< Yoshua 3 >

1 Yoshua na Waisraeli wote wakaondoka asubuhi na mapema kutoka Shitimu, wakaenda mpaka Mto Yordani, ambako walipiga kambi kabla ya kuvuka.
and to rise Joshua in/on/with morning and to set out from [the] Shittim and to come (in): come till [the] Jordan he/she/it and all son: descendant/people Israel and to lodge there before to pass
2 Baada ya siku tatu maafisa wakapita katika kambi yote,
and to be from end three day and to pass [the] official in/on/with entrails: among [the] camp
3 wakitoa maagizo kwa watu, wakiwaambia: “Mtakapoona Sanduku la Agano la Bwana Mungu wenu, likichukuliwa na Walawi ambao ndio makuhani, mtaondoka hapo mlipo na kulifuata.
and to command [obj] [the] people to/for to say like/as to see: see you [obj] ark covenant LORD God your and [the] priest [the] Levi to lift: bear [obj] him and you(m. p.) to set out from place your and to go: follow after him
4 Ndipo mtakapotambua njia mtakayoiendea, kwa kuwa hamjawahi kuipita kabla. Lakini msisogee karibu, bali kuwe na umbali wa dhiraa 2,000 kati yenu na Sanduku.”
surely distant to be between you (and between him *Q(k)*) like/as thousand cubit in/on/with measure not to present: come to(wards) him because which to know [obj] [the] way: road which to go: went in/on/with her for not to pass in/on/with way: road from yesterday three days ago
5 Ndipo Yoshua akawaambia hao watu, “Jitakaseni, kwa kuwa kesho Bwana atatenda mambo ya kushangaza katikati yenu.”
and to say Joshua to(wards) [the] people to consecrate: consecate for tomorrow to make: do LORD in/on/with entrails: among your to wonder
6 Yoshua akawaambia makuhani, “Liinueni Sanduku la Agano mkatangulie mbele ya watu.” Hivyo wakaliinua na kutangulia mbele yao.
and to say Joshua to(wards) [the] priest to/for to say to lift: raise [obj] ark [the] covenant and to pass to/for face: before [the] people and to lift: raise [obj] ark [the] covenant and to go: went to/for face: before [the] people
7 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Leo nitaanza kukutukuza machoni pa Israeli yote, ili wapate kujua kuwa niko pamoja nawe kama nilivyokuwa pamoja na Mose.
and to say LORD to(wards) Joshua [the] day: today [the] this to profane/begin: begin to magnify you in/on/with eye: seeing all Israel which to know [emph?] for like/as as which to be with Moses to be with you
8 Uwaambie makuhani wanaochukua Sanduku la Agano, ‘Mnapofika kwenye ukingo wa maji ya Yordani, nendeni mkasimame ndani ya mto.’”
and you(m. s.) to command [obj] [the] priest to lift: bear ark [the] covenant to/for to say like/as to come (in): come you till end water [the] Jordan in/on/with Jordan to stand: stand
9 Yoshua akawaambia Waisraeli, “Njooni hapa msikilize maneno ya Bwana Mungu wenu.
and to say Joshua to(wards) son: descendant/people Israel to approach: approach here/thus and to hear: hear [obj] word LORD God your
10 Hivi ndivyo mtakavyojua ya kuwa Mungu aliye hai yupo katikati yenu, na kwamba kwa hakika atawafukuza mbele yenu hao Wakanaani, Wahiti, Wahivi, Waperizi, Wagirgashi, Waamori na Wayebusi.
and to say Joshua in/on/with this to know [emph?] for God alive in/on/with entrails: among your and to possess: take to possess: take from face: before your [obj] [the] Canaanite and [obj] [the] Hittite and [obj] [the] Hivite and [obj] [the] Perizzite and [obj] [the] Girgashite and [the] Amorite and [the] Jebusite
11 Tazameni, Sanduku la Agano la Bwana wa dunia yote litaingia ndani ya Mto Yordani likiwa limewatangulia.
behold ark [the] covenant Lord all [the] land: country/planet to pass to/for face: before your in/on/with Jordan
12 Sasa basi, chagueni watu kumi na wawili kutoka makabila ya Israeli, mtu mmoja kutoka kila kabila.
and now to take: take to/for you two ten man from tribe Israel man one man one to/for tribe
13 Mara tu nyayo za makuhani walichukualo Sanduku la Bwana, Bwana wa dunia yote, zitakapokanyaga ndani ya Mto Yordani, maji hayo yatiririkayo kutoka juu yatatindika na kusimama kama chuguu.”
and to be like/as to rest palm: sole foot [the] priest to lift: bear ark LORD Lord all [the] land: country/planet in/on/with water [the] Jordan water [the] Jordan to cut: cut [emph?] [the] water [the] to go down from to/for above [to] and to stand: stand heap one
14 Basi, watu walipovunja kambi ili kuvuka Yordani, makuhani wakiwa wamebeba Sanduku la Agano waliwatangulia.
and to be in/on/with to set out [the] people from tent their to/for to pass [obj] [the] Jordan and [the] priest to lift: bear [the] ark [the] covenant to/for face: before [the] people
15 Wakati huu ulikuwa wakati wa mavuno, nao Mto Yordani ulikuwa umefurika hadi kwenye kingo zake. Ilikuwa kawaida ya Yordani kufurika nyakati zote za mavuno. Mara tu makuhani wale waliokuwa wamebeba Sanduku la Agano walipofika mtoni na nyayo zao kuzama ndani ya yale maji,
and like/as to come (in): come to lift: bear [the] ark till [the] Jordan and foot [the] priest to lift: bear [the] ark to dip in/on/with end [the] water and [the] Jordan to fill upon all bank his all day harvest
16 maji hayo yaliyotiririka kutoka upande wa juu yaliacha kutiririka yakasimama kama chuguu mbali kabisa nao, kwenye mji ulioitwa Adamu kwenye eneo la Sarethani, wakati yale maji yaliyokuwa yanatiririka kuingia kwenye Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), yalitindika kabisa. Hivyo watu wakavuka kukabili Yeriko.
and to stand: stand [the] water [the] to go down from to/for above [to] to arise: rise heap one to remove much (from Adam *Q(K)*) [the] city which from side Zarethan and [the] to go down upon sea [the] (Sea of) the Arabah sea [the] Salt (Sea) to finish to cut: cut and [the] people to pass before Jericho
17 Wale makuhani waliobeba Sanduku la Agano la Bwana, wakasimama imara mahali pakavu katikati ya Mto Yordani, wakati Waisraeli wote wakiwa wanapita hadi taifa lote likaisha kuvuka mahali pakavu.
and to stand: stand [the] priest to lift: bear [the] ark covenant LORD in/on/with dry ground in/on/with midst [the] Jordan to establish: establish and all Israel to pass in/on/with dry ground till which to finish all [the] nation to/for to pass [obj] [the] Jordan

< Yoshua 3 >