< Yoshua 2 >

1 Kisha Yoshua mwana wa Nuni kwa siri akawatuma wapelelezi wawili kutoka Shitimu, akawaambia, “Nendeni mkaikague hiyo nchi, hasa Yeriko.” Kwa hiyo wakaenda na kuingia kwenye nyumba ya kahaba mmoja jina lake Rahabu na kukaa humo.
Potem Jozue, syn Nuna, wysłał potajemnie z Szittim dwóch szpiegów, mówiąc: Idźcie, obejrzyjcie ziemię i Jerycho. Poszli więc i weszli do domu [pewnej] nierządnicy, która miała na imię Rachab, i tam odpoczęli.
2 Mfalme wa Yeriko akaambiwa, “Tazama! Baadhi ya Waisraeli wamekuja huku usiku huu kuipeleleza nchi.”
I doniesiono królowi Jerycha: Oto [jacyś] mężczyźni spośród synów Izraela przyszli tu tej nocy, aby wybadać tę ziemię.
3 Hivyo mfalme wa Yeriko akatuma huu ujumbe kwa Rahabu: “Watoe wale watu waliokujia na kuingia nyumbani mwako, kwa sababu wamekuja kuipeleleza nchi yote.”
Król Jerycha posłał więc do Rachab, rozkazując: Wyprowadź mężczyzn, którzy przyszli do ciebie i weszli do twego domu, bo przyszli wybadać całą tę ziemię.
4 Lakini huyo mwanamke alikuwa amewachukua hao watu wawili na kuwaficha. Akasema, “Naam, watu hao walikuja kwangu, lakini sikujua walikotoka.
Kobieta jednak wzięła tych dwóch mężczyzn, ukryła ich i powiedziała: To prawda, że przyszli do mnie mężczyźni, ale nie wiedziałam, skąd oni są.
5 Kulipoingia giza, wakati wa kufunga lango la mji, watu hao waliondoka. Sijui njia waliyoiendea. Wafuatilieni haraka. Huenda mkawapata.”
A gdy miano zamykać bramę o zmierzchu, mężczyźni ci wyszli i nie wiem, dokąd poszli. Ścigajcie ich prędko, to ich dogonicie.
6 (Lakini alikuwa amewapandisha darini akawafunika kwa mabua ya kitani aliyokuwa ameyatandika darini.)
Ona zaś zaprowadziła ich na dach i przykryła wiązkami lnu, które rozłożyła na dachu.
7 Basi hao watu wakaondoka kuwafuatilia hao wapelelezi katika njia ile inayoelekea vivuko vya Yordani, mara tu wafuatiliaji walipotoka nje, lango likafungwa.
[Wysłani] mężczyźni ścigali ich w kierunku Jordanu aż do brodów; i jak tylko ścigający wyszli, zamknięto bramę.
8 Kabla wale wapelelezi hawajalala, Rahabu akawaendea huko juu darini,
A zanim usnęli, ona wyszła do nich na dach;
9 akawaambia, “Ninajua kuwa Bwana amewapa nchi hii na hofu kuu imetuangukia kwa sababu yenu, kiasi kwamba wote waishio katika nchi hii wanayeyuka kwa hofu kwa sababu yenu.
I powiedziała do tych mężczyzn: Wiem, że PAN dał wam tę ziemię, bo strach przed wami padł na nas i wszyscy obywatele tej ziemi truchleją przed wami.
10 Tumesikia jinsi Bwana alivyokausha maji ya Bahari ya Shamu kwa ajili yenu mlipotoka Misri, pia lile mlilowatendea Sihoni na Ogu, wafalme wawili wa Waamori mashariki mwa Yordani, ambao mliwaangamiza kabisa.
Słyszeliśmy bowiem, jak PAN wysuszył przed wami wody Morza Czerwonego, gdy wychodziliście z Egiptu, i co uczyniliście dwom królom amoryckim, którzy byli po tamtej stronie Jordanu, Sichonowi i Ogowi, których pobiliście.
11 Tuliposikia juu ya hili, mioyo yetu iliyeyuka na kila mmoja alikosa ujasiri kwa sababu yenu, kwa maana Bwana Mungu wenu ni Mungu juu mbinguni na duniani chini.
Gdy [o tym] usłyszeliśmy, nasze serca struchlały i nie było już odwagi w nikim z waszego powodu; bo PAN, wasz Bóg, jest Bogiem wysoko na niebie i nisko na ziemi.
12 Sasa basi, tafadhali niapieni kwa Bwana, kwamba mtaitendea hisani jamaa ya baba yangu, kwa kuwa mimi nimewatendea hisani. Nipeni ishara ya uaminifu
Dlatego teraz, proszę, przysięgnijcie mi na PANA, że jak ja okazałam wam miłosierdzie, tak i wy okażecie miłosierdzie domowi mego ojca, i dajcie mi pewny znak;
13 kwamba mtayahifadhi maisha ya baba yangu na mama yangu, ndugu zangu wa kiume na wa kike, pamoja na wale wote walio wa kwao na kwamba mtatuokoa na kifo.”
Że zachowacie przy życiu mego ojca i moją matkę, moich braci i moje siostry, i wszystko, co do nich należy, i ocalicie nas od śmierci.
14 Wale watu wakamhakikishia Rahabu, “Uhai wetu kwa uhai wenu! Ikiwa hutatoa habari ya nini tunachofanya, wakati Bwana atakapotupa nchi hii, tutawatendea kwa hisani na kwa uaminifu.”
Odpowiedzieli jej mężczyźni: Ręczymy za was naszym życiem, jeśli nie wydacie tej naszej sprawy, i gdy PAN odda nam tę ziemię, okażemy ci miłosierdzie i wierność.
15 Kisha akawateremsha dirishani kwa kamba, kwa kuwa nyumba yake aliyokuwa anaishi ilikuwa sehemu ya ukuta wa mji.
Potem spuściła ich na sznurze z okna, bo jej dom przylegał do muru i ona mieszkała w murze.
16 Alikuwa amewaambia, “Nendeni vilimani ili wale wafuatiliaji wasiwapate. Jificheni huko kwa siku tatu mpaka watakaporudi, hatimaye mwende zenu.”
I powiedziała im: Idźcie w góry, by nie spotkali was ścigający; ukryjcie się tam przez trzy dni, aż powrócą ścigający, a potem pójdziecie swoją drogą.
17 Wale watu wakamwambia, “Hiki kiapo ulichotuapisha hakitatufunga,
Mężczyźni powiedzieli jej: Będziemy wolni od tej przysięgi, którą kazałaś nam złożyć;
18 isipokuwa, hapo tutakapoingia katika nchi hii, utakuwa umefunga hii kamba nyekundu dirishani pale ulipotuteremshia na kama utakuwa umewaleta baba yako na mama yako, ndugu zako na jamaa yako yote ndani ya nyumba yako.
Gdy wejdziemy do ziemi, przywiążesz do okna czerwony sznur, po którym nas spuściłaś, i zbierzesz u siebie, w domu swego ojca, swoją matkę, swoich braci i cały dom swego ojca.
19 Ikiwa mtu yeyote atatoka nje ya nyumba yako akaenda mtaani, damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe, hatutawajibika. Lakini yule ambaye atakuwa ndani pamoja nawe, kama mkono wa mtu yeyote ukiwa juu yake damu yake itakuwa juu ya vichwa vyetu.
Ktokolwiek bowiem wyjdzie poza drzwi twego domu, jego krew [spadnie] mu na głowę, a my [będziemy] bez winy. Lecz krew każdego, kto będzie z tobą w domu, [spadnie] na naszą głowę, jeśli czyjaś ręka go dotknie.
20 Lakini ikiwa utatoa habari ya shughuli yetu tunayofanya, tutakuwa tumefunguliwa kutoka kwenye kiapo hiki ulichotufanya tuape.”
Jeśli jednak wydasz naszą sprawę, będziemy wolni od przysięgi, którą kazałaś nam złożyć.
21 Naye akajibu, “Nimekubali. Na iwe kama mnavyosema.” Kwa hiyo akaagana nao, nao wakaondoka. Yeye akaifunga ile kamba nyekundu dirishani.
I odpowiedziała: Jak powiedzieliście, niech tak będzie. Wtedy wypuściła ich i poszli. I przywiązała czerwony sznur do okna.
22 Walipoondoka, wakaelekea vilimani na kukaa huko siku tatu, hadi wale waliokuwa wakiwafuatilia wakawa wamewatafuta njia nzima na kurudi pasipo kuwapata.
Odeszli więc i przyszli na górę, i pozostali tam przez trzy dni, aż powrócili ścigający. A ścigający szukali ich po wszystkich drogach, ale nie znaleźli.
23 Ndipo wale watu wawili wakaanza kurudi. Wakashuka kutoka kule vilimani, wakavuka mto na kuja kwa Yoshua mwana wa Nuni, na kumweleza kila kitu kilichowapata.
I zawrócili ci dwaj mężczyźni, zeszli z góry, przeprawili się [przez rzekę], przyszli do Jozuego, syna Nuna, i opowiedzieli mu wszystko, co się z nimi działo;
24 Wakamwambia Yoshua, “Hakika Bwana ametupa nchi yote mikononi mwetu; watu wote wanayeyuka kwa hofu kwa sababu yetu.”
I mówili do Jozuego: PAN oddał w nasze ręce całą tę ziemię, bo wszyscy obywatele tej ziemi struchleli przed nami.

< Yoshua 2 >