< Yoshua 19 >

1 Kura ya pili ikaangukia kabila la Simeoni, ukoo kwa ukoo. Urithi wao ulikuwa ndani ya eneo la Yuda.
Kitakat se akluo som nu sin sou in sruf lal Simeon. Acn lalos uhc oasr pana luin acn lun sruf lal Judah.
2 Ulijumuisha: Beer-Sheba (au Sheba), Molada,
Acn inge pa Beersheba, Sheba, Moladah,
3 Hasar-Shuali, Bala, Esemu,
Hazar Shual, Balah, Ezem,
4 Eltoladi, Bethuli, Horma,
Eltolad, Bethul, Hormah,
5 Siklagi, Beth-Markabothi, Hasar-Susa,
Ziklag, Beth Marcaboth, Hazar Susah,
6 Beth-Lebaothi na Sharuheni; hii ilikuwa miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake.
Beth Lebaoth, ac Sharuhen — siti singoul tolu nufon, wi inkul nukewa ma raunela.
7 Pia Aini, Rimoni, Etheri, na Ashani; hii ilikuwa miji minne na vijiji vyake,
Oayapa Ain, Rimmon, Ether, ac Ashan — siti akosr, wi inkul nukewa ma raunela,
8 pamoja na vijiji vyote vinavyoizunguka miji hii mpaka Baalath-Beeri (ambayo ndiyo Rama iliyo katika Negebu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simeoni ukoo kwa ukoo.
weang pacna acn nukewa raunela siti inge nwe Baalath Beer (ku Ramah), su oan nu eir. Pa inge acn ma itukyang nu sin sou in sruf lal Simeon tuh in ma lalos.
9 Urithi wa Wasimeoni ulitolewa kutoka fungu la Yuda, kwa kuwa fungu la Yuda lilikuwa kubwa kuliko walivyohitaji. Hivyo kabila la Simeoni lilipewa urithi wao ndani ya eneo la Yuda.
Ke sripen acn lal Judah yohk liki ma elos enenu, oru itukyang sie ip lalos inge nu sin sruf lal Simeon.
10 Kura ya tatu ikaangukia kabila la Zabuloni, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao uliendelea hadi Saridi.
Kitakat se aktolu som nu sin sou in sruf lal Zebulun. An se elos eis inge fahla na nwe sun acn Sarid.
11 Kuelekea upande wa magharibi ukafika Marala, ukagusa Dabeshethi, na kuendelea mpaka kwenye bonde karibu na Yokneamu.
Liki acn sacn, masrol an fahla roto lac nu Mareal, ac pusralla acn Dabbesheth ac infacl srisrik soko kutulap in acn Jokneam.
12 Ukageuka mashariki, kuanzia Saridi kuelekea mawio ya jua hadi kwenye nchi ya Kisiloth-Tabori, na kwenda hadi Daberathi, kupanda Yafia.
Ke layen kutulap in acn Sarid, masrol an fahla nu kutulap nu ke masrol nu Chisloth Tabor, na sifilpa fahla nu Daberath ac utyak nu Japhia.
13 Kisha ukaendelea mashariki hadi Gath-Heferi na kufika Eth-Kasini, ukatokea Rimoni na kugeuka kuelekea Nea.
Sifilpa fahla liki acn sacn nu kutulap nwe sun Gath Hepher ac Ethkazin, ac kuhfla nu Neah ke inkanek nu Rimmon.
14 Huko mpaka ukazungukia upande wa kaskazini hadi Hanathoni na kuishia katika Bonde la Ifta-Eli.
Ke masrol epang an, el kuhfla nu Hannathon, fahla safla Infahlfal Iphtahel.
15 Miji mingine iliyojumuishwa ni Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.
Acn inge pa Kattath, Nahalal, Shimron, Idalah, ac Bethlehem— siti singoul luo nufon, wi inkul nukewa ma raunela.
16 Miji hii na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa Zabuloni, ukoo kwa ukoo.
Siti inge wi acn ma raunela, oan in acn ma itukyang nu sin sou in sruf lal Zebulun tuh in ma lalos.
17 Kura ya nne ikamwangukia Isakari, ukoo kwa ukoo.
Kitakat se akakosr som nu sin sou in sruf lal Issachar.
18 Eneo lao lilijumuisha: Yezreeli, Kesulothi, Shunemu,
Acn inge pa Jezreel, Chesulloth, Shunem,
19 Hafaraimu, Shioni, Anaharathi,
Hapharaim, Shion, Anaharath,
20 Rabithi, Kishioni, Ebesi,
Rabbith, Kishion, Ebez,
21 Remethi, En-Ganimu, En-Hada na Beth-Pasesi.
Remeth, Engannim, Enhaddah, ac Bethpazzez.
22 Mpaka ule ukagusa Tabori, Shahasuma na Beth-Shemeshi, na ukaishia kwenye Yordani. Ilikuwa miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
Masrol in acn Issachar fahla pusralla Tabor, Shahazumah, Beth Shemesh, ac safla Infacl Jordan — siti singoul onkosr nufon, wi inkul nukewa ma raunela.
23 Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Isakari, ukoo kwa ukoo.
Siti inge wi acn ma raunela, oan in acn ma itukyang nu sin sou in sruf lal Issachar tuh in ma lalos.
24 Kura ya tano ikaangukia kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
Kitakat se aklimekosr som nu sin sou in sruf lal Asher.
25 Eneo lao lilijumuisha: Helkathi, Hali, Beteni, Akishafu,
Acn inge pa Helkath, Hali, Beten, Achshaph,
26 Alameleki, Amadi na Mishali. Upande wa magharibi mpaka uligusa Karmeli na Shihor-Libnathi.
Allam Melech, Amad, ac Mishal. Masrol nu roto an pusralla Carmel ac Shihor Libnath.
27 Tena ukageuka mashariki kuelekea Beth-Dagoni, ukagusa Zabuloni na Bonde la Ifta-Eli, ukaenda upande wa kaskazini hadi Beth-Emeki na Neyeli, ukipitia Kabul upande wa kushoto.
Ac nu kutulap, masrol an fahla sun acn Bethdagon, pusralla acn Zebulun ac Infahlfal Iphtahel nu epang nu Bethemek ac Neiel, na fahla na nwe epang nu Cabul,
28 Ukaendelea hadi Abdoni, Rehobu, Hamoni na Kana, na kufika Sidoni Kuu.
Ebron, Rehob, Hammon, ac Kanah nwe ke sun acn Sidon.
29 Mpaka huo ukageukia nyuma kuelekea Rama na kwenda hadi kwenye mji wenye ngome wa Tiro, ukageuka kuelekea Hosa na kutokeza baharini katika eneo la Akzibu,
Na masrol an kuhfla nu Ramah, ac sun Tyre (sie siti rauniyukla ke pot fulat) na sifil kuhfla nu Hosah, ac fahla safla ke Meoa Mediterranean. Siti inge oasr pac we: Mahalab, Achzib,
30 Uma, Afeki na Rehobu. Ilikuwepo miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
Ummah, Aphek, ac Rehob — siti longoul luo nufon, wi inkul nukewa ma raunela.
31 Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
Siti inge wi acn ma raunela, oan in acn ma itukyang nu sin sou in sruf lal Asher tuh in ma lalos.
32 Kura ya sita ikaangukia kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo:
Kitakat se akonkosr som nu sin sou in sruf lal Naphtali.
33 Mpaka wao uliendelea kutoka Helefi na kwenye mti mkubwa ulio katika Saananimu, ukipitia Adami-Nekebu na Yabineeli hadi Lakumu, na kuishia katika Mto Yordani.
Masrol ke acn se inge fahla Heleph lac nu ke sak oak in Zaanannim ac fahla nu Adaminekeb ac nu Jamnia, ac fahla nwe Lakkum ac safla ke Infacl Jordan.
34 Mpaka ukaendelea magharibi kupitia Aznoth-Tabori na kutokea Hukoki. Ukagusa Zabuloni upande wa kusini, Asheri upande wa magharibi, na Yordani upande wa mashariki.
Na masrol sacn kuhfla nu roto som nu Aznoth Tabor, ac liki acn sacn fahla nu Hukkok pusralla Zebulun nu eir, ac Asher nu roto, ac Infacl Jordan nu kutulap.
35 Miji yenye ngome ilikuwa Sidimu, Seri, Hamathi, Rakathi, Kinerethi,
Siti inge nukewa rauniyukla ke pot fulat: Ziddim, Zer, Hammath, Rakkath, Chinnereth,
36 Adama, Rama, Hazori,
Adamah, Ramah, Hazor,
37 Kedeshi, Edrei, na En-Hasori,
Kedesh, Edrei, Enhazor,
38 Ironi, Migdal-Eli, Horemu, Beth-Anathi na Beth-Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa na vijiji vyake.
Yiron, Migdalel, Horem, Bethanath, ac Beth Shemesh — siti singoul eu nufon wi inkul nukewa ma raunela.
39 Miji hiyo pamoja na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo.
Siti inge wi acn ma raunela, oan in acn ma itukyang nu sin sou in sruf lal Naphtali tuh in ma lalos.
40 Kura ya saba ikaangukia kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
Kitakat se akitkosr som nu sin sou in sruf lal Dan.
41 Eneo la urithi wao lilijumuisha: Sora, Eshtaoli, Iri-Shemeshi,
Acn inge pa Zorah, Eshtaol, Irshemesh,
42 Shaalabini, Aiyaloni, Ithla,
Shaalbim, Aijalon, Ithlah,
43 Eloni, Timna, Ekroni,
Elon, Timnah, Ekron,
44 Elteke, Gibethoni, Baalathi,
Eltekeh, Gibbethon, Baalath,
45 Yehudi, Bene-Beraki, Gath-Rimoni,
Jehud, Beneberak, Gathrimmon,
46 Me-Yarkoni na Rakoni, pamoja na eneo linalotazamana na Yafa.
Mejarkon, ac Rakkon, ac acn nukewa raunela Joppa.
47 (Lakini Wadani walipata shida kulimiliki eneo lao; kwa hiyo walipanda kuishambulia Leshemu, wakaitwaa, wakawaua watu wake kwa upanga na kuukalia. Walikaa Leshemu na kuuita Dani kufuatana na jina la baba yao.)
Ke itukla acn sin tulik natul Dan inge, elos som nu Laish ac mweuni. Elos sruokya ac onela mwet we, ac eisla acn sac lalos. Elos oakwuki we ac ekulla inen siti sac liki Laish nu ke Dan, in oana inen papa tumun sruf lalos.
48 Miji hii na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
Siti inge wi acn ma raunela, oan in acn ma itukyang nu sin sou in sruf lal Dan tuh in ma lalos.
49 Walipomaliza kugawanya nchi katika migawo kulingana na sehemu zao zilizowaangukia, Waisraeli wakampa Yoshua mwana wa Nuni urithi katikati yao,
Ke mwet Israel elos kitalik tari acn nukewa, elos sang ipin acn se nu sel Joshua wen natul Nun tuh in ma lal.
50 kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru. Walimpa mji alioutaka, ambao ni Timnath-Sera ulio katika nchi ya vilima ya Efraimu. Naye akajenga mji, akakaa huko.
In oana ma LEUM GOD El tuh sapkin, elos sang siti se el tuh siyuk ah: Timnath Serah, su oan fineol uh in Ephraim. Joshua el sifil musaela siti se inge ac muta we.
51 Haya ndiyo maeneo ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliyoyagawanya kwa kura huko Shilo mbele za Bwana penye ingilio la Hema la Kukutania. Hivyo wakamaliza kuigawanya nchi.
Eleazar mwet tol, Joshua wen natul Nun, ac mwet kol lun kais sie sou in sruf lun Israel, elos kitalik acn inge ke fa ye mutun LEUM GOD in acn Shiloh, ke mutunoa in Lohm Nuknuk sin LEUM GOD. Pa inge saflaiyen kitakatelik lun acn inge.

< Yoshua 19 >