< Yoshua 2 >
1 Kisha Yoshua mwana wa Nuni kwa siri akawatuma wapelelezi wawili kutoka Shitimu, akawaambia, “Nendeni mkaikague hiyo nchi, hasa Yeriko.” Kwa hiyo wakaenda na kuingia kwenye nyumba ya kahaba mmoja jina lake Rahabu na kukaa humo.
Sililimed ngarud a nangibaon ni Josue nga anak ni Nun iti dua a lallaki a kas espia manipud Settim. Kinunana, “Mapankayo iti entero a daga, nangnangruna iti Jerico.” Napanda ket dimtengda iti balay ti maysa a balangkantis nga agnagan iti Rahab, ket nagdagusda sadiay.
2 Mfalme wa Yeriko akaambiwa, “Tazama! Baadhi ya Waisraeli wamekuja huku usiku huu kuipeleleza nchi.”
Naipakaammo daytoy iti ari ti Jerico, “Immay ditoy dagiti lallaki manipud Israel a mangsiim iti daga.”
3 Hivyo mfalme wa Yeriko akatuma huu ujumbe kwa Rahabu: “Watoe wale watu waliokujia na kuingia nyumbani mwako, kwa sababu wamekuja kuipeleleza nchi yote.”
Nangipadanon ti ari iti sao kenni Rahab ket kinunana, “Iruarmo dagiti lallaki nga immay kenka a simrek iti balaymo, ta immayda a mangsiim iti entero a daga.”
4 Lakini huyo mwanamke alikuwa amewachukua hao watu wawili na kuwaficha. Akasema, “Naam, watu hao walikuja kwangu, lakini sikujua walikotoka.
Ngem innalan idi ti babai dagiti dua a lallaki ket inlemmengna ida. Ket kinunana, “Wen, immay kaniak dagiti lallaki, ngem saanko nga ammo no sadino ti naggapuanda.
5 Kulipoingia giza, wakati wa kufunga lango la mji, watu hao waliondoka. Sijui njia waliyoiendea. Wafuatilieni haraka. Huenda mkawapata.”
Pimmanawda idi sumipnget, idi agrikep ti ruangan ti siudad. Saanko nga ammo ti napananda. Mabalin a matiliwyo ida no darasenyo ida a kamaten.”
6 (Lakini alikuwa amewapandisha darini akawafunika kwa mabua ya kitani aliyokuwa ameyatandika darini.)
Ngem pinaulina idi ida iti bubungan ti balay ket inlemmengna ida kadagiti kayo ti lino nga inkabilna iti rabaw daytoy.
7 Basi hao watu wakaondoka kuwafuatilia hao wapelelezi katika njia ile inayoelekea vivuko vya Yordani, mara tu wafuatiliaji walipotoka nje, lango likafungwa.
Kinamat ngarud dagiti lallaki dagiti dua nga espia nga agturong iti pagballasiwan ti Jordan. Ket nagrikep dagiti ruangan apaman a nakaruar dagiti mangkamkamat.
8 Kabla wale wapelelezi hawajalala, Rahabu akawaendea huko juu darini,
Saan pay a nakaidda dagiti dua nga espia idi inuli ida ti babai idiay pangatepan.
9 akawaambia, “Ninajua kuwa Bwana amewapa nchi hii na hofu kuu imetuangukia kwa sababu yenu, kiasi kwamba wote waishio katika nchi hii wanayeyuka kwa hofu kwa sababu yenu.
Kinunana, “Ammok nga inted kadakayo ni Yahweh ti daga ta immay kadakami ti panagbuteng kadakayo. Agrunaw iti sangoananyo ti amin nga agnanaed iti daga.”
10 Tumesikia jinsi Bwana alivyokausha maji ya Bahari ya Shamu kwa ajili yenu mlipotoka Misri, pia lile mlilowatendea Sihoni na Ogu, wafalme wawili wa Waamori mashariki mwa Yordani, ambao mliwaangamiza kabisa.
Nangngeganmi no kasano a pinamaga ni Yahweh ti danum ti Baybay dagiti Runo para kadakayo idi rimuarkayo manipud Egipto. Ken nangngeganmi ti inaramidyo kadagiti dua nga ari dagiti Amorreo idiay bangir ti Jordan—ni Sihon ken ni Og— a naan-anay a dinadaelyo.
11 Tuliposikia juu ya hili, mioyo yetu iliyeyuka na kila mmoja alikosa ujasiri kwa sababu yenu, kwa maana Bwana Mungu wenu ni Mungu juu mbinguni na duniani chini.
Apaman a nangngeganmi daytoy, narunaw dagiti pusomi ket awan ti nabati a tured iti siasinoman—ta ni Yahweh a Diosyo ket Dios sadi-langit ken iti rabaw ti daga.
12 Sasa basi, tafadhali niapieni kwa Bwana, kwamba mtaitendea hisani jamaa ya baba yangu, kwa kuwa mimi nimewatendea hisani. Nipeni ishara ya uaminifu
Ita ngarud, pangngaasiyo ta isapatayo kaniak babaen kenni Yahweh a kas iti panangngaasik kadakayo, kaassianyonto met iti balay ti amak. Ikkandak iti natalged a pagilasinan
13 kwamba mtayahifadhi maisha ya baba yangu na mama yangu, ndugu zangu wa kiume na wa kike, pamoja na wale wote walio wa kwao na kwamba mtatuokoa na kifo.”
nga ispalenyonto ti biag ti amak, inak, kakabsatko a lallaki ken babbai, ken dagiti amin a pamiliada, ken isalakandakaminto manipud iti ipapatay.”
14 Wale watu wakamhakikishia Rahabu, “Uhai wetu kwa uhai wenu! Ikiwa hutatoa habari ya nini tunachofanya, wakati Bwana atakapotupa nchi hii, tutawatendea kwa hisani na kwa uaminifu.”
Kinuna dagiti lallaki kenkuana, “Para kenka ti biagmi, uray agingga iti patay! No saanmo a sarsaritaen ti maipapan iti rantami, maasi ken napudnokaminto ngarud kenka inton ited ni Yahweh daytoy a daga kadakami.”
15 Kisha akawateremsha dirishani kwa kamba, kwa kuwa nyumba yake aliyokuwa anaishi ilikuwa sehemu ya ukuta wa mji.
Pinaulogna ngarud ida idiay tawa babaen iti tali. Ti balay a pagnanaedanna ket naikapet iti pader ti siudad.
16 Alikuwa amewaambia, “Nendeni vilimani ili wale wafuatiliaji wasiwapate. Jificheni huko kwa siku tatu mpaka watakaporudi, hatimaye mwende zenu.”
Kinunana kadakuada, “Mapankayo kadagiti turturod ket aglemmengkayo ta no saan ket masarakandakayo dagiti mangkamkamat kadakayo. Aglemmengkayo sadiay iti tallo nga aldaw agingga a makasubli dagiti mangkamkamat. Ket mapankayo iti dalanyo.”
17 Wale watu wakamwambia, “Hiki kiapo ulichotuapisha hakitatufunga,
Kinuna dagiti dua nga espia kenni Rahab, “Awanto iti pagrebbenganmi kadagiti impasapatam kadakami, no saanmo nga aramiden daytoy:
18 isipokuwa, hapo tutakapoingia katika nchi hii, utakuwa umefunga hii kamba nyekundu dirishani pale ulipotuteremshia na kama utakuwa umewaleta baba yako na mama yako, ndugu zako na jamaa yako yote ndani ya nyumba yako.
Inton serkenmi ti daga, masapul a mangigalutka iti nalabaga a tali iti tawa a nangipaulogam kadakami, ket ummongem iti uneg ti balaymo ti ama ken inam, dagiti kakabsatmo ken amin a sangkabbalayan ti amam.
19 Ikiwa mtu yeyote atatoka nje ya nyumba yako akaenda mtaani, damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe, hatutawajibika. Lakini yule ambaye atakuwa ndani pamoja nawe, kama mkono wa mtu yeyote ukiwa juu yake damu yake itakuwa juu ya vichwa vyetu.
Siasinoman a rumuar manipud kadagiti ruangan ti balaymo, addanto iti rabaw ti uloda iti darada ket awanto ti pakabasolanmi. Ngem no madangran ti siasinoman kadakayo iti uneg ti balay, ti darananto ket adda iti rabaw ti ulomi.
20 Lakini ikiwa utatoa habari ya shughuli yetu tunayofanya, tutakuwa tumefunguliwa kutoka kwenye kiapo hiki ulichotufanya tuape.”
Ngem no ibagam daytoy a rantami, awanto ngarud ti pagrebbenganmi a mangtungpal iti inkarimi.
21 Naye akajibu, “Nimekubali. Na iwe kama mnavyosema.” Kwa hiyo akaagana nao, nao wakaondoka. Yeye akaifunga ile kamba nyekundu dirishani.
Simmungbat ni Rahab, “Mapasamak koma ti kinunayo.” Pinalubosanna ida ket pimmanawda. Ket nangigalut isuna iti nalabaga a tali iti tawa.
22 Walipoondoka, wakaelekea vilimani na kukaa huko siku tatu, hadi wale waliokuwa wakiwafuatilia wakawa wamewatafuta njia nzima na kurudi pasipo kuwapata.
Pimmanawda ket napanda idiay turturod ket nagtalinaedda sadiay iti tallo nga aldaw agingga a nagsubli dagiti mangkamkamat kadakuada. Sinapsapul ida dagiti mangkamkamat kadagiti daldalan ngem awan ti nasarakanda.
23 Ndipo wale watu wawili wakaanza kurudi. Wakashuka kutoka kule vilimani, wakavuka mto na kuja kwa Yoshua mwana wa Nuni, na kumweleza kila kitu kilichowapata.
Nagsubli dagiti dua a lallaki ket nagballasiwda a nagsublida kenni Josue nga anak ni Nun, ket imbagada kenkuana amin a napasamak kadakuada.
24 Wakamwambia Yoshua, “Hakika Bwana ametupa nchi yote mikononi mwetu; watu wote wanayeyuka kwa hofu kwa sababu yetu.”
Ket kinunada kenni Josue, “Pudno nga inted ni Yahweh daytoy a daga kadatayo. Agrunrunaw amin nga agnanaed iti daydiay a daga gapu kadatayo.