< Yoshua 2 >
1 Kisha Yoshua mwana wa Nuni kwa siri akawatuma wapelelezi wawili kutoka Shitimu, akawaambia, “Nendeni mkaikague hiyo nchi, hasa Yeriko.” Kwa hiyo wakaenda na kuingia kwenye nyumba ya kahaba mmoja jina lake Rahabu na kukaa humo.
And Joshua son of Nun silently sends two men, spies, from Shittim, saying, “Go, see the land—and Jericho”; and they go and come into the house of a woman, a harlot, and her name [is] Rahab, and they lie down there.
2 Mfalme wa Yeriko akaambiwa, “Tazama! Baadhi ya Waisraeli wamekuja huku usiku huu kuipeleleza nchi.”
And it is told to the king of Jericho, saying, “Behold, men have come in here tonight, from the sons of Israel, to search the land.”
3 Hivyo mfalme wa Yeriko akatuma huu ujumbe kwa Rahabu: “Watoe wale watu waliokujia na kuingia nyumbani mwako, kwa sababu wamekuja kuipeleleza nchi yote.”
And the king of Jericho sends to Rahab, saying, “Bring out the men who are coming to you, who have come into your house, for they have come to search the entirety of the land.”
4 Lakini huyo mwanamke alikuwa amewachukua hao watu wawili na kuwaficha. Akasema, “Naam, watu hao walikuja kwangu, lakini sikujua walikotoka.
And the woman takes the two men, and hides them, and says thus: “The men came to me, and I have not known where they [are] from;
5 Kulipoingia giza, wakati wa kufunga lango la mji, watu hao waliondoka. Sijui njia waliyoiendea. Wafuatilieni haraka. Huenda mkawapata.”
and it comes to pass—the gate is to [be] shut—in the dark, and the men have gone out; I have not known to where the men have gone; pursue, hurry after them, for you overtake them”;
6 (Lakini alikuwa amewapandisha darini akawafunika kwa mabua ya kitani aliyokuwa ameyatandika darini.)
and she has caused them to go up on the roof, and hides them with the flax wood, which is arranged for her on the roof.
7 Basi hao watu wakaondoka kuwafuatilia hao wapelelezi katika njia ile inayoelekea vivuko vya Yordani, mara tu wafuatiliaji walipotoka nje, lango likafungwa.
And the men have pursued after them the way of the Jordan, by the fords, and they have shut the gate afterward when the pursuers have gone out after them.
8 Kabla wale wapelelezi hawajalala, Rahabu akawaendea huko juu darini,
And before they lie down, she has gone up to them on the roof,
9 akawaambia, “Ninajua kuwa Bwana amewapa nchi hii na hofu kuu imetuangukia kwa sababu yenu, kiasi kwamba wote waishio katika nchi hii wanayeyuka kwa hofu kwa sababu yenu.
and she says to the men, “I have known that YHWH has given the land to you, and that your terror has fallen on us, and that all the inhabitants of the land have melted at your presence.
10 Tumesikia jinsi Bwana alivyokausha maji ya Bahari ya Shamu kwa ajili yenu mlipotoka Misri, pia lile mlilowatendea Sihoni na Ogu, wafalme wawili wa Waamori mashariki mwa Yordani, ambao mliwaangamiza kabisa.
For we have heard how YHWH dried up the waters of the Red Sea at your presence, in your going out of Egypt, and that which you have done to the two kings of the Amorite who [are] beyond the Jordan; to Sihon and to Og whom you devoted.
11 Tuliposikia juu ya hili, mioyo yetu iliyeyuka na kila mmoja alikosa ujasiri kwa sababu yenu, kwa maana Bwana Mungu wenu ni Mungu juu mbinguni na duniani chini.
And we hear, and our heart melts, and there has not stood anymore spirit in [any] man from your presence, for He, your God YHWH, [is] God in the heavens above and on the earth below.
12 Sasa basi, tafadhali niapieni kwa Bwana, kwamba mtaitendea hisani jamaa ya baba yangu, kwa kuwa mimi nimewatendea hisani. Nipeni ishara ya uaminifu
And now, please swear to me by YHWH—because I have done kindness with you—that you have done, even you, kindness with the house of my father, and have given a true token to me,
13 kwamba mtayahifadhi maisha ya baba yangu na mama yangu, ndugu zangu wa kiume na wa kike, pamoja na wale wote walio wa kwao na kwamba mtatuokoa na kifo.”
and have kept alive my father, and my mother, and my brothers, and my sisters, and all that they have, and have delivered our souls from death.”
14 Wale watu wakamhakikishia Rahabu, “Uhai wetu kwa uhai wenu! Ikiwa hutatoa habari ya nini tunachofanya, wakati Bwana atakapotupa nchi hii, tutawatendea kwa hisani na kwa uaminifu.”
And the men say to her, “Our soul to die for yours; if you do not declare this—our matter, then it has been, in YHWH’s giving this land to us, that we have done kindness and truth with you.”
15 Kisha akawateremsha dirishani kwa kamba, kwa kuwa nyumba yake aliyokuwa anaishi ilikuwa sehemu ya ukuta wa mji.
And she causes them to go down by a rope through the window, for her house [is] in the side of the wall, and she [is] dwelling in the wall;
16 Alikuwa amewaambia, “Nendeni vilimani ili wale wafuatiliaji wasiwapate. Jificheni huko kwa siku tatu mpaka watakaporudi, hatimaye mwende zenu.”
and she says to them, “Go to the mountain, lest the pursuers come on you; and you have been hidden there three days until the turning back of the pursuers, and afterward you go on your way.”
17 Wale watu wakamwambia, “Hiki kiapo ulichotuapisha hakitatufunga,
And the men say to her, “We are acquitted of this, your oath, which you have caused us to swear:
18 isipokuwa, hapo tutakapoingia katika nchi hii, utakuwa umefunga hii kamba nyekundu dirishani pale ulipotuteremshia na kama utakuwa umewaleta baba yako na mama yako, ndugu zako na jamaa yako yote ndani ya nyumba yako.
behold, we are coming into the land, bind this line of scarlet thread to the window by which you have caused us to go down, and gather your father, and your mother, and your brothers, and all the house of your father to you, to the house;
19 Ikiwa mtu yeyote atatoka nje ya nyumba yako akaenda mtaani, damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe, hatutawajibika. Lakini yule ambaye atakuwa ndani pamoja nawe, kama mkono wa mtu yeyote ukiwa juu yake damu yake itakuwa juu ya vichwa vyetu.
and it has been, anyone who goes out from the doors of your house outside, his blood [is] on his head, and we are innocent; and anyone who is with you in the house, his blood [is] on our head, if a hand is on him;
20 Lakini ikiwa utatoa habari ya shughuli yetu tunayofanya, tutakuwa tumefunguliwa kutoka kwenye kiapo hiki ulichotufanya tuape.”
and if you declare this—our matter, then we have been acquitted from your oath which you have caused us to swear.”
21 Naye akajibu, “Nimekubali. Na iwe kama mnavyosema.” Kwa hiyo akaagana nao, nao wakaondoka. Yeye akaifunga ile kamba nyekundu dirishani.
And she says, “According to your words, so it [is]”; and she sends them away, and they go; and she binds the scarlet line to the window.
22 Walipoondoka, wakaelekea vilimani na kukaa huko siku tatu, hadi wale waliokuwa wakiwafuatilia wakawa wamewatafuta njia nzima na kurudi pasipo kuwapata.
And they go, and come to the mountain, and abide there three days until the pursuers have turned back; and the pursuers seek in all the way, and have not found.
23 Ndipo wale watu wawili wakaanza kurudi. Wakashuka kutoka kule vilimani, wakavuka mto na kuja kwa Yoshua mwana wa Nuni, na kumweleza kila kitu kilichowapata.
And the two men turn back, and come down from the hill, and pass over, and come to Joshua son of Nun, and recount to him all that has come on them;
24 Wakamwambia Yoshua, “Hakika Bwana ametupa nchi yote mikononi mwetu; watu wote wanayeyuka kwa hofu kwa sababu yetu.”
and they say to Joshua, “Surely YHWH has given all the land into our hand; and also, all the inhabitants of the land have melted at our presence.”