< Yoshua 3 >

1 Yoshua na Waisraeli wote wakaondoka asubuhi na mapema kutoka Shitimu, wakaenda mpaka Mto Yordani, ambako walipiga kambi kabla ya kuvuka.
Et Josué fut debout de grand matin, et il leva le camp de Sétim. Ils marchèrent jusqu'au Jourdain; et là ils firent halte avant de le traverser.
2 Baada ya siku tatu maafisa wakapita katika kambi yote,
Après trois jours, les scribes parcoururent le camp.
3 wakitoa maagizo kwa watu, wakiwaambia: “Mtakapoona Sanduku la Agano la Bwana Mungu wenu, likichukuliwa na Walawi ambao ndio makuhani, mtaondoka hapo mlipo na kulifuata.
Ils donnèrent au peuple les ordres de Josué, et dirent: Lorsque vous verrez l'arche de l'alliance du Seigneur notre Dieu, et nos prêtres et nos lévites la portant, quittez chacun votre poste et marchez à sa suite.
4 Ndipo mtakapotambua njia mtakayoiendea, kwa kuwa hamjawahi kuipita kabla. Lakini msisogee karibu, bali kuwe na umbali wa dhiraa 2,000 kati yenu na Sanduku.”
Mais laissez un grand intervalle entre vous et elle, tenez-vous à une distance de deux mille coudées; gardez-vous d'en approcher, afin que vous sachiez la voie que vous devez suivre, car vous n'avez jamais fait semblable chemin.
5 Ndipo Yoshua akawaambia hao watu, “Jitakaseni, kwa kuwa kesho Bwana atatenda mambo ya kushangaza katikati yenu.”
Et Josué dit au peuple: Sanctifiez-vous pour demain, car demain le Seigneur fera au milieu de vous des merveilles.
6 Yoshua akawaambia makuhani, “Liinueni Sanduku la Agano mkatangulie mbele ya watu.” Hivyo wakaliinua na kutangulia mbele yao.
Et Josué dit aux prêtres: Enlevez l'arche de l'alliance du Seigneur et marchez devant le peuple. Les prêtres enlevèrent donc l'arche de l'alliance du Seigneur, et ils marchèrent devant le peuple.
7 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Leo nitaanza kukutukuza machoni pa Israeli yote, ili wapate kujua kuwa niko pamoja nawe kama nilivyokuwa pamoja na Mose.
Et le Seigneur dit à Josué: C'est aujourd'hui que je commence à te rehausser aux yeux de tous les fils d'Israël, afin qu'ils sachent que de même que j'étais avec Moïse, je serai avec toi.
8 Uwaambie makuhani wanaochukua Sanduku la Agano, ‘Mnapofika kwenye ukingo wa maji ya Yordani, nendeni mkasimame ndani ya mto.’”
Et maintenant, donne mes ordres aux prêtres qui portent l'arche de l'alliance; dis-leur: Lorsque vous serez entrés dans les eaux du Jourdain, arrêtez-vous.
9 Yoshua akawaambia Waisraeli, “Njooni hapa msikilize maneno ya Bwana Mungu wenu.
Et Josué dit aux fils d'Israël: Venez ici, écoutez les paroles du Seigneur votre Dieu.
10 Hivi ndivyo mtakavyojua ya kuwa Mungu aliye hai yupo katikati yenu, na kwamba kwa hakika atawafukuza mbele yenu hao Wakanaani, Wahiti, Wahivi, Waperizi, Wagirgashi, Waamori na Wayebusi.
Vous reconnaîtrez en elles, et en leur accomplissement, que le Dieu vivant est parmi vous, et qu'il exterminera devant votre face le Chananéen, l'Hettéen, l'Hevéen, le Phérézéen, le Gergéséen, le Jébuséen et l'Amorrhéen.
11 Tazameni, Sanduku la Agano la Bwana wa dunia yote litaingia ndani ya Mto Yordani likiwa limewatangulia.
Voilà que l'arche de l'alliance du Seigneur de toute la terre va traverser le Jourdain.
12 Sasa basi, chagueni watu kumi na wawili kutoka makabila ya Israeli, mtu mmoja kutoka kila kabila.
Choisissez douze hommes des fils d'Israël, un de chaque tribu.
13 Mara tu nyayo za makuhani walichukualo Sanduku la Bwana, Bwana wa dunia yote, zitakapokanyaga ndani ya Mto Yordani, maji hayo yatiririkayo kutoka juu yatatindika na kusimama kama chuguu.”
Et ceci arrivera: Lorsque les pieds des prêtres portant l'arche de l'alliance du Seigneur de toute la terre s'arrêteront dans l'eau du Jourdain, l'eau inférieure s'écoulera et les eaux supérieures s'arrêteront.
14 Basi, watu walipovunja kambi ili kuvuka Yordani, makuhani wakiwa wamebeba Sanduku la Agano waliwatangulia.
Et le peuple s'éloigna de ses tentes pour traverser le Jourdain; cependant, les prêtres transportèrent, en avant du peuple, l'arche de l'alliance du Seigneur.
15 Wakati huu ulikuwa wakati wa mavuno, nao Mto Yordani ulikuwa umefurika hadi kwenye kingo zake. Ilikuwa kawaida ya Yordani kufurika nyakati zote za mavuno. Mara tu makuhani wale waliokuwa wamebeba Sanduku la Agano walipofika mtoni na nyayo zao kuzama ndani ya yale maji,
Mais, au moment où entraient dans le Jourdain les prêtres portant l'arche de l'alliance du Seigneur, au moment où leurs pieds commencèrent à être baignés dans l'eau du fleuve du Jourdain, coulant à pleins bords, puisque c'était le temps de la moisson des froments,
16 maji hayo yaliyotiririka kutoka upande wa juu yaliacha kutiririka yakasimama kama chuguu mbali kabisa nao, kwenye mji ulioitwa Adamu kwenye eneo la Sarethani, wakati yale maji yaliyokuwa yanatiririka kuingia kwenye Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), yalitindika kabisa. Hivyo watu wakavuka kukabili Yeriko.
Les eaux supérieures s'arrêtèrent; elles s'arrêtèrent formant une masse compacte et immense, qui s'étendit bien loin, bien loin, jusqu'à Cariathiarim. L'eau qui descendait, s'écoula dans la mer d'Araba ou la mer de Sel, jusqu'à ce qu'il n'en restât plus, et le peuple s'arrêta devant Jéricho.
17 Wale makuhani waliobeba Sanduku la Agano la Bwana, wakasimama imara mahali pakavu katikati ya Mto Yordani, wakati Waisraeli wote wakiwa wanapita hadi taifa lote likaisha kuvuka mahali pakavu.
Et, pendant que tous les fils d'Israël traversaient à pied sec, les prêtres, qui portaient l'arche de l'alliance du Seigneur, se tinrent immobiles et à pied sec au milieu du fleuve, jusqu'à ce que tout le peuple en eut achevé le passage.

< Yoshua 3 >