< Yoshua 3 >

1 Yoshua na Waisraeli wote wakaondoka asubuhi na mapema kutoka Shitimu, wakaenda mpaka Mto Yordani, ambako walipiga kambi kabla ya kuvuka.
И воста заутра Иисус, и воздвигошася из Саттина, и приидоша до Иордана той и вси сынове Израилевы, и сташа тамо прежде неже прейти.
2 Baada ya siku tatu maafisa wakapita katika kambi yote,
И бысть по триех днех, проидоша книгочия чрез полк,
3 wakitoa maagizo kwa watu, wakiwaambia: “Mtakapoona Sanduku la Agano la Bwana Mungu wenu, likichukuliwa na Walawi ambao ndio makuhani, mtaondoka hapo mlipo na kulifuata.
и заповедаша людем, глаголюще: егда узрите кивот завета Господа Бога нашего, и жерцы нашя, и левиты воздвизающыя его, да воздвигнетеся и вы от мест ваших и пойдете вслед его:
4 Ndipo mtakapotambua njia mtakayoiendea, kwa kuwa hamjawahi kuipita kabla. Lakini msisogee karibu, bali kuwe na umbali wa dhiraa 2,000 kati yenu na Sanduku.”
но подалее да будет между вами и оным, елико две тысящы лакот станете: не приближитеся к нему, да увесте путь, по немуже пойдете: не ходисте бо путем тем ни вчера, ни третияго дне.
5 Ndipo Yoshua akawaambia hao watu, “Jitakaseni, kwa kuwa kesho Bwana atatenda mambo ya kushangaza katikati yenu.”
И рече Иисус к людем: очиститеся наутрие, яко заутра сотворит в вас Господь чудная.
6 Yoshua akawaambia makuhani, “Liinueni Sanduku la Agano mkatangulie mbele ya watu.” Hivyo wakaliinua na kutangulia mbele yao.
И рече Иисус к жерцем: воздвигните кивот завета Господня и предидите пред людьми. И взяша жерцы кивот завета Господня и идоша пред людьми.
7 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Leo nitaanza kukutukuza machoni pa Israeli yote, ili wapate kujua kuwa niko pamoja nawe kama nilivyokuwa pamoja na Mose.
И рече Господь ко Иисусу: в сей день начинаю возвышати тя пред всеми сынми Израилевыми, да уведят, якоже бех с Моисеом, тако буду и с тобою:
8 Uwaambie makuhani wanaochukua Sanduku la Agano, ‘Mnapofika kwenye ukingo wa maji ya Yordani, nendeni mkasimame ndani ya mto.’”
и ныне заповеждь жерцем воздвизающым кивот завета, глаголя: егда внидете на часть воды Иордана, и во Иордане станете.
9 Yoshua akawaambia Waisraeli, “Njooni hapa msikilize maneno ya Bwana Mungu wenu.
И рече Иисус сыном Израилевым: приступите семо, и слышите слово Господа Бога вашего:
10 Hivi ndivyo mtakavyojua ya kuwa Mungu aliye hai yupo katikati yenu, na kwamba kwa hakika atawafukuza mbele yenu hao Wakanaani, Wahiti, Wahivi, Waperizi, Wagirgashi, Waamori na Wayebusi.
в сих увесте, яко Господь живяй в вас и потребляяй потребит от лица вашего Хананеа и Хеттеа, и Ферезеа и Евеа, и Гергесеа и Аморреа и Иевусеа:
11 Tazameni, Sanduku la Agano la Bwana wa dunia yote litaingia ndani ya Mto Yordani likiwa limewatangulia.
се, кивот завета Господа всея земли преходит Иордан:
12 Sasa basi, chagueni watu kumi na wawili kutoka makabila ya Israeli, mtu mmoja kutoka kila kabila.
изберите себе дванадесять мужей от сынов Израилевых, единаго от коегождо племене,
13 Mara tu nyayo za makuhani walichukualo Sanduku la Bwana, Bwana wa dunia yote, zitakapokanyaga ndani ya Mto Yordani, maji hayo yatiririkayo kutoka juu yatatindika na kusimama kama chuguu.”
и будет егда почиют нози жерцев воздвизающих кивот завета Господа всея земли в воде Иордана, вода Иорданова оскудеет, вода же низтекущая станет.
14 Basi, watu walipovunja kambi ili kuvuka Yordani, makuhani wakiwa wamebeba Sanduku la Agano waliwatangulia.
И бысть егда воздвигнушася людие от кущ своих прейти Иордан, жерцы же воздвигоша кивот завета Господня пред людьми:
15 Wakati huu ulikuwa wakati wa mavuno, nao Mto Yordani ulikuwa umefurika hadi kwenye kingo zake. Ilikuwa kawaida ya Yordani kufurika nyakati zote za mavuno. Mara tu makuhani wale waliokuwa wamebeba Sanduku la Agano walipofika mtoni na nyayo zao kuzama ndani ya yale maji,
егда же внидоша жерцы воздвижуще кивот завета Господня во Иордан, и нози жерцев воздвизающих кивот завета Господня омочишася в части воды Иордана, Иордан же наполняшеся во вся краи своя, якоже во дни жатвы пшеницы:
16 maji hayo yaliyotiririka kutoka upande wa juu yaliacha kutiririka yakasimama kama chuguu mbali kabisa nao, kwenye mji ulioitwa Adamu kwenye eneo la Sarethani, wakati yale maji yaliyokuwa yanatiririka kuingia kwenye Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), yalitindika kabisa. Hivyo watu wakavuka kukabili Yeriko.
и сташа воды текущыя свыше, ста огустение едино отлучившееся далече зело зело от Адами града даже до страны Кариафиарима: низтекущая же низтече в море Аравско, в море Сланое, дондеже до конца оскуде.
17 Wale makuhani waliobeba Sanduku la Agano la Bwana, wakasimama imara mahali pakavu katikati ya Mto Yordani, wakati Waisraeli wote wakiwa wanapita hadi taifa lote likaisha kuvuka mahali pakavu.
И людие стояху прямо Иерихону. И сташа жерцы воздвизающии кивот завета Господня на сусе посреде Иордана: и вси сынове Израилевы прехождаху по суху, дондеже скончаша вси людие преходяще Иордан.

< Yoshua 3 >