< Yoshua 22 >

1 Ndipo Yoshua akawaita Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase,
Josué appela les Rubénites, les Gadites et la demi-tribu de Manassé,
2 naye akawaambia, “Mmeshafanya yale yote Mose mtumishi wa Bwana aliyowaamuru, nanyi mmenitii kwa kila jambo nililowaamuru.
et leur dit: « Vous avez observé tout ce que Moïse, serviteur de Yahvé, vous a prescrit, et vous avez écouté ma voix dans tout ce que je vous ai commandé.
3 Kwa muda mrefu sasa, hadi siku hii ya leo, hamkuwaacha ndugu zenu, bali ninyi mmetimiza ile kazi Bwana Mungu wenu aliyowapa.
Vous n'avez pas quitté vos frères depuis tant de jours jusqu'à ce jour, mais vous avez observé le commandement de l'Éternel, votre Dieu.
4 Sasa kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewapa ndugu zenu pumziko kama alivyoahidi, rudini nyumbani mwenu katika nchi ile ambayo Mose mtumishi wa Bwana aliwapa ngʼambo ya Yordani.
Maintenant, l'Éternel, ton Dieu, a donné du repos à tes frères, comme il le leur avait dit. Maintenant, retourne et va dans tes tentes, dans le pays que tu possèdes et que Moïse, serviteur de l'Éternel, t'a donné au-delà du Jourdain.
5 Lakini mwe waangalifu sana kushika amri na sheria zile Mose mtumishi wa Bwana alizowapa: yaani kumpenda Bwana Mungu wenu na kuenenda katika njia zake zote, kutii amri zake, kushikamana naye kwa uthabiti na kumtumikia kwa moyo wenu wote na roho yenu yote.”
Prends seulement garde de mettre en pratique le commandement et la loi que Moïse, serviteur de Yahvé, t'a prescrits, d'aimer Yahvé ton Dieu, de marcher dans toutes ses voies, de garder ses commandements, de t'attacher à lui et de le servir de tout ton cœur et de toute ton âme. »
6 Ndipo Yoshua akawabariki na kuwaaga waende zao, nao wakaenda nyumbani mwao.
Et Josué les bénit, et les renvoya; et ils s'en allèrent dans leurs tentes.
7 (Kwa nusu ya kabila la Manase Mose alikuwa amewapa eneo katika Bashani na ile nusu nyingine ya hilo kabila Yoshua aliwapa eneo upande wa magharibi ya Yordani pamoja na ndugu zao). Yoshua alipowaaga waende zao nyumbani, aliwabariki,
Moïse avait donné à l'une des demi-tribus de Manassé un héritage en Basan; mais Josué donna à l'autre moitié un héritage parmi leurs frères, au-delà du Jourdain, vers l'occident. Lorsque Josué les renvoya dans leurs tentes, il les bénit,
8 akisema, “Rudini nyumbani mwenu na utajiri wenu mwingi, yaani makundi makubwa ya mifugo, mkiwa na fedha, dhahabu, shaba na chuma, pia wingi wa nguo, nanyi mkagawane na ndugu zenu hizo nyara zilizotoka kwa adui zenu.”
et leur parla ainsi: « Retournez dans vos tentes avec beaucoup de richesses, avec beaucoup de bétail, avec de l'argent, de l'or, du bronze, du fer, et avec beaucoup de vêtements. Partagez le butin de vos ennemis avec vos frères. »
9 Kwa hiyo Wareubeni, Wagadi na hiyo nusu ya kabila la Manase wakawaacha Waisraeli huko Shilo katika nchi ya Kanaani ili kurudi Gileadi, nchi yao wenyewe waliyoipata sawasawa na agizo la Bwana kupitia Mose.
Les fils de Ruben, les fils de Gad et la demi-tribu de Manassé s'en retournèrent et quittèrent les enfants d'Israël de Silo, qui est dans le pays de Canaan, pour aller au pays de Galaad, dans le pays qui leur appartenait, selon le commandement de l'Éternel par Moïse.
10 Walipofika Gelilothi karibu na Yordani, katika nchi ya Kanaani, Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase wakajenga madhabahu ya fahari kubwa huko kando ya Yordani.
Lorsqu'ils arrivèrent dans la région proche du Jourdain, c'est-à-dire dans le pays de Canaan, les fils de Ruben, les fils de Gad et la demi-tribu de Manassé construisirent un autel près du Jourdain, un grand autel à contempler.
11 Waisraeli wengine waliposikia kwamba Wareubeni, Wagadi na ile nusu ya kabila la Manase walikuwa wamejenga madhabahu kwenye mpaka wa Kanaani huko Gelilothi karibu na Yordani kwenye upande wa Israeli,
Les enfants d'Israël entendirent ceci: « Voici que les fils de Ruben, les fils de Gad et la demi-tribu de Manassé ont bâti un autel le long de la frontière du pays de Canaan, dans la région du Jourdain, du côté des enfants d'Israël. »
12 kusanyiko lote la Israeli wakakusanyika huko Shilo ili wakapigane vita dhidi yao.
Lorsque les enfants d'Israël l'apprirent, toute l'assemblée des enfants d'Israël se rassembla à Silo, pour monter contre eux en guerre.
13 Kwa hiyo Waisraeli wengine wakamtuma Finehasi mwana wa kuhani Eleazari katika nchi ya Gileadi, kwa Wareubeni, Wagadi na hiyo nusu ya kabila la Manase.
Les enfants d'Israël envoyèrent aux fils de Ruben, aux fils de Gad et à la demi-tribu de Manassé, dans le pays de Galaad, Phinées, fils du sacrificateur Éléazar.
14 Wakatuma pamoja naye watu kumi ambao ni viongozi, mmoja kwa kila kabila la Israeli, kila mmoja aliyekuwa kiongozi katika mgawanyiko wa jamaa miongoni mwa koo za Israeli.
Il avait avec lui dix princes, un prince d'une maison paternelle pour chacune des tribus d'Israël, et ils étaient chacun à la tête de leur maison paternelle parmi les milliers d'Israël.
15 Walipofika Gileadi, kwa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase, wakawaambia:
Ils allèrent vers les fils de Ruben, les fils de Gad et la demi-tribu de Manassé, au pays de Galaad, et ils leur parlèrent ainsi:
16 “Kusanyiko lote la Bwana lasema: ‘Je, mmewezaje kuacha kumwamini Mungu wa Israeli jinsi hii? Mmewezaje kumwacha Bwana na kujijengea madhabahu dhidi yake na kumwasi?
« Toute l'assemblée de l'Éternel dit: Quelle faute avez-vous commise contre le Dieu d'Israël, en vous détournant aujourd'hui de l'Éternel, en vous construisant un autel, pour vous révolter aujourd'hui contre l'Éternel?
17 Je, dhambi ya Peori haikutosha? Hata ingawa kulikuja tauni juu ya kusanyiko la Bwana, mpaka leo hii hatujatakasika kutokana na dhambi hiyo!
L'iniquité de Péor est-elle trop légère pour nous, dont nous ne nous sommes pas purifiés jusqu'à ce jour, bien qu'une plaie ait frappé la congrégation de l'Éternel,
18 Je, sasa ndiyo mnamwacha Bwana? “‘Kama mkimwasi Bwana leo, kesho atalikasirikia kusanyiko lote la Israeli.
pour que vous vous détourniez aujourd'hui de l'Éternel? Puisque vous vous rebellez aujourd'hui contre l'Éternel, il s'irritera demain contre toute la congrégation d'Israël.
19 Kama nchi mnayomiliki imenajisika, vukeni mje katika nchi ya Bwana, mahali Maskani ya Bwana ilipo, nanyi mkajitwalie sehemu miongoni mwetu, lakini msije mkaasi dhidi ya Bwana wala dhidi yetu sisi kwa kujijengea madhabahu, zaidi ya madhabahu ya Bwana Mungu wetu.
Mais si le pays de votre propriété est impur, passez dans le pays de la propriété de l'Éternel, où habite le tabernacle de l'Éternel, et prenez possession au milieu de nous; mais ne vous révoltez pas contre l'Éternel, et ne vous révoltez pas contre nous, en bâtissant un autel autre que l'autel de l'Éternel, notre Dieu.
20 Wakati Akani mwana wa Zera alipokosa uaminifu kwa vitu vilivyowekwa wakfu, je, ghadhabu haikulipata kusanyiko lote la Israeli? Hakuwa yeye peke yake aliyekufa kwa ajili ya dhambi yake.’”
Acan, fils de Zérah, n'a-t-il pas commis une faute dans la chose dévouée, et la colère n'est-elle pas tombée sur toute la congrégation d'Israël? Cet homme n'a pas péri seul dans son iniquité.'"
21 Ndipo Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase walipowajibu viongozi wa koo za Israeli, wakisema:
Alors les fils de Ruben, les fils de Gad et la demi-tribu de Manassé prirent la parole et dirent aux chefs des milliers d'Israéliens:
22 “Yeye Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana! Yeye Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana! Yeye anajua! Israeli na wajue! Kama huu umekuwa ni uasi au kukosa utii kwa Bwana, msituache hai siku hii ya leo.
« Le Puissant, Dieu, Yahvé, le Puissant, Dieu, Yahvé, il le sait, et Israël le saura: si c'est par rébellion, ou par infidélité à Yahvé (ne nous sauve pas aujourd'hui),
23 Kama tumejijengea madhabahu yetu wenyewe ili kumwacha Bwana na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka, au kutoa sadaka za amani juu yake, Bwana mwenyewe na atupatilize leo.
que nous nous sommes bâti un autel pour nous détourner de Yahvé, ou si c'est pour offrir un holocauste ou une offrande, ou si c'est pour offrir des sacrifices d'actions de grâces, que Yahvé lui-même le demande.
24 “Sivyo! Tulifanya hivyo kwa hofu kwamba siku zijazo wazao wenu wanaweza wakawaambia wazao wetu, ‘Mna uhusiano gani na Bwana, Mungu wa Israeli?
Si nous n'avons pas agi ainsi, c'est pour une raison précise: « Dans l'avenir, vos enfants pourront parler à nos enfants en disant: « Qu'avez-vous à faire avec Yahvé, le Dieu d'Israël?
25 Bwana ameifanya Yordani kuwa mpaka kati yetu na ninyi, ninyi Wareubeni na Wagadi! Hamna fungu kwa Bwana.’ Kwa hiyo wazao wenu wanaweza wakawasababisha wazao wetu wakaacha kumcha Bwana.
Car Yahvé a fait du Jourdain une frontière entre nous et vous, enfants de Ruben et enfants de Gad. Vous n'avez pas de part dans Yahvé. »'' Ainsi vos enfants pourraient amener nos enfants à cesser de craindre Yahvé.
26 “Hii ndiyo sababu tulisema, ‘Tujiweke tayari na tujenge madhabahu, lakini si kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa au dhabihu.’
Nous avons donc dit: « Préparons-nous à nous bâtir un autel, non pour des holocaustes ou des sacrifices,
27 Badala yake, itakuwa ni ushahidi kati yetu na ninyi na vizazi vijavyo, kwamba tutamwabudu Bwana katika mahali patakatifu pake pamoja na sadaka zetu za kuteketezwa, dhabihu na sadaka za amani. Ndipo katika siku zijazo, wazao wenu hawataweza kuwaambia wazao wetu, ‘Ninyi hamna fungu katika Bwana.’
mais comme témoin entre nous et vous, et entre nos générations après nous, pour accomplir devant lui le service de l'Éternel par nos holocaustes, nos sacrifices et nos sacrifices d'actions de grâces, afin que vos enfants ne disent pas un jour à nos enfants: « Vous n'avez pas de part à l'Éternel ».
28 “Nasi tulisema, ‘Ikiwa wakati wowote watatuambia hilo, au kuwaambia uzao wetu, tutawajibu hivi: Angalieni nakala hii ya madhabahu ya Bwana, ambayo baba zetu waliijenga, si kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa na dhabihu, bali kama ushahidi kati yetu na ninyi.’
« C'est pourquoi nous avons dit: « Lorsqu'on nous le dira, à nous ou à nos descendants, dans l'avenir, nous dirons: « Voici le modèle de l'autel de Yahvé, que nos pères ont construit, non pour l'holocauste ou le sacrifice, mais comme témoin entre nous et vous ».
29 “Hili jambo la kumwasi Bwana na kumwacha siku hii ya leo kwa kujenga madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na dhabihu, zaidi ya madhabahu ya Bwana Mungu wetu iliyo mbele ya maskani yake na liwe mbali nasi.”
« Loin de nous l'idée de nous révolter contre Yahvé et de nous détourner aujourd'hui de Yahvé pour construire un autel pour des holocaustes, des offrandes ou des sacrifices, en dehors de l'autel de Yahvé, notre Dieu, qui est devant sa tente! »
30 Wakati kuhani Finehasi na viongozi wa kusanyiko na wakuu wa koo za Israeli, waliposikia hayo waliyosema Wareubeni, Wagadi na Manase, wakaridhika.
Le sacrificateur Phinées et les chefs de l'assemblée, les chefs des milliers d'Israélites qui étaient avec lui, entendirent les paroles que prononcèrent les fils de Ruben, les fils de Gad et les fils de Manassé, et cela leur plut.
31 Naye Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, akawaambia Wareubeni, Wagadi na Manase, “Leo tunajua kwamba Bwana yuko pamoja nasi, kwa sababu hamkukosa uaminifu kwa Bwana katika jambo hili. Sasa mmewaokoa Waisraeli na mkono wa Bwana.”
Phinées, fils du prêtre Éléazar, dit aux fils de Ruben, aux fils de Gad et aux fils de Manassé: « Nous savons aujourd'hui que l'Éternel est au milieu de nous, car vous n'avez pas commis cette faute contre l'Éternel. Maintenant, vous avez délivré les enfants d'Israël de la main de l'Éternel. »
32 Ndipo Finehasi, mwana wa kuhani Eleazari na viongozi wakarudi Kanaani kutoka kwenye kukutana kwao na Wareubeni na Wagadi huko Gileadi nao wakatoa taarifa kwa Waisraeli.
Phinées, fils du prêtre Éléazar, et les princes, revinrent des fils de Ruben et des fils de Gad, du pays de Galaad au pays de Canaan, vers les enfants d'Israël, et leur rapportèrent la parole.
33 Walifurahi kusikia taarifa hiyo, na wakamhimidi Mungu. Wala hawakuzungumza tena habari za kupigana vita dhidi yao ili kuharibu nchi ambayo Wareubeni na Wagadi waliishi.
La chose plut aux enfants d'Israël; et les enfants d'Israël bénirent Dieu, et ne parlèrent plus de monter contre eux pour faire la guerre et détruire le pays où habitaient les fils de Ruben et les fils de Gad.
34 Nao Wareubeni na Wagadi wakayaita yale madhabahu Edi, yaani Shahidi: kwa kuwa itakuwa shahidi kati yetu na ninyi kwamba Bwana ndiye Mungu.
Les fils de Ruben et les fils de Gad donnèrent à l'autel le nom de « Témoin entre nous que Yahvé est Dieu ».

< Yoshua 22 >