, kulingana na hesabu ya kabila za Waisraeli kama Bwana alivyomwambia Yoshua, nao wakayabeba hadi kambini mwao, mahali walipoyatua chini.
I učinili synové Izraelští tak, jakž přikázal Jozue, a vzali dvanácte kamenů z prostředku Jordánu, jakož mluvil Hospodin k Jozue, vedlé počtu pokolení synů Izraelských, a přinesli je s sebou na první stanoviště, a tu je složili.
9 Yoshua akayasimamisha yale mawe kumi na mawili ambayo yalikuwa katikati ya Mto Yordani, mahali pale ambapo miguu ya makuhani waliobeba Sanduku la Agano iliposimama. Nayo yako huko mpaka leo.
Jozue také vyzdvihl dvanácte kamenů u prostřed Jordánu na místě, kdež stály nohy kněží nesoucích truhlu smlouvy, a byli tam až do tohoto dne.
10 Makuhani waliobeba lile Sanduku walibakia wakiwa wamesimama katikati ya Mto Yordani mpaka kila kitu Bwana alichomwamuru Yoshua kilipokuwa kimefanywa na watu, sawasawa na vile Mose alivyokuwa amemwamuru Yoshua. Watu wakafanya haraka kuvuka,
Kněží pak, jenž nesli truhlu, stáli u prostřed Jordánu, dokudž se nevyplnilo všeliké slovo, kteréž přikázal Hospodin Jozue, aby oznámil lidu podlé všeho, jakž byl přikázal Mojžíš Jozue. I pospíšil lid a přešli.
11 na mara tu watu wote walipokwisha kuvuka, Sanduku la Bwana na makuhani wakavuka watu wakiwa wanatazama.
Když pak již přešel všecken lid, přešla také truhla Hospodinova i kněží, an lid na to hledí.
12 Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase wakavuka mbele ya Waisraeli, wakiwa wamevaa silaha, kama Mose alivyowaamuru.
Přešli i synové Rubenovi a synové Gádovi, a polovice pokolení Manassesova, vojensky zpořádaní před syny Izraelskými, jakož byl mluvil k nim Mojžíš.
13 Kiasi cha watu 40,000 waliojiandaa kwa vita walivuka mbele za Bwana hadi nchi tambarare za Yeriko kwa ajili ya vita.
Okolo čtyřidcíti tisíců oděných bojovníků šlo před Hospodinem k boji na roviny Jericha.
14 Siku ile Bwana akamtukuza Yoshua mbele ya Israeli yote, nao wakamheshimu siku zote za maisha yake, kama vile walivyomheshimu Mose.
V ten den zvelebil Hospodin Jozue před očima všeho Izraele. I báli se ho, jako se báli Mojžíše po všecky dny života jeho.
15 Basi Bwana akamwambia Yoshua,
Mluvil pak Hospodin k Jozue, řka:
16 “Waamuru hao makuhani wanaolibeba Sanduku la Ushuhuda, wapande kutoka ndani ya Mto Yordani.”
Přikaž kněžím, kteříž nesou truhlu svědectví, ať vystoupí z Jordánu.
17 Kwa hiyo Yoshua akawaamuru hao makuhani akisema, “Pandeni kutoka ndani ya Mto Yordani.”
I přikázal Jozue kněžím, řka: Vystupte z Jordánu.
18 Nao makuhani wakapanda kutoka ndani ya Mto Yordani wakilibeba hilo Sanduku la Agano la Bwana. Mara tu walipoiweka miguu yao penye kingo, nje ya mto, maji ya Yordani yakarudi kufurika kama ilivyokuwa kabla.
Když pak vystupovali kněží, jenž nesli truhlu smlouvy Hospodinovy, z prostřed Jordánu, jakž jen vytrhli kněží nohy na sucho, navrátily se vody Jordánské k místu svému, a tekly předce jako i prvé ve všech březích svých.
19 Siku ya kumi ya mwezi wa kwanza watu walipanda kutoka Yordani na kupiga kambi huko Gilgali, kwenye mpaka wa mashariki ya Yeriko.
Vyšed pak lid z Jordánu desátého dne měsíce prvního, položili se v Galgala k straně východní Jericha;
20 Naye Yoshua akayasimamisha huko Gilgali yale mawe kumi na mawili ambayo walikuwa wameyachukua katikati ya Mto Yordani.
A dvanácte kamenů těch, kteréž vynesli z Jordánu, postavil Jozue v Galgala.
21 Akawaambia Waisraeli, “Wazao wenu watakapowauliza baba zao siku zijazo wakisema, ‘Mawe haya maana yake ni nini?’
A mluvil k synům Izraelským takto: Když by se otázali potom synové vaši otců svých, řkouce: Co ti kamenové znamenají?
22 Basi waambieni, ‘Israeli ilivukia mahali pakavu katika Mto Yordani.’
Oznámíte synům svým a díte: Po suše přešel Izrael Jordán tento.
23 Kwa maana Bwana Mungu wenu alikausha maji ya Yordani mbele yenu, hadi mlipomaliza kuvuka. Bwana Mungu wenu alifanya haya kwa Mto Yordani sawasawa na kile alichoifanyia Bahari ya Shamu wakati alipoikausha mbele yetu hadi tulipomaliza kuvuka.
Nebo vysušil Hospodin Bůh váš vody Jordánské před tváří vaší, až jste přešli, jakož učinil Hospodin Bůh váš moři Rudému, kteréž vysušil před tváří naší, až jsme přešli,
24 Alifanya hivi ili kwamba mataifa yote ya dunia yapate kujua kuwa mkono wa Bwana ni wenye nguvu, na ili kwamba kila wakati mpate kumcha Bwana Mungu wenu.”
Aby poznali všickni národové země ruku Hospodinovu, že silná jest, a abyste se báli Hospodina Boha vašeho po všecky dny.

< Yoshua 4 >