< Yoshua 19 >

1 Kura ya pili ikaangukia kabila la Simeoni, ukoo kwa ukoo. Urithi wao ulikuwa ndani ya eneo la Yuda.
And the second lot came forth to Simeon, [even] for the tribe of the children of Simeon according to their families: and their inheritance was within the inheritance of the children of Judah.
2 Ulijumuisha: Beer-Sheba (au Sheba), Molada,
And they had in their inheritance, Beer-sheba, and Sheba, and Moladah.
3 Hasar-Shuali, Bala, Esemu,
And Hazar-shual, and Balah, and Azem,
4 Eltoladi, Bethuli, Horma,
And Eltolad, and Bethul, and Hormah,
5 Siklagi, Beth-Markabothi, Hasar-Susa,
And Ziklag, and Beth-marcaboth, and Hazar-susah,
6 Beth-Lebaothi na Sharuheni; hii ilikuwa miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake.
And Beth-lebaoth, and Sheruhen; thirteen cities and their villages:
7 Pia Aini, Rimoni, Etheri, na Ashani; hii ilikuwa miji minne na vijiji vyake,
Ain, Remmon, and Ether, and Ashan; four cities and their villages:
8 pamoja na vijiji vyote vinavyoizunguka miji hii mpaka Baalath-Beeri (ambayo ndiyo Rama iliyo katika Negebu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simeoni ukoo kwa ukoo.
And all the villages that [were] around these cities to Baalath-beer, Ramath of the south. This [is] the inheritance of the tribe of the children of Simeon according to their families.
9 Urithi wa Wasimeoni ulitolewa kutoka fungu la Yuda, kwa kuwa fungu la Yuda lilikuwa kubwa kuliko walivyohitaji. Hivyo kabila la Simeoni lilipewa urithi wao ndani ya eneo la Yuda.
Out of the portion of the children of Judah [was] the inheritance of the children of Simeon: for the part of the children of Judah was too much for them: therefore the children of Simeon had their inheritance within the inheritance of them.
10 Kura ya tatu ikaangukia kabila la Zabuloni, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao uliendelea hadi Saridi.
And the third lot came up for the children of Zebulun according to their families: and the border of their inheritance was to Sarid:
11 Kuelekea upande wa magharibi ukafika Marala, ukagusa Dabeshethi, na kuendelea mpaka kwenye bonde karibu na Yokneamu.
And their border went up towards the sea, and Maralah, and reached to Dabbasheth, and reached to the river that [is] before Jokneam,
12 Ukageuka mashariki, kuanzia Saridi kuelekea mawio ya jua hadi kwenye nchi ya Kisiloth-Tabori, na kwenda hadi Daberathi, kupanda Yafia.
And turned from Sarid eastward, towards the sun-rising, to the border of Chisloth-tabor, and then goeth out to Daberath, and goeth up to Japhia,
13 Kisha ukaendelea mashariki hadi Gath-Heferi na kufika Eth-Kasini, ukatokea Rimoni na kugeuka kuelekea Nea.
And from thence passeth along on the east to Gittah-hepher, to Ittah-kazin, and goeth out to Remmon-methoar to Neah;
14 Huko mpaka ukazungukia upande wa kaskazini hadi Hanathoni na kuishia katika Bonde la Ifta-Eli.
And the border compasseth it on the north side to Hannathon: and the limits of it are in the valley of Jiphthah-el:
15 Miji mingine iliyojumuishwa ni Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.
And Kattath, and Nahallal, and Shimron, and Idalah, and Beth-lehem; twelve cities with their villages.
16 Miji hii na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa Zabuloni, ukoo kwa ukoo.
This [is] the inheritance of the children of Zebulun according to their families, these cities with their villages.
17 Kura ya nne ikamwangukia Isakari, ukoo kwa ukoo.
[And] the fourth lot came out to Issachar, for the children of Issachar according to their families.
18 Eneo lao lilijumuisha: Yezreeli, Kesulothi, Shunemu,
And their border was towards Jezreel, and Chesulloth, and Shunem,
19 Hafaraimu, Shioni, Anaharathi,
And Hapharaim, and Shihon, and Anaharath,
20 Rabithi, Kishioni, Ebesi,
And Rabbith, and Kishion, and Abez,
21 Remethi, En-Ganimu, En-Hada na Beth-Pasesi.
And Remeth, and En-gannim, and En-haddah, and Beth-pazzez;
22 Mpaka ule ukagusa Tabori, Shahasuma na Beth-Shemeshi, na ukaishia kwenye Yordani. Ilikuwa miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
And the border reacheth to Tabor, and Shahazimah, and Beth-shemesh, and the limits of their border were at Jordan: sixteen cities with their villages.
23 Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Isakari, ukoo kwa ukoo.
This [is] the inheritance of the tribe of the children of Issachar according to their families, the cities and their villages.
24 Kura ya tano ikaangukia kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
And the fifth lot came out for the tribe of the children of Asher according to their families.
25 Eneo lao lilijumuisha: Helkathi, Hali, Beteni, Akishafu,
And their border was Helkath, and Hali, and Beten, and Achshaph,
26 Alameleki, Amadi na Mishali. Upande wa magharibi mpaka uligusa Karmeli na Shihor-Libnathi.
And Alammelech, and Amad, and Misheal; and reacheth to Carmel westward, and to Shihor-libnath;
27 Tena ukageuka mashariki kuelekea Beth-Dagoni, ukagusa Zabuloni na Bonde la Ifta-Eli, ukaenda upande wa kaskazini hadi Beth-Emeki na Neyeli, ukipitia Kabul upande wa kushoto.
And turneth towards the sun-rising to Beth-dagon, and reacheth to Zebulun, and to the valley of Jiphthah-el towards the north side of Beth-emek, and Neiel, and goeth out to Cabul on the left hand,
28 Ukaendelea hadi Abdoni, Rehobu, Hamoni na Kana, na kufika Sidoni Kuu.
And Hebron, and Rehob, and Hammon, and Kanah, [even] to great Zidon;
29 Mpaka huo ukageukia nyuma kuelekea Rama na kwenda hadi kwenye mji wenye ngome wa Tiro, ukageuka kuelekea Hosa na kutokeza baharini katika eneo la Akzibu,
And [then] the border turneth to Ramah, and to the strong city Tyre; and the border turneth to Hosah: and the limits of it are at the sea from the coast to Achzib:
30 Uma, Afeki na Rehobu. Ilikuwepo miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
Ummah also, and Aphek, and Rehob: twenty and two cities with their villages.
31 Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
This [is] the inheritance of the tribe of the children of Asher according to their families, these cities with their villages.
32 Kura ya sita ikaangukia kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo:
The sixth lot came out to the children of Naphtali, [even] for the children of Naphtali according to their families.
33 Mpaka wao uliendelea kutoka Helefi na kwenye mti mkubwa ulio katika Saananimu, ukipitia Adami-Nekebu na Yabineeli hadi Lakumu, na kuishia katika Mto Yordani.
And their border was from Heleph, from Allon to Zaanannim, and Adami, Nekeb, and Jabneel, to Lakum; and the limits thereof were at Jordan:
34 Mpaka ukaendelea magharibi kupitia Aznoth-Tabori na kutokea Hukoki. Ukagusa Zabuloni upande wa kusini, Asheri upande wa magharibi, na Yordani upande wa mashariki.
And [then] the border turneth westward to Aznoth-tabor, and goeth out from thence to Hukkok, and reacheth to Zebulun on the south side, and reacheth to Asher on the west side, and to Judah upon Jordan towards the sun-rising.
35 Miji yenye ngome ilikuwa Sidimu, Seri, Hamathi, Rakathi, Kinerethi,
And the fortified cities [are] Ziddim, Zer, and Hammath, Rakkath, and Chinnereth,
36 Adama, Rama, Hazori,
And Adamah, and Ramah, and Hazor,
37 Kedeshi, Edrei, na En-Hasori,
And Kedesh, and Edrei, and En-hazor,
38 Ironi, Migdal-Eli, Horemu, Beth-Anathi na Beth-Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa na vijiji vyake.
And Iron, and Migdal-el, Horem, and Beth-anath, and Beth-shemesh; nineteen cities with their villages.
39 Miji hiyo pamoja na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo.
This [is] the inheritance of the tribe of the children of Naphtali according to their families, the cities and their villages.
40 Kura ya saba ikaangukia kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
[And] the seventh lot came out for the tribe of the children of Dan according to their families.
41 Eneo la urithi wao lilijumuisha: Sora, Eshtaoli, Iri-Shemeshi,
And the border of their inheritance was Zorah, and Eshtaol, and Ir-shemesh,
42 Shaalabini, Aiyaloni, Ithla,
And Shaalabbim, and Ajalon, and Jethlah,
43 Eloni, Timna, Ekroni,
And Elon, and Thimnathah, and Ekron,
44 Elteke, Gibethoni, Baalathi,
And Eltekeh, and Gibbethon, and Baalath,
45 Yehudi, Bene-Beraki, Gath-Rimoni,
And Jehud, and Bene-berak, and Gath-rimmon,
46 Me-Yarkoni na Rakoni, pamoja na eneo linalotazamana na Yafa.
And Me-jarkon, and Rakkon, with the border before Japho.
47 (Lakini Wadani walipata shida kulimiliki eneo lao; kwa hiyo walipanda kuishambulia Leshemu, wakaitwaa, wakawaua watu wake kwa upanga na kuukalia. Walikaa Leshemu na kuuita Dani kufuatana na jina la baba yao.)
And the border of the children of Dan, went out [too little] for them: therefore the children of Dan went up to fight against Leshem, and took it, and smote it with the edge of the sword, and possessed it, and dwelt in it, and called Leshem, Dan, after the name of Dan their father.
48 Miji hii na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
This [is] the inheritance of the tribe of the children of Dan according to their families, these cities with their villages.
49 Walipomaliza kugawanya nchi katika migawo kulingana na sehemu zao zilizowaangukia, Waisraeli wakampa Yoshua mwana wa Nuni urithi katikati yao,
When they had made an end of dividing the land for inheritance by their borders, the children of Israel gave an inheritance to Joshua the son of Nun among them:
50 kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru. Walimpa mji alioutaka, ambao ni Timnath-Sera ulio katika nchi ya vilima ya Efraimu. Naye akajenga mji, akakaa huko.
According to the word of the LORD they gave him the city which he asked, [even] Timnath-serah in mount Ephraim: and he built the city, and dwelt in it.
51 Haya ndiyo maeneo ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliyoyagawanya kwa kura huko Shilo mbele za Bwana penye ingilio la Hema la Kukutania. Hivyo wakamaliza kuigawanya nchi.
These [are] the inheritances which Eleazar the priest, and Joshua the son of Nun, and the heads of the fathers of the tribes of the children of Israel, divided for an inheritance by lot in Shiloh before the LORD, at the door of the tabernacle of the congregation. So they made an end of dividing the country.

< Yoshua 19 >