< Yoshua 21 >

1 Basi viongozi wa jamaa ya Walawi, wakamwendea kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa jamaa nyingine za makabila ya Israeli
Les chefs de famille des Lévites s'approchèrent du prêtre Éléazar, de Josué, fils de Noun, et des chefs de famille des tribus des enfants d'Israël.
2 huko Shilo katika Kanaani na kuwaambia, “Bwana aliamuru kupitia Mose kuwa mtupe miji ya kuishi yenye sehemu za malisho kwa mifugo yetu.”
Ils leur parlèrent à Silo, dans le pays de Canaan, en disant: « L'Éternel a ordonné par Moïse de nous donner des villes pour y habiter, avec leurs pâturages pour notre bétail. »
3 Hivyo kama vile Bwana alivyoamuru, Waisraeli wakawapa Walawi miji ifuatayo pamoja na sehemu zake za malisho kutoka urithi wao wenyewe.
Les enfants d'Israël donnèrent aux Lévites, sur leur héritage, selon le commandement de l'Éternel, ces villes et leurs pâturages.
4 Kura ya kwanza ikaangukia Wakohathi, ukoo kwa ukoo. Walawi waliokuwa wazao wa kuhani Aroni walipewa miji kumi na mitatu kutoka makabila ya Yuda, Simeoni na Benyamini.
Le sort sortit pour les familles des Kehathites. Les fils du prêtre Aaron, qui faisaient partie des Lévites, eurent par tirage au sort treize villes de la tribu de Juda, de la tribu des Siméonites et de la tribu de Benjamin.
5 Wazao wengine waliobaki wa Wakohathi walipewa miji kumi kutoka koo za makabila ya Efraimu, Dani na nusu ya Manase.
Les autres fils de Kehath eurent dix villes par le sort, appartenant aux familles de la tribu d'Ephraïm, de la tribu de Dan et de la demi-tribu de Manassé.
6 Wazao wa Gershoni walipewa miji kumi na mitatu kutoka koo za makabila ya Isakari, Asheri, Naftali na nusu ya Manase huko Bashani.
Les fils de Guershon eurent treize villes par le sort, des familles de la tribu d'Issacar, de la tribu d'Aser, de la tribu de Nephtali et de la demi-tribu de Manassé, en Basan.
7 Wazao wa Merari, ukoo kwa ukoo, walipewa miji kumi na miwili kutoka makabila ya Reubeni, Gadi na Zabuloni.
Les fils de Merari, selon leurs familles, eurent douze villes de la tribu de Ruben, de la tribu de Gad et de la tribu de Zabulon.
8 Kwa hiyo Waisraeli wakawapa Walawi miji hii pamoja na sehemu zake za malisho, kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru kupitia kwa Mose.
Les enfants d'Israël donnèrent ces villes et leurs pâturages par tirage au sort aux Lévites, comme l'Yahvé l'avait ordonné par Moïse.
9 Kutoka makabila ya Yuda na Simeoni waligawa miji ifuatayo kwa majina
Ils donnèrent de la tribu des fils de Juda et de la tribu des fils de Siméon les villes mentionnées par leur nom.
10 (miji hii walipewa wazao wa Aroni ambao walitokana na koo za Wakohathi wa Walawi, kwa sababu kura ya kwanza iliwaangukia):
Elles étaient destinées aux fils d'Aaron, des familles des Kehathites, qui étaient des fils de Lévi, car c'était le premier lot.
11 Waliwapa Kiriath-Arba (yaani Hebroni), pamoja na sehemu zake za malisho zilizoizunguka, katika nchi ya vilima ya Yuda. (Arba alikuwa baba wa Anaki.)
Ils leur donnèrent Kiriath Arba, du nom du père d'Anak (appelée aussi Hébron), dans la montagne de Juda, avec les pâturages qui l'entourent.
12 Lakini mashamba na vijiji vilivyozunguka mji mkubwa walikuwa wamempa Kalebu mwana wa Yefune kuwa milki yake.
Mais ils donnèrent les champs de la ville et de ses villages à Caleb, fils de Jephunné, pour sa possession.
13 Kwa hiyo wazao wa kuhani Aroni wakapewa Hebroni (mji mkuu wa makimbilio kwa ajili ya yeyote aliyeshtakiwa kwa mauaji), Libna,
Aux fils du sacrificateur Aaron, ils donnèrent Hébron et ses pâturages, la ville de refuge du meurtrier, Libna et ses pâturages,
14 Yatiri, Eshtemoa,
Jattir et ses pâturages, Eshtemoa et ses pâturages,
15 Holoni, Debiri,
Holon et ses pâturages, Debir et ses pâturages,
16 Aini, Yuta na Beth-Shemeshi, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji tisa kutoka kwa makabila haya mawili.
Ain et ses pâturages, Juttah et ses pâturages, Beth Shemesh et ses pâturages: neuf villes de ces deux tribus.
17 Kutoka kabila la Benyamini wakawapa Gibeoni, Geba,
Pour la tribu de Benjamin: Gabeon et ses pâturages, Guéba et ses pâturages,
18 Anathothi na Almoni, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
Anathoth et ses pâturages, et Almon et ses pâturages: quatre villes.
19 Miji yote waliyopewa makuhani, wazao wa Aroni, ilikuwa kumi na mitatu, pamoja na sehemu zake za malisho.
Toutes les villes des fils d'Aaron, les sacrificateurs, étaient au nombre de treize, avec leurs pâturages.
20 Koo nyingine za Wakohathi, ambao pia ni Walawi, walipewa miji kutoka kabila la Efraimu:
Les familles des fils de Kehath, les Lévites, le reste des fils de Kehath, eurent les villes de leur lot sur la tribu d'Éphraïm.
21 Katika nchi ya vilima ya Efraimu walipewa Shekemu (mji mkubwa wa makimbilio kwa yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji) na Gezeri,
On leur donna Sichem et ses pâturages, dans la montagne d'Éphraïm, ville de refuge pour l'homme meurtrier, Guézer et ses pâturages,
22 Kibsaimu na Beth-Horoni, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
Kibzaïm et ses pâturages, et Beth Horon et ses pâturages: quatre villes.
23 Pia kutoka kabila la Dani wakapokea Elteke, Gibethoni,
De la tribu de Dan, Elteke et ses pâturages, Gibbethon et ses pâturages,
24 Aiyaloni na Gath-Rimoni pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne
Aijalon et ses pâturages, Gath Rimmon et ses pâturages: quatre villes.
25 Kutoka nusu ya kabila la Manase, wakapokea Taanaki na Gath-Rimoni pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili.
De la demi-tribu de Manassé, Taanac et ses pâturages, et Gath Rimmon et ses pâturages: deux villes.
26 Miji yote hii kumi pamoja na sehemu zake za malisho ilipewa koo za Wakohathi zilizobaki.
Toutes les villes des familles du reste des fils de Kehath furent au nombre de dix, avec leurs pâturages.
27 Koo za Walawi za Wagershoni walipewa: kutoka nusu ya kabila la Manase, Golani katika Bashani (mji mkuu wa makimbilio kwa yeyote aliyeshtakiwa kwa mauaji) na Beeshtera, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili;
On donna aux fils de Guerschon, des familles de Lévites, de la demi-tribu de Manassé, Golan en Basan et ses pâturages, la ville de refuge pour le meurtrier, et Be Eshterah et ses pâturages: deux villes.
28 kutoka kabila la Isakari walipewa, Kishioni, Daberathi,
De la tribu d'Issacar: Kishion et ses pâturages, Daberath et ses pâturages,
29 Yarmuthi na En-Ganimu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne
Jarmuth et ses pâturages, En Gannim et ses pâturages: quatre villes.
30 kutoka kabila la Asheri walipewa, Mishali, Abdoni,
Pour la tribu d'Aser, Mishal et ses pâturages, Abdon et ses pâturages,
31 Helkathi na Rehobu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
Helkath et ses pâturages, et Rehob et ses pâturages: quatre villes.
32 Kutoka kabila la Naftali walipewa, Kedeshi katika Galilaya (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji), Hamoth-Dori na Kartani, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji mitano.
De la tribu de Nephtali, Kedesh en Galilée et ses pâturages, la ville de refuge pour le meurtrier, Hammothdor et ses pâturages, et Kartan et ses pâturages: trois villes.
33 Miji yote ya koo za Wagershoni ilikuwa kumi na mitatu, pamoja na sehemu zake za malisho.
Toutes les villes des Guershonites, selon leurs familles, étaient au nombre de treize, avec leurs pâturages.
34 Koo za Wamerari (Walawi waliobaki) walipewa: kutoka kabila la Zabuloni, Yokneamu, Karta,
Pour les familles des fils de Merari, le reste des Lévites, de la tribu de Zabulon: Jokneam et ses pâturages, Karta et ses pâturages,
35 Dimna na Nahalali, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne;
Dimnah et ses pâturages, et Nahalal et ses pâturages: quatre villes.
36 kutoka kabila la Reubeni walipewa Bezeri, Yahasa,
Pour la tribu de Ruben: Betser et ses pâturages, Jahaz et ses pâturages,
37 Kedemothi na Mefaathi, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne;
Kedemoth et ses pâturages, et Mephaath et ses pâturages: quatre villes.
38 kutoka kabila la Gadi walipewa, Ramothi katika Gileadi (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa ajili ya mauaji), Mahanaimu,
De la tribu de Gad, Ramoth en Galaad et ses pâturages, la ville de refuge du meurtrier, Mahanaïm et ses pâturages,
39 Heshboni na Yazeri, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
Hesbon et ses pâturages, Jazer et ses pâturages: quatre villes en tout.
40 Miji yote waliyopewa koo za Wamerari, waliokuwa mabaki ya Walawi, ilikuwa ni kumi na miwili.
Telles furent les villes des fils de Merari, selon leurs familles, le reste des familles des Lévites. Leur lot était de douze villes.
41 Miji yote ya Walawi katika eneo lililoshikwa na Waisraeli lilikuwa arobaini na minane, pamoja na sehemu zake za malisho.
Toutes les villes des Lévites parmi les possessions des enfants d'Israël étaient au nombre de quarante-huit, avec leurs pâturages.
42 Kila mmoja wa miji hii ulikuwa na sehemu ya malisho kuuzunguka; ndivyo ilivyokuwa kwa miji hii yote.
Chacune de ces villes était entourée de ses pâturages. Il en était ainsi pour toutes ces villes.
43 Kwa hiyo Bwana akawapa Israeli nchi yote aliyokuwa ameapa kuwapa baba zao, nao wakaimiliki na kukaa humo.
Yahvé donna à Israël tout le pays qu'il avait juré de donner à leurs pères. Ils le possédèrent et l'habitèrent.
44 Bwana akawapa pumziko kila upande, kama vile alivyokuwa amewaapia baba zao, hakuna hata mmoja wa adui zao aliyeweza kusimama mbele yao, Bwana akawatia adui zao wote mikononi mwao.
Yahvé leur donna du repos tout autour, selon tout ce qu'il avait juré à leurs pères. Pas un homme de tous leurs ennemis ne se tint devant eux. L'Éternel livra tous leurs ennemis entre leurs mains.
45 Hakuna hata mojawapo ya ahadi nzuri ya Bwana kwa nyumba ya Israeli ambayo haikutimia; kila moja ilitimia.
Rien ne manqua de ce que Yahvé avait dit de bon à la maison d'Israël. Tout s'accomplit.

< Yoshua 21 >