< Yoshua 2 >

1 Kisha Yoshua mwana wa Nuni kwa siri akawatuma wapelelezi wawili kutoka Shitimu, akawaambia, “Nendeni mkaikague hiyo nchi, hasa Yeriko.” Kwa hiyo wakaenda na kuingia kwenye nyumba ya kahaba mmoja jina lake Rahabu na kukaa humo.
Poslal pak byl Jozue, syn Nun, z Setim dva muže špehéře tajně, řka: Jděte, shlédněte zemi, zvlášť Jericho. I šli a vešli do domu ženy nevěstky, jejíž jméno bylo Raab, a odpočinuli tu.
2 Mfalme wa Yeriko akaambiwa, “Tazama! Baadhi ya Waisraeli wamekuja huku usiku huu kuipeleleza nchi.”
Ale jakž oznámeno bylo králi Jericha a povědíno: Aj, muži přišli sem této noci z synů Izraelských, aby shlédli zemi,
3 Hivyo mfalme wa Yeriko akatuma huu ujumbe kwa Rahabu: “Watoe wale watu waliokujia na kuingia nyumbani mwako, kwa sababu wamekuja kuipeleleza nchi yote.”
Tedy poslal král Jericha k Raab, řka: Vyveď muže, kteříž přišli k tobě, a vešli do domu tvého, nebo k vyšpehování vší země přišli.
4 Lakini huyo mwanamke alikuwa amewachukua hao watu wawili na kuwaficha. Akasema, “Naam, watu hao walikuja kwangu, lakini sikujua walikotoka.
(Pojavši pak žena ty dva muže, skryla je.) Kteráž odpověděla: Pravda jest, přišliť jsou ke mně muži, ale nevěděla jsem, odkud jsou.
5 Kulipoingia giza, wakati wa kufunga lango la mji, watu hao waliondoka. Sijui njia waliyoiendea. Wafuatilieni haraka. Huenda mkawapata.”
A když bránu zavírati měli v soumrak, vyšli muži ti, a nevím, kam jsou šli; hoňte je rychle, nebo dostihnete jich.
6 (Lakini alikuwa amewapandisha darini akawafunika kwa mabua ya kitani aliyokuwa ameyatandika darini.)
Ale ona rozkázala jim vstoupiti na střechu, a skryla je v pazdeří lněném, kteréž byla skladla na střeše.
7 Basi hao watu wakaondoka kuwafuatilia hao wapelelezi katika njia ile inayoelekea vivuko vya Yordani, mara tu wafuatiliaji walipotoka nje, lango likafungwa.
Muži pak vyslaní honili je cestou Jordánskou až k brodům; a zavřína jest brána, jakž vyšli ti, kteříž je honili.
8 Kabla wale wapelelezi hawajalala, Rahabu akawaendea huko juu darini,
Prvé pak, než usnuli špehéři, vstoupila k nim ona na střechu,
9 akawaambia, “Ninajua kuwa Bwana amewapa nchi hii na hofu kuu imetuangukia kwa sababu yenu, kiasi kwamba wote waishio katika nchi hii wanayeyuka kwa hofu kwa sababu yenu.
A řekla mužům těm: Vím, že Hospodin dal vám zemi tuto, nebo připadl na nás strach váš, tak že oslábli všickni obyvatelé země před tváří vaší.
10 Tumesikia jinsi Bwana alivyokausha maji ya Bahari ya Shamu kwa ajili yenu mlipotoka Misri, pia lile mlilowatendea Sihoni na Ogu, wafalme wawili wa Waamori mashariki mwa Yordani, ambao mliwaangamiza kabisa.
Slyšeli jsme zajisté, jak vysušil Hospodin vody moře Rudého před tváří vaší, když jste vyšli z Egypta, a co jste učinili dvěma králům Amorejským, kteříž byli za Jordánem, Seonovi a Ogovi, kteréž jste zahladili jako proklaté.
11 Tuliposikia juu ya hili, mioyo yetu iliyeyuka na kila mmoja alikosa ujasiri kwa sababu yenu, kwa maana Bwana Mungu wenu ni Mungu juu mbinguni na duniani chini.
Což když jsme uslyšeli, osláblo srdce naše, aniž zůstává více v kom duše před tváří vaší, nebo Hospodin Bůh váš jest Bůh na nebi svrchu, i na zemi dole.
12 Sasa basi, tafadhali niapieni kwa Bwana, kwamba mtaitendea hisani jamaa ya baba yangu, kwa kuwa mimi nimewatendea hisani. Nipeni ishara ya uaminifu
Nyní tedy, prosím, přisáhněte mi skrze Hospodina, poněvadž jsem učinila vám milosrdenství, že i vy učiníte s domem otce mého milosrdenství, a dáte mi znamení jisté,
13 kwamba mtayahifadhi maisha ya baba yangu na mama yangu, ndugu zangu wa kiume na wa kike, pamoja na wale wote walio wa kwao na kwamba mtatuokoa na kifo.”
Že budete živiti otce mého i matku mou, bratří mé i sestry mé a všecko, cožkoli jejich jest, a vysvobodíte duše naše od smrti.
14 Wale watu wakamhakikishia Rahabu, “Uhai wetu kwa uhai wenu! Ikiwa hutatoa habari ya nini tunachofanya, wakati Bwana atakapotupa nchi hii, tutawatendea kwa hisani na kwa uaminifu.”
I řekli jí muži ti: Duše naše za vás nechť jsou na smrt; jestliže však nepronesete řeči naší této, takť se jistě stane, že když nám dá Hospodin zemi tuto, tehdy učiníme s tebou milosrdenství a pravdu.
15 Kisha akawateremsha dirishani kwa kamba, kwa kuwa nyumba yake aliyokuwa anaishi ilikuwa sehemu ya ukuta wa mji.
Protož spustila je oknem po provazu; nebo dům její byl při zdi městské, a na zdi ona bydlila.
16 Alikuwa amewaambia, “Nendeni vilimani ili wale wafuatiliaji wasiwapate. Jificheni huko kwa siku tatu mpaka watakaporudi, hatimaye mwende zenu.”
I řekla jim: Jděte k této hoře, aby se nepotkali s vámi, kteříž vás honí, a krejte se tam za tři dni, až se oni zase navrátí, a potom půjdete cestou svou.
17 Wale watu wakamwambia, “Hiki kiapo ulichotuapisha hakitatufunga,
Tedy řekli muži k ní: Prosti budeme od této přísahy tvé, kterouž jsi zavázala nás,
18 isipokuwa, hapo tutakapoingia katika nchi hii, utakuwa umefunga hii kamba nyekundu dirishani pale ulipotuteremshia na kama utakuwa umewaleta baba yako na mama yako, ndugu zako na jamaa yako yote ndani ya nyumba yako.
Jestliže, když vejdeme do země, neuvážeš provázku tohoto z nití hedbáví červeného dvakrát barveného v tomto okně, jímž jsi nás spustila, také otce svého a matky své, i bratří svých, a všeho domu otce svého neshromáždíš-li k sobě do domu.
19 Ikiwa mtu yeyote atatoka nje ya nyumba yako akaenda mtaani, damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe, hatutawajibika. Lakini yule ambaye atakuwa ndani pamoja nawe, kama mkono wa mtu yeyote ukiwa juu yake damu yake itakuwa juu ya vichwa vyetu.
Také kdo by vyšel ven ze dveří domu tvého, krev jeho bude na hlavu jeho, ale my budeme bez viny; a každého toho, kdož bude s tebou v domě, jestliže by se kdo rukou dotekl, krev jeho na hlavy naše připadni.
20 Lakini ikiwa utatoa habari ya shughuli yetu tunayofanya, tutakuwa tumefunguliwa kutoka kwenye kiapo hiki ulichotufanya tuape.”
Jestliže pak proneseš tuto řeč naši, budeme prosti od přísahy tvé, kterouž jsi nás zavázala.
21 Naye akajibu, “Nimekubali. Na iwe kama mnavyosema.” Kwa hiyo akaagana nao, nao wakaondoka. Yeye akaifunga ile kamba nyekundu dirishani.
Odpověděla ona: Nechť jest tak, jakž jste řekli. I propustila je a odešli; i uvázala provázek z hedbáví červeného dvakrát barveného v tom okně.
22 Walipoondoka, wakaelekea vilimani na kukaa huko siku tatu, hadi wale waliokuwa wakiwafuatilia wakawa wamewatafuta njia nzima na kurudi pasipo kuwapata.
Odšedše pak, přišli na horu, a pobyli tam za tři dni, dokudž se nenavrátili, kteříž je honili; nebo jich hledali ti, kteříž je honili po všech cestách, ale nic nenalezli.
23 Ndipo wale watu wawili wakaanza kurudi. Wakashuka kutoka kule vilimani, wakavuka mto na kuja kwa Yoshua mwana wa Nuni, na kumweleza kila kitu kilichowapata.
Ti pak dva muži sšedše s hory, navrátili se a přeplavili se přes Jordán; i přišli k Jozue, synu Nun, a vypravovali jemu všecko, co se s nimi dálo.
24 Wakamwambia Yoshua, “Hakika Bwana ametupa nchi yote mikononi mwetu; watu wote wanayeyuka kwa hofu kwa sababu yetu.”
A řekli k Jozue: Dalť jest Hospodin v ruce naše všecku zemi, nebo se zděsili všickni obyvatelé země tváři naší.

< Yoshua 2 >