< Yoshua 3 >

1 Yoshua na Waisraeli wote wakaondoka asubuhi na mapema kutoka Shitimu, wakaenda mpaka Mto Yordani, ambako walipiga kambi kabla ya kuvuka.
Josué, s'étant levé de bon matin, partit de Sétim, lui et tous les enfants d'Israël; arrivés au Jourdain, ils firent une halte avant de le traverser.
2 Baada ya siku tatu maafisa wakapita katika kambi yote,
Au bout de trois jours, les officiers parcoururent le camp,
3 wakitoa maagizo kwa watu, wakiwaambia: “Mtakapoona Sanduku la Agano la Bwana Mungu wenu, likichukuliwa na Walawi ambao ndio makuhani, mtaondoka hapo mlipo na kulifuata.
et donnèrent cet ordre au peuple: « Lorsque vous verrez l'arche de l'alliance de Yahweh, votre Dieu, portée par les prêtres lévites, partez de ce lieu où vous campez et mettez-vous en marche après elle,
4 Ndipo mtakapotambua njia mtakayoiendea, kwa kuwa hamjawahi kuipita kabla. Lakini msisogee karibu, bali kuwe na umbali wa dhiraa 2,000 kati yenu na Sanduku.”
— mais qu'il y ait entre vous et elle une distance de deux mille coudées environ, n'en approchez pas, — afin que vous sachiez bien le chemin que vous devez suivre, car vous n'avez jamais passé par ce chemin. »
5 Ndipo Yoshua akawaambia hao watu, “Jitakaseni, kwa kuwa kesho Bwana atatenda mambo ya kushangaza katikati yenu.”
Et Josué dit au peuple: « Sanctifiez-vous, car demain Yahweh fera des prodiges au milieu de vous. »
6 Yoshua akawaambia makuhani, “Liinueni Sanduku la Agano mkatangulie mbele ya watu.” Hivyo wakaliinua na kutangulia mbele yao.
Puis Josué parla aux prêtres, en disant: « Portez l'arche d'alliance, et passez en avant du peuple. » Ils portèrent l'arche d'alliance et s'avancèrent devant le peuple.
7 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Leo nitaanza kukutukuza machoni pa Israeli yote, ili wapate kujua kuwa niko pamoja nawe kama nilivyokuwa pamoja na Mose.
Yahweh dit à Josué: « Aujourd'hui je commencerai à t'élever aux yeux de tout Israël, afin qu'ils sachent que je serai avec toi comme j'ai été avec Moïse.
8 Uwaambie makuhani wanaochukua Sanduku la Agano, ‘Mnapofika kwenye ukingo wa maji ya Yordani, nendeni mkasimame ndani ya mto.’”
Toi, donne cet ordre aux prêtres qui portent l'arche d'alliance: Lorsque vous arriverez au bord des eaux du Jourdain, vous vous arrêterez dans le Jourdain. »
9 Yoshua akawaambia Waisraeli, “Njooni hapa msikilize maneno ya Bwana Mungu wenu.
Josué dit aux enfants d'Israël: « Approchez et écoutez les paroles de Yahweh, votre Dieu. »
10 Hivi ndivyo mtakavyojua ya kuwa Mungu aliye hai yupo katikati yenu, na kwamba kwa hakika atawafukuza mbele yenu hao Wakanaani, Wahiti, Wahivi, Waperizi, Wagirgashi, Waamori na Wayebusi.
Et Josué dit: « A ceci vous reconnaîtrez que le Dieu vivant est au milieu de vous, et qu'il ne manquera pas de chasser devant vous les Chananéens, les Héthéens, les Hévéens, les Phérézéens, les Gergéséens, les Amorrhéens et les Jébuséens.
11 Tazameni, Sanduku la Agano la Bwana wa dunia yote litaingia ndani ya Mto Yordani likiwa limewatangulia.
Voici que l'arche de l'alliance du Seigneur de toute la terre va passer devant vous dans le Jourdain.
12 Sasa basi, chagueni watu kumi na wawili kutoka makabila ya Israeli, mtu mmoja kutoka kila kabila.
Maintenant, prenez douze hommes parmi les tribus d'Israël, un homme par chaque tribu.
13 Mara tu nyayo za makuhani walichukualo Sanduku la Bwana, Bwana wa dunia yote, zitakapokanyaga ndani ya Mto Yordani, maji hayo yatiririkayo kutoka juu yatatindika na kusimama kama chuguu.”
Et dès que les prêtres qui portent l'arche de Yahweh, le Seigneur de toute la terre, poseront la plante des pieds dans les eaux du Jourdain, les eaux du Jourdain seront coupées, celles qui descendent d'en haut, et elles s'arrêteront en un monceau. »
14 Basi, watu walipovunja kambi ili kuvuka Yordani, makuhani wakiwa wamebeba Sanduku la Agano waliwatangulia.
Quand le peuple fut sorti de ses tentes pour passer le Jourdain, les prêtres qui portaient l'arche de l'alliance marchèrent devant le peuple.
15 Wakati huu ulikuwa wakati wa mavuno, nao Mto Yordani ulikuwa umefurika hadi kwenye kingo zake. Ilikuwa kawaida ya Yordani kufurika nyakati zote za mavuno. Mara tu makuhani wale waliokuwa wamebeba Sanduku la Agano walipofika mtoni na nyayo zao kuzama ndani ya yale maji,
Au moment où les porteurs de l'arche arrivèrent au Jourdain et où les pieds des prêtres qui portaient l'arche plongèrent au bord de l'eau, — car le Jourdain déborde par-dessus toutes ses rives tout le temps de la moisson, —
16 maji hayo yaliyotiririka kutoka upande wa juu yaliacha kutiririka yakasimama kama chuguu mbali kabisa nao, kwenye mji ulioitwa Adamu kwenye eneo la Sarethani, wakati yale maji yaliyokuwa yanatiririka kuingia kwenye Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), yalitindika kabisa. Hivyo watu wakavuka kukabili Yeriko.
alors les eaux qui descendent d'en haut s'arrêtèrent; elles s'élevèrent en un monceau, à une très grande distance, près de la ville d'Adom, qui est à côté de Sarthan; et celles qui descendent vers la mer de l'Arabah, la mer Salée, furent complètement coupées; et le peuple passa vis-à-vis de Jéricho.
17 Wale makuhani waliobeba Sanduku la Agano la Bwana, wakasimama imara mahali pakavu katikati ya Mto Yordani, wakati Waisraeli wote wakiwa wanapita hadi taifa lote likaisha kuvuka mahali pakavu.
Les prêtres qui portaient l'arche de l'alliance de Yahweh se tinrent de pied ferme sur la terre sèche au milieu du Jourdain, pendant que tout Israël passait à sec, jusqu'à ce que toute la nation eut achevé de passer le Jourdain.

< Yoshua 3 >