< Yoshua 21 >

1 Basi viongozi wa jamaa ya Walawi, wakamwendea kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa jamaa nyingine za makabila ya Israeli
Overhodene for levittenes familier trådte frem for Eleasar, presten, og Josva, Nuns sønn, og for familie-overhodene i Israels barns stammer
2 huko Shilo katika Kanaani na kuwaambia, “Bwana aliamuru kupitia Mose kuwa mtupe miji ya kuishi yenye sehemu za malisho kwa mifugo yetu.”
og talte til dem i Silo i Kana'ans land og sa: Herren bød ved Moses at der skulde gis oss byer å bo i med jordet omkring for vårt fe.
3 Hivyo kama vile Bwana alivyoamuru, Waisraeli wakawapa Walawi miji ifuatayo pamoja na sehemu zake za malisho kutoka urithi wao wenyewe.
Da gav Israels barn efter Herrens befaling av sine arvelodder levittene disse byer med tilhørende jorder:
4 Kura ya kwanza ikaangukia Wakohathi, ukoo kwa ukoo. Walawi waliokuwa wazao wa kuhani Aroni walipewa miji kumi na mitatu kutoka makabila ya Yuda, Simeoni na Benyamini.
Først kom loddet ut for kahatittenes ætter, og blandt disse levitter fikk Arons, prestens, sønner ved loddkastingen tretten byer av Juda stamme og av simeonittenes stamme og av Benjamins stamme,
5 Wazao wengine waliobaki wa Wakohathi walipewa miji kumi kutoka koo za makabila ya Efraimu, Dani na nusu ya Manase.
og de andre Kahats barn fikk ved loddkastingen ti byer av Efra'ims stammes ætter og av Dans stamme og av den halve Manasse stamme.
6 Wazao wa Gershoni walipewa miji kumi na mitatu kutoka koo za makabila ya Isakari, Asheri, Naftali na nusu ya Manase huko Bashani.
Gersons barn fikk ved loddkastingen tretten byer av Issakars stammes ætter og av Asers stamme og av Naftali stamme og av den halve Manasse stamme i Basan.
7 Wazao wa Merari, ukoo kwa ukoo, walipewa miji kumi na miwili kutoka makabila ya Reubeni, Gadi na Zabuloni.
Meraris barn fikk efter sine ætter tolv byer av Rubens stamme og av Gads stamme og av Sebulons stamme.
8 Kwa hiyo Waisraeli wakawapa Walawi miji hii pamoja na sehemu zake za malisho, kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru kupitia kwa Mose.
Disse byer med tilhørende jorder gav Israels barn levittene ved loddkasting, således som Herren hadde befalt ved Moses.
9 Kutoka makabila ya Yuda na Simeoni waligawa miji ifuatayo kwa majina
Av Judas barns stamme og av Simeons barns stamme avgav de de byer som nu skal nevnes:
10 (miji hii walipewa wazao wa Aroni ambao walitokana na koo za Wakohathi wa Walawi, kwa sababu kura ya kwanza iliwaangukia):
Arons sønner av kahatittenes ætter, de av Levis barn som loddet først kom ut for,
11 Waliwapa Kiriath-Arba (yaani Hebroni), pamoja na sehemu zake za malisho zilizoizunguka, katika nchi ya vilima ya Yuda. (Arba alikuwa baba wa Anaki.)
fikk Arbas, anakittenes stamfars by, det er Hebron, i Juda-fjellene med tilhørende jorder rundt omkring;
12 Lakini mashamba na vijiji vilivyozunguka mji mkubwa walikuwa wamempa Kalebu mwana wa Yefune kuwa milki yake.
men byens mark og dens landsbyer gav de Kaleb, Jefunnes sønn, til eiendom.
13 Kwa hiyo wazao wa kuhani Aroni wakapewa Hebroni (mji mkuu wa makimbilio kwa ajili ya yeyote aliyeshtakiwa kwa mauaji), Libna,
Arons, prestens, sønner fikk både Hebron, som var tilfluktsstad for manndrapere, med tilhørende jorder og Libna med jorder
14 Yatiri, Eshtemoa,
og Jattir med jorder og Estemoa med jorder
15 Holoni, Debiri,
og Holon med jorder og Debir med jorder
16 Aini, Yuta na Beth-Shemeshi, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji tisa kutoka kwa makabila haya mawili.
og A'in med jorder og Jutta med jorder og Bet-Semes med jorder - ni byer av disse to stammer;
17 Kutoka kabila la Benyamini wakawapa Gibeoni, Geba,
og av Benjamins stamme: Gibeon med jorder, Geba med jorder,
18 Anathothi na Almoni, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
Anatot med jorder og Almon med jorder - fire byer.
19 Miji yote waliyopewa makuhani, wazao wa Aroni, ilikuwa kumi na mitatu, pamoja na sehemu zake za malisho.
Således fikk Arons sønner, prestene, i alt tretten byer med tilhørende jorder.
20 Koo nyingine za Wakohathi, ambao pia ni Walawi, walipewa miji kutoka kabila la Efraimu:
Og Kahats barns ætter av levittene - de andre av Kahats barn - fikk av Efra'ims stamme disse byer, som utgjorde deres lodd:
21 Katika nchi ya vilima ya Efraimu walipewa Shekemu (mji mkubwa wa makimbilio kwa yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji) na Gezeri,
De fikk Sikem, som var tilfluktsstad for manndrapere, med tilhørende jorder i Efra'im-fjellene og Geser med jorder
22 Kibsaimu na Beth-Horoni, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
og Kibsa'im med jorder og Bet-Horon med jorder - fire byer;
23 Pia kutoka kabila la Dani wakapokea Elteke, Gibethoni,
og av Dans stamme: Elteke med jorder, Gibbeton med jorder,
24 Aiyaloni na Gath-Rimoni pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne
Ajalon med jorder, Gat-Rimmon med jorder - fire byer;
25 Kutoka nusu ya kabila la Manase, wakapokea Taanaki na Gath-Rimoni pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili.
og av den halve Manasse stamme: Ta'anak med jorder og Gat-Rimmon med jorder - to byer.
26 Miji yote hii kumi pamoja na sehemu zake za malisho ilipewa koo za Wakohathi zilizobaki.
Det var i alt ti byer med tilhørende jorder som de andre kahatitters ætter fikk.
27 Koo za Walawi za Wagershoni walipewa: kutoka nusu ya kabila la Manase, Golani katika Bashani (mji mkuu wa makimbilio kwa yeyote aliyeshtakiwa kwa mauaji) na Beeshtera, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili;
Og Gersons barn av levittenes ætter fikk av den halve Manasse stamme Galon i Basan, som var tilfluktsstad for manndrapere, med tilhørende jorder, og Be'estera med jorder - to byer;
28 kutoka kabila la Isakari walipewa, Kishioni, Daberathi,
og av Issakars stamme: Kisjon med jorder, Daberat med jorder.
29 Yarmuthi na En-Ganimu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne
Jarmut med jorder, En-Gannim med jorder - fire byer;
30 kutoka kabila la Asheri walipewa, Mishali, Abdoni,
og av Asers stamme: Misal med jorder, Abdon med jorder,
31 Helkathi na Rehobu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
Helkat med jorder og Rehob med jorder - fire byer;
32 Kutoka kabila la Naftali walipewa, Kedeshi katika Galilaya (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji), Hamoth-Dori na Kartani, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji mitano.
og av Naftali stamme: Kedes i Galilea, som var tilfluktsstad for manndrapere, med tilhørende jorder, og Hammot-Dor med jorder og Kartan med jorder - tre byer.
33 Miji yote ya koo za Wagershoni ilikuwa kumi na mitatu, pamoja na sehemu zake za malisho.
Gersonittenes byer efter deres ætter utgjorde således i alt tretten byer med tilhørende jorder.
34 Koo za Wamerari (Walawi waliobaki) walipewa: kutoka kabila la Zabuloni, Yokneamu, Karta,
Og Meraris barns ætter, resten av levittene, fikk av Sebulons stamme: Jokneam med jorder, Karta med jorder,
35 Dimna na Nahalali, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne;
Dimna med jorder, Nahalal med jorder - fire byer;
36 kutoka kabila la Reubeni walipewa Bezeri, Yahasa,
og av Rubens stamme: Beser med jorder og Jahsa med jorder,
37 Kedemothi na Mefaathi, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne;
Kedemot med jorder og Mefa'at med jorder - fire byer;
38 kutoka kabila la Gadi walipewa, Ramothi katika Gileadi (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa ajili ya mauaji), Mahanaimu,
og av Gads stamme: Ramot i Gilead, som var tilfluktsstad for manndrapere, med tilhørende jorder, og Mahana'im med jorder,
39 Heshboni na Yazeri, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
Hesbon med jorder, Jaser med jorder - i alt fire byer.
40 Miji yote waliyopewa koo za Wamerari, waliokuwa mabaki ya Walawi, ilikuwa ni kumi na miwili.
De byer som Meraris barn, resten av levittenes ætter, fikk som sin lodd efter sine ætter, var i alt tolv byer.
41 Miji yote ya Walawi katika eneo lililoshikwa na Waisraeli lilikuwa arobaini na minane, pamoja na sehemu zake za malisho.
I alt utgjorde levittenes byer i Israels barns eiendomsland åtte og firti byer med tilhørende jorder.
42 Kila mmoja wa miji hii ulikuwa na sehemu ya malisho kuuzunguka; ndivyo ilivyokuwa kwa miji hii yote.
Disse byer hadde hver for sig sine jorder rundt omkring sig; så var det med alle disse byer.
43 Kwa hiyo Bwana akawapa Israeli nchi yote aliyokuwa ameapa kuwapa baba zao, nao wakaimiliki na kukaa humo.
Således gav Herren Israel hele det land han hadde svoret å ville gi deres fedre; og de inntok det og bosatte sig der.
44 Bwana akawapa pumziko kila upande, kama vile alivyokuwa amewaapia baba zao, hakuna hata mmoja wa adui zao aliyeweza kusimama mbele yao, Bwana akawatia adui zao wote mikononi mwao.
Og Herren lot dem ha ro på alle kanter, aldeles som han hadde tilsvoret deres fedre; og ingen av alle deres fiender kunde holde stand imot dem; alle deres fiender gav Herren i deres hånd.
45 Hakuna hata mojawapo ya ahadi nzuri ya Bwana kwa nyumba ya Israeli ambayo haikutimia; kila moja ilitimia.
Ikke ett ord blev til intet av alle de gode ord Herren hadde talt til Israels hus; det blev opfylt alt sammen.

< Yoshua 21 >