< Yoshua 20 >
1 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua,
And Yahweh spake unto Joshua, saying:
2 “Waambie Waisraeli, watenge miji mikubwa ya kukimbilia, kama nilivyokuagiza kupitia Mose,
Speak unto the sons of Israel, saying, —Set out for you the cities of refuge, whereof I spake unto you, by the hand of Moses:
3 ili mtu yeyote atakayemuua mtu kwa bahati mbaya na pasipo kukusudia aweze kukimbilia huko na kujiepusha na mlipiza kisasi wa damu.
that the manslayer who slayeth a person by mistake, unwittingly, may flee thither, —so shall they be unto you for refuge from the blood-redeemer,
4 “Anapokimbilia mojawapo ya hii miji mikubwa atasimama kwenye maingilio ya lango la mji mkuu na kueleza wazee wa mji kuhusu shauri lake. Kisha watampokea katika mji wao na kumpa mahali pa kuishi nao.
and he shall flee unto one of these cities and present himself at the entrance of the gate of the city, and shall speak, in the ears of the elders of that city, his defence, —and they shall take him for protection into the city unto them, and shall give him a place, so shall he dwell with them.
5 Kama mlipiza kisasi wa damu akimfuatilia, wasimkabidhi yule mshtakiwa, kwa sababu alimuua jirani yake bila kukusudia, na bila kuwa na nia ya kudhuru.
And, when the blood-redeemer pursueth after him, then shall they not deliver up the manslayer, into his hand, —because, unwittingly, it was that he slew his neighbour, and had not been, cherishing hatred, towards him, aforetime;
6 Huyu aliyeua atakaa kwenye mji mkubwa huo mpaka awe amesimama kukabili mashtaka yake mbele ya kusanyiko na mpaka kuhani mkuu anayehudumu kwa wakati huo atakapokufa. Ndipo atakapoweza kurudi nyumbani kwake katika mji ambao aliukimbia.”
so shall he remain in that city, until he standeth before the assembly, for judgment, until the death of the high-priest who shall be in those days, —then, shall the manslayer return, and enter into his own city, and into his own house, within the city from whence he fled.
7 Basi wakatenga Kedeshi katika Galilaya kwenye nchi ya vilima ya Naftali, Shekemu katika nchi ya vilima ya Efraimu, na Kiriath-Arba (yaani Hebroni) kwenye nchi ya vilima ya Yuda.
So then they set apart Kadesh in Galilee, in the hill country of Naphtali, and Shechem, in the hill country of Ephraim, and Kiriath-arba, the same, is Hebron, in the hill country of Judah.
8 Katika upande wa mashariki mwa Yordani ya Yeriko wakatenga Bezeri katika jangwa katika uwanda wa juu katika kabila la Reubeni, Ramothi katika Gileadi katika kabila la Gadi, na Golani huko Bashani katika kabila la Manase.
And, beyond the Jordan, by Jericho eastward, they appointed Bezer in the wilderness, in the table-land, out of the tribe of Reuben, —and Ramoth in Gilead, out of the tribe of Gad, and Golan in Bashan, out of the tribe of Manasseh.
9 Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote aishiye miongoni mwao aliyemuua mtu kwa bahati mbaya, angeweza kukimbilia katika miji mikubwa hiyo iliyotengwa na asiuawe na mlipiza kisasi wa damu kabla hajasimama kukabili mashtaka mbele ya kusanyiko.
These, were the cities appointed for all the sons of Israel, and for the sojourner who sojourneth in their midst, that whosoever should slay a person by mistake, might flee thither, —and not die by the hand of the blood-redeemer, until he should stand before the assembly.