< Yoshua 3 >

1 Yoshua na Waisraeli wote wakaondoka asubuhi na mapema kutoka Shitimu, wakaenda mpaka Mto Yordani, ambako walipiga kambi kabla ya kuvuka.
Tidligt næste Morgen gjorde Josua sig rede, og hele Israel brød op fra Sjittim sammen med ham og kom til Jordan, og de tilbragte Natten der, før de drog over.
2 Baada ya siku tatu maafisa wakapita katika kambi yote,
Efter tre Dages Forløb gik Tilsynsmændene omkring i Lejren
3 wakitoa maagizo kwa watu, wakiwaambia: “Mtakapoona Sanduku la Agano la Bwana Mungu wenu, likichukuliwa na Walawi ambao ndio makuhani, mtaondoka hapo mlipo na kulifuata.
og bød Folket: "Når I ser HERREN eders Guds Pagts Ark og Levitpræsterne komme bærende med den, så skal I bryde op fra eders Plads og følge efter
4 Ndipo mtakapotambua njia mtakayoiendea, kwa kuwa hamjawahi kuipita kabla. Lakini msisogee karibu, bali kuwe na umbali wa dhiraa 2,000 kati yenu na Sanduku.”
dog skal der være en Afstand af 2000 Alen mellem eder og den; I må ikke komme den for nær for at I kan vide, hvilken Vej I skal gå; thi I er ikke kommet den Vej før!"
5 Ndipo Yoshua akawaambia hao watu, “Jitakaseni, kwa kuwa kesho Bwana atatenda mambo ya kushangaza katikati yenu.”
Og Josua sagde til Folket: "Helliger eder; thi i Morgen vil HERREN gøre Undere iblandt eder!"
6 Yoshua akawaambia makuhani, “Liinueni Sanduku la Agano mkatangulie mbele ya watu.” Hivyo wakaliinua na kutangulia mbele yao.
Og Josua sagde til Præsterne: "Løft Pagtens Ark op og drag over foran Folket!" Så løftede de Pagtens Ark op og gik foran Folket.
7 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Leo nitaanza kukutukuza machoni pa Israeli yote, ili wapate kujua kuwa niko pamoja nawe kama nilivyokuwa pamoja na Mose.
Men HERREN sagde til Josua: "I Dag begynder jeg at gøre dig stor i hele Israels Øjne, for at de kan vide, at jeg vil være med dig, som jeg var med Moses.
8 Uwaambie makuhani wanaochukua Sanduku la Agano, ‘Mnapofika kwenye ukingo wa maji ya Yordani, nendeni mkasimame ndani ya mto.’”
Du skal byde Præsterne, som bærer Pagtens Ark: Når I kommer til Kanten af Jordans Vand, skal I standse der ved Jordan!"
9 Yoshua akawaambia Waisraeli, “Njooni hapa msikilize maneno ya Bwana Mungu wenu.
Da sagde Josua til Israeliterne: "Kom hid og hør HERREN eders Guds Ord!"
10 Hivi ndivyo mtakavyojua ya kuwa Mungu aliye hai yupo katikati yenu, na kwamba kwa hakika atawafukuza mbele yenu hao Wakanaani, Wahiti, Wahivi, Waperizi, Wagirgashi, Waamori na Wayebusi.
Og Josua sagde: "Derpå skal I kende, at der er en levende Gud iblandt eder, og at han vil drive Kana'anæerne, Hetiterne, Hivviterne, Perizziterne, Girgasjiterne, Amoriterne og Jebusiterne bort foran eder:
11 Tazameni, Sanduku la Agano la Bwana wa dunia yote litaingia ndani ya Mto Yordani likiwa limewatangulia.
Se, HERRENs, al Jordens Herres, Ark skal gå foran eder gennem Jordan.
12 Sasa basi, chagueni watu kumi na wawili kutoka makabila ya Israeli, mtu mmoja kutoka kila kabila.
Vælg eder nu tolv Mænd af Israels Stammer, een Mand af hver Stamme.
13 Mara tu nyayo za makuhani walichukualo Sanduku la Bwana, Bwana wa dunia yote, zitakapokanyaga ndani ya Mto Yordani, maji hayo yatiririkayo kutoka juu yatatindika na kusimama kama chuguu.”
Og så snart Præsterne, som bærer HERRENs, al Jordens Herres, Ark, sætter Foden i Jordans Vand, skal Jordans Vand standse, det Vand, som kommer ovenfra, og stå som en Vold."
14 Basi, watu walipovunja kambi ili kuvuka Yordani, makuhani wakiwa wamebeba Sanduku la Agano waliwatangulia.
Da Folket så brød op fra deres Telte for at gå over Jordan med Præsterne, som bar Arken, i Spidsen,
15 Wakati huu ulikuwa wakati wa mavuno, nao Mto Yordani ulikuwa umefurika hadi kwenye kingo zake. Ilikuwa kawaida ya Yordani kufurika nyakati zote za mavuno. Mara tu makuhani wale waliokuwa wamebeba Sanduku la Agano walipofika mtoni na nyayo zao kuzama ndani ya yale maji,
og da de, som bar Arken, kom til Jordan, og Præsterne, som bar Arken, rørte ved Vandkanten med deres Fødder Jordan gik overalt over sine Bredder i hele Høsttiden
16 maji hayo yaliyotiririka kutoka upande wa juu yaliacha kutiririka yakasimama kama chuguu mbali kabisa nao, kwenye mji ulioitwa Adamu kwenye eneo la Sarethani, wakati yale maji yaliyokuwa yanatiririka kuingia kwenye Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), yalitindika kabisa. Hivyo watu wakavuka kukabili Yeriko.
standsede Vandet, som kom ovenfra, og stod som en Vold langt borte, oppe ved Byen Adam, som ligger ved Zaretan, medens det Vand, som flød ned mod Arabaeller Salthavet, løb helt bort; således gik Folket over lige over for Jeriko.
17 Wale makuhani waliobeba Sanduku la Agano la Bwana, wakasimama imara mahali pakavu katikati ya Mto Yordani, wakati Waisraeli wote wakiwa wanapita hadi taifa lote likaisha kuvuka mahali pakavu.
Men Præsterne, som bar HERRENs Pagts Ark, blev stående på tør Bund midt i Jordan, medens hele Israel gik over på tør Bund, indtil hele Folket havde tilendebragt Overgangen over Jordan.

< Yoshua 3 >