< Yoshua 19 >

1 Kura ya pili ikaangukia kabila la Simeoni, ukoo kwa ukoo. Urithi wao ulikuwa ndani ya eneo la Yuda.
Et egressa est sors secunda filiorum Simeon per cognationes suas: fuitque hereditas
2 Ulijumuisha: Beer-Sheba (au Sheba), Molada,
eorum in medio possessionis filiorum Iuda: Bersabee et Sabee et Molada
3 Hasar-Shuali, Bala, Esemu,
et Hasersual, Bala et Asem
4 Eltoladi, Bethuli, Horma,
et Eltholad, Bethul et Harma
5 Siklagi, Beth-Markabothi, Hasar-Susa,
et Siceleg et Bethmarchaboth et Hasersusa
6 Beth-Lebaothi na Sharuheni; hii ilikuwa miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake.
et Bethlebaoth et Sarohen: civitates tredecim, et villæ earum.
7 Pia Aini, Rimoni, Etheri, na Ashani; hii ilikuwa miji minne na vijiji vyake,
Ain et Remmon et Athar et Asan: civitates quattuor, et villæ earum:
8 pamoja na vijiji vyote vinavyoizunguka miji hii mpaka Baalath-Beeri (ambayo ndiyo Rama iliyo katika Negebu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simeoni ukoo kwa ukoo.
omnes viculi per circuitum urbium istarum usque ad Baalath Beer Ramath contra australem plagam. Hæc est hereditas filiorum Simeon iuxta cognationes suas,
9 Urithi wa Wasimeoni ulitolewa kutoka fungu la Yuda, kwa kuwa fungu la Yuda lilikuwa kubwa kuliko walivyohitaji. Hivyo kabila la Simeoni lilipewa urithi wao ndani ya eneo la Yuda.
in possessione et funiculo filiorum Iuda: quia maior erat. et idcirco filii Simeon possederunt in medio hereditatis eorum.
10 Kura ya tatu ikaangukia kabila la Zabuloni, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao uliendelea hadi Saridi.
Ceciditque sors tertia filiorum Zabulon per cognationes suas: factus est terminus possessionis eorum usque Sarid.
11 Kuelekea upande wa magharibi ukafika Marala, ukagusa Dabeshethi, na kuendelea mpaka kwenye bonde karibu na Yokneamu.
Ascenditque de Mari et Merala, et pervenit in Debbaseth, usque ad torrentem qui est contra Ieconam.
12 Ukageuka mashariki, kuanzia Saridi kuelekea mawio ya jua hadi kwenye nchi ya Kisiloth-Tabori, na kwenda hadi Daberathi, kupanda Yafia.
Et revertitur de Sared contra Orientem in fines Ceseleththabor: et egreditur ad Dabereth, ascenditque contra Iaphie.
13 Kisha ukaendelea mashariki hadi Gath-Heferi na kufika Eth-Kasini, ukatokea Rimoni na kugeuka kuelekea Nea.
Et inde pertransit usque ad orientalem plagam Gethhepher et Thacasin: et egreditur in Remmon, Amthar et Noa.
14 Huko mpaka ukazungukia upande wa kaskazini hadi Hanathoni na kuishia katika Bonde la Ifta-Eli.
Et circuit ad Aquilonem Hanathon: suntque egressus eius Vallis Iephthael,
15 Miji mingine iliyojumuishwa ni Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.
et Cateth et Naalol et Semeron et Ierala et Bethlehem: civitates duodecim, et villæ earum.
16 Miji hii na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa Zabuloni, ukoo kwa ukoo.
Hæc est hereditas tribus filiorum Zabulon per cognationes suas, urbes et viculi earum.
17 Kura ya nne ikamwangukia Isakari, ukoo kwa ukoo.
Issachar egressa est sors quarta per cognationes suas.
18 Eneo lao lilijumuisha: Yezreeli, Kesulothi, Shunemu,
fuitque eius hereditas Iezrael et Casaloth et Sunem
19 Hafaraimu, Shioni, Anaharathi,
et Hapharaim et Seon, et Anaharath
20 Rabithi, Kishioni, Ebesi,
et Rabboth et Cesion, Abes,
21 Remethi, En-Ganimu, En-Hada na Beth-Pasesi.
et Rameth, et Engannim, et Enhadda et Bethpheses.
22 Mpaka ule ukagusa Tabori, Shahasuma na Beth-Shemeshi, na ukaishia kwenye Yordani. Ilikuwa miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
Et pervenit terminus eius usque Thabor et Sehesima et Bethsames: eruntque exitus eius Iordanis: civitates sedecim, et villæ earum.
23 Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Isakari, ukoo kwa ukoo.
Hæc est possessio filiorum Issachar per cognationes suas, urbes, et viculi earum.
24 Kura ya tano ikaangukia kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
Ceciditque sors quinta tribui filiorum Aser per cognationes suas:
25 Eneo lao lilijumuisha: Helkathi, Hali, Beteni, Akishafu,
fuitque terminus eorum Halcath et Chali et Beten et Axaph
26 Alameleki, Amadi na Mishali. Upande wa magharibi mpaka uligusa Karmeli na Shihor-Libnathi.
et Elmelech et Amaad et Messal: et pervenit usque ad Carmelum maris et Sihor et Labanath.
27 Tena ukageuka mashariki kuelekea Beth-Dagoni, ukagusa Zabuloni na Bonde la Ifta-Eli, ukaenda upande wa kaskazini hadi Beth-Emeki na Neyeli, ukipitia Kabul upande wa kushoto.
Ac revertitur contra orientem Bethdagon: et pertransit usque Zabulon et Vallem Iephthael contra Aquilonem in Bethemec et Nehiel. Egrediturque ad lævam Cabul,
28 Ukaendelea hadi Abdoni, Rehobu, Hamoni na Kana, na kufika Sidoni Kuu.
et Abran et Rohob et Hamon et Cana, usque ad Sidonem magnam.
29 Mpaka huo ukageukia nyuma kuelekea Rama na kwenda hadi kwenye mji wenye ngome wa Tiro, ukageuka kuelekea Hosa na kutokeza baharini katika eneo la Akzibu,
revertiturque in Horma usque ad civitatem munitissimam Tyrum, et usque Hosa: eruntque exitus eius in mare de funiculo Achziba:
30 Uma, Afeki na Rehobu. Ilikuwepo miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
et Amma et Aphec et Rohob. civitates viginti duæ, et villæ earum.
31 Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
Hæc est possessio filiorum Aser per cognationes suas, urbesque et viculi earum.
32 Kura ya sita ikaangukia kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo:
Filiorum Nephthali sexta sors cecidit per familias suas:
33 Mpaka wao uliendelea kutoka Helefi na kwenye mti mkubwa ulio katika Saananimu, ukipitia Adami-Nekebu na Yabineeli hadi Lakumu, na kuishia katika Mto Yordani.
et cœpit terminus de Heleph et Elon in Saananim, et Adami, quæ est Neceb, et Iebnael usque Lecum: et egressus eorum usque ad Iordanem:
34 Mpaka ukaendelea magharibi kupitia Aznoth-Tabori na kutokea Hukoki. Ukagusa Zabuloni upande wa kusini, Asheri upande wa magharibi, na Yordani upande wa mashariki.
revertiturque terminus contra Occidentem in Azanotthabor, atque inde egreditur in Hucuca, et pertransit in Zabulon contra Meridiem, et in Aser contra Occidentem, et in Iuda ad Iordanem contra ortum solis.
35 Miji yenye ngome ilikuwa Sidimu, Seri, Hamathi, Rakathi, Kinerethi,
civitates munitissimæ, Assedim, Ser, et Emath, et Reccath et Cenereth,
36 Adama, Rama, Hazori,
et Edema et Arama, Asor
37 Kedeshi, Edrei, na En-Hasori,
et Cedes et Edrai, Enhasor
38 Ironi, Migdal-Eli, Horemu, Beth-Anathi na Beth-Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa na vijiji vyake.
et Ieron et Magdalel, Horem et Bethanath et Bethsames: civitates decem et novem, et villæ earum.
39 Miji hiyo pamoja na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo.
Hæc est possessio tribus filiorum Nephthali per cognationes suas, urbes et viculi earum.
40 Kura ya saba ikaangukia kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
Tribui filiorum Dan per familias suas egressa est sors septima:
41 Eneo la urithi wao lilijumuisha: Sora, Eshtaoli, Iri-Shemeshi,
et fuit terminus possessionis eius Sara et Esthaol, et Hirsemes, id est civitas solis.
42 Shaalabini, Aiyaloni, Ithla,
Selebin et Aialon et Iethela,
43 Eloni, Timna, Ekroni,
Elon et Themna et Acron,
44 Elteke, Gibethoni, Baalathi,
Elthece, Gebbethon et Balaath,
45 Yehudi, Bene-Beraki, Gath-Rimoni,
et Iud et Bane et Barach et Gethremmon:
46 Me-Yarkoni na Rakoni, pamoja na eneo linalotazamana na Yafa.
et Meiarcon et Arecon, cum termino qui respicit Ioppen,
47 (Lakini Wadani walipata shida kulimiliki eneo lao; kwa hiyo walipanda kuishambulia Leshemu, wakaitwaa, wakawaua watu wake kwa upanga na kuukalia. Walikaa Leshemu na kuuita Dani kufuatana na jina la baba yao.)
et ipso fine concluditur. Ascenderuntque filii Dan, et pugnaverunt contra Lesem, ceperuntque eam: et percusserunt eam in ore gladii, et possederunt, et habitaverunt in ea, vocantes nomen eius Lesem Dan, ex nomine Dan patris sui.
48 Miji hii na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
Hæc est possessio tribus filiorum Dan, per cognationes suas, urbes et viculi earum.
49 Walipomaliza kugawanya nchi katika migawo kulingana na sehemu zao zilizowaangukia, Waisraeli wakampa Yoshua mwana wa Nuni urithi katikati yao,
Cumque complesset sorte dividere Terram singulis per tribus suas, dederunt filii Israel possessionem Iosue filio Nun in medio sui,
50 kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru. Walimpa mji alioutaka, ambao ni Timnath-Sera ulio katika nchi ya vilima ya Efraimu. Naye akajenga mji, akakaa huko.
iuxta præceptum Domini, urbem quam postulavit, Thamnath Saraa in monte Ephraim: et ædificavit civitatem, habitavitque in ea.
51 Haya ndiyo maeneo ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliyoyagawanya kwa kura huko Shilo mbele za Bwana penye ingilio la Hema la Kukutania. Hivyo wakamaliza kuigawanya nchi.
Hæ sunt possessiones, quas sorte diviserunt Eleazar sacerdos, et Iosue filius Nun, et principes familiarum, ac tribuum filiorum Israel in Silo, coram Domino ad ostium tabernaculi testimonii, partitique sunt Terram.

< Yoshua 19 >