< Yoshua 21 >

1 Basi viongozi wa jamaa ya Walawi, wakamwendea kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa jamaa nyingine za makabila ya Israeli
Leeviläisten perhekunta-päämiehet astuivat pappi Eleasarin ja Joosuan, Nuunin pojan, eteen ja israelilaisten sukukuntien perhekunta-päämiesten eteen
2 huko Shilo katika Kanaani na kuwaambia, “Bwana aliamuru kupitia Mose kuwa mtupe miji ya kuishi yenye sehemu za malisho kwa mifugo yetu.”
ja puhuivat heille Siilossa Kanaanin maassa, sanoen: "Herra käski Mooseksen kautta antaa meille kaupunkeja asuaksemme ja niiden laidunmaat karjaamme varten".
3 Hivyo kama vile Bwana alivyoamuru, Waisraeli wakawapa Walawi miji ifuatayo pamoja na sehemu zake za malisho kutoka urithi wao wenyewe.
Niin israelilaiset antoivat leeviläisille perintöosastaan Herran käskyn mukaan nämä kaupungit laidunmaineen:
4 Kura ya kwanza ikaangukia Wakohathi, ukoo kwa ukoo. Walawi waliokuwa wazao wa kuhani Aroni walipewa miji kumi na mitatu kutoka makabila ya Yuda, Simeoni na Benyamini.
Arpa tuli kehatilaisten suvuille niin, että leeviläisistä pappi Aaronin jälkeläiset saivat arvalla Juudan sukukunnalta, Simeonin sukukunnalta ja Benjaminin sukukunnalta kolmetoista kaupunkia.
5 Wazao wengine waliobaki wa Wakohathi walipewa miji kumi kutoka koo za makabila ya Efraimu, Dani na nusu ya Manase.
Mutta muut kehatilaiset saivat arvalla Efraimin sukukunnan suvuilta, Daanin sukukunnalta ja toiselta puolelta Manassen sukukuntaa kymmenen kaupunkia.
6 Wazao wa Gershoni walipewa miji kumi na mitatu kutoka koo za makabila ya Isakari, Asheri, Naftali na nusu ya Manase huko Bashani.
Geersonilaiset saivat arvalla Isaskarin sukukunnan suvuilta, Asserin sukukunnalta ja Naftalin sukukunnalta, sekä toiselta puolelta Manassen sukukuntaa Baasanista, kolmetoista kaupunkia.
7 Wazao wa Merari, ukoo kwa ukoo, walipewa miji kumi na miwili kutoka makabila ya Reubeni, Gadi na Zabuloni.
Merarilaiset, heidän sukunsa, saivat Ruubenin sukukunnalta, Gaadin sukukunnalta ja Sebulonin sukukunnalta kaksitoista kaupunkia.
8 Kwa hiyo Waisraeli wakawapa Walawi miji hii pamoja na sehemu zake za malisho, kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru kupitia kwa Mose.
Israelilaiset antoivat arvalla leeviläisille nämä kaupungit laidunmaineen, niinkuin Herra oli Mooseksen kautta käskenyt.
9 Kutoka makabila ya Yuda na Simeoni waligawa miji ifuatayo kwa majina
Juudan jälkeläisten sukukunnasta ja simeonilaisten sukukunnasta annettiin nämä nimeltä mainitut kaupungit:
10 (miji hii walipewa wazao wa Aroni ambao walitokana na koo za Wakohathi wa Walawi, kwa sababu kura ya kwanza iliwaangukia):
Leevin jälkeläisiin, kehatilaisten sukuihin, kuuluville Aaronin jälkeläisille, sillä heille tuli arpa ensin,
11 Waliwapa Kiriath-Arba (yaani Hebroni), pamoja na sehemu zake za malisho zilizoizunguka, katika nchi ya vilima ya Yuda. (Arba alikuwa baba wa Anaki.)
annettiin Kirjat-Arba, anakilaisten kantaisän Arban kaupunki, se on Hebron, Juudan vuoristosta, ympärillä olevine laidunmaineen.
12 Lakini mashamba na vijiji vilivyozunguka mji mkubwa walikuwa wamempa Kalebu mwana wa Yefune kuwa milki yake.
Mutta kaupungin peltomaat kylineen annettiin Kaalebille, Jefunnen pojalle, perintömaaksi.
13 Kwa hiyo wazao wa kuhani Aroni wakapewa Hebroni (mji mkuu wa makimbilio kwa ajili ya yeyote aliyeshtakiwa kwa mauaji), Libna,
Pappi Aaronin jälkeläisille annettiin tappajan turvakaupunki Hebron laidunmaineen, Libna laidunmaineen,
14 Yatiri, Eshtemoa,
Jattir laidunmaineen, Estemoa laidunmaineen,
15 Holoni, Debiri,
Hoolon laidunmaineen, Debir laidunmaineen,
16 Aini, Yuta na Beth-Shemeshi, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji tisa kutoka kwa makabila haya mawili.
Ain laidunmaineen, Jutta laidunmaineen ja Beet-Semes laidunmaineen-yhdeksän kaupunkia näistä kahdesta sukukunnasta;
17 Kutoka kabila la Benyamini wakawapa Gibeoni, Geba,
ja Benjaminin sukukunnasta Gibeon laidunmaineen, Geba laidunmaineen,
18 Anathothi na Almoni, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
Anatot laidunmaineen ja Almon laidunmaineen-neljä kaupunkia.
19 Miji yote waliyopewa makuhani, wazao wa Aroni, ilikuwa kumi na mitatu, pamoja na sehemu zake za malisho.
Aaronin jälkeläisten, pappien, kaupunkeja oli kaikkiaan kolmetoista kaupunkia laidunmaineen.
20 Koo nyingine za Wakohathi, ambao pia ni Walawi, walipewa miji kutoka kabila la Efraimu:
Muut leeviläisiin kuuluvat kehatilaisten suvut, muut kehatilaiset, saivat arvalla Efraimin sukukunnalta seuraavat kaupungit:
21 Katika nchi ya vilima ya Efraimu walipewa Shekemu (mji mkubwa wa makimbilio kwa yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji) na Gezeri,
heille annettiin tappajan turvakaupunki Sikem laidunmaineen Efraimin vuoristosta, Geser laidunmaineen,
22 Kibsaimu na Beth-Horoni, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
Kibsaim laidunmaineen, Beet-Hooron laidunmaineen-neljä kaupunkia;
23 Pia kutoka kabila la Dani wakapokea Elteke, Gibethoni,
ja Daanin sukukunnasta Elteke laidunmaineen, Gibbeton laidunmaineen,
24 Aiyaloni na Gath-Rimoni pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne
Aijalon laidunmaineen ja Gat-Rimmon laidunmaineen-neljä kaupunkia,
25 Kutoka nusu ya kabila la Manase, wakapokea Taanaki na Gath-Rimoni pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili.
ja toisesta puolesta Manassen sukukuntaa Taanak laidunmaineen ja Gat-Rimmon laidunmaineen-kaksi kaupunkia.
26 Miji yote hii kumi pamoja na sehemu zake za malisho ilipewa koo za Wakohathi zilizobaki.
Näiden muiden kehatilaisten sukujen kaupunkeja laidunmaineen oli kaikkiaan kymmenen.
27 Koo za Walawi za Wagershoni walipewa: kutoka nusu ya kabila la Manase, Golani katika Bashani (mji mkuu wa makimbilio kwa yeyote aliyeshtakiwa kwa mauaji) na Beeshtera, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili;
Leeviläisten sukuihin kuuluvat geersonilaiset saivat toiselta puolelta Manassen sukukuntaa tappajan turvakaupungin Goolanin laidunmaineen Baasanista ja Beesteran laidunmaineen-kaksi kaupunkia;
28 kutoka kabila la Isakari walipewa, Kishioni, Daberathi,
ja Isaskarin sukukunnalta Kisjonin laidunmaineen, Daberatin laidunmaineen,
29 Yarmuthi na En-Ganimu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne
Jarmutin laidunmaineen ja Een-Gannimin laidunmaineen-neljä kaupunkia;
30 kutoka kabila la Asheri walipewa, Mishali, Abdoni,
ja Asserin sukukunnalta Misalin laidunmaineen, Abdonin laidunmaineen,
31 Helkathi na Rehobu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
Helkatin laidunmaineen ja Rehobin laidunmaineen-neljä kaupunkia;
32 Kutoka kabila la Naftali walipewa, Kedeshi katika Galilaya (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji), Hamoth-Dori na Kartani, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji mitano.
ja Naftalin sukukunnalta tappajan turvakaupungin Kedeksen laidunmaineen Galileasta, Hammot-Doorin laidunmaineen ja Kartanin laidunmaineen-kolme kaupunkia.
33 Miji yote ya koo za Wagershoni ilikuwa kumi na mitatu, pamoja na sehemu zake za malisho.
Geersonilaisten, heidän sukujensa, kaupunkeja oli kaikkiaan kolmetoista kaupunkia laidunmaineen.
34 Koo za Wamerari (Walawi waliobaki) walipewa: kutoka kabila la Zabuloni, Yokneamu, Karta,
Muut leeviläisiin kuuluvat merarilaisten suvut saivat Sebulonin sukukunnalta Jokneamin laidunmaineen, Kartan laidunmaineen,
35 Dimna na Nahalali, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne;
Dimnan laidunmaineen, Nahalalin laidunmaineen-neljä kaupunkia;
36 kutoka kabila la Reubeni walipewa Bezeri, Yahasa,
ja Ruubenin sukukunnalta Beserin laidunmaineen, Jahaan laidunmaineen,
37 Kedemothi na Mefaathi, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne;
Kedemotin laidunmaineen ja Meefaatin laidunmaineen-neljä kaupunkia;
38 kutoka kabila la Gadi walipewa, Ramothi katika Gileadi (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa ajili ya mauaji), Mahanaimu,
ja Gaadin sukukunnalta tappajan turvakaupungin Raamotin laidunmaineen Gileadista ja Mahanaimin laidunmaineen,
39 Heshboni na Yazeri, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
Hesbonin laidunmaineen ja Jaeserin laidunmaineen-yhteensä neljä kaupunkia.
40 Miji yote waliyopewa koo za Wamerari, waliokuwa mabaki ya Walawi, ilikuwa ni kumi na miwili.
Niitä kaupunkeja, jotka nämä muut leeviläisten sukuihin kuuluvat merarilaiset, heidän sukunsa, saivat arvalla, oli kaikkiaan kaksitoista kaupunkia.
41 Miji yote ya Walawi katika eneo lililoshikwa na Waisraeli lilikuwa arobaini na minane, pamoja na sehemu zake za malisho.
Kaikkiaan oli leeviläisten kaupunkeja israelilaisten perintömaassa neljäkymmentä kahdeksan kaupunkia laidunmaineen.
42 Kila mmoja wa miji hii ulikuwa na sehemu ya malisho kuuzunguka; ndivyo ilivyokuwa kwa miji hii yote.
Näihin kaupunkeihin kuului kuhunkin itse kaupunki ja sen ympärillä olevat laidunmaat; sellaisia olivat kaikki nämä kaupungit.
43 Kwa hiyo Bwana akawapa Israeli nchi yote aliyokuwa ameapa kuwapa baba zao, nao wakaimiliki na kukaa humo.
Niin Herra antoi Israelille koko sen maan, jonka hän oli vannonut antavansa heidän isilleen; ja he ottivat sen omaksensa ja asettuivat siihen.
44 Bwana akawapa pumziko kila upande, kama vile alivyokuwa amewaapia baba zao, hakuna hata mmoja wa adui zao aliyeweza kusimama mbele yao, Bwana akawatia adui zao wote mikononi mwao.
Ja Herra soi heidän päästä rauhaan kaikkialla, aivan niinkuin hän valalla vannoen oli luvannut heidän isillensä; eikä yksikään heidän vihollisistaan kestänyt heidän edessään, vaan kaikki heidän vihollisensa Herra antoi heidän käsiinsä.
45 Hakuna hata mojawapo ya ahadi nzuri ya Bwana kwa nyumba ya Israeli ambayo haikutimia; kila moja ilitimia.
Ei jäänyt täyttämättä ainoakaan kaikista niistä lupauksista, jotka Herra oli antanut Israelin heimolle, vaan kaikki toteutui.

< Yoshua 21 >