< Yoshua 3 >

1 Yoshua na Waisraeli wote wakaondoka asubuhi na mapema kutoka Shitimu, wakaenda mpaka Mto Yordani, ambako walipiga kambi kabla ya kuvuka.
And so, Joshua arose in the night, and he moved the camp. And they departed from Shittim, and they went to the Jordan: he, and all the sons of Israel, and they remained there for three days.
2 Baada ya siku tatu maafisa wakapita katika kambi yote,
After these things unfolded, announcers passed through the midst of the camp,
3 wakitoa maagizo kwa watu, wakiwaambia: “Mtakapoona Sanduku la Agano la Bwana Mungu wenu, likichukuliwa na Walawi ambao ndio makuhani, mtaondoka hapo mlipo na kulifuata.
and they began to proclaim: “When you will see the ark of the covenant of the Lord your God, and the priests of the stock of Levi carrying it, you also shall rise up and follow those who are going before you.
4 Ndipo mtakapotambua njia mtakayoiendea, kwa kuwa hamjawahi kuipita kabla. Lakini msisogee karibu, bali kuwe na umbali wa dhiraa 2,000 kati yenu na Sanduku.”
And let there be, between you and the ark, the space of two thousand cubits, so that you may be able to see it from far away, and to know along which way you should advance. For you have not walked this way before. And be careful that you do not approach the ark.”
5 Ndipo Yoshua akawaambia hao watu, “Jitakaseni, kwa kuwa kesho Bwana atatenda mambo ya kushangaza katikati yenu.”
And Joshua said to the people: “Be sanctified. For tomorrow the Lord will accomplish miracles among you.”
6 Yoshua akawaambia makuhani, “Liinueni Sanduku la Agano mkatangulie mbele ya watu.” Hivyo wakaliinua na kutangulia mbele yao.
And he said to the priests: “Take up the ark of the covenant, and go before the people.” And they fulfilled the orders, and they took it and walked before them.
7 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Leo nitaanza kukutukuza machoni pa Israeli yote, ili wapate kujua kuwa niko pamoja nawe kama nilivyokuwa pamoja na Mose.
And the Lord said to Joshua: “Today I will begin to exalt you in the sight of all Israel, so that they may know that, just as I was with Moses, so also am I with you.
8 Uwaambie makuhani wanaochukua Sanduku la Agano, ‘Mnapofika kwenye ukingo wa maji ya Yordani, nendeni mkasimame ndani ya mto.’”
Now instruct the priests, who are carrying the ark of the covenant, and say to them, ‘When you will have entered into a part of the water of the Jordan, stand still in it.’”
9 Yoshua akawaambia Waisraeli, “Njooni hapa msikilize maneno ya Bwana Mungu wenu.
And Joshua said to the sons of Israel, “Approach to here, and listen to the word of the Lord your God.”
10 Hivi ndivyo mtakavyojua ya kuwa Mungu aliye hai yupo katikati yenu, na kwamba kwa hakika atawafukuza mbele yenu hao Wakanaani, Wahiti, Wahivi, Waperizi, Wagirgashi, Waamori na Wayebusi.
And again, he said: “By this shall you know that the Lord, the living God, is in your midst, and that he shall scatter in your sight, the Canaanite and the Hittite, the Hivite and the Perizzite, likewise the Girgashite, and the Jebusite, and the Amorite.
11 Tazameni, Sanduku la Agano la Bwana wa dunia yote litaingia ndani ya Mto Yordani likiwa limewatangulia.
Behold, the ark of the covenant of the Lord of all the earth shall go before you through the Jordan.
12 Sasa basi, chagueni watu kumi na wawili kutoka makabila ya Israeli, mtu mmoja kutoka kila kabila.
Prepare twelve men from the tribes of Israel, one from each tribe.
13 Mara tu nyayo za makuhani walichukualo Sanduku la Bwana, Bwana wa dunia yote, zitakapokanyaga ndani ya Mto Yordani, maji hayo yatiririkayo kutoka juu yatatindika na kusimama kama chuguu.”
And when the priests who are carrying the ark of the Lord, the God of the entire earth, will have placed the steps of their feet in the waters of the Jordan, the waters that are lower will run down and pass away, and those that are approaching above will stand together in a mass.”
14 Basi, watu walipovunja kambi ili kuvuka Yordani, makuhani wakiwa wamebeba Sanduku la Agano waliwatangulia.
And the people departed from their tents, so that they might cross the Jordan. And the priests who were carrying the ark of the covenant were advancing before them.
15 Wakati huu ulikuwa wakati wa mavuno, nao Mto Yordani ulikuwa umefurika hadi kwenye kingo zake. Ilikuwa kawaida ya Yordani kufurika nyakati zote za mavuno. Mara tu makuhani wale waliokuwa wamebeba Sanduku la Agano walipofika mtoni na nyayo zao kuzama ndani ya yale maji,
And as soon as they entered into the Jordan, and their feet were dipped in a portion of the water, (now the Jordan, since it was the time of the harvest, had filled the banks of its channel, )
16 maji hayo yaliyotiririka kutoka upande wa juu yaliacha kutiririka yakasimama kama chuguu mbali kabisa nao, kwenye mji ulioitwa Adamu kwenye eneo la Sarethani, wakati yale maji yaliyokuwa yanatiririka kuingia kwenye Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), yalitindika kabisa. Hivyo watu wakavuka kukabili Yeriko.
the descending waters stood still in one place, and, swelling up like a mountain, they were seen from far away, from the city that is called Adam, even as far as the place of Zarethan. But those that were lower ran down into the Sea of the Wilderness, (which is now called the Dead Sea, ) until they entirely passed away.
17 Wale makuhani waliobeba Sanduku la Agano la Bwana, wakasimama imara mahali pakavu katikati ya Mto Yordani, wakati Waisraeli wote wakiwa wanapita hadi taifa lote likaisha kuvuka mahali pakavu.
Then the people advanced opposite Jericho. And the priests who were carrying the ark of the covenant of the Lord were standing, fully-dressed, upon dry soil in the midst of the Jordan, and all the people passed over, through the channel that was dried up.

< Yoshua 3 >