< Yoshua 20 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua,
Jahve reče Jošui:
2 “Waambie Waisraeli, watenge miji mikubwa ya kukimbilia, kama nilivyokuagiza kupitia Mose,
“Kaži sinovima Izraelovim i reci im: 'Odredite sebi gradove-utočišta za koje sam vam govorio preko Mojsija,
3 ili mtu yeyote atakayemuua mtu kwa bahati mbaya na pasipo kukusudia aweze kukimbilia huko na kujiepusha na mlipiza kisasi wa damu.
da bi onamo mogao pobjeći ubojica koji nehotice ubije koga i da vam budu utočišta od krvnoga osvetnika.
4 “Anapokimbilia mojawapo ya hii miji mikubwa atasimama kwenye maingilio ya lango la mji mkuu na kueleza wazee wa mji kuhusu shauri lake. Kisha watampokea katika mji wao na kumpa mahali pa kuishi nao.
Ako ubojica utekne u koji od tih gradova, neka stane pred gradska vrata i neka starješinama toga grada iznese svoju stvar. Oni neka ga prime u svoj grad i odrede mu mjesto gdje će prebivati među njima.
5 Kama mlipiza kisasi wa damu akimfuatilia, wasimkabidhi yule mshtakiwa, kwa sababu alimuua jirani yake bila kukusudia, na bila kuwa na nia ya kudhuru.
Ako ga krvni osvetnik progoni, ne smiju izručiti ubojicu u njegove ruke: tÓa nehotice je ubio svoga bližnjega, a ne iz mržnje.
6 Huyu aliyeua atakaa kwenye mji mkubwa huo mpaka awe amesimama kukabili mashtaka yake mbele ya kusanyiko na mpaka kuhani mkuu anayehudumu kwa wakati huo atakapokufa. Ndipo atakapoweza kurudi nyumbani kwake katika mji ambao aliukimbia.”
Ubojica neka ostane u tom gradu sve dok ne stupi pred sud zajednice ili do smrti velikoga svećenika koji bude u ono vrijeme. Tada neka se ubojica vrati i neka ode u svoj grad i svome domu - u grad iz kojega je utekao.'”
7 Basi wakatenga Kedeshi katika Galilaya kwenye nchi ya vilima ya Naftali, Shekemu katika nchi ya vilima ya Efraimu, na Kiriath-Arba (yaani Hebroni) kwenye nchi ya vilima ya Yuda.
I posvete Kedeš u Galileji, u Naftalijevoj gori; Šekem u Efrajimovoj gori; Kirjat-Arbu, to jest Hebron, u Judinoj gori.
8 Katika upande wa mashariki mwa Yordani ya Yeriko wakatenga Bezeri katika jangwa katika uwanda wa juu katika kabila la Reubeni, Ramothi katika Gileadi katika kabila la Gadi, na Golani huko Bashani katika kabila la Manase.
S druge strane Jordana, istočno od Jerihona, odrede Beser u pustinji, u ravnici plemena Rubenova, i Ramot u Gileadu od plemena Gadova, i Golan u Bašanu od plemena Manašeova.
9 Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote aishiye miongoni mwao aliyemuua mtu kwa bahati mbaya, angeweza kukimbilia katika miji mikubwa hiyo iliyotengwa na asiuawe na mlipiza kisasi wa damu kabla hajasimama kukabili mashtaka mbele ya kusanyiko.
To su bili gradovi određeni svim Izraelcima i došljacima koji borave među njima: ovamo je mogao uteći svaki koji nehotice drugoga ubije, a da sam ne pogine od osvetničke ruke dok ne izađe na sud, pred zajednicu.

< Yoshua 20 >