< Yoshua 19 >
1 Kura ya pili ikaangukia kabila la Simeoni, ukoo kwa ukoo. Urithi wao ulikuwa ndani ya eneo la Yuda.
And the second lot went out, for the sons of Simeon by their families. And their inheritance was,
2 Ulijumuisha: Beer-Sheba (au Sheba), Molada,
in the midst of the possession of the sons of Judah: Beersheba, and Sheba, and Moladah,
3 Hasar-Shuali, Bala, Esemu,
and Hazar-shual, Balah, and Ezem,
4 Eltoladi, Bethuli, Horma,
and Eltolad, Bethul, and Hormah,
5 Siklagi, Beth-Markabothi, Hasar-Susa,
and Ziklag, and Beth-marcaboth, and Hazar-susah,
6 Beth-Lebaothi na Sharuheni; hii ilikuwa miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake.
and Bethlebaoth, and Sharuhen: thirteen cities, and their villages;
7 Pia Aini, Rimoni, Etheri, na Ashani; hii ilikuwa miji minne na vijiji vyake,
Ain and Enrimmon, and Ether and Ashan: four cities, and their villages;
8 pamoja na vijiji vyote vinavyoizunguka miji hii mpaka Baalath-Beeri (ambayo ndiyo Rama iliyo katika Negebu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simeoni ukoo kwa ukoo.
all villages around these cities, as far as Baalath-beer, the high place facing the southern region. This is the inheritance of the sons of Simeon, according to their families,
9 Urithi wa Wasimeoni ulitolewa kutoka fungu la Yuda, kwa kuwa fungu la Yuda lilikuwa kubwa kuliko walivyohitaji. Hivyo kabila la Simeoni lilipewa urithi wao ndani ya eneo la Yuda.
within the possession and lot of the sons of Judah, which was greater. And for this reason, the sons of Simeon had a possession in the midst of their inheritance.
10 Kura ya tatu ikaangukia kabila la Zabuloni, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao uliendelea hadi Saridi.
And the third lot fell to the sons of Zebulun, by their families; and the limit of their possession was set as far as Sarid.
11 Kuelekea upande wa magharibi ukafika Marala, ukagusa Dabeshethi, na kuendelea mpaka kwenye bonde karibu na Yokneamu.
And it ascends from the sea and from Mareal. And it passes on to Dabbesheth, as far as the torrent, which is opposite Jokneam.
12 Ukageuka mashariki, kuanzia Saridi kuelekea mawio ya jua hadi kwenye nchi ya Kisiloth-Tabori, na kwenda hadi Daberathi, kupanda Yafia.
And it turns back from Sarid, to the east, to the end of Chisloth-tabor. And it goes out to Daberath, and it ascends opposite Japhia.
13 Kisha ukaendelea mashariki hadi Gath-Heferi na kufika Eth-Kasini, ukatokea Rimoni na kugeuka kuelekea Nea.
And from there, it continues to the eastern region of Gathhepher and Ethkazin. And goes out to Rimmon, Amthar, and Neah.
14 Huko mpaka ukazungukia upande wa kaskazini hadi Hanathoni na kuishia katika Bonde la Ifta-Eli.
And it circles to the north at Hannathon. And its exits are at the Valley of Iphtahel;
15 Miji mingine iliyojumuishwa ni Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.
and Kattath and Nahalal, and Shimron and Idalah, and Bethlehem: twelve cities, and their villages.
16 Miji hii na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa Zabuloni, ukoo kwa ukoo.
This is the inheritance of the tribe of the sons of Zebulun, by their families, the cities and their villages.
17 Kura ya nne ikamwangukia Isakari, ukoo kwa ukoo.
The fourth lot went out to Issachar, by their families.
18 Eneo lao lilijumuisha: Yezreeli, Kesulothi, Shunemu,
And his inheritance was: Jezreel, and Chesulloth, and Shunem,
19 Hafaraimu, Shioni, Anaharathi,
and Hapharaim, and Shion, and Anaharath,
20 Rabithi, Kishioni, Ebesi,
and Rabbith and Kishion, Ebez
21 Remethi, En-Ganimu, En-Hada na Beth-Pasesi.
and Remeth, and Engannim, and Enhaddah, and Bethpazzez.
22 Mpaka ule ukagusa Tabori, Shahasuma na Beth-Shemeshi, na ukaishia kwenye Yordani. Ilikuwa miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
And its limit reaches to Tabor and Shahazumah and Beth-shemesh; and its exits shall be at the Jordan: sixteen cities, and their villages.
23 Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Isakari, ukoo kwa ukoo.
This is the possession of the sons of Issachar by their families, the cities and their villages.
24 Kura ya tano ikaangukia kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
And the fifth lot fell to the tribe of the sons of Asher, by their families.
25 Eneo lao lilijumuisha: Helkathi, Hali, Beteni, Akishafu,
And their border was: Helkath, and Hali, and Beten, and Achshaph,
26 Alameleki, Amadi na Mishali. Upande wa magharibi mpaka uligusa Karmeli na Shihor-Libnathi.
and Allammelech, and Amad, and Mishal. And it extends even to Carmel by the sea, and Shihor, and Libnath.
27 Tena ukageuka mashariki kuelekea Beth-Dagoni, ukagusa Zabuloni na Bonde la Ifta-Eli, ukaenda upande wa kaskazini hadi Beth-Emeki na Neyeli, ukipitia Kabul upande wa kushoto.
And it turns back toward the east at Bethdagon. And it continues on as far as Zebulun and the Valley of Iphtahel, toward the north, at Beth-emek and Neiel. And it goes out to the left of Cabul,
28 Ukaendelea hadi Abdoni, Rehobu, Hamoni na Kana, na kufika Sidoni Kuu.
and to Ebron, and Rehob, and Hammon, and Kanah, as far as the great Sidon.
29 Mpaka huo ukageukia nyuma kuelekea Rama na kwenda hadi kwenye mji wenye ngome wa Tiro, ukageuka kuelekea Hosa na kutokeza baharini katika eneo la Akzibu,
And it turns back at Ramah, even to the very fortified city of Tyre, and even to Hosah. And its exits shall be at the sea, from the lot of Achzib;
30 Uma, Afeki na Rehobu. Ilikuwepo miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
and Ummah, and Aphek, and Rehob: twenty-two cities, and their villages.
31 Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
This is the possession of the sons of Asher, by their families, and the cities and their villages.
32 Kura ya sita ikaangukia kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo:
The sixth lot fell to the sons of Naphtali, by their families.
33 Mpaka wao uliendelea kutoka Helefi na kwenye mti mkubwa ulio katika Saananimu, ukipitia Adami-Nekebu na Yabineeli hadi Lakumu, na kuishia katika Mto Yordani.
And its border begins from Heleph and Elon, into Zaanannim, and Adami, which is Nekeb, and Jabneel, as far as Lakkum. And its exits are as far as the Jordan.
34 Mpaka ukaendelea magharibi kupitia Aznoth-Tabori na kutokea Hukoki. Ukagusa Zabuloni upande wa kusini, Asheri upande wa magharibi, na Yordani upande wa mashariki.
And the border turns back to the west at Aznoth-tabor, and it goes out from there to Hukkok. And continues on to Zebulun, in the south, and to Asher, in the west, and to Judah, at the Jordan, toward the rising of the sun.
35 Miji yenye ngome ilikuwa Sidimu, Seri, Hamathi, Rakathi, Kinerethi,
And the most fortified cities are Ziddim, Zer and Hammath, and Rakkath, and Chinnereth,
and Adamah and Ramah, Hazor
37 Kedeshi, Edrei, na En-Hasori,
and Kedesh and Edrei, Enhazor
38 Ironi, Migdal-Eli, Horemu, Beth-Anathi na Beth-Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa na vijiji vyake.
and Yiron and Migdalel, Horem and Bethanath, and Beth-shemesh: nineteen cities, and their villages.
39 Miji hiyo pamoja na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo.
This is the possession of the tribe of the sons of Naphtali, by their families, the cities and their villages.
40 Kura ya saba ikaangukia kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
The seventh lot went out to the tribe of the sons of Dan, by their families.
41 Eneo la urithi wao lilijumuisha: Sora, Eshtaoli, Iri-Shemeshi,
And the border of their possession was Zorah, and Eshtaol, and Ir-shemesh, that is, the City of the Sun,
42 Shaalabini, Aiyaloni, Ithla,
Sha-alabbin, and Aijalon, and Ithlah,
Elon, and Timnah, and Ekron,
44 Elteke, Gibethoni, Baalathi,
Eltekeh, Gibbethon and Baalath,
45 Yehudi, Bene-Beraki, Gath-Rimoni,
and Jehud, and Bene and Berak, and Gath-Rimmon,
46 Me-Yarkoni na Rakoni, pamoja na eneo linalotazamana na Yafa.
and Mejarkon and Rakkon, with a border that looks toward Joppa,
47 (Lakini Wadani walipata shida kulimiliki eneo lao; kwa hiyo walipanda kuishambulia Leshemu, wakaitwaa, wakawaua watu wake kwa upanga na kuukalia. Walikaa Leshemu na kuuita Dani kufuatana na jina la baba yao.)
and there the last part is concluded. And the sons of Dan ascended and fought against Leshem, and they seized it. And they struck it with the mouth of the sword, and they possessed it, and they lived in it, calling it by the name of Leshem-Dan, according to the name of their father Dan.
48 Miji hii na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
This is the possession of the tribe of the sons of Dan, by their families, the cities and their villages.
49 Walipomaliza kugawanya nchi katika migawo kulingana na sehemu zao zilizowaangukia, Waisraeli wakampa Yoshua mwana wa Nuni urithi katikati yao,
And when he had completed dividing the land by lot to each one by their tribes, the sons of Israel gave a possession to Joshua, the son of Nun, in their midst,
50 kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru. Walimpa mji alioutaka, ambao ni Timnath-Sera ulio katika nchi ya vilima ya Efraimu. Naye akajenga mji, akakaa huko.
in accord with the precept of the Lord, the city he requested, Timnath-Serah, on mount Ephraim. And he built up the city, and he lived in it.
51 Haya ndiyo maeneo ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliyoyagawanya kwa kura huko Shilo mbele za Bwana penye ingilio la Hema la Kukutania. Hivyo wakamaliza kuigawanya nchi.
These are the possessions which Eleazar, the priest, and Joshua, the son of Nun, and the leaders of the families and tribes of the sons of Israel divided by lot at Shiloh, before the Lord, at the door of the Tabernacle of the Testimony. And so did they divide the land.