< Yoshua 3 >

1 Yoshua na Waisraeli wote wakaondoka asubuhi na mapema kutoka Shitimu, wakaenda mpaka Mto Yordani, ambako walipiga kambi kabla ya kuvuka.
Therfor Josue roos bi nyyt, and mouede tentis; and thei yeden out of Sechym, and camen to Jordan, he and alle the sones of Israel, and dwelliden there thre daies.
2 Baada ya siku tatu maafisa wakapita katika kambi yote,
And whanne tho daies weren passid, crieris yeden thorouy the myddis of tentis,
3 wakitoa maagizo kwa watu, wakiwaambia: “Mtakapoona Sanduku la Agano la Bwana Mungu wenu, likichukuliwa na Walawi ambao ndio makuhani, mtaondoka hapo mlipo na kulifuata.
and bigunnen to crie, Whanne ye seen the arke of boond of pees of youre Lord God, and the preestis of the generacioun of Leuy berynge it, also rise ye, and sue the biforgoeris;
4 Ndipo mtakapotambua njia mtakayoiendea, kwa kuwa hamjawahi kuipita kabla. Lakini msisogee karibu, bali kuwe na umbali wa dhiraa 2,000 kati yenu na Sanduku.”
and a space of twey thousynde cubitis be bitwixe you and the arke, that ye moun se fer, and knowe bi what weie ye schulen entre, for ye `yeden not bifore bi it; and be ye war, that ye neiye not to the arke.
5 Ndipo Yoshua akawaambia hao watu, “Jitakaseni, kwa kuwa kesho Bwana atatenda mambo ya kushangaza katikati yenu.”
And Josue seide to the puple, Be ye halewid, for to morew the Lord schal make merueilis among you.
6 Yoshua akawaambia makuhani, “Liinueni Sanduku la Agano mkatangulie mbele ya watu.” Hivyo wakaliinua na kutangulia mbele yao.
And Josue seide to the preestis, Take ye the arke of the boond of pees `of the Lord, and go ye bifor the puple. Whiche filliden the heestis, and tooken the arke, and yeden bifor hem.
7 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Leo nitaanza kukutukuza machoni pa Israeli yote, ili wapate kujua kuwa niko pamoja nawe kama nilivyokuwa pamoja na Mose.
And the Lord seide to Josue, To dai Y schal bigynne to enhaunse thee bifor al Israel, that thei wite, that as Y was with Moises, so Y am also with thee.
8 Uwaambie makuhani wanaochukua Sanduku la Agano, ‘Mnapofika kwenye ukingo wa maji ya Yordani, nendeni mkasimame ndani ya mto.’”
Forsothe comaunde thou to preestis, that beren the arke of bond of pees, and seie thou to hem, Whanne ye han entrid in to a part of the watir of Jordan, stonde ye therynne.
9 Yoshua akawaambia Waisraeli, “Njooni hapa msikilize maneno ya Bwana Mungu wenu.
And Josue seide to the sones of Israel, Neiye ye hidur, and here ye the word of youre Lord God.
10 Hivi ndivyo mtakavyojua ya kuwa Mungu aliye hai yupo katikati yenu, na kwamba kwa hakika atawafukuza mbele yenu hao Wakanaani, Wahiti, Wahivi, Waperizi, Wagirgashi, Waamori na Wayebusi.
And eft he seide, In this ye schulen wite that the Lord God lyuynge is in the myddis of you; and he schal distrye in youre siyt Cananey, Ethei, Euey, and Feresei, and Gergesei, and Jebusei, and Amorrei.
11 Tazameni, Sanduku la Agano la Bwana wa dunia yote litaingia ndani ya Mto Yordani likiwa limewatangulia.
Lo! the arke of boond of pees of the Lord of al erthe schal go bifor you thorouy Jordan.
12 Sasa basi, chagueni watu kumi na wawili kutoka makabila ya Israeli, mtu mmoja kutoka kila kabila.
Make ye redi twelue men of the twelue lynagis of Israel, bi ech lynage o man.
13 Mara tu nyayo za makuhani walichukualo Sanduku la Bwana, Bwana wa dunia yote, zitakapokanyaga ndani ya Mto Yordani, maji hayo yatiririkayo kutoka juu yatatindika na kusimama kama chuguu.”
And whanne the preestis, that beren the arke of boond of pees of the Lord God of al erthe, han set the steppis of her feet in the watris of Jordan, the watris that ben lowere schulen renne doun, and schulen faile; forsothe the watris that comen fro aboue schulen stonde togidere in o gobet.
14 Basi, watu walipovunja kambi ili kuvuka Yordani, makuhani wakiwa wamebeba Sanduku la Agano waliwatangulia.
Therfor the puple yede out of her tabernaclis to passe Jordan; and the preestis that baren the arke of boond of pees yeden bifor the puple.
15 Wakati huu ulikuwa wakati wa mavuno, nao Mto Yordani ulikuwa umefurika hadi kwenye kingo zake. Ilikuwa kawaida ya Yordani kufurika nyakati zote za mavuno. Mara tu makuhani wale waliokuwa wamebeba Sanduku la Agano walipofika mtoni na nyayo zao kuzama ndani ya yale maji,
And whanne the preestis entriden in to Jordan, and her feet weren dippid in the part of watir; forsothe Jordan `hadde fillid the brynkis of his trow in the tyme of `ripe corn;
16 maji hayo yaliyotiririka kutoka upande wa juu yaliacha kutiririka yakasimama kama chuguu mbali kabisa nao, kwenye mji ulioitwa Adamu kwenye eneo la Sarethani, wakati yale maji yaliyokuwa yanatiririka kuingia kwenye Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), yalitindika kabisa. Hivyo watu wakavuka kukabili Yeriko.
the watris yeden doun, and stoden in o place, and wexiden grete at the licnesse of an hil, and apperiden fer fro the citee that was clepid Edom, `til to the place of Sarthan; sotheli the watris that weren lowere yeden doun in to the see of wildirnesse, which is now clepid the deed see, `til the watris failiden outirli.
17 Wale makuhani waliobeba Sanduku la Agano la Bwana, wakasimama imara mahali pakavu katikati ya Mto Yordani, wakati Waisraeli wote wakiwa wanapita hadi taifa lote likaisha kuvuka mahali pakavu.
Forsothe the puple yede thorouy Jordan; and the preestis, that baren the arke of the boond of pees of the Lord, stoden gird on the drie erthe in the myddis of Jordan, and al the puple passide thorouy the drie trow.

< Yoshua 3 >