< Yoshua 22 >

1 Ndipo Yoshua akawaita Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase,
Alors, Josué convoqua les fils de Ruben, les fils de Gad et la demi-tribu de Manassé.
2 naye akawaambia, “Mmeshafanya yale yote Mose mtumishi wa Bwana aliyowaamuru, nanyi mmenitii kwa kila jambo nililowaamuru.
Et il leur dit: Vous avez obéi à tout ce que vous avait ordonné Moïse, serviteur de Dieu; vous avez été dociles à ma voix, quand je vous ai rappelé tout ce qu'il vous avait prescrit.
3 Kwa muda mrefu sasa, hadi siku hii ya leo, hamkuwaacha ndugu zenu, bali ninyi mmetimiza ile kazi Bwana Mungu wenu aliyowapa.
Vous n'avez point abandonné vos frères, durant tous ces jours nombreux, et jusqu'à ce moment vous avez exécuté l'ordre du Seigneur notre Dieu.
4 Sasa kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewapa ndugu zenu pumziko kama alivyoahidi, rudini nyumbani mwenu katika nchi ile ambayo Mose mtumishi wa Bwana aliwapa ngʼambo ya Yordani.
Or, maintenant le Seigneur notre Dieu a donné la paix à nos frères, comme il le leur avait promis. Partez donc, retournez en vos demeures et dans la terre que Moïse vous a assignée au delà du Jourdain.
5 Lakini mwe waangalifu sana kushika amri na sheria zile Mose mtumishi wa Bwana alizowapa: yaani kumpenda Bwana Mungu wenu na kuenenda katika njia zake zote, kutii amri zake, kushikamana naye kwa uthabiti na kumtumikia kwa moyo wenu wote na roho yenu yote.”
Mais veillez diligemment à mettre en pratique les commandements et la loi que Moïse, serviteur de Dieu, vous a ordonné de pratiquer, savoir: d'aimer le Seigneur votre Dieu, de marcher en toutes ses voies, d'observer ses commandements, de vous attacher étroitement à lui, de le servir de tout votre esprit et de toute votre âme.
6 Ndipo Yoshua akawabariki na kuwaaga waende zao, nao wakaenda nyumbani mwao.
Et Josué les bénit, les congédia, et ils retournèrent en leurs demeures.
7 (Kwa nusu ya kabila la Manase Mose alikuwa amewapa eneo katika Bashani na ile nusu nyingine ya hilo kabila Yoshua aliwapa eneo upande wa magharibi ya Yordani pamoja na ndugu zao). Yoshua alipowaaga waende zao nyumbani, aliwabariki,
(Moïse avait donné des terres à la demi-tribu de Manassé dans le royaume de Basan, et Josué en avait donné à l'autre demi-tribu parmi leurs frères de ce côté du Jourdain à l'occident.) Lorsque Josué les renvoya dans leurs demeures, et qu'il les bénit,
8 akisema, “Rudini nyumbani mwenu na utajiri wenu mwingi, yaani makundi makubwa ya mifugo, mkiwa na fedha, dhahabu, shaba na chuma, pia wingi wa nguo, nanyi mkagawane na ndugu zenu hizo nyara zilizotoka kwa adui zenu.”
Ils retournèrent en leurs demeures avec beaucoup de richesses. Ils avaient partagé avec leurs frères un immense butin fait sur les ennemis: de nombreux troupeaux de bétail, de l'argent, de l'or et du fer, et beaucoup de vêtements.
9 Kwa hiyo Wareubeni, Wagadi na hiyo nusu ya kabila la Manase wakawaacha Waisraeli huko Shilo katika nchi ya Kanaani ili kurudi Gileadi, nchi yao wenyewe waliyoipata sawasawa na agizo la Bwana kupitia Mose.
Les fils de Ruben, les fils de Gad et la demi-tribu de Manassé se séparèrent donc des fils d'Israël à Silo, dans la terre de Chanaan, pour retourner en Galaad, dans la contrée qu'ils possédaient, et que le Seigneur, par la main de Moïse, leur avait donnée pour héritage.
10 Walipofika Gelilothi karibu na Yordani, katika nchi ya Kanaani, Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase wakajenga madhabahu ya fahari kubwa huko kando ya Yordani.
Et ils arrivèrent en Galaad sur le Jourdain, qui est dans la terre de Chanaan. Et les fils de Ruben, les fils de Gad et la demi-tribu de Manassé bâtirent en ce lieu, sur la rive du Jourdain, un grand autel qu'on apercevait de loin.
11 Waisraeli wengine waliposikia kwamba Wareubeni, Wagadi na ile nusu ya kabila la Manase walikuwa wamejenga madhabahu kwenye mpaka wa Kanaani huko Gelilothi karibu na Yordani kwenye upande wa Israeli,
Or, les fils d'Israël l'apprirent de gens qui leur dirent: Voilà que les fils de Ruben, les fils de Gad et la demi-tribu de Manassé, ont bâti un autel sur les confins de la terre de Chanaan, en Galaad aux bords du Jourdain, hors du territoire des fils d'Israël.
12 kusanyiko lote la Israeli wakakusanyika huko Shilo ili wakapigane vita dhidi yao.
Aussitôt, tous les fils d'Israël se rassemblèrent en Silo, pour s'en aller leur faire la guerre.
13 Kwa hiyo Waisraeli wengine wakamtuma Finehasi mwana wa kuhani Eleazari katika nchi ya Gileadi, kwa Wareubeni, Wagadi na hiyo nusu ya kabila la Manase.
Et les fils d'Israël envoyèrent aux fils de Ruben, aux fils de Gad, et aux fils de la demi-tribu de Manassé, en la terre de Galaad, Phinées, fils d'Eléazar, fils d'Aaron le grand prêtre,
14 Wakatuma pamoja naye watu kumi ambao ni viongozi, mmoja kwa kila kabila la Israeli, kila mmoja aliyekuwa kiongozi katika mgawanyiko wa jamaa miongoni mwa koo za Israeli.
Et avec lui dix chefs, chacun chef d'une famille paternelle de toutes les tribus d'Israël; ces chefs de famille, en Israël, sont commandants de mille hommes.
15 Walipofika Gileadi, kwa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase, wakawaambia:
Ils se rendirent auprès des fils de Ruben, des fils de Gad et de la demi- tribu de Manassé, en la terre de Galaad, et ils leur parlèrent, disant:
16 “Kusanyiko lote la Bwana lasema: ‘Je, mmewezaje kuacha kumwamini Mungu wa Israeli jinsi hii? Mmewezaje kumwacha Bwana na kujijengea madhabahu dhidi yake na kumwasi?
Toute la synagogue du Seigneur dit ces choses: Quel est ce péché que vous avez commis devant le Dieu d'Israël, en vous détournant aujourd'hui du Seigneur, et en vous bâtissant un autel, pour être des apostats du Seigneur?
17 Je, dhambi ya Peori haikutosha? Hata ingawa kulikuja tauni juu ya kusanyiko la Bwana, mpaka leo hii hatujatakasika kutokana na dhambi hiyo!
Est-ce si peu de chose à vos yeux que le crime de Phogor dont nous ne sommes pas encore purifiés, et qui a été une plaie dans la synagogue du Seigneur?
18 Je, sasa ndiyo mnamwacha Bwana? “‘Kama mkimwasi Bwana leo, kesho atalikasirikia kusanyiko lote la Israeli.
Et vous, vous vous détournez du Seigneur; or, si vous vous en détournez aujourd'hui, demain sa colère éclatera contre tout Israël.
19 Kama nchi mnayomiliki imenajisika, vukeni mje katika nchi ya Bwana, mahali Maskani ya Bwana ilipo, nanyi mkajitwalie sehemu miongoni mwetu, lakini msije mkaasi dhidi ya Bwana wala dhidi yetu sisi kwa kujijengea madhabahu, zaidi ya madhabahu ya Bwana Mungu wetu.
Mais quoi! la terre que vous possédez est-elle trop petite? Passez dans la terre que possède le Seigneur, dans celle où est dressé le tabernacle du Seigneur; venez la partager avec nous, et ne vous détournez pas du Seigneur; ne soyez pas apostats du Seigneur en élevant un autel autre que l'autel du Seigneur notre Dieu.
20 Wakati Akani mwana wa Zera alipokosa uaminifu kwa vitu vilivyowekwa wakfu, je, ghadhabu haikulipata kusanyiko lote la Israeli? Hakuwa yeye peke yake aliyekufa kwa ajili ya dhambi yake.’”
N'avez-vous pas vu Achar, fils de Zaré, quand il a péché au sujet de l'anathème? La colère du Seigneur n'a-t-elle pas éclaté contre tout Israël? A-t-il péri seul à cause du péché que lui seul avait commis?
21 Ndipo Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase walipowajibu viongozi wa koo za Israeli, wakisema:
Les fils de Ruben, les fils de Gad et la demi-tribu de Manassé, répondirent aux chefs d'Israël, et ils dirent:
22 “Yeye Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana! Yeye Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana! Yeye anajua! Israeli na wajue! Kama huu umekuwa ni uasi au kukosa utii kwa Bwana, msituache hai siku hii ya leo.
Dieu est le Seigneur Dieu, et Dieu, Dieu lui-même sait, et toute la synagogue d'Israël saura si nous avons commis contre le Seigneur le péché d'apostasie; si cela est, qu'il cesse dès ce jour de nous protéger.
23 Kama tumejijengea madhabahu yetu wenyewe ili kumwacha Bwana na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka, au kutoa sadaka za amani juu yake, Bwana mwenyewe na atupatilize leo.
Si nous avons bâti pour nous un autel en esprit d'apostasie contre le Seigneur notre Dieu, pour brûler sur cet autel des holocaustes, y offrir des hosties pacifiques, le Seigneur se vengera.
24 “Sivyo! Tulifanya hivyo kwa hofu kwamba siku zijazo wazao wenu wanaweza wakawaambia wazao wetu, ‘Mna uhusiano gani na Bwana, Mungu wa Israeli?
Mais nous avons fait cela par précaution, de peur que plus tard vos enfants ne disent aux nôtres: Qu'y a-t-il entre vous et le Dieu d'Israël?
25 Bwana ameifanya Yordani kuwa mpaka kati yetu na ninyi, ninyi Wareubeni na Wagadi! Hamna fungu kwa Bwana.’ Kwa hiyo wazao wenu wanaweza wakawasababisha wazao wetu wakaacha kumcha Bwana.
Le Seigneur vous a séparés de nous par le Jourdain, et vous n'avez point part au Seigneur. Ainsi, vos fils repousseront nos fils comme des étrangers, pour qu'ils n'honorent point le Seigneur.
26 “Hii ndiyo sababu tulisema, ‘Tujiweke tayari na tujenge madhabahu, lakini si kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa au dhabihu.’
Nous avons donc résolu d'élever cet autel, non pour y faire des oblations, non pour y sacrifier des victimes,
27 Badala yake, itakuwa ni ushahidi kati yetu na ninyi na vizazi vijavyo, kwamba tutamwabudu Bwana katika mahali patakatifu pake pamoja na sadaka zetu za kuteketezwa, dhabihu na sadaka za amani. Ndipo katika siku zijazo, wazao wenu hawataweza kuwaambia wazao wetu, ‘Ninyi hamna fungu katika Bwana.’
Mais pour qu'il soit entre vous et nous, entre votre postérité et la nôtre, un témoignage du culte que nous rendrons au Seigneur devant son tabernacle, par nos oblations de fruits, nos victimes et nos hosties pacifiques; de sorte que plus tard vos enfants ne disent point aux nôtres: Vous n'avez point part au Seigneur.
28 “Nasi tulisema, ‘Ikiwa wakati wowote watatuambia hilo, au kuwaambia uzao wetu, tutawajibu hivi: Angalieni nakala hii ya madhabahu ya Bwana, ambayo baba zetu waliijenga, si kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa na dhabihu, bali kama ushahidi kati yetu na ninyi.’
Et nous avons dit: S'il arrive un jour qu'ils tiennent ce langage à nous ou à notre postérité, il leur sera répondu: Voyez cette image de l'autel du Seigneur que nos pères ont faite, non pour y offrir des fruits ou des victimes, mais pour qu'elle soit un témoignage entre vous et nous et entre nos fils.
29 “Hili jambo la kumwasi Bwana na kumwacha siku hii ya leo kwa kujenga madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na dhabihu, zaidi ya madhabahu ya Bwana Mungu wetu iliyo mbele ya maskani yake na liwe mbali nasi.”
Que Dieu nous préserve donc aujourd'hui de nous détourner du Seigneur, d'être apostats du Seigneur, au point de bâtir pour nous un autel d'holocaustes et d'hosties pacifiques, autre que l'autel du Seigneur qui existe devant son tabernacle.
30 Wakati kuhani Finehasi na viongozi wa kusanyiko na wakuu wa koo za Israeli, waliposikia hayo waliyosema Wareubeni, Wagadi na Manase, wakaridhika.
Après avoir entendu les explications des fils de Ruben, des fils de Gad et de la demi-tribu de Manassé, Phinées le prêtre, et les chefs de la synagogue d'Israël en furent réjouis,
31 Naye Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, akawaambia Wareubeni, Wagadi na Manase, “Leo tunajua kwamba Bwana yuko pamoja nasi, kwa sababu hamkukosa uaminifu kwa Bwana katika jambo hili. Sasa mmewaokoa Waisraeli na mkono wa Bwana.”
Et Phinées le prêtre dit aux fils de Ruben, aux fils de Gad et à la demi- tribu de Manassé: Nous reconnaissons maintenant que le Seigneur est avec vous, parce que vous n'avez point commis de péché contre le Seigneur, et que vous sauvez les fils d'Israël de la main du Seigneur.
32 Ndipo Finehasi, mwana wa kuhani Eleazari na viongozi wakarudi Kanaani kutoka kwenye kukutana kwao na Wareubeni na Wagadi huko Gileadi nao wakatoa taarifa kwa Waisraeli.
Et Phinées le prêtre, et les chefs, quittant les fils de Ruben, les fils de Gad et la demi-tribu de Manassé, retournèrent de la terre de Galaad en celle de Chanaan auprès des fils d'Israël, et ils leur rapportèrent tout ce qui s'était dit.
33 Walifurahi kusikia taarifa hiyo, na wakamhimidi Mungu. Wala hawakuzungumza tena habari za kupigana vita dhidi yao ili kuharibu nchi ambayo Wareubeni na Wagadi waliishi.
Et cela réjouit les fils d'Israël; et, après leur avoir parle, ils bénirent tous le Dieu des fils d'Israël, et ils renoncèrent à marcher contre eux en guerre, et à ravager le domaine des fils de Ruben, des fils de Gad et de la demi-tribu de Manassé, qui continuèrent de l'habiter.
34 Nao Wareubeni na Wagadi wakayaita yale madhabahu Edi, yaani Shahidi: kwa kuwa itakuwa shahidi kati yetu na ninyi kwamba Bwana ndiye Mungu.
Et Josué appela l'autel des fils de Ruben, des fils de Gad et de la demi- tribu de Manassé: Autel du témoignage, parce que, dit-il, il rend entre eux témoignage que le Seigneur est leur Dieu.

< Yoshua 22 >