< Yoshua 22 >

1 Ndipo Yoshua akawaita Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase,
یوشع مردان جنگی قبایل رئوبین، جاد و نصف قبیلهٔ منسی را فرا خواند
2 naye akawaambia, “Mmeshafanya yale yote Mose mtumishi wa Bwana aliyowaamuru, nanyi mmenitii kwa kila jambo nililowaamuru.
و به ایشان چنین فرمود: «هر چه موسی خدمتگزار خداوند به شما امر فرموده بود، انجام داده‌اید، و تمام دستورهای مرا نیز اطاعت کرده‌اید.
3 Kwa muda mrefu sasa, hadi siku hii ya leo, hamkuwaacha ndugu zenu, bali ninyi mmetimiza ile kazi Bwana Mungu wenu aliyowapa.
هر چند جنگ خیلی طول کشید، ولی شما در این مدت برادران خود را ترک نکردید بلکه مأموریتی را که یهوه، خدایتان به شما داده بود، انجام دادید.
4 Sasa kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewapa ndugu zenu pumziko kama alivyoahidi, rudini nyumbani mwenu katika nchi ile ambayo Mose mtumishi wa Bwana aliwapa ngʼambo ya Yordani.
اکنون یهوه، خدای شما مطابق وعدهٔ خود، به برادرانتان پیروزی و آرامش بخشیده است. پس به خانه‌های خود در آن سوی رود اردن که خداوند توسط خدمتگزار خود موسی به شما به ملکیت داده است، برگردید.
5 Lakini mwe waangalifu sana kushika amri na sheria zile Mose mtumishi wa Bwana alizowapa: yaani kumpenda Bwana Mungu wenu na kuenenda katika njia zake zote, kutii amri zake, kushikamana naye kwa uthabiti na kumtumikia kwa moyo wenu wote na roho yenu yote.”
به دقت آنچه را که موسی به شما دستور داده است، انجام دهید: یهوه، خدای خود را دوست بدارید، در راه او گام بردارید، احکامش را اطاعت کنید، به او بچسبید و با دل و جان او را خدمت نمایید.»
6 Ndipo Yoshua akawabariki na kuwaaga waende zao, nao wakaenda nyumbani mwao.
پس یوشع آنها را برکت داده، ایشان را به خانه‌هایشان روانه ساخت.
7 (Kwa nusu ya kabila la Manase Mose alikuwa amewapa eneo katika Bashani na ile nusu nyingine ya hilo kabila Yoshua aliwapa eneo upande wa magharibi ya Yordani pamoja na ndugu zao). Yoshua alipowaaga waende zao nyumbani, aliwabariki,
(موسی قبلاً در شرق رود اردن در باشان به نصف قبیلهٔ منسی زمین داده بود، و یوشع هم در غرب رود اردن به نصف دیگر آن قبیله، در میان قبایل دیگر، زمین بخشید.) در حالی که مردان جنگی عازم خانه‌های خود بودند، یوشع ایشان را برکت داده، گفت: «با ثروت بسیار، گله و رمه‌های بی‌شمار، طلا و نقره، مس و آهن، و پوشاک فراوان به خانه‌های خود بازگردید و این غنایم را با بستگان خود تقسیم نمایید.»
8 akisema, “Rudini nyumbani mwenu na utajiri wenu mwingi, yaani makundi makubwa ya mifugo, mkiwa na fedha, dhahabu, shaba na chuma, pia wingi wa nguo, nanyi mkagawane na ndugu zenu hizo nyara zilizotoka kwa adui zenu.”
9 Kwa hiyo Wareubeni, Wagadi na hiyo nusu ya kabila la Manase wakawaacha Waisraeli huko Shilo katika nchi ya Kanaani ili kurudi Gileadi, nchi yao wenyewe waliyoipata sawasawa na agizo la Bwana kupitia Mose.
پس مردان جنگی قبایل رئوبین، جاد، و نصف قبیلهٔ منسی، بنی‌اسرائیل را در شیلوه در سرزمین کنعان ترک نمودند و به سوی سرزمین خود در جلعاد که بنا به دستور خداوند به موسی، آن را تصرف کرده بودند، روانه شدند.
10 Walipofika Gelilothi karibu na Yordani, katika nchi ya Kanaani, Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase wakajenga madhabahu ya fahari kubwa huko kando ya Yordani.
وقتی قبایل رئوبین، جاد و نصف قبیله منسی به جلیلوت در کنار رود اردن در کنعان رسیدند، مذبح بسیار بزرگ و چشمگیری در کنار رود اردن بنا کردند. اما هنگامی که بقیهٔ قبایل اسرائیل این را شنیدند، در شیلوه جمع شدند تا به جنگ آنها بروند.
11 Waisraeli wengine waliposikia kwamba Wareubeni, Wagadi na ile nusu ya kabila la Manase walikuwa wamejenga madhabahu kwenye mpaka wa Kanaani huko Gelilothi karibu na Yordani kwenye upande wa Israeli,
12 kusanyiko lote la Israeli wakakusanyika huko Shilo ili wakapigane vita dhidi yao.
13 Kwa hiyo Waisraeli wengine wakamtuma Finehasi mwana wa kuhani Eleazari katika nchi ya Gileadi, kwa Wareubeni, Wagadi na hiyo nusu ya kabila la Manase.
ولی اول، عده‌ای را به رهبری فینحاس پسر العازار کاهن نزد ایشان به سرزمین جلعاد فرستادند.
14 Wakatuma pamoja naye watu kumi ambao ni viongozi, mmoja kwa kila kabila la Israeli, kila mmoja aliyekuwa kiongozi katika mgawanyiko wa jamaa miongoni mwa koo za Israeli.
افرادی که همراه فینحاس رفتند ده نفر بودند که هر کدام از آنها مقام سرپرستی خاندانی را بر عهده داشتند و به نمایندگی از طرف قبیلهٔ خود آمده بودند.
15 Walipofika Gileadi, kwa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase, wakawaambia:
وقتی این گروه به نزد قبایل رئوبین، جاد و نصف قبیلهٔ منسی در سرزمین جلعاد رسیدند،
16 “Kusanyiko lote la Bwana lasema: ‘Je, mmewezaje kuacha kumwamini Mungu wa Israeli jinsi hii? Mmewezaje kumwacha Bwana na kujijengea madhabahu dhidi yake na kumwasi?
به نمایندگی از طرف تمام قوم خداوند گفتند: «چرا از پیروی خداوند برگشته‌اید و با ساختن این مذبح از او روگردان شده، بر ضد خدای اسرائیل برخاسته‌اید؟
17 Je, dhambi ya Peori haikutosha? Hata ingawa kulikuja tauni juu ya kusanyiko la Bwana, mpaka leo hii hatujatakasika kutokana na dhambi hiyo!
آیا عقوبت پرستش بت بعل فغور برای ما کم بود؟ مگر فراموش کرده‌اید چه بلای وحشتناکی بر قوم خداوند عارض شد، به طوری که هنوز هم از آن کاملاً آزاد نشده‌ایم؟ مگر نمی‌دانید اگر امروز از دستور خداوند سرپیچی کنید فردا او بار دیگر بر همهٔ قوم اسرائیل خشمگین خواهد شد؟
18 Je, sasa ndiyo mnamwacha Bwana? “‘Kama mkimwasi Bwana leo, kesho atalikasirikia kusanyiko lote la Israeli.
19 Kama nchi mnayomiliki imenajisika, vukeni mje katika nchi ya Bwana, mahali Maskani ya Bwana ilipo, nanyi mkajitwalie sehemu miongoni mwetu, lakini msije mkaasi dhidi ya Bwana wala dhidi yetu sisi kwa kujijengea madhabahu, zaidi ya madhabahu ya Bwana Mungu wetu.
اگر زمین شما برای عبادت خداوند مناسب نیست، بهتر است به سرزمین خداوند که خیمهٔ عبادت در آنجاست بیایید و در این سرزمین با ما زندگی کنید، و با ساختن یک مذبح دیگر علاوه بر مذبحی که برای خداوند، خدای ما ساخته شده است، بر ضد خداوند و بر ضد ما برنخیزید.
20 Wakati Akani mwana wa Zera alipokosa uaminifu kwa vitu vilivyowekwa wakfu, je, ghadhabu haikulipata kusanyiko lote la Israeli? Hakuwa yeye peke yake aliyekufa kwa ajili ya dhambi yake.’”
آیا فراموش کرده‌اید که وقتی عخان پسر زارح مال حرام را برداشت، نه فقط او بلکه تمام قوم اسرائیل با او مجازات شدند؟»
21 Ndipo Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase walipowajibu viongozi wa koo za Israeli, wakisema:
قبایل رئوبین، جاد و نصف قبیلهٔ منسی به نمایندگان قبایل چنین پاسخ دادند:
22 “Yeye Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana! Yeye Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana! Yeye anajua! Israeli na wajue! Kama huu umekuwa ni uasi au kukosa utii kwa Bwana, msituache hai siku hii ya leo.
«یهوه، خدای خدایان می‌داند که قصد ما از بنای این مذبح چه بوده است و می‌خواهیم شما نیز بدانید. اگر ما با این کار از پیروی خداوند روگردان شده‌ایم و به او خیانت ورزیده‌ایم، شما ما را زنده نگذارید.
23 Kama tumejijengea madhabahu yetu wenyewe ili kumwacha Bwana na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka, au kutoa sadaka za amani juu yake, Bwana mwenyewe na atupatilize leo.
اگر از خداوند برگشته و این مذبح را ساخته‌ایم تا روی آن قربانی سوختنی، هدیه آردی و قربانی سلامتی تقدیم کنیم، خداوند خودش ما را مجازات کند.
24 “Sivyo! Tulifanya hivyo kwa hofu kwamba siku zijazo wazao wenu wanaweza wakawaambia wazao wetu, ‘Mna uhusiano gani na Bwana, Mungu wa Israeli?
ما این کار را از روی احتیاط انجام داده‌ایم، چون می‌ترسیم در آینده فرزندان شما به فرزندان ما بگویند: شما حق ندارید خداوند، خدای اسرائیل را پرستش کنید،
25 Bwana ameifanya Yordani kuwa mpaka kati yetu na ninyi, ninyi Wareubeni na Wagadi! Hamna fungu kwa Bwana.’ Kwa hiyo wazao wenu wanaweza wakawasababisha wazao wetu wakaacha kumcha Bwana.
زیرا شما سهمی در خداوند ندارید. خداوند رود اردن را بین ما و شما قرار داده است. و به این ترتیب فرزندان شما، فرزندان ما را از پرستش خداوند باز دارند.
26 “Hii ndiyo sababu tulisema, ‘Tujiweke tayari na tujenge madhabahu, lakini si kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa au dhabihu.’
پس تصمیم گرفتیم آن مذبح را بنا کنیم، البته نه برای تقدیم قربانی سوختنی و سایر قربانیها، بلکه تا بین ما و شما و فرزندانمان شاهدی باشد که ما هم حق داریم در خانهٔ خداوند او را با تقدیم قربانیهای سوختنی و سلامتی پرستش نماییم، و اگر فرزندان شما به فرزندان ما بگویند: شما سهمی در خداوند ندارید،
27 Badala yake, itakuwa ni ushahidi kati yetu na ninyi na vizazi vijavyo, kwamba tutamwabudu Bwana katika mahali patakatifu pake pamoja na sadaka zetu za kuteketezwa, dhabihu na sadaka za amani. Ndipo katika siku zijazo, wazao wenu hawataweza kuwaambia wazao wetu, ‘Ninyi hamna fungu katika Bwana.’
28 “Nasi tulisema, ‘Ikiwa wakati wowote watatuambia hilo, au kuwaambia uzao wetu, tutawajibu hivi: Angalieni nakala hii ya madhabahu ya Bwana, ambayo baba zetu waliijenga, si kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa na dhabihu, bali kama ushahidi kati yetu na ninyi.’
فرزندان ما بتوانند بگویند: این مذبح را نگاه کنید که پدران ما از روی نمونهٔ مذبح خداوند ساخته‌اند. این مذبح، برای تقدیم قربانیهای سوختنی و سایر قربانیها نیست بلکه نشانهٔ این است که ما هم حق داریم بیاییم و خدا را بپرستیم.
29 “Hili jambo la kumwasi Bwana na kumwacha siku hii ya leo kwa kujenga madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na dhabihu, zaidi ya madhabahu ya Bwana Mungu wetu iliyo mbele ya maskani yake na liwe mbali nasi.”
ما هرگز از پیروی خداوند دست برنمی‌داریم و با ساختن مذبحی برای تقدیم قربانی سوختنی، هدیهٔ آردی و سایر قربانیها از دستورهای او سرپیچی نمی‌کنیم. ما می‌دانیم تنها مذبحی که باید بر آن قربانی کرد، همان است که در عبادتگاه خداوند قرار دارد.»
30 Wakati kuhani Finehasi na viongozi wa kusanyiko na wakuu wa koo za Israeli, waliposikia hayo waliyosema Wareubeni, Wagadi na Manase, wakaridhika.
فینحاس کاهن و نمایندگان قبایل بنی‌اسرائیل که همراه وی بودند، چون این سخنان را از قبیله‌های رئوبین، جاد و نصف قبیلهٔ منسی شنیدند، قانع شدند.
31 Naye Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, akawaambia Wareubeni, Wagadi na Manase, “Leo tunajua kwamba Bwana yuko pamoja nasi, kwa sababu hamkukosa uaminifu kwa Bwana katika jambo hili. Sasa mmewaokoa Waisraeli na mkono wa Bwana.”
فینحاس پسر العازار به ایشان گفت: «امروز فهمیدیم که خداوند در میان ماست، زیرا شما بر ضد او برنخاسته‌اید بلکه برعکس، قوم ما را از نابودی نجات داده‌اید.»
32 Ndipo Finehasi, mwana wa kuhani Eleazari na viongozi wakarudi Kanaani kutoka kwenye kukutana kwao na Wareubeni na Wagadi huko Gileadi nao wakatoa taarifa kwa Waisraeli.
پس فینحاس پسر العازار و نمایندگان، از جلعاد به کنعان بازگشتند و هر آنچه را که شنیده بودند به بنی‌اسرائیل گزارش دادند.
33 Walifurahi kusikia taarifa hiyo, na wakamhimidi Mungu. Wala hawakuzungumza tena habari za kupigana vita dhidi yao ili kuharibu nchi ambayo Wareubeni na Wagadi waliishi.
با شنیدن گزارش آنها، همهٔ مردم اسرائیل شاد شدند و خدا را شکر نمودند و دیگر سخنی از جنگ با قبایل رئوبین و جاد و یا خراب کردن سرزمین آنها به میان نیامد.
34 Nao Wareubeni na Wagadi wakayaita yale madhabahu Edi, yaani Shahidi: kwa kuwa itakuwa shahidi kati yetu na ninyi kwamba Bwana ndiye Mungu.
قبایل رئوبین و جاد آن مذبحی را که بنا کرده بودند «مذبح شاهد» نامیدند و گفتند: «این مذبح بین ما و برادران ما شاهد است که خداوند، خدای ما نیز هست.»

< Yoshua 22 >