< Yoshua 22 >
1 Ndipo Yoshua akawaita Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase,
Dans le même temps, Josué appela les Rubénites et les Gadites et la demi-tribu de Manassé,
2 naye akawaambia, “Mmeshafanya yale yote Mose mtumishi wa Bwana aliyowaamuru, nanyi mmenitii kwa kila jambo nililowaamuru.
Et leur dit: Vous avez fait tout ce que vous a ordonné Moïse, serviteur du Seigneur: à moi aussi, vous m’avez obéi en toutes choses,
3 Kwa muda mrefu sasa, hadi siku hii ya leo, hamkuwaacha ndugu zenu, bali ninyi mmetimiza ile kazi Bwana Mungu wenu aliyowapa.
Et dans ce long temps, vous n’avez pas abandonné vos frères jusqu’au présent jour, gardant le commandement du Seigneur votre Dieu.
4 Sasa kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewapa ndugu zenu pumziko kama alivyoahidi, rudini nyumbani mwenu katika nchi ile ambayo Mose mtumishi wa Bwana aliwapa ngʼambo ya Yordani.
Puis donc que le Seigneur votre Dieu a donné à vos frères le repos et la paix, comme il a promis, retournez et allez dans vos tabernacles et dans la terre de possession que vous a livrée Moïse, serviteur du Seigneur, au-delà du Jourdain;
5 Lakini mwe waangalifu sana kushika amri na sheria zile Mose mtumishi wa Bwana alizowapa: yaani kumpenda Bwana Mungu wenu na kuenenda katika njia zake zote, kutii amri zake, kushikamana naye kwa uthabiti na kumtumikia kwa moyo wenu wote na roho yenu yote.”
En sorte seulement que vous gardiez attentivement et que vous accomplissiez par vos œuvres le commandement et la loi que vous a prescrite Moïse, serviteur du Seigneur, que vous aimiez le Seigneur votre Dieu, que vous marchiez dans toutes ses voies, que vous observiez ses commandements, que vous vous attachiez à lui, et que vous le serviez en tout votre cœur et en toute votre âme.
6 Ndipo Yoshua akawabariki na kuwaaga waende zao, nao wakaenda nyumbani mwao.
Et Josué les bénit et les renvoya; et ils retournèrent dans leurs tabernacles.
7 (Kwa nusu ya kabila la Manase Mose alikuwa amewapa eneo katika Bashani na ile nusu nyingine ya hilo kabila Yoshua aliwapa eneo upande wa magharibi ya Yordani pamoja na ndugu zao). Yoshua alipowaaga waende zao nyumbani, aliwabariki,
Quant à la demi-tribu de Manassé, Moïse lui avait donné une possession en Basan; et c’est pour cela que Josué donna à l’autre demi-tribu un lot parmi ses autres frères, au-delà du Jourdain, vers la partie occidentale. Lorsqu’il les renvoya dans leurs tabernacles, après les avoir bénis,
8 akisema, “Rudini nyumbani mwenu na utajiri wenu mwingi, yaani makundi makubwa ya mifugo, mkiwa na fedha, dhahabu, shaba na chuma, pia wingi wa nguo, nanyi mkagawane na ndugu zenu hizo nyara zilizotoka kwa adui zenu.”
Il leur dit: Retournez en vos demeures avec beaucoup de biens et de richesses, avec de l’argent et de l’or, de l’airain, du fer et beaucoup de vêtements; partagez avec vos frères le butin remporté sur les ennemis.
9 Kwa hiyo Wareubeni, Wagadi na hiyo nusu ya kabila la Manase wakawaacha Waisraeli huko Shilo katika nchi ya Kanaani ili kurudi Gileadi, nchi yao wenyewe waliyoipata sawasawa na agizo la Bwana kupitia Mose.
Ainsi, les enfants de Ruben, les enfants de Gad et la demi-tribu de Manassé s’éloignèrent des enfants d’Israël de Silo, qui est située en Chanaan, pour venir à Galaad, terre de leur possession, qu’ils avaient obtenue, selon le commandement du Seigneur par l’entremise de Moïse.
10 Walipofika Gelilothi karibu na Yordani, katika nchi ya Kanaani, Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase wakajenga madhabahu ya fahari kubwa huko kando ya Yordani.
Et lorsqu’ils furent revenus aux digues du Jourdain, dans la terre de Chanaan, ils bâtirent près du Jourdain un autel d’une immense grandeur.
11 Waisraeli wengine waliposikia kwamba Wareubeni, Wagadi na ile nusu ya kabila la Manase walikuwa wamejenga madhabahu kwenye mpaka wa Kanaani huko Gelilothi karibu na Yordani kwenye upande wa Israeli,
Lorsque les enfants d’Israël l’eurent appris, et que des messagers fidèles leur eurent rapporté que les enfants de Ruben, de Gad et de la demi-tribu de Manassé avaient bâti un autel dans la terre de Chanaan, sur les digues du Jourdain vis-à-vis des enfants d’Israël,
12 kusanyiko lote la Israeli wakakusanyika huko Shilo ili wakapigane vita dhidi yao.
Ils s’assemblèrent tous à Silo, pour monter et combattre contre eux.
13 Kwa hiyo Waisraeli wengine wakamtuma Finehasi mwana wa kuhani Eleazari katika nchi ya Gileadi, kwa Wareubeni, Wagadi na hiyo nusu ya kabila la Manase.
Et cependant ils envoyèrent vers eux, dans la terre de Galaad, Phinéès, fils d’Eléazar, le prêtre,
14 Wakatuma pamoja naye watu kumi ambao ni viongozi, mmoja kwa kila kabila la Israeli, kila mmoja aliyekuwa kiongozi katika mgawanyiko wa jamaa miongoni mwa koo za Israeli.
Et dix princes du peuple avec lui, un de chaque tribu.
15 Walipofika Gileadi, kwa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase, wakawaambia:
Lesquels vinrent vers les enfants de Ruben, de Gad et de la demi-tribu de Manassé, dans la terre de Galaad, et leur dirent:
16 “Kusanyiko lote la Bwana lasema: ‘Je, mmewezaje kuacha kumwamini Mungu wa Israeli jinsi hii? Mmewezaje kumwacha Bwana na kujijengea madhabahu dhidi yake na kumwasi?
Voici ce que mande tout le peuple du Seigneur: Quelle est cette transgression? Pourquoi avez-vous abandonné le Seigneur Dieu d’Israël, bâtissant un autel sacrilège, et vous éloignant de son culte?
17 Je, dhambi ya Peori haikutosha? Hata ingawa kulikuja tauni juu ya kusanyiko la Bwana, mpaka leo hii hatujatakasika kutokana na dhambi hiyo!
Est-ce peu pour vous, que vous ayez péché à Béelphégor, que jusqu’au présent jour la tache de ce crime demeure sur nous, et qu’un grand nombre d’entre le peuple ait succombé?
18 Je, sasa ndiyo mnamwacha Bwana? “‘Kama mkimwasi Bwana leo, kesho atalikasirikia kusanyiko lote la Israeli.
Et vous, aujourd’hui, vous avez abandonné le Seigneur, et demain contre tout Israël sa colère sévira.
19 Kama nchi mnayomiliki imenajisika, vukeni mje katika nchi ya Bwana, mahali Maskani ya Bwana ilipo, nanyi mkajitwalie sehemu miongoni mwetu, lakini msije mkaasi dhidi ya Bwana wala dhidi yetu sisi kwa kujijengea madhabahu, zaidi ya madhabahu ya Bwana Mungu wetu.
Que si vous croyez que la terre de votre possession est impure, passez à la terre dans laquelle est le tabernacle du Seigneur, et habitez parmi nous; seulement, ne vous éloignez point du Seigneur et de notre société, en bâtissant un autel, outre l’autel du Seigneur notre Dieu.
20 Wakati Akani mwana wa Zera alipokosa uaminifu kwa vitu vilivyowekwa wakfu, je, ghadhabu haikulipata kusanyiko lote la Israeli? Hakuwa yeye peke yake aliyekufa kwa ajili ya dhambi yake.’”
Est-ce qu’Achan, fils de Zaré, ne viola pas le commandement du Seigneur, et que la colère du Seigneur ne tomba pas sur tout le peuple d’Israël? Et lui était un seul homme; et plût à Dieu que, seul, il eût péri dans son crime!
21 Ndipo Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase walipowajibu viongozi wa koo za Israeli, wakisema:
Et les enfants de Ruben et de Gad, et la demi-tribu d’Israël répondirent aux princes de la légation d’Israël:
22 “Yeye Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana! Yeye Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana! Yeye anajua! Israeli na wajue! Kama huu umekuwa ni uasi au kukosa utii kwa Bwana, msituache hai siku hii ya leo.
Le très fort Dieu Seigneur, le très fort Dieu Seigneur, lui-même le sait, et Israël aussi le comprendra: si c’est dans un esprit de prévarication que nous avons construit cet autel, que le Seigneur ne nous garde point, mais qu’il nous punisse présentement;
23 Kama tumejijengea madhabahu yetu wenyewe ili kumwacha Bwana na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka, au kutoa sadaka za amani juu yake, Bwana mwenyewe na atupatilize leo.
Et si nous l’avons fait dans l’intention d’y offrir des holocaustes, un sacrifice et des victimes pacifiques, que lui-même instruise et juge;
24 “Sivyo! Tulifanya hivyo kwa hofu kwamba siku zijazo wazao wenu wanaweza wakawaambia wazao wetu, ‘Mna uhusiano gani na Bwana, Mungu wa Israeli?
Et si ce n’est pas plutôt dans la pensée et dans le but de dire: Demain, vos enfants diront à nos enfants: Qu’importe à vous et au Seigneur Dieu d’Israël?
25 Bwana ameifanya Yordani kuwa mpaka kati yetu na ninyi, ninyi Wareubeni na Wagadi! Hamna fungu kwa Bwana.’ Kwa hiyo wazao wenu wanaweza wakawasababisha wazao wetu wakaacha kumcha Bwana.
Le Seigneur a mis une borne entre nous et vous, ô enfants de Ruben et enfants de Gad! le fleuve du Jourdain; et c’est pour cela que vous n’avez point de part dans le Seigneur. Et à cette occasion vos enfants détourneront nos enfants de la crainte du Seigneur. Ainsi nous avons mieux pensé,
26 “Hii ndiyo sababu tulisema, ‘Tujiweke tayari na tujenge madhabahu, lakini si kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa au dhabihu.’
Et nous avons dit: Dressons-nous un autel, non pour offrir des holocaustes ou des victimes,
27 Badala yake, itakuwa ni ushahidi kati yetu na ninyi na vizazi vijavyo, kwamba tutamwabudu Bwana katika mahali patakatifu pake pamoja na sadaka zetu za kuteketezwa, dhabihu na sadaka za amani. Ndipo katika siku zijazo, wazao wenu hawataweza kuwaambia wazao wetu, ‘Ninyi hamna fungu katika Bwana.’
Mais en témoignage entre vous et nous, entre notre race et votre lignée, que nous servirons le Seigneur, qu’il est de notre droit d’offrir des holocaustes, des victimes et des hosties pacifiques, et qu’en aucune manière vos enfants ne diront demain à nos enfants: Il n’y a point de part pour vous dans le Seigneur.
28 “Nasi tulisema, ‘Ikiwa wakati wowote watatuambia hilo, au kuwaambia uzao wetu, tutawajibu hivi: Angalieni nakala hii ya madhabahu ya Bwana, ambayo baba zetu waliijenga, si kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa na dhabihu, bali kama ushahidi kati yetu na ninyi.’
Que s’ils veulent le dire, ils leur répondront: Voici l’autel du Seigneur, qu’ont fait nos pères, non pour des holocaustes ni pour un sacrifice, mais en témoignage entre nous et vous.
29 “Hili jambo la kumwasi Bwana na kumwacha siku hii ya leo kwa kujenga madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na dhabihu, zaidi ya madhabahu ya Bwana Mungu wetu iliyo mbele ya maskani yake na liwe mbali nasi.”
Loin de nous, le crime de nous séparer du Seigneur, et de quitter ses traces, en dressant un autel, pour offrir des holocaustes, des sacrifices et des victimes, hors l’autel du Seigneur notre Dieu, qui a été dressé devant son tabernacle.
30 Wakati kuhani Finehasi na viongozi wa kusanyiko na wakuu wa koo za Israeli, waliposikia hayo waliyosema Wareubeni, Wagadi na Manase, wakaridhika.
Ces paroles entendues, Phinéès, le prêtre, et les princes de la légation d’Israël, qui étaient avec lui, s’apaisèrent, et accueillirent du meilleur cœur les paroles des enfants de Ruben, de Gad et de la demi-tribu de Manassé.
31 Naye Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, akawaambia Wareubeni, Wagadi na Manase, “Leo tunajua kwamba Bwana yuko pamoja nasi, kwa sababu hamkukosa uaminifu kwa Bwana katika jambo hili. Sasa mmewaokoa Waisraeli na mkono wa Bwana.”
Alors Phinéès, le prêtre, fils d’Eléazar, leur dit: Maintenant nous savons que le Seigneur est avec nous, puisque vous êtes étrangers à cette prévarication, et que vous avez délivré les enfants d’Israël de la main du Seigneur.
32 Ndipo Finehasi, mwana wa kuhani Eleazari na viongozi wakarudi Kanaani kutoka kwenye kukutana kwao na Wareubeni na Wagadi huko Gileadi nao wakatoa taarifa kwa Waisraeli.
Après cela, il revint avec les princes du peuple d’auprès des enfants de Ruben et de Gad, de la terre de Galaad, confins de Chanaan, vers les enfants d’Israël, et il leur fit son rapport.
33 Walifurahi kusikia taarifa hiyo, na wakamhimidi Mungu. Wala hawakuzungumza tena habari za kupigana vita dhidi yao ili kuharibu nchi ambayo Wareubeni na Wagadi waliishi.
Or, ce discours plut à tous ceux qui l’entendirent, et les enfants d’Israël louèrent Dieu, et ils ne dirent plus qu’ils monteraient contre eux, qu’ils les combattraient, et qu’ils détruiraient la terre de leur possession.
34 Nao Wareubeni na Wagadi wakayaita yale madhabahu Edi, yaani Shahidi: kwa kuwa itakuwa shahidi kati yetu na ninyi kwamba Bwana ndiye Mungu.
Et les enfants de Ruben et les enfants de Gad appelèrent l’autel qu’ils avaient dressé, Notre témoignage que, c’est le Seigneur lui-même qui est Dieu.