< Yoshua 24 >
1 Ndipo Yoshua akaita pamoja makabila yote ya Israeli huko Shekemu. Akawaita wazee, viongozi, waamuzi na maafisa wa Israeli, nao wakaja mbele za Mungu.
And Josue gaderide alle the lynagis of Israel in to Sechem; and he clepide the grettere men in birthe, and the princes, and iugis, and maistris; and thei stoden in the siyt of the Lord.
2 Yoshua akawaambia watu wote, “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Hapo zamani baba zenu, pamoja na Tera baba yake Abrahamu na Nahori, waliishi ngʼambo ya Mto nao waliiabudu miungu mingine.
And he spak thus to the puple, The Lord God of Israel seith these thingis, Youre fadris dwelliden at the bigynnyng biyende the flood Eufrates, Thare, the fadir of Abraham, and Nachor, and thei serueden alien goddis.
3 Lakini nilimwondoa baba yenu Abrahamu kutoka nchi hiyo ngʼambo ya Mto, nami nikamwongoza katika nchi yote ya Kanaani, nikampa wazao wengi. Nikampa Isaki,
Therfor Y took youre fadir Abraham fro the coostis of Mesopotanye, and Y brouyte hym in to the lond of Canaan; and Y multipliede `the seed of hym,
4 naye Isaki nikampa Yakobo na Esau. Esau nikampa nchi ya vilima ya Seiri, lakini Yakobo pamoja na wanawe wakashuka Misri.
and Y yaf Isaac to hym; and eft Y yaf to Isaac, Jacob, and Esau, of whiche Y yaf to Esau the hil of Seir, to `haue in possessioun; forsothe Jacob and hise sones yeden doun in to Egipt.
5 “‘Kisha nikawatuma Mose na Aroni, nami nikawapiga Wamisri kwa kile nilichokitenda huko, tena nikawatoa ninyi huko.
And Y sente Moises and Aaron, and Y smoot Egipt with many signes and wondris,
6 Nilipowatoa baba zenu Misri, mlifika kwenye bahari, nao Wamisri wakawafuatia baba zenu kwa magari na wapanda farasi mpaka kwenye Bahari ya Shamu.
and Y ledde you and youre fadris out of Egipt. And ye camen to the see, and Egipcians pursueden youre fadris with charis, and multitude of knyytis, `til to the Reed See.
7 Lakini wakamlilia Bwana wakitaka msaada, naye akaweka giza kati yenu na Wamisri, akaileta bahari juu yao ikawafunika. Ninyi mliona kwa macho yenu wenyewe kile nilichowatendea Wamisri. Kisha mliishi jangwani kwa muda mrefu.
Forsothe the sones of Israel crieden to the Lord, and he settide derknessis bitwixe you and Egipcians; and he brouyte the see on hem, and hilide hem. Youre iyen sien alle thingis, whiche Y dide in Egipt. And ye dwelliden in wildirnesse in myche tyme.
8 “‘Nikawaleta katika nchi ya Waamori ambao waliishi mashariki mwa Yordani. Wakapigana nanyi, lakini nikawatia mikononi mwenu. Nikawaangamiza mbele yenu nanyi mkaimiliki nchi yao.
And Y brouyte you in to the lond of Ammorrei, that dwellide biyende Jordan; and whanne thei fouyten ayens you, Y bitook hem in to youre hondis, and ye hadden in possessioun `the lond of hem, and ye killiden hem.
9 Wakati Balaki mwana wa Sipori, mfalme wa Moabu, alipojiandaa kupigana dhidi ya Israeli, alimwita Balaamu mwana wa Beori apate kuwalaani.
Sotheli Balach, the sone of Sephor, the king of Moab, roos, and fauyt ayens Israel; and he sente, and clepide Balaam, the sone of Beor, that he schulde curse you.
10 Lakini sikumkubali Balaamu, kwa hiyo aliwabariki tena na tena, nami niliwaokoa toka mkononi mwake.
And Y nolde here hym, but ayenward bi hym Y blesside you, and delyuerede you fro hise hondis.
11 “‘Ndipo mlipovuka Yordani mkafika Yeriko. Raiya wa Yeriko wakapigana nanyi, kama walivyofanya Waamori, Waperizi, Wakanaani, Wahiti, Wagirgashi, Wahivi na Wayebusi, lakini niliwatia mikononi mwenu.
And ye passiden Jordan, and camen to Jerico; and men of that citee fouyten ayens you, Ammorrei, and Feresei, and Cananei, Ethei, and Gergesei, and Euei, and Jebusei; and Y bitook hem in to youre hondis.
12 Nikatuma manyigu mbele yenu, ambao pia waliwafukuza mbele yenu, hao wafalme wawili wa Waamori. Siyo upanga au upinde wenu wenyewe vilivyowapatia ushindi.
And Y sente flies with venemouse tongis bifor you, and Y castide hem out of her places; Y kyllide twei kyngis of Ammorreis, not in thi swerd and bowe.
13 Hivyo nikawapa ninyi nchi ambayo hamkuitaabikia na miji ambayo hamkuijenga na mnaishi ndani yake na kula toka kwa mashamba ya mizabibu na mizeituni msiyoipanda.’
And Y yaf to you the lond in which ye traueiliden not, and citees whiche ye bildiden not, that ye schulden dwelle in tho, and vyneris, and places of olyue trees, whiche ye plauntiden not.
14 “Sasa basi mcheni Bwana na kumtumikia kwa uaminifu wote. Itupeni mbali miungu ambayo baba zenu waliiabudu huko ngʼambo ya Mto Frati na huko Misri, nanyi mtumikieni Bwana.
Now therfor drede ye the Lord, and serue ye hym with perfite herte and moost trewe; and do ye awei the goddis, to whiche youre fadris seruyden in Mesopotanye, and in Egipt; and serue ye the Lord.
15 Lakini msipoona vyema kumtumikia Bwana, chagueni hivi leo mtakayemtumikia, kama ni miungu ile ambayo baba zenu waliitumikia ngʼambo Frati, au miungu ya Waamori, ambao mnakaa katika nchi yao. Lakini mimi na nyumba yangu, tutamtumikia Bwana.”
But if it semeth yuel to you, `that ye serue the Lord, chesyng is youun to you; chese ye to you to dai that, that plesith, whom ye owen most to serue; whether to goddis, whiche youre fadris serueden in Mesopotanye, whether to the goddis of Ammorreis, in whose lond ye dwellen; forsothe Y, and myn hows schulen serue the Lord.
16 Ndipo hao watu wakajibu, “Hili jambo liwe mbali nasi la kumsahau Bwana na kuitumikia miungu mingine!
And al the puple answeride and seide, Fer be it fro vs that we forsake the Lord, and serue alien goddis.
17 Bwana Mungu wetu mwenyewe ndiye alitutoa sisi na baba zetu akatupandisha kutoka Misri, kutoka nchi ile ya utumwa, na kutenda zile ishara kubwa mbele ya macho yetu. Ndiye aliyetulinda katika safari yetu yote na kutokana na mataifa yote ambayo tulipita katikati yao.
`Oure Lord God hym silf ledde vs and oure fadris out of the lond of Egipt, fro the hows of seruage, and dide grete signes in oure siyt; and he kepte vs in al the weie, bi which we yeden, and in alle puplis, bi whiche we passiden; and he castide out alle folkis,
18 Bwana akayafukuza mbele yetu mataifa yote pamoja na Waamori, walioishi katika nchi hii. Hivyo sisi nasi tutamtumikia Bwana kwa kuwa yeye ndiye Mungu wetu.”
Ammorrei, the dwellere of the lond, in to which we entriden. Therfor we schulen serue the Lord, for he is `oure Lord God.
19 Yoshua akawaambia watu, “Hamwezi kumtumikia Bwana. Yeye ni Mungu Mtakatifu, ni Mungu mwenye wivu. Hatasamehe uasi wenu na dhambi zenu.
And Josue seide to the puple, Ye moun not serue the Lord; for God is hooli, and a strong feruent louyere, and he foryyueth not youre trespassis and synnes.
20 Ikiwa mkimwacha Bwana na kuitumikia miungu migeni, atageuka na kuwaleteeni maafa na kuwaangamiza, baada ya kuwa mwema kwenu.”
If ye forsaken the Lord, and seruen alien goddis, the Lord schal turne `hym silf, and schal turment you, and schal distrie, after that he hath youe goodis to you.
21 Lakini watu wakamwambia Yoshua, “Sivyo! Sisi tutamtumikia Bwana.”
And the puple seide to Josue, It schal not be so, as thou spekist, but we schulen serue the Lord.
22 Ndipo Yoshua akawaambia, “Ninyi mmekuwa mashahidi juu yenu wenyewe kuwa mmechagua kumtumikia Bwana.” Nao wakajibu, “Ndiyo, tu mashahidi.”
And Josue seide to the puple, Ye ben witnessis, that ye han chose the Lord to you, that ye serue him. And thei answeriden, We ben witnessis.
23 Yoshua akawaambia, “Sasa basi, itupeni mbali hiyo miungu migeni iliyo katikati yenu, nanyi mtoleeni Bwana, Mungu wa Israeli, mioyo yenu.”
Therfor, he seide, Now do ye awei alien goddis fro the myddis of you, and bowe ye youre hertis to the Lord God of Israel.
24 Nao watu wakamwambia Yoshua, “Tutamtumikia Bwana Mungu wetu na kumtii yeye.”
And the puple seide to Josue, We schulen serue `oure Lord God, and we schulen be obedient to hise heestis.
25 Siku ile Yoshua akafanya agano kwa ajili ya watu na hapo Shekemu ndipo alipowaandikia amri na sheria.
Therfor Josue smoot a boond of pees in that dai, and settide forth to the puple comaundementis and domes in Sichen.
26 Naye Yoshua akayaandika mambo haya katika Kitabu cha Sheria ya Mungu. Ndipo akalitwaa jiwe kubwa, akalisimamisha huko chini ya mwaloni, karibu na mahali patakatifu pa Bwana.
And he wroot alle these wordis in the book of Goddis lawe. And he took a greet stoon, and puttide it vndur an ook, that was in the seyntuarie of the Lord.
27 Yoshua akawaambia watu wote, “Angalieni! Jiwe hili litakuwa shahidi juu yetu. Limesikia maneno yote Bwana aliyotuambia. Litakuwa shahidi juu yenu kama mtakuwa waongo kwa Mungu wenu.”
And he seide to al the puple, Lo! this stoon schal be to you in to witnessing, that ye herden alle the wordis of the Lord, whiche he spak to you, lest perauenture ye wolden denye aftirward, and lye to youre Lord God.
28 Basi Yoshua akawatuma watu kila mmoja aende katika urithi wake mwenyewe.
And he lefte the puple, ech man in to his possessioun.
29 Baada ya mambo haya, Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Bwana akafa akiwa na umri wa miaka mia moja na kumi.
And after these thingis Josue, the sone of Nun, the `seruaunt of the Lord, diede, an hundride yeer eld and ten.
30 Nao wakamzika katika nchi ya urithi wake, huko Timnath-Sera katika nchi ya vilima ya Efraimu, kaskazini ya Mlima wa Gaashi.
And thei birieden hym in the costis of his possessioun, in Thannath of Sare, which is set in the hil of Effraym, fro the north part of the hil Gaas.
31 Israeli wakamtumikia Bwana siku zote za maisha ya Yoshua, na za hao wazee walioishi baada ya Yoshua kufa, ambao waliona kila kitu Bwana alichowatendea Israeli.
And Israel seruede the Lord in alle the daies of Josue, and of the eldre men, that lyueden in long tyme aftir Josue, and whiche eldre men knewen alle the werkis of the Lord, whiche he hadde do in Israel.
32 Nayo ile mifupa ya Yosefu, ambayo Waisraeli waliipandisha kutoka huko Misri, wakaizika huko Shekemu kwenye eneo, ambalo Yakobo alilinunua kwa wana wa Hamori baba yake Shekemu, kwa vipande mia vya fedha. Eneo hili likawa ni urithi wa uzao wa Yosefu.
Also `the sones of Israel birieden the boonys of Joseph, whiche thei baren fro Egipt in Sichen, in the part of the feeld, which feeld Jacob bouyte of the sones of Emor, fadir of Sichen, for an hundrid yonge scheep; and it was in to possessioun of the sones of Joseph.
33 Naye Eleazari mwana wa Aroni akafariki akazikwa huko Gibea, mlima aliokuwa amepewa mtoto wake Finehasi, kwenye nchi ya vilima ya Efraimu.
Also Eliazar, sone of Aaron, preest, diede; and Fynees and hise sones biryden hym in Gabaa, which was youun to hym in the hil of Efraym.