< Yoshua 2 >
1 Kisha Yoshua mwana wa Nuni kwa siri akawatuma wapelelezi wawili kutoka Shitimu, akawaambia, “Nendeni mkaikague hiyo nchi, hasa Yeriko.” Kwa hiyo wakaenda na kuingia kwenye nyumba ya kahaba mmoja jina lake Rahabu na kukaa humo.
Nun oğlu Yeşu Şittim'den gizlice iki casus gönderdi. “Gidip ülkeyi, özellikle de Eriha'yı araştırın” dedi. Böylece yola çıkan casuslar, Rahav adında bir fahişenin evine gidip geceyi orada geçirdiler.
2 Mfalme wa Yeriko akaambiwa, “Tazama! Baadhi ya Waisraeli wamekuja huku usiku huu kuipeleleza nchi.”
Bu arada Eriha Kralı'na, “Ülkemizi araştırmak üzere bu gece İsrail halkından buraya adamlar geldi” diye haber verildi.
3 Hivyo mfalme wa Yeriko akatuma huu ujumbe kwa Rahabu: “Watoe wale watu waliokujia na kuingia nyumbani mwako, kwa sababu wamekuja kuipeleleza nchi yote.”
Bunun üzerine Eriha Kralı, Rahav'a, “Sana gelip evinde kalan o adamları dışarı çıkar” diye haber gönderdi, “Çünkü onlar ülkemizi araştırmak için geldiler.”
4 Lakini huyo mwanamke alikuwa amewachukua hao watu wawili na kuwaficha. Akasema, “Naam, watu hao walikuja kwangu, lakini sikujua walikotoka.
İki adamı saklamış olan Rahav, “Adamların bana geldikleri doğru” dedi, “Ama ben nereli olduklarını bilmiyordum.
5 Kulipoingia giza, wakati wa kufunga lango la mji, watu hao waliondoka. Sijui njia waliyoiendea. Wafuatilieni haraka. Huenda mkawapata.”
Karanlık basar basmaz, kentin kapısı kapanmak üzereyken çıktılar. Nereye gittiklerini bilmiyorum. Hemen peşlerinden giderseniz yetişirsiniz.”
6 (Lakini alikuwa amewapandisha darini akawafunika kwa mabua ya kitani aliyokuwa ameyatandika darini.)
Aslında kadın onları dama çıkarmış, oraya sermiş olduğu keten saplarının altına gizlemişti.
7 Basi hao watu wakaondoka kuwafuatilia hao wapelelezi katika njia ile inayoelekea vivuko vya Yordani, mara tu wafuatiliaji walipotoka nje, lango likafungwa.
Kralın adamlarıysa casusları Şeria Irmağı'nın geçitlerine giden yol boyunca kovaladılar. Onlar kentten çıkar çıkmaz kapı sürgülenmişti.
8 Kabla wale wapelelezi hawajalala, Rahabu akawaendea huko juu darini,
Damdaki adamlar yatmadan önce kadın yanlarına çıktı.
9 akawaambia, “Ninajua kuwa Bwana amewapa nchi hii na hofu kuu imetuangukia kwa sababu yenu, kiasi kwamba wote waishio katika nchi hii wanayeyuka kwa hofu kwa sababu yenu.
“RAB'bin bu ülkeyi size verdiğini biliyorum” dedi, “Sizden ötürü dehşete kapıldık; ülkede yaşayan herkesin korkudan dizlerinin bağı çözüldü.
10 Tumesikia jinsi Bwana alivyokausha maji ya Bahari ya Shamu kwa ajili yenu mlipotoka Misri, pia lile mlilowatendea Sihoni na Ogu, wafalme wawili wa Waamori mashariki mwa Yordani, ambao mliwaangamiza kabisa.
Çünkü Mısır'dan çıktığınızda RAB'bin Kamış Denizi'ni önünüzde nasıl kuruttuğunu, Şeria Irmağı'nın ötesindeki Amorlu iki krala –Sihon ve Og'a– neler yaptığınızı, onları nasıl yok ettiğinizi duyduk.
11 Tuliposikia juu ya hili, mioyo yetu iliyeyuka na kila mmoja alikosa ujasiri kwa sababu yenu, kwa maana Bwana Mungu wenu ni Mungu juu mbinguni na duniani chini.
Bunları duyduğumuzda korkudan dizlerimizin bağı çözüldü. Sizin korkunuzdan kimsede derman kalmadı. Çünkü Tanrınız RAB hem yukarıda göklerde, hem de aşağıda yeryüzünde Tanrı'dır.
12 Sasa basi, tafadhali niapieni kwa Bwana, kwamba mtaitendea hisani jamaa ya baba yangu, kwa kuwa mimi nimewatendea hisani. Nipeni ishara ya uaminifu
Size iyilik ettiğim gibi, siz de aileme iyilik edeceğinize lütfen RAB adına ant için. Annemi, babamı, erkek ve kız kardeşlerimle ailelerini ölümden kurtarıp hepimizi sağ bırakacağınıza ilişkin bana güvenilir bir işaret verin.”
13 kwamba mtayahifadhi maisha ya baba yangu na mama yangu, ndugu zangu wa kiume na wa kike, pamoja na wale wote walio wa kwao na kwamba mtatuokoa na kifo.”
14 Wale watu wakamhakikishia Rahabu, “Uhai wetu kwa uhai wenu! Ikiwa hutatoa habari ya nini tunachofanya, wakati Bwana atakapotupa nchi hii, tutawatendea kwa hisani na kwa uaminifu.”
Adamlar, “Eğer bu yaptıklarımızı açığa vurmazsanız, yerinize ölmeye hazırız” dediler, “RAB bu ülkeyi bize verdiğinde sana iyilik edip sözümüzü tutacağız.”
15 Kisha akawateremsha dirishani kwa kamba, kwa kuwa nyumba yake aliyokuwa anaishi ilikuwa sehemu ya ukuta wa mji.
Kent surlarında bir evde oturan Rahav, adamları iple pencereden aşağı indirdi.
16 Alikuwa amewaambia, “Nendeni vilimani ili wale wafuatiliaji wasiwapate. Jificheni huko kwa siku tatu mpaka watakaporudi, hatimaye mwende zenu.”
Onlara, “Dağa çıkın, yoksa sizi kovalayanlarla karşılaşabilirsiniz” dedi, “Onlar dönene kadar üç gün orada saklanın. Sonra yolunuza devam edersiniz.”
17 Wale watu wakamwambia, “Hiki kiapo ulichotuapisha hakitatufunga,
Adamlar Rahav'a, “Bize içirdiğin andı tutmasına tutarız” dediler,
18 isipokuwa, hapo tutakapoingia katika nchi hii, utakuwa umefunga hii kamba nyekundu dirishani pale ulipotuteremshia na kama utakuwa umewaleta baba yako na mama yako, ndugu zako na jamaa yako yote ndani ya nyumba yako.
“Ama ülkeye girdiğimizde şu kırmızı ipi bizi indirdiğin pencereye bağla. Anneni, babanı, kardeşlerinle babanın bütün ev halkını yanına, kendi evine topla.
19 Ikiwa mtu yeyote atatoka nje ya nyumba yako akaenda mtaani, damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe, hatutawajibika. Lakini yule ambaye atakuwa ndani pamoja nawe, kama mkono wa mtu yeyote ukiwa juu yake damu yake itakuwa juu ya vichwa vyetu.
Evinin kapısından dışarıya çıkan, kendi kanından sorumlu olacak; böyle biri için sorumluluk kabul etmeyiz. Ama seninle birlikte evinde olan herhangi birine gelecek zarardan biz sorumluyuz.
20 Lakini ikiwa utatoa habari ya shughuli yetu tunayofanya, tutakuwa tumefunguliwa kutoka kwenye kiapo hiki ulichotufanya tuape.”
Ancak bu yaptıklarımızı açığa vurursan, içirdiğin ant bizi bağlamaz.”
21 Naye akajibu, “Nimekubali. Na iwe kama mnavyosema.” Kwa hiyo akaagana nao, nao wakaondoka. Yeye akaifunga ile kamba nyekundu dirishani.
Kadın, “Dediğiniz gibi olsun” diye karşılık verdi. Onları yola çıkarıp uğurladıktan sonra kırmızı ipi pencereye bağladı.
22 Walipoondoka, wakaelekea vilimani na kukaa huko siku tatu, hadi wale waliokuwa wakiwafuatilia wakawa wamewatafuta njia nzima na kurudi pasipo kuwapata.
Adamlar ayrılıp dağa çıktılar; kendilerini kovalayanlar dönünceye dek üç gün orada kaldılar. Kovalayanlar yol boyu onları aradılarsa da bulamadılar.
23 Ndipo wale watu wawili wakaanza kurudi. Wakashuka kutoka kule vilimani, wakavuka mto na kuja kwa Yoshua mwana wa Nuni, na kumweleza kila kitu kilichowapata.
İki adam geri dönmek üzere dağdan indi. Irmağı geçip Nun oğlu Yeşu'nun yanına vardılar ve başlarından geçen her şeyi ona anlattılar.
24 Wakamwambia Yoshua, “Hakika Bwana ametupa nchi yote mikononi mwetu; watu wote wanayeyuka kwa hofu kwa sababu yetu.”
Yeşu'ya, “RAB gerçekten bütün ülkeyi elimize teslim etti” dediler, “Orada yaşayan herkesin korkudan dizlerinin bağı çözüldü.”