< Yoshua 21 >

1 Basi viongozi wa jamaa ya Walawi, wakamwendea kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa jamaa nyingine za makabila ya Israeli
Et les chefs des pères des Lévites s’approchèrent d’Éléazar, le sacrificateur, et de Josué, fils de Nun, et des chefs des pères des tribus des fils d’Israël,
2 huko Shilo katika Kanaani na kuwaambia, “Bwana aliamuru kupitia Mose kuwa mtupe miji ya kuishi yenye sehemu za malisho kwa mifugo yetu.”
et leur parlèrent à Silo, dans le pays de Canaan, disant: L’Éternel a commandé par Moïse qu’on nous donne des villes pour y habiter, et leurs banlieues pour nos bêtes.
3 Hivyo kama vile Bwana alivyoamuru, Waisraeli wakawapa Walawi miji ifuatayo pamoja na sehemu zake za malisho kutoka urithi wao wenyewe.
Et les fils d’Israël donnèrent de leur héritage aux Lévites, selon le commandement de l’Éternel, ces villes-ci, avec leurs banlieues:
4 Kura ya kwanza ikaangukia Wakohathi, ukoo kwa ukoo. Walawi waliokuwa wazao wa kuhani Aroni walipewa miji kumi na mitatu kutoka makabila ya Yuda, Simeoni na Benyamini.
Et le lot échut aux familles des Kehathites. Et il y eut, par le sort, pour les fils d’Aaron, le sacrificateur, d’entre les Lévites, 13 villes de la tribu de Juda, et de la tribu des Siméonites, et de la tribu de Benjamin;
5 Wazao wengine waliobaki wa Wakohathi walipewa miji kumi kutoka koo za makabila ya Efraimu, Dani na nusu ya Manase.
et pour les autres fils de Kehath, dix villes des familles de la tribu d’Éphraïm, et de la tribu de Dan, et de la demi-tribu de Manassé, par le sort;
6 Wazao wa Gershoni walipewa miji kumi na mitatu kutoka koo za makabila ya Isakari, Asheri, Naftali na nusu ya Manase huko Bashani.
et pour les fils de Guershon, 13 villes des familles de la tribu d’Issacar, et de la tribu d’Aser, et de la tribu de Nephthali, et de la demi-tribu de Manassé, en Basan, par le sort;
7 Wazao wa Merari, ukoo kwa ukoo, walipewa miji kumi na miwili kutoka makabila ya Reubeni, Gadi na Zabuloni.
[et] pour les fils de Merari, selon leurs familles, douze villes de la tribu de Ruben, et de la tribu de Gad, et de la tribu de Zabulon.
8 Kwa hiyo Waisraeli wakawapa Walawi miji hii pamoja na sehemu zake za malisho, kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru kupitia kwa Mose.
Et les fils d’Israël donnèrent aux Lévites, par le sort, ces villes-là et leurs banlieues, comme l’Éternel l’avait commandé par Moïse.
9 Kutoka makabila ya Yuda na Simeoni waligawa miji ifuatayo kwa majina
Et ils donnèrent, de la tribu des fils de Juda et de la tribu des fils de Siméon, ces villes-ci, qu’on nomma par leurs noms,
10 (miji hii walipewa wazao wa Aroni ambao walitokana na koo za Wakohathi wa Walawi, kwa sababu kura ya kwanza iliwaangukia):
et qui furent pour les fils d’Aaron, des familles des Kehathites, d’entre les fils de Lévi; car le premier lot fut pour eux.
11 Waliwapa Kiriath-Arba (yaani Hebroni), pamoja na sehemu zake za malisho zilizoizunguka, katika nchi ya vilima ya Yuda. (Arba alikuwa baba wa Anaki.)
On leur donna: Kiriath-Arba ([Arba était] père d’Anak), c’est Hébron, dans la montagne de Juda, et sa banlieue autour d’elle.
12 Lakini mashamba na vijiji vilivyozunguka mji mkubwa walikuwa wamempa Kalebu mwana wa Yefune kuwa milki yake.
Mais la campagne de la ville et ses hameaux, ils les donnèrent à Caleb, fils de Jephunné, pour sa possession.
13 Kwa hiyo wazao wa kuhani Aroni wakapewa Hebroni (mji mkuu wa makimbilio kwa ajili ya yeyote aliyeshtakiwa kwa mauaji), Libna,
Et ils donnèrent aux fils d’Aaron, le sacrificateur, la ville de refuge pour l’homicide: Hébron et sa banlieue; et Libna et sa banlieue,
14 Yatiri, Eshtemoa,
et Jatthir et sa banlieue, et Eshtemoa et sa banlieue,
15 Holoni, Debiri,
et Holon et sa banlieue, et Debir et sa banlieue,
16 Aini, Yuta na Beth-Shemeshi, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji tisa kutoka kwa makabila haya mawili.
et Aïn et sa banlieue, et Jutta et sa banlieue, [et] Beth-Shémesh et sa banlieue, neuf villes de ces deux tribus-là;
17 Kutoka kabila la Benyamini wakawapa Gibeoni, Geba,
et de la tribu de Benjamin: Gabaon et sa banlieue, Guéba et sa banlieue,
18 Anathothi na Almoni, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
Anathoth et sa banlieue, et Almon et sa banlieue, quatre villes.
19 Miji yote waliyopewa makuhani, wazao wa Aroni, ilikuwa kumi na mitatu, pamoja na sehemu zake za malisho.
Toutes les villes des fils d’Aaron, sacrificateurs: 13 villes et leurs banlieues.
20 Koo nyingine za Wakohathi, ambao pia ni Walawi, walipewa miji kutoka kabila la Efraimu:
Et pour les familles des fils de Kehath, les autres Lévites d’entre les fils de Kehath, les villes de leur lot furent de la tribu d’Éphraïm.
21 Katika nchi ya vilima ya Efraimu walipewa Shekemu (mji mkubwa wa makimbilio kwa yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji) na Gezeri,
Ils leur donnèrent la ville de refuge pour l’homicide: Sichem et sa banlieue, dans la montagne d’Éphraïm; et Guézer et sa banlieue,
22 Kibsaimu na Beth-Horoni, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
et Kibtsaïm et sa banlieue, et Beth-Horon et sa banlieue, quatre villes;
23 Pia kutoka kabila la Dani wakapokea Elteke, Gibethoni,
et de la tribu de Dan: Eltheké et sa banlieue, Guibbethon et sa banlieue,
24 Aiyaloni na Gath-Rimoni pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne
Ajalon et sa banlieue, Gath-Rimmon et sa banlieue, quatre villes;
25 Kutoka nusu ya kabila la Manase, wakapokea Taanaki na Gath-Rimoni pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili.
et de la demi-tribu de Manassé: Thaanac et sa banlieue, et Gath-Rimmon et sa banlieue, deux villes.
26 Miji yote hii kumi pamoja na sehemu zake za malisho ilipewa koo za Wakohathi zilizobaki.
En tout dix villes et leurs banlieues, pour les familles des autres fils de Kehath.
27 Koo za Walawi za Wagershoni walipewa: kutoka nusu ya kabila la Manase, Golani katika Bashani (mji mkuu wa makimbilio kwa yeyote aliyeshtakiwa kwa mauaji) na Beeshtera, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili;
Et pour les fils de Guershon, d’entre les familles des Lévites, il y eut, de la demi-tribu de Manassé, la ville de refuge pour l’homicide: Golan, en Basan, et sa banlieue; et Beeshtra et sa banlieue, deux villes;
28 kutoka kabila la Isakari walipewa, Kishioni, Daberathi,
et de la tribu d’Issacar: Kishion et sa banlieue, Dabrath et sa banlieue,
29 Yarmuthi na En-Ganimu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne
Jarmuth et sa banlieue, En-Gannim et sa banlieue, quatre villes;
30 kutoka kabila la Asheri walipewa, Mishali, Abdoni,
et de la tribu d’Aser: Misheal et sa banlieue, Abdon et sa banlieue,
31 Helkathi na Rehobu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
Helkath et sa banlieue, et Rehob et sa banlieue, quatre villes;
32 Kutoka kabila la Naftali walipewa, Kedeshi katika Galilaya (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji), Hamoth-Dori na Kartani, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji mitano.
et de la tribu de Nephthali, la ville de refuge pour l’homicide: Kédesh, en Galilée, et sa banlieue; et Hammoth-Dor et sa banlieue, et Karthan et sa banlieue, trois villes.
33 Miji yote ya koo za Wagershoni ilikuwa kumi na mitatu, pamoja na sehemu zake za malisho.
Toutes les villes des Guershonites, selon leurs familles: 13 villes et leurs banlieues.
34 Koo za Wamerari (Walawi waliobaki) walipewa: kutoka kabila la Zabuloni, Yokneamu, Karta,
Et pour les familles des fils de Merari, les autres Lévites, [on donna], de la tribu de Zabulon: Jokneam et sa banlieue, Kartha et sa banlieue,
35 Dimna na Nahalali, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne;
Dimna et sa banlieue, Nahalal et sa banlieue, quatre villes;
36 kutoka kabila la Reubeni walipewa Bezeri, Yahasa,
et de la tribu de Ruben: Bétser et sa banlieue, et Jahtsa et sa banlieue,
37 Kedemothi na Mefaathi, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne;
Kedémoth et sa banlieue, et Méphaath et sa banlieue, quatre villes;
38 kutoka kabila la Gadi walipewa, Ramothi katika Gileadi (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa ajili ya mauaji), Mahanaimu,
et de la tribu de Gad, la ville de refuge pour l’homicide: Ramoth, en Galaad, et sa banlieue; et Mahanaïm et sa banlieue,
39 Heshboni na Yazeri, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
Hesbon et sa banlieue, Jahzer et sa banlieue: en tout, quatre villes.
40 Miji yote waliyopewa koo za Wamerari, waliokuwa mabaki ya Walawi, ilikuwa ni kumi na miwili.
Toutes ces villes étaient aux fils de Merari, selon leurs familles, – le reste des familles des Lévites; leur lot fut de douze villes.
41 Miji yote ya Walawi katika eneo lililoshikwa na Waisraeli lilikuwa arobaini na minane, pamoja na sehemu zake za malisho.
Toutes les villes des Lévites, au milieu de la possession des fils d’Israël: 48 villes et leurs banlieues.
42 Kila mmoja wa miji hii ulikuwa na sehemu ya malisho kuuzunguka; ndivyo ilivyokuwa kwa miji hii yote.
Chacune de ces villes avait sa banlieue autour d’elle; il en était ainsi pour toutes ces villes.
43 Kwa hiyo Bwana akawapa Israeli nchi yote aliyokuwa ameapa kuwapa baba zao, nao wakaimiliki na kukaa humo.
Et l’Éternel donna à Israël tout le pays qu’il avait juré de donner à leurs pères; et ils le possédèrent, et y habitèrent.
44 Bwana akawapa pumziko kila upande, kama vile alivyokuwa amewaapia baba zao, hakuna hata mmoja wa adui zao aliyeweza kusimama mbele yao, Bwana akawatia adui zao wote mikononi mwao.
Et l’Éternel leur donna du repos à l’entour, selon tout ce qu’il avait juré à leurs pères; et, de tous leurs ennemis, pas un homme ne tint devant eux; l’Éternel livra tous leurs ennemis entre leurs mains.
45 Hakuna hata mojawapo ya ahadi nzuri ya Bwana kwa nyumba ya Israeli ambayo haikutimia; kila moja ilitimia.
Il ne tomba pas un mot de toutes les bonnes paroles que l’Éternel avait dites à la maison d’Israël: tout arriva.

< Yoshua 21 >