< Yoshua 19 >

1 Kura ya pili ikaangukia kabila la Simeoni, ukoo kwa ukoo. Urithi wao ulikuwa ndani ya eneo la Yuda.
The second casting of lots fell to Simeon, clan by clan. Their inheritance was in the middle of the inheritance that belonged to the tribe of Judah.
2 Ulijumuisha: Beer-Sheba (au Sheba), Molada,
They had for their inheritance Beersheba, Sheba, Moladah,
3 Hasar-Shuali, Bala, Esemu,
Hazar Shual, Balah, Ezem,
4 Eltoladi, Bethuli, Horma,
Eltolad, Bethul, and Hormah.
5 Siklagi, Beth-Markabothi, Hasar-Susa,
Simeon also had Ziklag, Beth Markaboth, Hazar Susah,
6 Beth-Lebaothi na Sharuheni; hii ilikuwa miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake.
Beth Lebaoth, and Sharuhen. These were thirteen cities, including their villages.
7 Pia Aini, Rimoni, Etheri, na Ashani; hii ilikuwa miji minne na vijiji vyake,
Simeon also had Ain, Rimmon, Ether, and Ashan. These were four cities, including their villages.
8 pamoja na vijiji vyote vinavyoizunguka miji hii mpaka Baalath-Beeri (ambayo ndiyo Rama iliyo katika Negebu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simeoni ukoo kwa ukoo.
These were together, including their the villages around these cities as far as Baalath Beer (the same as Ramah in the Negev). This was the inheritance of the tribe of Simeon, clan by clan.
9 Urithi wa Wasimeoni ulitolewa kutoka fungu la Yuda, kwa kuwa fungu la Yuda lilikuwa kubwa kuliko walivyohitaji. Hivyo kabila la Simeoni lilipewa urithi wao ndani ya eneo la Yuda.
The inheritance of the tribe of Simeon formed part of the territory of the tribe of Judah. Because the portion of land assigned to the tribe of Judah was too large for them, the tribe of Simeon received their inheritance out of the middle of their portion.
10 Kura ya tatu ikaangukia kabila la Zabuloni, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao uliendelea hadi Saridi.
The third casting of lots fell to the tribe of Zebulun, clan by clan. The border of their inheritance began at Sarid.
11 Kuelekea upande wa magharibi ukafika Marala, ukagusa Dabeshethi, na kuendelea mpaka kwenye bonde karibu na Yokneamu.
Their border went up westward toward Maralah and touched Dabbesheth; then it extended to the brook that was opposite Jokneam.
12 Ukageuka mashariki, kuanzia Saridi kuelekea mawio ya jua hadi kwenye nchi ya Kisiloth-Tabori, na kwenda hadi Daberathi, kupanda Yafia.
From Sarid the border turned eastward toward the east and went to the border of Kisloth Tabor. From there it went to Daberath and then up to Japhia.
13 Kisha ukaendelea mashariki hadi Gath-Heferi na kufika Eth-Kasini, ukatokea Rimoni na kugeuka kuelekea Nea.
From there it passed on eastward to Gath Hepher, and then to Eth Kazin; next it went to Rimmon and turned toward Neah.
14 Huko mpaka ukazungukia upande wa kaskazini hadi Hanathoni na kuishia katika Bonde la Ifta-Eli.
The border made a turn to the north to Hannathon and ended at the Valley of Iphtah El.
15 Miji mingine iliyojumuishwa ni Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.
This region included the cities of Kattath, Nahalal, Shimron, Idalah, and Bethlehem. There were twelve cities, including their villages.
16 Miji hii na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa Zabuloni, ukoo kwa ukoo.
This was the inheritance of the tribe of Zebulun, clan by clan, including these cities, including their villages.
17 Kura ya nne ikamwangukia Isakari, ukoo kwa ukoo.
The fourth casting of lots fell to Issachar, clan by clan.
18 Eneo lao lilijumuisha: Yezreeli, Kesulothi, Shunemu,
Their territory included Jezreel, Chesulloth, Shunem,
19 Hafaraimu, Shioni, Anaharathi,
Hapharaim, Shion, and Anaharath.
20 Rabithi, Kishioni, Ebesi,
It also included Rabbith, Kishion, Ebez,
21 Remethi, En-Ganimu, En-Hada na Beth-Pasesi.
Remeth, En Gannim, En Haddah, and Beth Pazzez.
22 Mpaka ule ukagusa Tabori, Shahasuma na Beth-Shemeshi, na ukaishia kwenye Yordani. Ilikuwa miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
Their border also touched Tabor, Shahazumah, and Beth Shemesh, and ended at the Jordan. There were sixteen cities, including their villages.
23 Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Isakari, ukoo kwa ukoo.
This was the inheritance of the tribe of Issachar, according to their clans—the cities, including their villages.
24 Kura ya tano ikaangukia kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
The fifth casting of lots fell to the tribe of Asher, clan by clan.
25 Eneo lao lilijumuisha: Helkathi, Hali, Beteni, Akishafu,
Their territory included Helkath, Hali, Beten, Akshaph,
26 Alameleki, Amadi na Mishali. Upande wa magharibi mpaka uligusa Karmeli na Shihor-Libnathi.
Allammelek, Amad, and Mishall. On the west the boundary extended to Carmel and Shihor Libnath.
27 Tena ukageuka mashariki kuelekea Beth-Dagoni, ukagusa Zabuloni na Bonde la Ifta-Eli, ukaenda upande wa kaskazini hadi Beth-Emeki na Neyeli, ukipitia Kabul upande wa kushoto.
Then it turned eastward to Beth Dagon and went as far as Zebulun, and then to the Valley of Iphtah El, northward to Beth Emek and Neiel. Then it continued on to Kabul toward the north.
28 Ukaendelea hadi Abdoni, Rehobu, Hamoni na Kana, na kufika Sidoni Kuu.
It then went on to Abdon, Rehob, Hammon, and Kanah, as far as Greater Sidon.
29 Mpaka huo ukageukia nyuma kuelekea Rama na kwenda hadi kwenye mji wenye ngome wa Tiro, ukageuka kuelekea Hosa na kutokeza baharini katika eneo la Akzibu,
The border turned back to Ramah, and then to the fortified city of Tyre. Then the border turned to Hosah and ended at the sea, in the region of Akzib,
30 Uma, Afeki na Rehobu. Ilikuwepo miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
Ummah, Aphek, and Rehob. There were twenty-two cities, including their villages.
31 Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
This was the inheritance of the tribe of Asher, clan by clan—the cities, including their villages.
32 Kura ya sita ikaangukia kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo:
The sixth casting of lots fell to tribe of Naphtali, clan by clan.
33 Mpaka wao uliendelea kutoka Helefi na kwenye mti mkubwa ulio katika Saananimu, ukipitia Adami-Nekebu na Yabineeli hadi Lakumu, na kuishia katika Mto Yordani.
Their border ran from Heleph, from the oak at Zaanannim, on to Adami Nekeb and Jabneel, as far as Lakkum; it ended at the Jordan.
34 Mpaka ukaendelea magharibi kupitia Aznoth-Tabori na kutokea Hukoki. Ukagusa Zabuloni upande wa kusini, Asheri upande wa magharibi, na Yordani upande wa mashariki.
The border turned westward to Aznoth Tabor and went on to Hukkok; it touched Zebulun on the south, and reached to Asher on the west and Judah on the east at the Jordan River.
35 Miji yenye ngome ilikuwa Sidimu, Seri, Hamathi, Rakathi, Kinerethi,
The fortified cities were Ziddim, Zer, Hammath, Rakkath, Kinnereth,
36 Adama, Rama, Hazori,
Adamah, Ramah, Hazor,
37 Kedeshi, Edrei, na En-Hasori,
Kedesh, Edrei, and En Hazor.
38 Ironi, Migdal-Eli, Horemu, Beth-Anathi na Beth-Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa na vijiji vyake.
There were also Yiron, Migdal El, Horem, Beth Anath, and Beth Shemesh. There were nineteen cities, including their villages.
39 Miji hiyo pamoja na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo.
This was the inheritance of the tribe of Naphtali, clan by clan—the cities, including their villages.
40 Kura ya saba ikaangukia kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
The seventh casting of lots fell to the tribe of Dan, clan by clan.
41 Eneo la urithi wao lilijumuisha: Sora, Eshtaoli, Iri-Shemeshi,
The territory of its inheritance included Zorah, Eshtaol, Ir Shemesh,
42 Shaalabini, Aiyaloni, Ithla,
Shaalabbin, Aijalon, and Ithlah.
43 Eloni, Timna, Ekroni,
It also included Elon, Timnah, Ekron,
44 Elteke, Gibethoni, Baalathi,
Eltekeh, Gibbethon, Baalath,
45 Yehudi, Bene-Beraki, Gath-Rimoni,
Jehud, Bene Berak, Gath Rimmon,
46 Me-Yarkoni na Rakoni, pamoja na eneo linalotazamana na Yafa.
Me Jarkon, and Rakkon along with the territory across from Joppa.
47 (Lakini Wadani walipata shida kulimiliki eneo lao; kwa hiyo walipanda kuishambulia Leshemu, wakaitwaa, wakawaua watu wake kwa upanga na kuukalia. Walikaa Leshemu na kuuita Dani kufuatana na jina la baba yao.)
When the territory of the tribe of Dan was lost to them, Dan attacked Leshem, fought against it, capturing it and striking it with the sword; taking possession of it and settled in it. They renamed Leshem, calling it Dan after their ancestor.
48 Miji hii na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
This was the inheritance of the tribe of Dan, clan by clan—the cities, including their villages.
49 Walipomaliza kugawanya nchi katika migawo kulingana na sehemu zao zilizowaangukia, Waisraeli wakampa Yoshua mwana wa Nuni urithi katikati yao,
When they finished the allocation of the land as an inheritance, the people of Israel gave an inheritance among themselves to Joshua son of Nun.
50 kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru. Walimpa mji alioutaka, ambao ni Timnath-Sera ulio katika nchi ya vilima ya Efraimu. Naye akajenga mji, akakaa huko.
By the command of Yahweh they gave him the city for which he asked, Timnath Serah in the hill country of Ephraim. He rebuilt the city and lived there.
51 Haya ndiyo maeneo ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliyoyagawanya kwa kura huko Shilo mbele za Bwana penye ingilio la Hema la Kukutania. Hivyo wakamaliza kuigawanya nchi.
These are the inheritances that Eleazar the priest, Joshua son of Nun, and the leaders of the tribes of the people of Israel assigned by lot at Shiloh, before Yahweh, at the entrance of the tent of meeting. So they finished assigning the land.

< Yoshua 19 >