< Yoshua 21 >

1 Basi viongozi wa jamaa ya Walawi, wakamwendea kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa jamaa nyingine za makabila ya Israeli
Les chefs de famille des Lévites s'approchèrent du prêtre Eléazar, de Josué, fils de Nun, et des chefs de famille des tribus des enfants d'Israël;
2 huko Shilo katika Kanaani na kuwaambia, “Bwana aliamuru kupitia Mose kuwa mtupe miji ya kuishi yenye sehemu za malisho kwa mifugo yetu.”
ils leur parlèrent à Silo, dans le pays de Chanaan, en disant: « Yahweh a ordonné par Moïse qu'on nous donnât des villes pour notre habitation, et leurs banlieues pour notre bétail. »
3 Hivyo kama vile Bwana alivyoamuru, Waisraeli wakawapa Walawi miji ifuatayo pamoja na sehemu zake za malisho kutoka urithi wao wenyewe.
Les enfants d'Israël donnèrent aux Lévites, sur leur héritage, selon l'ordre de Yahweh, les villes suivantes et leurs banlieues.
4 Kura ya kwanza ikaangukia Wakohathi, ukoo kwa ukoo. Walawi waliokuwa wazao wa kuhani Aroni walipewa miji kumi na mitatu kutoka makabila ya Yuda, Simeoni na Benyamini.
Le sort fut tiré d'abord pour les familles des Caathites; et les fils du prêtre Aaron, d'entre les Lévites, obtinrent par le sort treize villes de la tribu de Juda, de la tribu de Siméon et de la tribu de Benjamin;
5 Wazao wengine waliobaki wa Wakohathi walipewa miji kumi kutoka koo za makabila ya Efraimu, Dani na nusu ya Manase.
les autres fils de Caath obtinrent par le sort dix villes des familles de la tribu d'Ephraïm, de la tribu de Dan et de la demi-tribu de Manassé.
6 Wazao wa Gershoni walipewa miji kumi na mitatu kutoka koo za makabila ya Isakari, Asheri, Naftali na nusu ya Manase huko Bashani.
Les fils de Gerson obtinrent par le sort treize villes des familles de la tribu d'Issachar, de la tribu d'Aser, de la tribu de Nephthali et de la demi-tribu de Manassé en Basan.
7 Wazao wa Merari, ukoo kwa ukoo, walipewa miji kumi na miwili kutoka makabila ya Reubeni, Gadi na Zabuloni.
Les fils de Mérari, selon leurs familles, obtinrent douze villes de la tribu de Ruben, de la tribu de Gad et de la tribu de Zabulon.
8 Kwa hiyo Waisraeli wakawapa Walawi miji hii pamoja na sehemu zake za malisho, kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru kupitia kwa Mose.
Les enfants d'Israël donnèrent par le sort aux Lévites, ces villes et leurs banlieues, comme Yahweh l'avait ordonné par Moïse.
9 Kutoka makabila ya Yuda na Simeoni waligawa miji ifuatayo kwa majina
Ils donnèrent de la tribu des fils de Juda et de la tribu des fils de Siméon les villes suivantes désignées par leurs noms;
10 (miji hii walipewa wazao wa Aroni ambao walitokana na koo za Wakohathi wa Walawi, kwa sababu kura ya kwanza iliwaangukia):
ce fut pour les fils d'Aaron, d'entre les familles des Caathites, d'entre les fils de Lévi, car le sort fut d'abord tiré pour eux.
11 Waliwapa Kiriath-Arba (yaani Hebroni), pamoja na sehemu zake za malisho zilizoizunguka, katika nchi ya vilima ya Yuda. (Arba alikuwa baba wa Anaki.)
Ils leurs donnèrent, dans la montagne de Juda, la ville d'Arbé, père d'Enac, laquelle est Hébron, et sa banlieue tout autour.
12 Lakini mashamba na vijiji vilivyozunguka mji mkubwa walikuwa wamempa Kalebu mwana wa Yefune kuwa milki yake.
Mais la campagne de cette ville et ses villages, ils les donnèrent en possession à Caleb, fils de Jéphoné.
13 Kwa hiyo wazao wa kuhani Aroni wakapewa Hebroni (mji mkuu wa makimbilio kwa ajili ya yeyote aliyeshtakiwa kwa mauaji), Libna,
Ils donnèrent aux fils du prêtre Aaron la ville de refuge pour le meurtrier, Hébron et sa banlieue, ainsi que Lebna avec sa banlieue,
14 Yatiri, Eshtemoa,
Jéther et sa banlieue, Estémo et sa banlieue,
15 Holoni, Debiri,
Holon et sa banlieue, Dabir et sa banlieue,
16 Aini, Yuta na Beth-Shemeshi, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji tisa kutoka kwa makabila haya mawili.
Aïn et sa banlieue, Jéta et sa banlieue, Bethsamès et sa banlieue: neuf villes de ces deux tribus.
17 Kutoka kabila la Benyamini wakawapa Gibeoni, Geba,
De la tribu de Benjamin: Gabaon et sa banlieue, Gabaa et sa banlieue,
18 Anathothi na Almoni, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
Anathoth et sa banlieue, Almon et sa banlieue: quatre villes.
19 Miji yote waliyopewa makuhani, wazao wa Aroni, ilikuwa kumi na mitatu, pamoja na sehemu zake za malisho.
Total des villes des prêtres, fils d'Aaron: treize villes et leurs banlieues.
20 Koo nyingine za Wakohathi, ambao pia ni Walawi, walipewa miji kutoka kabila la Efraimu:
Quant aux familles des fils de Caath, Lévites, aux autres fils de Caath, les villes qui leur échurent par le sort furent de la tribu d'Ephraïm.
21 Katika nchi ya vilima ya Efraimu walipewa Shekemu (mji mkubwa wa makimbilio kwa yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji) na Gezeri,
Les enfants d'Israël leur donnèrent la ville de refuge pour le meurtrier, Sichem et sa banlieue, dans la montagne d'Ephraïm, ainsi que Gazer et sa banlieue,
22 Kibsaimu na Beth-Horoni, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
Cibsaïm et sa banlieue, Beth-Horon et sa banlieue: quatre villes.
23 Pia kutoka kabila la Dani wakapokea Elteke, Gibethoni,
De la tribu de Dan: Elthéco et sa banlieue, Gabathon et sa banlieue,
24 Aiyaloni na Gath-Rimoni pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne
Ajalon et sa banlieue, Geth-Remmon et sa banlieue: quatre villes.
25 Kutoka nusu ya kabila la Manase, wakapokea Taanaki na Gath-Rimoni pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili.
De la demi-tribu de Manassé: Thanach et sa banlieue, et Geth-Remmon et sa banlieue: deux villes.
26 Miji yote hii kumi pamoja na sehemu zake za malisho ilipewa koo za Wakohathi zilizobaki.
Total: dix villes avec leurs banlieues, pour les familles des autres fils de Caath.
27 Koo za Walawi za Wagershoni walipewa: kutoka nusu ya kabila la Manase, Golani katika Bashani (mji mkuu wa makimbilio kwa yeyote aliyeshtakiwa kwa mauaji) na Beeshtera, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili;
Aux fils de Gerson, d'entre les familles des Lévites, ils donnèrent, de la demi-tribu de Manassé, la ville de refuge pour le meurtrier, Gaulon, en Basan, et sa banlieue, ainsi que Bosra et sa banlieue: deux villes.
28 kutoka kabila la Isakari walipewa, Kishioni, Daberathi,
De la tribu d'Issachar: Césion et sa banlieue, Dabéreth et sa banlieue,
29 Yarmuthi na En-Ganimu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne
Jaramoth et sa banlieue, En-Gannim et sa banlieue: quatre villes.
30 kutoka kabila la Asheri walipewa, Mishali, Abdoni,
De la tribu d'Aser: Masal et sa banlieue, Abdon et sa banlieue,
31 Helkathi na Rehobu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
Helcath et sa banlieue, Rohob et sa banlieue: quatre villes.
32 Kutoka kabila la Naftali walipewa, Kedeshi katika Galilaya (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji), Hamoth-Dori na Kartani, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji mitano.
De la tribu de Nephthali: la ville de refuge pour le meurtrier, Cédès en Galilée et sa banlieue, ainsi que Hamoth-Dor et sa banlieue, Carthan et sa banlieue: trois villes.
33 Miji yote ya koo za Wagershoni ilikuwa kumi na mitatu, pamoja na sehemu zake za malisho.
Total des villes des Gersonites, selon leurs familles: treize villes et leurs banlieues.
34 Koo za Wamerari (Walawi waliobaki) walipewa: kutoka kabila la Zabuloni, Yokneamu, Karta,
Aux familles des fils de Mérari, au reste des Lévites, ils donnèrent, de la tribu de Zabulon: Jecnam et sa banlieue, Cartha et sa banlieue,
35 Dimna na Nahalali, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne;
Damna et sa banlieue, Naalol et sa banlieue: quatre villes.
36 kutoka kabila la Reubeni walipewa Bezeri, Yahasa,
Et de la tribu de Gad: la ville de refuge pour le meurtrier, Ramoth en Galaad et sa banlieue, ainsi que Manaïm et sa banlieue,
37 Kedemothi na Mefaathi, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne;
Hésebon et sa banlieue, Jaser et sa banlieue: en tout quatre villes.
38 kutoka kabila la Gadi walipewa, Ramothi katika Gileadi (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa ajili ya mauaji), Mahanaimu,
39 Heshboni na Yazeri, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
40 Miji yote waliyopewa koo za Wamerari, waliokuwa mabaki ya Walawi, ilikuwa ni kumi na miwili.
Total des villes assignées par le sort aux fils de Mérari, selon leurs familles, formant le reste des familles des Lévites: douze villes.
41 Miji yote ya Walawi katika eneo lililoshikwa na Waisraeli lilikuwa arobaini na minane, pamoja na sehemu zake za malisho.
Total des villes des Lévites au milieu des possessions des enfants d'Israël: quarante-huit villes et leurs banlieues.
42 Kila mmoja wa miji hii ulikuwa na sehemu ya malisho kuuzunguka; ndivyo ilivyokuwa kwa miji hii yote.
Chacune de ces villes avait sa banlieue tout autour; il en était ainsi pour toutes ces villes.
43 Kwa hiyo Bwana akawapa Israeli nchi yote aliyokuwa ameapa kuwapa baba zao, nao wakaimiliki na kukaa humo.
C'est ainsi que Yahweh donna à Israël tout le pays qu'il avait juré de donner à leurs pères; ils en prirent possession et s'y établirent.
44 Bwana akawapa pumziko kila upande, kama vile alivyokuwa amewaapia baba zao, hakuna hata mmoja wa adui zao aliyeweza kusimama mbele yao, Bwana akawatia adui zao wote mikononi mwao.
Yahweh leur accorda du repos tout autour d'eux, comme il l'avait juré à leurs pères; aucun de leurs ennemis ne put leur résister, et Yahweh les livra tous entre leurs mains.
45 Hakuna hata mojawapo ya ahadi nzuri ya Bwana kwa nyumba ya Israeli ambayo haikutimia; kila moja ilitimia.
De toutes les bonnes paroles que Yahweh avait dites à la maison d'Israël, aucune ne resta sans effet; toutes s'accomplirent.

< Yoshua 21 >