< Yoshua 2 >
1 Kisha Yoshua mwana wa Nuni kwa siri akawatuma wapelelezi wawili kutoka Shitimu, akawaambia, “Nendeni mkaikague hiyo nchi, hasa Yeriko.” Kwa hiyo wakaenda na kuingia kwenye nyumba ya kahaba mmoja jina lake Rahabu na kukaa humo.
And so Joshua, the son of Nun, sent two men from Shittim to explore in secret. And he said to them, “Go and consider the land and the city of Jericho.” And while traveling, they entered into the house of a harlot woman named Rahab, and they rested with her.
2 Mfalme wa Yeriko akaambiwa, “Tazama! Baadhi ya Waisraeli wamekuja huku usiku huu kuipeleleza nchi.”
And it was reported to the king of Jericho, and it was said: “Behold, men have entered to this place in the night, from the sons of Israel, so that they might explore the land.”
3 Hivyo mfalme wa Yeriko akatuma huu ujumbe kwa Rahabu: “Watoe wale watu waliokujia na kuingia nyumbani mwako, kwa sababu wamekuja kuipeleleza nchi yote.”
And the king of Jericho sent to Rahab, saying: “Bring out the men who came to you, and who entered into your house. For certainly they are spies, and they have arrived to consider the entire land.”
4 Lakini huyo mwanamke alikuwa amewachukua hao watu wawili na kuwaficha. Akasema, “Naam, watu hao walikuja kwangu, lakini sikujua walikotoka.
And the woman, taking the men, hid them. And she said: “I admit that they came to me, but I did not know where they were from.
5 Kulipoingia giza, wakati wa kufunga lango la mji, watu hao waliondoka. Sijui njia waliyoiendea. Wafuatilieni haraka. Huenda mkawapata.”
And when the gate was closed, they went out together in the darkness. I do not know where they have gone. Pursue them quickly, and you will overtake them.”
6 (Lakini alikuwa amewapandisha darini akawafunika kwa mabua ya kitani aliyokuwa ameyatandika darini.)
But she caused the men to ascend to the roof of her house, and she covered them with the stalks of flax that were there.
7 Basi hao watu wakaondoka kuwafuatilia hao wapelelezi katika njia ile inayoelekea vivuko vya Yordani, mara tu wafuatiliaji walipotoka nje, lango likafungwa.
But those who had been sent pursued after them along the way that leads to the ford of the Jordan. And as soon as they went out, the gate was closed.
8 Kabla wale wapelelezi hawajalala, Rahabu akawaendea huko juu darini,
Those who were hiding had not yet fallen asleep, and behold, the woman went up to them, and she said:
9 akawaambia, “Ninajua kuwa Bwana amewapa nchi hii na hofu kuu imetuangukia kwa sababu yenu, kiasi kwamba wote waishio katika nchi hii wanayeyuka kwa hofu kwa sababu yenu.
“I know that the Lord has given this land to you. For the terror of you has fallen upon us, and all the inhabitants of the land have languished.
10 Tumesikia jinsi Bwana alivyokausha maji ya Bahari ya Shamu kwa ajili yenu mlipotoka Misri, pia lile mlilowatendea Sihoni na Ogu, wafalme wawili wa Waamori mashariki mwa Yordani, ambao mliwaangamiza kabisa.
We have heard that the Lord dried up the water of the Red Sea upon your arrival, when you were departing from Egypt, and we heard of the things that you did to the two kings of the Amorites, who were beyond the Jordan, Sihon and Og, whom you put to death.
11 Tuliposikia juu ya hili, mioyo yetu iliyeyuka na kila mmoja alikosa ujasiri kwa sababu yenu, kwa maana Bwana Mungu wenu ni Mungu juu mbinguni na duniani chini.
And upon hearing these things, we were very afraid, and our heart languished. Neither did there remain in us any spirit at your arrival. For the Lord your God is the very God in heaven above and on earth below.
12 Sasa basi, tafadhali niapieni kwa Bwana, kwamba mtaitendea hisani jamaa ya baba yangu, kwa kuwa mimi nimewatendea hisani. Nipeni ishara ya uaminifu
Now, therefore, swear to me by the Lord that in the same way that I have acted with mercy toward you, so also shall you act toward the house of my father. And may you give me a true sign
13 kwamba mtayahifadhi maisha ya baba yangu na mama yangu, ndugu zangu wa kiume na wa kike, pamoja na wale wote walio wa kwao na kwamba mtatuokoa na kifo.”
that you will save my father and mother, my brothers and sisters, and all that is theirs, and that you may rescue our souls from death.”
14 Wale watu wakamhakikishia Rahabu, “Uhai wetu kwa uhai wenu! Ikiwa hutatoa habari ya nini tunachofanya, wakati Bwana atakapotupa nchi hii, tutawatendea kwa hisani na kwa uaminifu.”
They responded to her: “May our lives be yours unto death, if only you do not betray us. And when the Lord will have delivered the land to us, we will act toward you with mercy and truth.”
15 Kisha akawateremsha dirishani kwa kamba, kwa kuwa nyumba yake aliyokuwa anaishi ilikuwa sehemu ya ukuta wa mji.
Therefore, she sent them down from a window with a rope. For her house was joined to the wall.
16 Alikuwa amewaambia, “Nendeni vilimani ili wale wafuatiliaji wasiwapate. Jificheni huko kwa siku tatu mpaka watakaporudi, hatimaye mwende zenu.”
And she said to them: “Climb up to the mountains; otherwise, they may meet you as they are returning. And lay hidden there for three days, until they return. And then you will go on your way.”
17 Wale watu wakamwambia, “Hiki kiapo ulichotuapisha hakitatufunga,
And they said to her: “We shall be innocent of this oath, to which you have sworn us,
18 isipokuwa, hapo tutakapoingia katika nchi hii, utakuwa umefunga hii kamba nyekundu dirishani pale ulipotuteremshia na kama utakuwa umewaleta baba yako na mama yako, ndugu zako na jamaa yako yote ndani ya nyumba yako.
if, when we enter into the land, this scarlet cord has been placed as a sign, and you have tied it at the window by which you let us down. And so, gather your father, and mother, and brothers, and all your family into your house.
19 Ikiwa mtu yeyote atatoka nje ya nyumba yako akaenda mtaani, damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe, hatutawajibika. Lakini yule ambaye atakuwa ndani pamoja nawe, kama mkono wa mtu yeyote ukiwa juu yake damu yake itakuwa juu ya vichwa vyetu.
Whoever will have exited from the door of your house, his blood will be on his own head, and we will be uninvolved. But the blood of all who will be with you in the house shall fall back upon our own head, if anyone touches them.
20 Lakini ikiwa utatoa habari ya shughuli yetu tunayofanya, tutakuwa tumefunguliwa kutoka kwenye kiapo hiki ulichotufanya tuape.”
But if you will have betrayed us, so that you spread this word in their midst, we will be free from this oath, to which you have sworn us.”
21 Naye akajibu, “Nimekubali. Na iwe kama mnavyosema.” Kwa hiyo akaagana nao, nao wakaondoka. Yeye akaifunga ile kamba nyekundu dirishani.
And she responded, “Just as you have spoken, so let it be done.” And sending them to travel on, she hung the scarlet cord at the window.
22 Walipoondoka, wakaelekea vilimani na kukaa huko siku tatu, hadi wale waliokuwa wakiwafuatilia wakawa wamewatafuta njia nzima na kurudi pasipo kuwapata.
And truly, walking on, they arrived at the mountains, and they stayed there for three days, until those who had been pursuing them returned. For having sought them along the entire way, they did not find them.
23 Ndipo wale watu wawili wakaanza kurudi. Wakashuka kutoka kule vilimani, wakavuka mto na kuja kwa Yoshua mwana wa Nuni, na kumweleza kila kitu kilichowapata.
And when they returned and entered the city, the explorers descended from the mountain. And crossing the Jordan, they went to Joshua, the son of Nun, and they reported to him all that had happened to them.
24 Wakamwambia Yoshua, “Hakika Bwana ametupa nchi yote mikononi mwetu; watu wote wanayeyuka kwa hofu kwa sababu yetu.”
And they said, “The Lord has delivered this entire land into our hands, and all its inhabitants have been struck down by fear.”