< Yoshua 3 >

1 Yoshua na Waisraeli wote wakaondoka asubuhi na mapema kutoka Shitimu, wakaenda mpaka Mto Yordani, ambako walipiga kambi kabla ya kuvuka.
Or Josué se leva de bon matin; ils partirent de Sittim, ils vinrent jusqu'au Jourdain, lui et tous les enfants d'Israël, et ils logèrent là cette nuit, avant qu'ils passassent.
2 Baada ya siku tatu maafisa wakapita katika kambi yote,
Et au bout de trois jours les officiers passèrent par le camp;
3 wakitoa maagizo kwa watu, wakiwaambia: “Mtakapoona Sanduku la Agano la Bwana Mungu wenu, likichukuliwa na Walawi ambao ndio makuhani, mtaondoka hapo mlipo na kulifuata.
Et ils commandèrent au peuple en disant: Sitôt que vous verrez l'Arche de l'alliance de l'Eternel votre Dieu, et les Sacrificateurs de la race de Lévi qui la porteront, vous partirez de votre quartier, et vous marcherez après elle.
4 Ndipo mtakapotambua njia mtakayoiendea, kwa kuwa hamjawahi kuipita kabla. Lakini msisogee karibu, bali kuwe na umbali wa dhiraa 2,000 kati yenu na Sanduku.”
Et afin que vous n'approchiez point d'elle, il y aura entre vous et elle une distance de la mesure d'environ deux mille coudées, afin que vous connaissiez le chemin par lequel vous devez marcher; car vous n'avez point ci-devant passé par ce chemin.
5 Ndipo Yoshua akawaambia hao watu, “Jitakaseni, kwa kuwa kesho Bwana atatenda mambo ya kushangaza katikati yenu.”
Josué dit aussi au peuple: Sanctifiez-vous; car l'Eternel fera demain, au milieu de vous des choses merveilleuses.
6 Yoshua akawaambia makuhani, “Liinueni Sanduku la Agano mkatangulie mbele ya watu.” Hivyo wakaliinua na kutangulia mbele yao.
Josué parla aussi aux Sacrificateurs, en disant: Chargez [sur vous] l'Arche de l'alliance, et passez devant le peuple. Ainsi ils chargèrent [sur eux] l'Arche de l'alliance, et marchèrent devant le peuple.
7 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Leo nitaanza kukutukuza machoni pa Israeli yote, ili wapate kujua kuwa niko pamoja nawe kama nilivyokuwa pamoja na Mose.
Or l'Eternel avait dit à Josué: Aujourd'hui je commencerai de t'élever à la vue de tout Israël; afin qu'ils connaissent que comme j'ai été avec Moïse, je serai [aussi] avec toi.
8 Uwaambie makuhani wanaochukua Sanduku la Agano, ‘Mnapofika kwenye ukingo wa maji ya Yordani, nendeni mkasimame ndani ya mto.’”
Tu commanderas donc aux Sacrificateurs qui portent l'Arche de l'alliance, en [leur] disant: Sitôt que vous arriverez au bord de l'eau du Jourdain, vous vous arrêterez au Jourdain.
9 Yoshua akawaambia Waisraeli, “Njooni hapa msikilize maneno ya Bwana Mungu wenu.
Et Josué dit aux enfants d'Israël: Approchez-vous d'ici, et écoutez les paroles de l'Eternel votre Dieu.
10 Hivi ndivyo mtakavyojua ya kuwa Mungu aliye hai yupo katikati yenu, na kwamba kwa hakika atawafukuza mbele yenu hao Wakanaani, Wahiti, Wahivi, Waperizi, Wagirgashi, Waamori na Wayebusi.
Puis Josué dit: Vous reconnaîtrez à ceci que le [Dieu] Fort, [et] vivant, est au milieu de vous, et qu'il chassera certainement de devant vous les Cananéens, les Héthiens, les Héviens, les Phérésiens, les Guirgasiens, les Amorrhéens, et les Jébusiens.
11 Tazameni, Sanduku la Agano la Bwana wa dunia yote litaingia ndani ya Mto Yordani likiwa limewatangulia.
Voici, l'Arche de l'alliance du Dominateur de toute la terre s'en va passer devant vous au travers du Jourdain.
12 Sasa basi, chagueni watu kumi na wawili kutoka makabila ya Israeli, mtu mmoja kutoka kila kabila.
Maintenant donc choisissez douze hommes des Tribus d'Israël, un homme de chaque Tribu.
13 Mara tu nyayo za makuhani walichukualo Sanduku la Bwana, Bwana wa dunia yote, zitakapokanyaga ndani ya Mto Yordani, maji hayo yatiririkayo kutoka juu yatatindika na kusimama kama chuguu.”
Et il arrivera qu'aussitôt que les plantes des pieds des Sacrificateurs qui portent l'Arche de l'Eternel, le Dominateur de toute la terre, seront posées dans les eaux du Jourdain, les eaux du Jourdain seront coupées, les eaux, [dis-je], qui descendent d'en haut, et elles s'arrêteront en un monceau.
14 Basi, watu walipovunja kambi ili kuvuka Yordani, makuhani wakiwa wamebeba Sanduku la Agano waliwatangulia.
Et il arriva que le peuple étant parti de ses tentes pour passer le Jourdain, les Sacrificateurs qui portaient l'Arche de l'alliance, étaient devant le peuple.
15 Wakati huu ulikuwa wakati wa mavuno, nao Mto Yordani ulikuwa umefurika hadi kwenye kingo zake. Ilikuwa kawaida ya Yordani kufurika nyakati zote za mavuno. Mara tu makuhani wale waliokuwa wamebeba Sanduku la Agano walipofika mtoni na nyayo zao kuzama ndani ya yale maji,
Et sitôt que ceux qui portaient l'Arche furent arrivés au Jourdain, et que les pieds des Sacrificateurs qui portaient l'Arche furent mouillés au bord de l'eau, (or le Jourdain regorge par dessus tous ses bords durant tout le temps de la moisson.)
16 maji hayo yaliyotiririka kutoka upande wa juu yaliacha kutiririka yakasimama kama chuguu mbali kabisa nao, kwenye mji ulioitwa Adamu kwenye eneo la Sarethani, wakati yale maji yaliyokuwa yanatiririka kuingia kwenye Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), yalitindika kabisa. Hivyo watu wakavuka kukabili Yeriko.
Les eaux qui descendaient d'en-haut, s'arrêtèrent, et s'élevèrent en un monceau fort loin, depuis la ville d'Adam, qui [est] à côté de Tsartan; et celles [d'embas], qui descendaient vers la mer de la campagne, qui est la mer salée, défaillirent et s'écoulèrent, et le peuple passa vis-à-vis de Jérico.
17 Wale makuhani waliobeba Sanduku la Agano la Bwana, wakasimama imara mahali pakavu katikati ya Mto Yordani, wakati Waisraeli wote wakiwa wanapita hadi taifa lote likaisha kuvuka mahali pakavu.
Mais les Sacrificateurs qui portaient l'Arche de l'alliance de l'Eternel, s'arrêtèrent [de pied] ferme sur le sec au milieu du Jourdain, pendant que tout Israël passa à sec, jusqu'à ce que tout le peuple eût achevé de passer le Jourdain.

< Yoshua 3 >