< Yoshua 22 >

1 Ndipo Yoshua akawaita Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase,
Tada sazove Jošua sinove Rubenove i Gadove i polovinu plemena Manašeova
2 naye akawaambia, “Mmeshafanya yale yote Mose mtumishi wa Bwana aliyowaamuru, nanyi mmenitii kwa kila jambo nililowaamuru.
i reče im: “Izvršili ste sve što vam je Mojsije, sluga Jahvin, zapovjedio i poslušali ste me u svemu što sam vam zapovjedio.
3 Kwa muda mrefu sasa, hadi siku hii ya leo, hamkuwaacha ndugu zenu, bali ninyi mmetimiza ile kazi Bwana Mungu wenu aliyowapa.
Niste ostavili svoje braće unatoč dugom vojevanju do današnjega dana i vršili ste vjerno zapovijedi Jahve, Boga svojega.
4 Sasa kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewapa ndugu zenu pumziko kama alivyoahidi, rudini nyumbani mwenu katika nchi ile ambayo Mose mtumishi wa Bwana aliwapa ngʼambo ya Yordani.
Sada je Jahve, Bog vaš, dao mir braći vašoj, kako im bijaše obećao. Vratite se sada u svoje šatore, u zemlju koju vam je dao Mojsije, sluga Jahvin, u baštinu s onu stranu Jordana.
5 Lakini mwe waangalifu sana kushika amri na sheria zile Mose mtumishi wa Bwana alizowapa: yaani kumpenda Bwana Mungu wenu na kuenenda katika njia zake zote, kutii amri zake, kushikamana naye kwa uthabiti na kumtumikia kwa moyo wenu wote na roho yenu yote.”
Samo pazite da vršite zapovijedi i Zakon što vam ga dade Mojsije, sluga Jahvin: da ljubite Jahvu, Boga svojega, da uvijek idete putovima njegovim, da čuvate zapovijedi njegove, da se držite uz njega i da mu služite svim srcem i svom dušom.”
6 Ndipo Yoshua akawabariki na kuwaaga waende zao, nao wakaenda nyumbani mwao.
I blagoslovi ih Jošua i otpusti, a oni se zatim vrate u svoje šatore.
7 (Kwa nusu ya kabila la Manase Mose alikuwa amewapa eneo katika Bashani na ile nusu nyingine ya hilo kabila Yoshua aliwapa eneo upande wa magharibi ya Yordani pamoja na ndugu zao). Yoshua alipowaaga waende zao nyumbani, aliwabariki,
Mojsije bijaše jednoj polovini plemena Manašeova dao baštinu u Bašanu; a drugoj polovini dade je Jošua usred njihove braće zapadno od Jordana. Otpuštajući ih u njihove šatore, Jošua ih blagoslovi.
8 akisema, “Rudini nyumbani mwenu na utajiri wenu mwingi, yaani makundi makubwa ya mifugo, mkiwa na fedha, dhahabu, shaba na chuma, pia wingi wa nguo, nanyi mkagawane na ndugu zenu hizo nyara zilizotoka kwa adui zenu.”
I reče im: “Vratite se u svoje šatore s velikim blagom i s mnogom stokom, sa srebrom, zlatom, tučem, željezom i haljinama u izobilju i podijelite plijen od neprijatelja svojih s braćom svojom.”
9 Kwa hiyo Wareubeni, Wagadi na hiyo nusu ya kabila la Manase wakawaacha Waisraeli huko Shilo katika nchi ya Kanaani ili kurudi Gileadi, nchi yao wenyewe waliyoipata sawasawa na agizo la Bwana kupitia Mose.
Vratiše se sinovi Rubenovi i sinovi Gadovi i polovina plemena Manašeova; odoše od sinova Izraelovih iz Šila u zemlji kanaanskoj da krenu u zemlju gileadsku, na svoju baštinu koju su zaposjeli, kako im je zapovjedio Jahve preko Mojsija.
10 Walipofika Gelilothi karibu na Yordani, katika nchi ya Kanaani, Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase wakajenga madhabahu ya fahari kubwa huko kando ya Yordani.
Kad su stigli do jordanskog područja u zemlji kanaanskoj, podigoše sinovi Rubenovi, sinovi Gadovi i polovina plemena Manašeova žrtvenik na Jordanu, žrtvenik velik, izdaleka se vidio.
11 Waisraeli wengine waliposikia kwamba Wareubeni, Wagadi na ile nusu ya kabila la Manase walikuwa wamejenga madhabahu kwenye mpaka wa Kanaani huko Gelilothi karibu na Yordani kwenye upande wa Israeli,
Čuli Izraelci gdje se govori: “Evo, sinovi Rubenovi, sinovi Gadovi i polovina plemena Manašeova podigoše žrtvenik prema zemlji kanaanskoj, kod Jordana, na izraelskoj strani.”
12 kusanyiko lote la Israeli wakakusanyika huko Shilo ili wakapigane vita dhidi yao.
Na to se skupi sva zajednica sinova Izraelovih u Šilu da pođu u boj na njih.
13 Kwa hiyo Waisraeli wengine wakamtuma Finehasi mwana wa kuhani Eleazari katika nchi ya Gileadi, kwa Wareubeni, Wagadi na hiyo nusu ya kabila la Manase.
Izraelci sinovima Rubenovim, sinovima Gadovim i polovini plemena Manašeova u gileadsku zemlju poslaše Pinhasa, sina svećenika Eleazara,
14 Wakatuma pamoja naye watu kumi ambao ni viongozi, mmoja kwa kila kabila la Israeli, kila mmoja aliyekuwa kiongozi katika mgawanyiko wa jamaa miongoni mwa koo za Israeli.
i s njime deset knezova, po jednoga rodovskog glavara od svakoga plemena Izraelova, a svaki je od njih bio glavar obitelji među tisućama porodica Izraelovih.
15 Walipofika Gileadi, kwa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase, wakawaambia:
I kad oni dođoše k sinovima Rubenovim, sinovima Gadovim i polovini plemena Manašeova u zemlju gileadsku, rekoše im:
16 “Kusanyiko lote la Bwana lasema: ‘Je, mmewezaje kuacha kumwamini Mungu wa Israeli jinsi hii? Mmewezaje kumwacha Bwana na kujijengea madhabahu dhidi yake na kumwasi?
“Evo što veli sva zajednica Jahvina: 'Što znači nevjera koju činite protiv Jahve, Boga Izraelova? Zašto se odvrgoste danas od Jahve i, podigavši žrtvenik, zašto se bunite protiv Jahve?
17 Je, dhambi ya Peori haikutosha? Hata ingawa kulikuja tauni juu ya kusanyiko la Bwana, mpaka leo hii hatujatakasika kutokana na dhambi hiyo!
Zar vam nije dosta zločina iz Peora, od kojega se nismo očistili do dana današnjega i zbog kojega je došao pomor na zajednicu Jahvinu?
18 Je, sasa ndiyo mnamwacha Bwana? “‘Kama mkimwasi Bwana leo, kesho atalikasirikia kusanyiko lote la Israeli.
Ako se danas odvraćate od Jahve i bunite se danas protiv njega, neće li se sutra izliti njegov gnjev na svu zajednicu Izraelovu?
19 Kama nchi mnayomiliki imenajisika, vukeni mje katika nchi ya Bwana, mahali Maskani ya Bwana ilipo, nanyi mkajitwalie sehemu miongoni mwetu, lakini msije mkaasi dhidi ya Bwana wala dhidi yetu sisi kwa kujijengea madhabahu, zaidi ya madhabahu ya Bwana Mungu wetu.
Ili vam je možda zemlja vaše baštine nečista? Onda prijeđite u zemlju baštine Jahvine, u kojoj je Jahvino Prebivalište, i prebivajte među nama. Ali se ne bunite protiv Jahve i ne bunite se protiv nas dižući sebi žrtvenik mimo žrtvenik Jahve, Boga našega.
20 Wakati Akani mwana wa Zera alipokosa uaminifu kwa vitu vilivyowekwa wakfu, je, ghadhabu haikulipata kusanyiko lote la Israeli? Hakuwa yeye peke yake aliyekufa kwa ajili ya dhambi yake.’”
Nije li se Akan, Zerahov sin, sam ogriješio o 'herem' te se oborila srdžba na svu zajednicu Izraelovu? Zar nije umro zbog krivice svoje?'”
21 Ndipo Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase walipowajibu viongozi wa koo za Israeli, wakisema:
Tada odgovoriše sinovi Rubenovi, sinovi Gadovi i polovina plemena Manašeova govoreći plemenskim glavarima Izraelovim:
22 “Yeye Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana! Yeye Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana! Yeye anajua! Israeli na wajue! Kama huu umekuwa ni uasi au kukosa utii kwa Bwana, msituache hai siku hii ya leo.
“Bog, Bog Jahve, Bog nad bogovima, Jahve zna i neka zna Izrael: ako je to bila pobuna ili nevjernost prema Jahvi, neka nam uskrati svoju pomoć danas;
23 Kama tumejijengea madhabahu yetu wenyewe ili kumwacha Bwana na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka, au kutoa sadaka za amani juu yake, Bwana mwenyewe na atupatilize leo.
ako smo podigli žrtvenik da se odvrgnemo od Jahve i da prinosimo žrtve paljenice, prinosnice i žrtve pričesnice, neka nam onda sudi Jahve!
24 “Sivyo! Tulifanya hivyo kwa hofu kwamba siku zijazo wazao wenu wanaweza wakawaambia wazao wetu, ‘Mna uhusiano gani na Bwana, Mungu wa Israeli?
Učinismo to od brige i skrbi i rekosmo: 'Jednoga će dana sinovi vaši reći našima: Što vam je zajedničko s Jahvom, Bogom Izraelovim?
25 Bwana ameifanya Yordani kuwa mpaka kati yetu na ninyi, ninyi Wareubeni na Wagadi! Hamna fungu kwa Bwana.’ Kwa hiyo wazao wenu wanaweza wakawasababisha wazao wetu wakaacha kumcha Bwana.
Zar nije, sinovi Rubenovi i sinovi Gadovi, postavio Jahve između vas i nas među našu - Jordan? Vi nemate dijela s Jahvom.' I tako bi sinovi vaši mogli učiniti da se sinovi naši odvrate te ne štuju Jahvu.
26 “Hii ndiyo sababu tulisema, ‘Tujiweke tayari na tujenge madhabahu, lakini si kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa au dhabihu.’
Zato smo rekli: 'Podignimo žrtvenik, ali ne za žrtve paljenice niti za klanice,
27 Badala yake, itakuwa ni ushahidi kati yetu na ninyi na vizazi vijavyo, kwamba tutamwabudu Bwana katika mahali patakatifu pake pamoja na sadaka zetu za kuteketezwa, dhabihu na sadaka za amani. Ndipo katika siku zijazo, wazao wenu hawataweza kuwaambia wazao wetu, ‘Ninyi hamna fungu katika Bwana.’
nego da bude svjedočanstvo između nas i vas, među potomcima našim, da želimo služiti Jahvi paljenicama, klanicama i pričesnicama. Tako da ne mognu jednom vaši sinovi reći našima: Nemate dijela s Jahvom.'
28 “Nasi tulisema, ‘Ikiwa wakati wowote watatuambia hilo, au kuwaambia uzao wetu, tutawajibu hivi: Angalieni nakala hii ya madhabahu ya Bwana, ambayo baba zetu waliijenga, si kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa na dhabihu, bali kama ushahidi kati yetu na ninyi.’
Ako bi kada tako rekli nama i potomcima našim, mogli bismo odgovoriti: 'Pogledajte slog žrtvenika Jahvina što su ga podigli oci naši ne za žrtve paljenice ni klanice, nego za svjedočanstvo između nas i vas.'
29 “Hili jambo la kumwasi Bwana na kumwacha siku hii ya leo kwa kujenga madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na dhabihu, zaidi ya madhabahu ya Bwana Mungu wetu iliyo mbele ya maskani yake na liwe mbali nasi.”
Nije nam ni na kraj pameti pomisao da se bunimo protiv Jahve i da se odvraćamo od njega dižući žrtvenik za žrtve paljenice, prinosnice i klanice, mimo žrtvenik Jahve, Boga našega, koji je pred njegovim Prebivalištem!”
30 Wakati kuhani Finehasi na viongozi wa kusanyiko na wakuu wa koo za Israeli, waliposikia hayo waliyosema Wareubeni, Wagadi na Manase, wakaridhika.
Kad svećenik Pinhas, knezovi zbora i glavari izraelskih plemena koji su bili s njim čuše riječi koje im rekoše sinovi Gadovi, sinovi Rubenovi i sinovi Manašeovi, umiriše se.
31 Naye Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, akawaambia Wareubeni, Wagadi na Manase, “Leo tunajua kwamba Bwana yuko pamoja nasi, kwa sababu hamkukosa uaminifu kwa Bwana katika jambo hili. Sasa mmewaokoa Waisraeli na mkono wa Bwana.”
Tada svećenik Pinhas, sin Eleazarov, odgovori sinovima Rubenovim, sinovima Gadovim i sinovima Manašeovim: “Spoznali smo sada da je Jahve među nama, jer mu se niste iznevjerili: tako ste sačuvali sinove Izraelove od kazne Jahvine.”
32 Ndipo Finehasi, mwana wa kuhani Eleazari na viongozi wakarudi Kanaani kutoka kwenye kukutana kwao na Wareubeni na Wagadi huko Gileadi nao wakatoa taarifa kwa Waisraeli.
Svećenik Pinhas, sin Eleazarov, i knezovi odoše od sinova Rubenovih i sinova Gadovih i vratiše se iz zemlje gileadske u kanaansku k sinovima Izraelovim i kazaše im odgovor.
33 Walifurahi kusikia taarifa hiyo, na wakamhimidi Mungu. Wala hawakuzungumza tena habari za kupigana vita dhidi yao ili kuharibu nchi ambayo Wareubeni na Wagadi waliishi.
Izraelovim sinovima bijaše drag taj odgovor: hvalili su Boga i odustali su od nauma da udare na njih i da opustoše zemlju u kojoj su živjeli sinovi Rubenovi i sinovi Gadovi.
34 Nao Wareubeni na Wagadi wakayaita yale madhabahu Edi, yaani Shahidi: kwa kuwa itakuwa shahidi kati yetu na ninyi kwamba Bwana ndiye Mungu.
Sinovi Rubenovi i sinovi Gadovi nazvali su žrtvenik “Ed” - “Svjedočanstvo”, jer rekoše: “To je svjedočanstvo među nama: Jahve je Bog.”

< Yoshua 22 >