< Yoshua 2 >

1 Kisha Yoshua mwana wa Nuni kwa siri akawatuma wapelelezi wawili kutoka Shitimu, akawaambia, “Nendeni mkaikague hiyo nchi, hasa Yeriko.” Kwa hiyo wakaenda na kuingia kwenye nyumba ya kahaba mmoja jina lake Rahabu na kukaa humo.
Un Jozuas, Nuna dēls, sūtīja slepeni divus izlūkus no Sitimas sacīdams: ejat, izlūkojiet to zemi un Jēriku. Un tie gāja un nāca kādas sievas namā, tā bija mauka, tai vārds bija Rahaba, un tie tur gulēja.
2 Mfalme wa Yeriko akaambiwa, “Tazama! Baadhi ya Waisraeli wamekuja huku usiku huu kuipeleleza nchi.”
Un Jērikus ķēniņam tapa sacīts: redzi, šinī naktī vīri nākuši no Israēla bērniem, to zemi izlūkot.
3 Hivyo mfalme wa Yeriko akatuma huu ujumbe kwa Rahabu: “Watoe wale watu waliokujia na kuingia nyumbani mwako, kwa sababu wamekuja kuipeleleza nchi yote.”
Tad Jērikus ķēniņš sūtīja pie Rahabas un sacīja: dod šurp tos vīrus, kas pie tevis nākuši tavā namā, jo tie ir nākuši, visu šo zemi izlūkot.
4 Lakini huyo mwanamke alikuwa amewachukua hao watu wawili na kuwaficha. Akasema, “Naam, watu hao walikuja kwangu, lakini sikujua walikotoka.
Bet tā sieva ņēma tos divus vīrus un tos paslēpa un sacīja tā: tie vīri gan pie manis bija nākuši, bet es nezināju, no kurienes tie bija.
5 Kulipoingia giza, wakati wa kufunga lango la mji, watu hao waliondoka. Sijui njia waliyoiendea. Wafuatilieni haraka. Huenda mkawapata.”
Un kad vārti bija jāaizslēdz, kad metās tumšs, tad tie vīri izgāja. Es nezinu, kurp tie vīri gājuši; dzenaties tiem steigšus pakaļ, tad jūs tos panāksiet.
6 (Lakini alikuwa amewapandisha darini akawafunika kwa mabua ya kitani aliyokuwa ameyatandika darini.)
Bet viņa tiem bija likusi uz jumtu uzkāpt un tos bija paslēpusi apakš linājiem, ko uz jumta bija izklājusi.
7 Basi hao watu wakaondoka kuwafuatilia hao wapelelezi katika njia ile inayoelekea vivuko vya Yordani, mara tu wafuatiliaji walipotoka nje, lango likafungwa.
Un tie vīri tiem dzinās pakaļ pa Jardānes ceļu līdz tai pārceļamai vietai, un vārti tapa aizslēgti pēc tam, kad bija izgājuši, kas tiem dzinās pakaļ.
8 Kabla wale wapelelezi hawajalala, Rahabu akawaendea huko juu darini,
Un pirms tie apgūlās, viņa pie tiem uzkāpa uz jumtu.
9 akawaambia, “Ninajua kuwa Bwana amewapa nchi hii na hofu kuu imetuangukia kwa sababu yenu, kiasi kwamba wote waishio katika nchi hii wanayeyuka kwa hofu kwa sababu yenu.
Un sacīja uz tiem vīriem: es zinu, ka Tas Kungs jums šo zemi devis un ka bailes no jums mums uzkritušas, un ka visi zemes iedzīvotāji jūsu priekšā izbijušies.
10 Tumesikia jinsi Bwana alivyokausha maji ya Bahari ya Shamu kwa ajili yenu mlipotoka Misri, pia lile mlilowatendea Sihoni na Ogu, wafalme wawili wa Waamori mashariki mwa Yordani, ambao mliwaangamiza kabisa.
Jo mēs esam dzirdējuši, kā Tas Kungs licis izsīkt niedru jūras ūdeņiem jūsu priekšā, jums no Ēģiptes zemes izejot, un ko jūs esat darījuši viņpus Jardānes tiem diviem Amoriešu ķēniņiem, Sihonam un Ogam, ko jūs esat izdeldējuši.
11 Tuliposikia juu ya hili, mioyo yetu iliyeyuka na kila mmoja alikosa ujasiri kwa sababu yenu, kwa maana Bwana Mungu wenu ni Mungu juu mbinguni na duniani chini.
Un to dzirdot mūsu sirds palikusi bailīga, un nav vairs drošības nevienam pret jums; jo Tas Kungs, jūsu Dievs, Viņš ir Dievs augšā debesīs un apakšā virs zemes.
12 Sasa basi, tafadhali niapieni kwa Bwana, kwamba mtaitendea hisani jamaa ya baba yangu, kwa kuwa mimi nimewatendea hisani. Nipeni ishara ya uaminifu
Nu tad zvērējiet man jel pie Tā Kunga, tāpēc ka es žēlastību pie jums esmu darījusi, ka arī jūs darīsiet žēlastību pie mana tēva nama, un dodat man kādu ticamu zīmi,
13 kwamba mtayahifadhi maisha ya baba yangu na mama yangu, ndugu zangu wa kiume na wa kike, pamoja na wale wote walio wa kwao na kwamba mtatuokoa na kifo.”
Ka jūs atstāsiet dzīvus manu tēvu, manu māti un manus brāļus un manas māsas ar visu, kas tiem pieder, un ka jūs mūsu dvēseles izglābsiet no nāves.
14 Wale watu wakamhakikishia Rahabu, “Uhai wetu kwa uhai wenu! Ikiwa hutatoa habari ya nini tunachofanya, wakati Bwana atakapotupa nchi hii, tutawatendea kwa hisani na kwa uaminifu.”
Tad tie vīri uz to sacīja: ja mēs nedarīsim žēlastību un uzticību pie tevis, kad Tas Kungs mums šo zemi dos, tad lai mirst mūsu dvēsele jūsu vietā, ja tik jūs šo mūsu lietu nedarīsiet zināmu.
15 Kisha akawateremsha dirishani kwa kamba, kwa kuwa nyumba yake aliyokuwa anaishi ilikuwa sehemu ya ukuta wa mji.
Tad viņa tos ar virvi nolaida pa logu, jo viņas nams bija pie pilsētas mūra un viņa dzīvoja pie tā mūra.
16 Alikuwa amewaambia, “Nendeni vilimani ili wale wafuatiliaji wasiwapate. Jificheni huko kwa siku tatu mpaka watakaporudi, hatimaye mwende zenu.”
Un viņa uz tiem sacīja: ejat kalnos, ka tie jūs nesastop, kas jums dzenās pakaļ, un paslēpjaties tur trīs dienas, tiekams tie vajātāji atgriezīsies, tad pēc ejat savu ceļu.
17 Wale watu wakamwambia, “Hiki kiapo ulichotuapisha hakitatufunga,
Tad tie vīri uz viņu sacīja: mēs būsim vaļā no šī tava zvēresta, ko tu mums lieci zvērēt:
18 isipokuwa, hapo tutakapoingia katika nchi hii, utakuwa umefunga hii kamba nyekundu dirishani pale ulipotuteremshia na kama utakuwa umewaleta baba yako na mama yako, ndugu zako na jamaa yako yote ndani ya nyumba yako.
Redzi, kad mēs nākam tai zemē, tad piesien pie sava loga šo sarkano virvi, ar ko tu mūs nolaidi, un sapulcini pie sevis šai namā savu tēvu un savu māti un savus brāļus un visu tava tēva namu.
19 Ikiwa mtu yeyote atatoka nje ya nyumba yako akaenda mtaani, damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe, hatutawajibika. Lakini yule ambaye atakuwa ndani pamoja nawe, kama mkono wa mtu yeyote ukiwa juu yake damu yake itakuwa juu ya vichwa vyetu.
Un ikviens, kas pa tava nama durvīm izies ārā, tā asinis lai paliek uz viņa galvas, un mēs būsim nevainīgi. Bet ikviens, kas pie tevis būs namā, tā asinis lai paliek uz mūsu galvas, ja kas savu roku pie viņa pieliks.
20 Lakini ikiwa utatoa habari ya shughuli yetu tunayofanya, tutakuwa tumefunguliwa kutoka kwenye kiapo hiki ulichotufanya tuape.”
Bet ja tu šo mūsu lietu darīsi zināmu, tad mēs būsim vaļā no šī zvēresta, ko tu mums likusi zvērēt.
21 Naye akajibu, “Nimekubali. Na iwe kama mnavyosema.” Kwa hiyo akaagana nao, nao wakaondoka. Yeye akaifunga ile kamba nyekundu dirishani.
Tad viņa sacīja: lai tā ir, kā jūs sakāt. Un viņa tos atlaida, un tie aizgāja; un viņa to sarkano virvi piesēja pie loga.
22 Walipoondoka, wakaelekea vilimani na kukaa huko siku tatu, hadi wale waliokuwa wakiwafuatilia wakawa wamewatafuta njia nzima na kurudi pasipo kuwapata.
Tā tie aizgāja un nāca kalnos un palika tur trīs dienas, tiekams tie vajātāji bija atpakaļ griezušies; jo tie vajātāji tos bija meklējuši pa visiem ceļiem, bet nebija atraduši.
23 Ndipo wale watu wawili wakaanza kurudi. Wakashuka kutoka kule vilimani, wakavuka mto na kuja kwa Yoshua mwana wa Nuni, na kumweleza kila kitu kilichowapata.
Tad tie divi vīri griezās atpakaļ un nonāca no tiem kalniem un cēlās pāri un nāca pie Jozuas, Nuna dēla, un teica tam visu, kas tiem bija noticis.
24 Wakamwambia Yoshua, “Hakika Bwana ametupa nchi yote mikononi mwetu; watu wote wanayeyuka kwa hofu kwa sababu yetu.”
Un tie sacīja uz Jozua: tiešām Tas Kungs visu to zemi ir devis mūsu rokās, un visi zemes iedzīvotāji no mums bīstas.

< Yoshua 2 >